Mafunzo ya Database MySQL database somo la 10

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database.

Katika somo la 9 tuliona namna ya kutumia database yaani kusoma taarifa kwenye database kwa kutumia SQL. Katika somo hili tutajifunza namna ya kupangilia data zako yaani sorting data kulingana na mahitaji yako. Hapa tutakwenda kutumia command kama WHERE, ORDER BY, AND, OR, ASC, DESC, RAND(). pia katika somo hili tutatumia sana SQL kama tulivyofanya katika somo lililopita:-

 

Katika somo hili tutatumia database yetu yenye jina hotel na table menu. Hivyo tutakwenda kujifunza somo letu kwa kutumia database hii. 

 

1. Kupangilia data kutoka kubwa kwenda ndodo

Katika SQL unapotaka kupangilia data kuwa zionekane kwa mpangilio upi tunatumia ORDER BY kisha unakuja kuweka hiyo column ambayo unataka iangaiwe. Kisha unakuja kuweka huo mpangilio wako, kama ni kuanzia kubwa kuja ndogo hapo tutatumia DESCENGING order ambapo kifupi chake ni DESC. Baada ya hapo unaweza kutumia LIMIT kama tulivyoona katika somo lililopita.

 

Mfano:

Katika menu yetu tunataka zijipange kutoka chakula chenye gharama kubwa kuja chakula chenye gharama ndogo. Hvyo kama tulivyoona katika somo lililopita utatumia select kama ni coumn zote utaweka * kisha from kisha jina la table kisha ORDER BY hapa sasa tuta zipanga kulingana na price zao, hivyo itakuwa ORDER BY price kisha tutaweka mpangilio tunaotaka kama ni kubwa kja ndogo tutatumia DESC unaweza kuongeza LIMIT 5 kwa mfano ili kuona idadi maalumu Hivyo command yote itaonekana hivi:-

SELECT * FROM `menu` ORDER BY `price` DESC LIMIT 5;

 

2. Kupangilia data kutoka ndogo kwenda kubwa

Mfano huu haupo tofauti sana na huo wa juu. Hapa tunataka data zijipange kulungana na gharama zao lakini zianze ndogo zije kubwa. Pia tutataka kuoan 5 tu za mwanzo. Ili kuweza kupanga ndogo kwenda kubwa tunatumia ASCENDING ORDER ambayo kifupi chake ni ASC. Hivyo command nzima itakuwa hivi

SELECT * FROM `menu` ORDER BY `price` ASC LIMIT 5;

 

3. Kupangilia data random (yaani bila mpangilio maalumu)

Yaani tunataka taarifa zijipango kwa mchanganyiko bila kujali kubwa ama ndogo. Yaani hovyohovyo. Kufanya hivi tutatumia ORDER BY RAND(). Yaani random. Hivyo command itakuwa hivi 

SELECT * FROM `menu` ORDER BY RAND() LIMIT 5

 

4. Kupanga kutoka A kwenda Z ama kutoka Z kwenda A.

Sasa menu yetu tunataka kuzisoma data kwa majina yake kutoka A kwenda Z. kitu cha kwanza ni kujuwa column yenye majina ni ipi. Katika table yetu majina yapo kwenye column yenye jina name. Kupanga tutoka A kwenda Z tutatumia ASC kama tulivyoona kwenye mfano uliotangaulia. Na kupanda kutoka Z kwenda A tutatumia DESC kama tulvyoona huko juu. 

 

Kikubwa hapa tumebadili column. Hapo mwanzo tulitumia column ya price kwani tulikuwa tunazipanga kulingana na price zao. Sasa tutatumia column ya name kwani tunapanga kulingana na majina yao.

 

A. Hivyo kupanga A to Z tutatumia

SELECT * FROM `menu` ORDER BY name ASC LIMIT 5

Hapo data zako zitajipanga kwa majina yao kutoka A to Z

 

B. Kupanga Z to A

SELECT * FROM `menu` ORDER BY name DESC LIMIT 5

Hapodata zako zitajipanga kutoka Z to A kulingana na majina (name)

 

5. Pia unaweza kuchaguwa column za kuona kama tulivyoona somo la tisa. Yaani namaanisha unataka kuosma majina na gharama tu, ila zijipange kulingana na gharama zake kutoka kubwa kwenda ndogo mathalan. Utofauti wa mfano huu na ulotangulia ni kuwa hapo mwanzo umezisoma data zote kuanzia id, name, description na price. (rejea matumizi ya nyota * kwenye somo la tisa)

 

Hivyo kwa mfano huo comand itakuwa hivi:

SELECT name, price FROM `menu`ORDER BY price DESC LIMIT 8;

Hapo utaona column mbili tua mbayo ni ya name na price na zitajipanga kutoka yenye gharama kubwa kwenda ndogo na itaonyesha row 8 tu.

 

Endelea nami kwenye somo la 11 ambapo tutajifunza namna ya kutumia where, and, or . kwa sasa endelea kufanyia mazoezi ya kutosha database hii.

 

Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 1349

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

PHP level 1 somo la nane (8)

Hapa utajifunza utofauti kati ya php constant na variable. Na hili ni somo la nane katika mfululizo wa masomo haya ya php level 1.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 1 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 1)

hili ni somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2 html full course for beginners. Katika somo hili tutaangalia utangulizi juu ya HTML na pia utajifunza faida za HTML.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL - DATABASE somo la 6

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 6. Katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza table kwa kutumia MySQL na kwa kutuma SQL.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la sita (6)

Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 4 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 4 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 4)

Karibu tena katika somo la nne la mafunzo ya HTML level2 html full course for beginners. Katika somo hili utajifunza kuhusu attributes na namna zinavyofanya kazi

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la kumi (10)

Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)

Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi.

Soma Zaidi...
Utangulizi wa Android App Development

Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 8 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 8)

Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners)

Soma Zaidi...