Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database.
Katika somo la 9 tuliona namna ya kutumia database yaani kusoma taarifa kwenye database kwa kutumia SQL. Katika somo hili tutajifunza namna ya kupangilia data zako yaani sorting data kulingana na mahitaji yako. Hapa tutakwenda kutumia command kama WHERE, ORDER BY, AND, OR, ASC, DESC, RAND(). pia katika somo hili tutatumia sana SQL kama tulivyofanya katika somo lililopita:-
Katika somo hili tutatumia database yetu yenye jina hotel na table menu. Hivyo tutakwenda kujifunza somo letu kwa kutumia database hii.
1. Kupangilia data kutoka kubwa kwenda ndodo
Katika SQL unapotaka kupangilia data kuwa zionekane kwa mpangilio upi tunatumia ORDER BY kisha unakuja kuweka hiyo column ambayo unataka iangaiwe. Kisha unakuja kuweka huo mpangilio wako, kama ni kuanzia kubwa kuja ndogo hapo tutatumia DESCENGING order ambapo kifupi chake ni DESC. Baada ya hapo unaweza kutumia LIMIT kama tulivyoona katika somo lililopita.
Mfano:
Katika menu yetu tunataka zijipange kutoka chakula chenye gharama kubwa kuja chakula chenye gharama ndogo. Hvyo kama tulivyoona katika somo lililopita utatumia select kama ni coumn zote utaweka * kisha from kisha jina la table kisha ORDER BY hapa sasa tuta zipanga kulingana na price zao, hivyo itakuwa ORDER BY price kisha tutaweka mpangilio tunaotaka kama ni kubwa kja ndogo tutatumia DESC unaweza kuongeza LIMIT 5 kwa mfano ili kuona idadi maalumu Hivyo command yote itaonekana hivi:-
SELECT * FROM `menu` ORDER BY `price` DESC LIMIT 5;
2. Kupangilia data kutoka ndogo kwenda kubwa
Mfano huu haupo tofauti sana na huo wa juu. Hapa tunataka data zijipange kulungana na gharama zao lakini zianze ndogo zije kubwa. Pia tutataka kuoan 5 tu za mwanzo. Ili kuweza kupanga ndogo kwenda kubwa tunatumia ASCENDING ORDER ambayo kifupi chake ni ASC. Hivyo command nzima itakuwa hivi
SELECT * FROM `menu` ORDER BY `price` ASC LIMIT 5;
3. Kupangilia data random (yaani bila mpangilio maalumu)
Yaani tunataka taarifa zijipango kwa mchanganyiko bila kujali kubwa ama ndogo. Yaani hovyohovyo. Kufanya hivi tutatumia ORDER BY RAND(). Yaani random. Hivyo command itakuwa hivi
SELECT * FROM `menu` ORDER BY RAND() LIMIT 5
4. Kupanga kutoka A kwenda Z ama kutoka Z kwenda A.
Sasa menu yetu tunataka kuzisoma data kwa majina yake kutoka A kwenda Z. kitu cha kwanza ni kujuwa column yenye majina ni ipi. Katika table yetu majina yapo kwenye column yenye jina name. Kupanga tutoka A kwenda Z tutatumia ASC kama tulivyoona kwenye mfano uliotangaulia. Na kupanda kutoka Z kwenda A tutatumia DESC kama tulvyoona huko juu.
Kikubwa hapa tumebadili column. Hapo mwanzo tulitumia column ya price kwani tulikuwa tunazipanga kulingana na price zao. Sasa tutatumia column ya name kwani tunapanga kulingana na majina yao.
A. Hivyo kupanga A to Z tutatumia
SELECT * FROM `menu` ORDER BY name ASC LIMIT 5
Hapo data zako zitajipanga kwa majina yao kutoka A to Z
B. Kupanga Z to A
SELECT * FROM `menu` ORDER BY name DESC LIMIT 5
Hapodata zako zitajipanga kutoka Z to A kulingana na majina (name)
5. Pia unaweza kuchaguwa column za kuona kama tulivyoona somo la tisa. Yaani namaanisha unataka kuosma majina na gharama tu, ila zijipange kulingana na gharama zake kutoka kubwa kwenda ndogo mathalan. Utofauti wa mfano huu na ulotangulia ni kuwa hapo mwanzo umezisoma data zote kuanzia id, name, description na price. (rejea matumizi ya nyota * kwenye somo la tisa)
Hivyo kwa mfano huo comand itakuwa hivi:
SELECT name, price FROM `menu`ORDER BY price DESC LIMIT 8;
Hapo utaona column mbili tua mbayo ni ya name na price na zitajipanga kutoka yenye gharama kubwa kwenda ndogo na itaonyesha row 8 tu.
Endelea nami kwenye somo la 11 ambapo tutajifunza namna ya kutumia where, and, or . kwa sasa endelea kufanyia mazoezi ya kutosha database hii.
Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email: mafunzo@bongoclass.com
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.
Soma Zaidi...Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia.
Soma Zaidi...Karibu kwenye mafunzo ya PHP level 1 na hili ni somo la kwanza. Hapa utajifunza maana ya php, inavyofanya kazi pamoja na historia yake kwa ufupi
Soma Zaidi...katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment
Soma Zaidi...Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.
Soma Zaidi...Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.
Soma Zaidi...hili ni somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2 html full course for beginners. Katika somo hili tutaangalia utangulizi juu ya HTML na pia utajifunza faida za HTML.
Soma Zaidi...Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement.
Soma Zaidi...hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.
Soma Zaidi...Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.
Soma Zaidi...