Mafunzo ya Database MySQL database somo la 10

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database.

Katika somo la 9 tuliona namna ya kutumia database yaani kusoma taarifa kwenye database kwa kutumia SQL. Katika somo hili tutajifunza namna ya kupangilia data zako yaani sorting data kulingana na mahitaji yako. Hapa tutakwenda kutumia command kama WHERE, ORDER BY, AND, OR, ASC, DESC, RAND(). pia katika somo hili tutatumia sana SQL kama tulivyofanya katika somo lililopita:-

 

Katika somo hili tutatumia database yetu yenye jina hotel na table menu. Hivyo tutakwenda kujifunza somo letu kwa kutumia database hii. 

 

1. Kupangilia data kutoka kubwa kwenda ndodo

Katika SQL unapotaka kupangilia data kuwa zionekane kwa mpangilio upi tunatumia ORDER BY kisha unakuja kuweka hiyo column ambayo unataka iangaiwe. Kisha unakuja kuweka huo mpangilio wako, kama ni kuanzia kubwa kuja ndogo hapo tutatumia DESCENGING order ambapo kifupi chake ni DESC. Baada ya hapo unaweza kutumia LIMIT kama tulivyoona katika somo lililopita.

 

Mfano:

Katika menu yetu tunataka zijipange kutoka chakula chenye gharama kubwa kuja chakula chenye gharama ndogo. Hvyo kama tulivyoona katika somo lililopita utatumia select kama ni coumn zote utaweka * kisha from kisha jina la table kisha ORDER BY hapa sasa tuta zipanga kulingana na price zao, hivyo itakuwa ORDER BY price kisha tutaweka mpangilio tunaotaka kama ni kubwa kja ndogo tutatumia DESC unaweza kuongeza LIMIT 5 kwa mfano ili kuona idadi maalumu Hivyo command yote itaonekana hivi:-

SELECT * FROM `menu` ORDER BY `price` DESC LIMIT 5;

 

2. Kupangilia data kutoka ndogo kwenda kubwa

Mfano huu haupo tofauti sana na huo wa juu. Hapa tunataka data zijipange kulungana na gharama zao lakini zianze ndogo zije kubwa. Pia tutataka kuoan 5 tu za mwanzo. Ili kuweza kupanga ndogo kwenda kubwa tunatumia ASCENDING ORDER ambayo kifupi chake ni ASC. Hivyo command nzima itakuwa hivi

SELECT * FROM `menu` ORDER BY `price` ASC LIMIT 5;

 

3. Kupangilia data random (yaani bila mpangilio maalumu)

Yaani tunataka taarifa zijipango kwa mchanganyiko bila kujali kubwa ama ndogo. Yaani hovyohovyo. Kufanya hivi tutatumia ORDER BY RAND(). Yaani random. Hivyo command itakuwa hivi 

SELECT * FROM `menu` ORDER BY RAND() LIMIT 5

 

4. Kupanga kutoka A kwenda Z ama kutoka Z kwenda A.

Sasa menu yetu tunataka kuzisoma data kwa majina yake kutoka A kwenda Z. kitu cha kwanza ni kujuwa column yenye majina ni ipi. Katika table yetu majina yapo kwenye column yenye jina name. Kupanga tutoka A kwenda Z tutatumia ASC kama tulivyoona kwenye mfano uliotangaulia. Na kupanda kutoka Z kwenda A tutatumia DESC kama tulvyoona huko juu. 

 

Kikubwa hapa tumebadili column. Hapo mwanzo tulitumia column ya price kwani tulikuwa tunazipanga kulingana na price zao. Sasa tutatumia column ya name kwani tunapanga kulingana na majina yao.

 

A. Hivyo kupanga A to Z tutatumia

SELECT * FROM `menu` ORDER BY name ASC LIMIT 5

Hapo data zako zitajipanga kwa majina yao kutoka A to Z

 

B. Kupanga Z to A

SELECT * FROM `menu` ORDER BY name DESC LIMIT 5

Hapodata zako zitajipanga kutoka Z to A kulingana na majina (name)

 

5. Pia unaweza kuchaguwa column za kuona kama tulivyoona somo la tisa. Yaani namaanisha unataka kuosma majina na gharama tu, ila zijipange kulingana na gharama zake kutoka kubwa kwenda ndogo mathalan. Utofauti wa mfano huu na ulotangulia ni kuwa hapo mwanzo umezisoma data zote kuanzia id, name, description na price. (rejea matumizi ya nyota * kwenye somo la tisa)

 

Hivyo kwa mfano huo comand itakuwa hivi:

SELECT name, price FROM `menu`ORDER BY price DESC LIMIT 8;

Hapo utaona column mbili tua mbayo ni ya name na price na zitajipanga kutoka yenye gharama kubwa kwenda ndogo na itaonyesha row 8 tu.

 

Endelea nami kwenye somo la 11 ambapo tutajifunza namna ya kutumia where, and, or . kwa sasa endelea kufanyia mazoezi ya kutosha database hii.

 

Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021/12/21/Tuesday - 12:21:32 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1031

Post zifazofanana:-

Safari ya kwanza ya sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat al qariah
Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume. Soma Zaidi...

Hatua za Kuzuia Maambukizi ya Uvimbe kwenye ovari na mirija ya uzazi
Posti hii inazungumzia kuhusiana na hatua za kujikinga na Maambukizi ya Uvimbe kwenye ovari na kwenye mirija ya uzazi Soma Zaidi...

Nguzo za kufunga ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Je unazijuwa dalili za Ukimwi na HIV?
Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mw Soma Zaidi...

Matatizo ya mapigo ya moyo
posti hii inazungumzia kuhusiana na matatizo ya mapigo ya moyo.Mapigo ya moyo ni hisia za kuwa na moyo wa haraka, unaodunda. Mapigo ya moyo yanaweza kuchochewa na mafadhaiko, mazoezi, dawa au, mara chache, hali ya kiafya. Ingawa mapigo ya moyo yanaweza k Soma Zaidi...

Zijue dalili za upungufu wa maji mwilini
Posti hii inaelezea kuhusiana na upungufu wa maji mwilini Soma Zaidi...

Utajuwaje kama kidonda kupona
Posti hii inahusu zaidi juu ya kuhakiki kama kidonda kimepona kwa mgonjwa mwenye vidonda, kwanza kabisa tunajua kuwa vidonda uwanyima Watu raha na pengine kuwafanya wakate tamaa kama wapo hospitalini kwa hiyo tunapaswa kutumia njia zifuatazo ili kuweza ku Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ukoma, ni Ugonjwa unaosababishwa na mdudu anayeitwa mycobacterium leprae, mdudu huyu kwa kawaida uathiri sana sehemu za ngozi na sehemu za Neva mbalimbali za mwili Soma Zaidi...

Siri ya wageni wale inafichuka
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Dalili za Ugonjwa wa ini
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa inni, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye ugonjwa wa inni, Dalili zenyewe ni kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Tofauti ya Trojan na virusi
Posti hii inakwenda kukupa tofauti za trojani na virusi Soma Zaidi...