image

Mafunzo ya database MySQL database somo la 9

haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE.

SOMO LA TISA.

Katika somo hili la tisa tutakqenda kuona namna ya kutumia database. Somo hili tutajifunza jinsi ya kusoma data kwenye database. Hapa tutaona jinsi ya kutumia command kama:-

  1. Select
  2. limit

Somo hili ni msingi mzuri sana kwa masomo yajayo. Somo hili tutakwenda kutumia sana uwanja wa SQL tofauti na masomo yaliyotangalia ambapo tulikuwa tukitumia MySQL interface na SQL .

 

Maandalizi ya somo la tisa:

tengeneza database yemye jina hoteli kisha tengeneza table yennye jina menu ama pest code hizi kwenye uwanja wa sql:-

CREATE TABLE IF NOT EXISTS `menu` (

  `id` int(100) NOT NULL,

  `name` varchar(255) NOT NULL,

  `description` varchar(255) NOT NULL,

  `price` int(100) NOT NULL

) ENGINE=InnoDB DEFAULT CHARSET=utf8mb4;

 

Kisha jaza data kwenye table yako. Unaweza kupest data hizi kwenye uwanja wa sql:-

INSERT INTO `menu` (`id`, `name`, `description`, `price`) VALUES

(1, 'ugali', 'Pata ugali na mchuzi, ama ugali na nyama ama ugali na samaki. Ugali wa mahindi na muhogo', 1500),

(2, 'Wali', 'Pata waki na mchuzi, ama wali na nyama ama wali na samaki.', 2000),

(3, 'chai', 'Pata chai maandazi, chapati, ndizi, na supu', 3000),

(4, 'internet', 'Pata huduma za internet free huku ukijipatia chakula hapa, utalipia kila nusu saa utakalotuia', 700),

(5, 'simu', 'Pata huduma za simu bre huku ukijipatia chakula hapa, utalipia kila nusu saa utakalotuia', 1200),

(6, 'ushauri', 'Tunatowa huduma za ushauri nasaha, utalipia kwa kila nusu saa utakaloluwa unapewa ushauri', 1000),

(7, 'huduma za Afya', 'Hapa utapata huduma za afya za awali kama bipimo vya uti, malaria, mimba na vinginevyo. utalipia kwa kila kipimo', 5000),

(8, 'Mapishi', 'pia tunatowa mafunzo ya mapishi kwa gharama nafuu. Utalipia kwa kila nusu saa utakalokuwa unafundishwa.', 9500),

(9, 'matanazo', 'Pia tunatowa matangazo mbalimbali kuwapatia waeja wetu. utalipia kwa kila tangazo litakapotagazwa', 25000),

(10, 'maji ya kunywa', 'huduma hii itatoka kwa gharama nafuu. utajipatia maji ya kunywa baridi. Utalipia kwa kila glasi', 300);

 

Baada yahapo utakuwa upo tayari pamoja nami katika somo hili la tisa katika mafunzo ya database kwa kutumia software ya MySQl.

 

1. Kusoma taarifa (data) zilizopo kwenye database

Hapa tunatumia command ya SELECT. Lakini pia tunaweza kutumia MySQL interface kufanya hili. Hapa nitaanza kukuonyesha namna ya kutumia MySQL intrface.

 

  1. Kusoma taarifa kwenye database kwa kutumia MySQL interface.
  1. Kwanza bofya database yako hoteli
  2. Kisha tfuta neno lililoandikwa Browse bofya hapo utaona data zote zilizopo.
  3. Utaweza kufanya mengine utakayotaka kama tulivyojifunza kama kufuta, kuedit ama kufanya chochote.

 

2. Kusoma taarifa kwenye database kwa kutumia SQl

  1. Bofya database yako
  2. Imgia kwenye uwanja wa SQl
  3. Andika SELECT kisha weka * kisha weka FROM kisha weka jina la table yenye hizo data kisha weka ;  itaonekana kama hivi:
  4. SELECT * FROM `menu`
  5. Kisha bofya Go
  6. Utaona taarifa zote kwenye hiyotable zimeorodheshwa chini.
  7. Hiyo nyota hapo inamaana all yaani select all. Ndio maana hapo data zote zimetokea.

 

Kwa kutumia mfano huo hapo tumechaguwa data zote. Sasa chukulia mfano unataka kuona majina tu ya menu na si gharama na maelezo meengi. Kufanya hivi utahitajika kutaja hivyo unachotaka kukiona pale tulipoweka nota: Mfano:-

 

Table yetu inaitwa menu. Na ina column kama name, descriptions, na price. Sasa hapa ninataka kusoma column ya name tu. Hapa tutatumia command hii

SELECT name FROM `menu`;

 

Utaona hapo pale kwenye nyota ambapo ilimaanisha All data tumeitowa na kuweka name kwa maana tunataka kuona name tu na si data zote. Hapo ukibofya Go ukurasa utakaokuja ni wa name tu. Kwa kufanya hivi utaweza kuchaguwa chochote kwa mfano:

  1. SELECT description FROM `menu`; hii itakuletea description tu
  2. SELECT price FROM `menu`; hii itakuonyesha price tu
  3. SELECT id FROM `menu`; hii itakuonyesha id tu

 

Pia unaweza kuchaguwa viwili ama vitatu. Yaani kwa mfano ninahitaji kuonyesha name na price tu sitaki kuona maelezo meengi. Kufanya hivi utatengenisha kwa kutumia koma (,) ila neno la mwisho halitakiwi kuwa na koma.

 

Sasa tuseme tunataka kusoma name na price tu yaani utaona majina ya menu na gharama zake. Kufanya hivi tutatumia command hii:-

SELECT name, price FROM `menu`; ukibpfya Go utaoona rodha ya majina ya menu na gharama tu. Kwa kufanya hivi utaweza kubadili chohote hapo ama hata ukitaka kuta vyote mfano SELECT name, price, description FROM `menu`;

 

Taarifa zako zitajipanga kulingana na ulivyoandika wewe hizi command na sio kulingana na mpangilio wake kwenye database. Mfano kwenye database kilichoanza ni id kisha name kisha description kisha price. Sasa sisi tunataka kupangilia ianze gharama kisha id kisha description kisha name. Weka command hii SELECT price, id, description, name FROM `menu`; ukibofya go hapo data zitajipanga hivyohivyo kama ulivyoandika.

 

 

3. Kulimit kiasi cha taarifa

Hii ina maana kuwa chukulia mfano table yako ina orodha ya row 1000 za data na wewe huna huo muda wa kusoma zote. Hivyo utahitaji lamda kusoma kwanza 20 za mwano ama ishirini za mwisho. Kufanya hivi tutatumia LIMIT kisha tutaweka idadi ya row unazotaka kuzisoma kwa mfano kama 4 utaweka LIMIT 4.

 

Mfano tunataka kusoma name na price ila tunataka zionekane row 20 hpata tutaweka command hii:-

SELECT name, price FROM `menu` LIMIT 4  hapo ukibofya Go utaletewa orodha ya row nne tu. Unaweza kutumia mfano huu kwa command nyingine. Mfano

SELECT name FROM `menu` LIMIT 6;

SELECT  price FROM `menu` LIMIT 7;

SELECT * FROM `menu` LIMIT 8;

 

Katika somo linalofata tutajifunza namna ya kupangilia hizo orodha za data. Mfano unataka zijipange kutoka yenye price kubwa kwenda ndogo, ama zijipange kutoka A to Z ama zijipage random. Command tutakayokuja kuitumia ni ORDER BY hivyo nakusihi usikose somo la 10.

 

NB: course hii itakusanya masomo 12 tu, kabla ya kuingia course ya pili. Level hii hatutakuwa na project. Ila natumai tutakuwa pamoja level ya pili ambapo utapata fursa ya kufanya project nasi:

 

Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 846


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

PHP level 1 somo la nane (8)
Hapa utajifunza utofauti kati ya php constant na variable. Na hili ni somo la nane katika mfululizo wa masomo haya ya php level 1. Soma Zaidi...

Php level 1 somo la saba (7)
Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe. Soma Zaidi...

PHP level 1 somo la kumi na mbili (12) final
Mafunzo ya php level 1 somo ka 12 mwisho wa mafunzo. Hapa utaona project ambazo unaweza kufanya kutokana na mafunzo haya. Soma Zaidi...

Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8
Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho. Soma Zaidi...

Mafunzo ya Database MySQL database somo la 10
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 4 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 8 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 8)
Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners) Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 5 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 3 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Hili ni somo la Tatu katika mfululizo wetu wa mafunzo ya HTML kwa basic level kwa wanaoanza kujifunza. Hapa tutakwenda kujifunza tag za html ambazo huwa zinatumika katika uandishi. Soma Zaidi...

Utangulizi wa Android App Development
Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake. Soma Zaidi...

PHP level 1 somo la tano (5)
Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions. Soma Zaidi...