Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8

Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.

SOMO LA NANE

Katika somo lililotangulia tumejifunz namna ya kubadili jina kwenye table pia tukaona kuongeza column. Sasa katika somo hili hasa ndipo tunakwenda kuweka data kwenye table yetu, yaani kuweka data kwenye database. Katika somo hili tunakwenda kutumia ile table tulioiita post.

 

1. Kuweka data kwenye table kwa kutumia MySQL

Kama tulivyofanya kwenye masomo yaliyotangulia kuwa tunatumia MySQl kisha tunatumia SQL statement hivyohivyo ndivyo tutakavyofanya kwenye somo hili.Ili kuweka taarifa kwenye database yako fuata hatuwa zifuata:-

 

  1. Fifya hiyo table yenye jina post
  2. Kwenye menu juu bofya neno insert
  3. Ukurasa wenye vijumba vingi utafunguka
  4. utaona kuna column zile ambazo tumetengeneza aina zake za data na character leght. Sasa wewe unachotakiwa ni kutafuta palipoandikwa value chini yake kuna hivyo vijumba.
  5. Angalia mpangilio wa hiyo menu. Imeanza column, kisha type kisha Function kisha Null kisha Value.
  6. Hivyo utaangalia kwenye column kama ni Id utaweka value yake kwenye kijumba cha value. Weka namba moja kwenye id
  7. Angalia kwenye column baada ya id inafata title nenda upande wa kulia kwenye value weka jina la kichwa cha habari cha post yako mfanp “mafunzo ya html”
  8. Angalia column nyngine ambayo ni summaery kwenye value weka mhutasari wa ppost yako mafano “post hii itakwenda kukujuwa maana ya HTML”
  9. Cheki tene kenye column inafata content hapo weka maudhui ya post yako mfano “HTML ni kifupisho cha Hypertext Markup Language”
  10. Kisha kwenye image weka link ya picha yako mfano  unaweza kutumia link hii “https://bongomakataba.web.app/images/sampo.png”
  11. Kwenye publisher weka jina lako mfano “Bongoclass”
  12. Kwenye date angalia kwenye value utaona kajialama ka kalenda kadogo bofya hako kisha bofya tarehe ya leo utaona imekaa.
  13. Kisha bofya GO.
  14. Mpaka kufika hapo utakuwa umeongeza data. Kwenye menu juu bofya browser utaona post yako.
  15. Baada ya hapo ingia kwenye structure
  16. Kwenye column ya id kulia bofya change kama vile unataka kuiedit
  17. Angalia kwenye A_I au autoincement kama pana tiki, kama hapana weka tiki kisha save, kama ipo rudi nyuma.
  18. Angalia kwenye column ya edit kuliani mwa neno change kuna neno linasomeka more bofya hapo kisha kwenye menu itakayokuja bofya unique, kuna kaujumbe katakuja weka ok
  19. Kuipa column unique maana yake tunataka isifanane datazake. Kwa mfano kama post ina id 1 isitokee nyingine ikawa na namba hiyohiyo.
  20. Rudi kwenye browser.
  21. Utaona post yako uliyoweka pamoja na menu nyingine kama edit na nyinginezo.

Fanya hivi kuweka posta zaidi na kwenye menu weka menu inayoitwa afya.

 

2. Kuweka data kwenye table kwa kutumia SQL

Sasa tunakwenda kuongeza data kwenye table yetu menu. Tujaalie tunataka kuweka menu ya afya kwenye blog yetu sasa tunakwenda kuongeza menu ya afya.

 

Kwanza tuedit table ya menu nayo iwena unique kama tulivyofanya kwenye post. Hivyo ingia kwenye structure, kwenye id bofya change, angalia kwenye Null kama kuna tiki ondoa, angalia kwenye A_I  kama hakuna tiki weka, kisha save.

 

Kwenye id nenda pembeni ya change bofya more, kisha unique kisha kwenye kaujumbe utakaokuja bofya OK.

 

Kisha edit na hiyo title ingia change kwenye null ondoa tiki kisha save. Baada ya hapo table yetu tutakuwa tumeiandaa vyema kwa ajili ya kutumia SQL kwa urahisi kabisa. Sasa ili uweze kuweka data kwa kutumia SQl fuata hatuwa hizi:-

 

  1. Ingia kwenye uwanja wa SQl
  2. Ili kuweka data kwa kutumia SQl huwa tunatumia INSERT INTO kisha jina la table kisha weka mabano na ndani yake utaandika majina ya column mfano id na title utatenganisha kwa kutumia alama ya koma (,) ila neno la mwisho halina koma kisha utafunga mabano. Baada ya hapo ni kuweka value, value maana ya ke ni thamani, aua hicho unachotaka kukiweka kwenye hiyo column. Value nayo itakuwa ndani ya mabano kwa kulingana na mabano ya mwanzo.
  3. Yaani thamani ya id itaana kisha itafata thamani ya title. Hivyo itasome ka kama:-
  4. INSERT INTO `menu` (`id`, `title`) VALUES (NULL, 'afya'); hapo kwenye null kule itaweka namba yenye kwa kuwa umeiambia kwenye A_I. ila ukitaka unaweza kuweka namba wewe mfano
  5. INSERT INTO `menu` (`id`, `title`) VALUES (4, 'afya');
  6. Mpaka kufikia hapo utakuwa umeongeza menu ya afya kwenye table yako.
  7. Fanya hivi kuongeza menu zaidi.

 

3. Kuedit na kufuta data kwenye table

Kuedit data kwenye MySQl rahisi sana. Kwanza bofya hiyo table mfano post. Kisha bofya browser utaona data zako.utaone katika kila row yako ya data kuna neno edit na delete. Unachotakiwa kufanya ni kubofya edit ama delete. Ukibofya delete maana yake unafuta. Na ukibofya edit maana yake utaedit.ukimaliza kuedit bofya neno GO na hapo data yako itakuwa imebadilika.

 

Pia MySQL inakupa fursa ya kuedit humohumo huku tunaita inline edit. Unachotakiwa kufanya kama unataka kuedit column ya conten bofya hapo, kwenye data yenyewe ya kontente yaani maandishi ambayo umesha andika. Baada ya hapo utaona kamsitari ka kuonesha sasa unaweza kuedit. Hakuna haja ya kusave ukiodoka tu hapo itasave automatik. Ama unaweza pia kubofya pembeni ambapo hapana maandishi itasave yenyewe automatiki.

 

4. Kufuta ama kuedit kwa kutumia SQL

Kwa kutumia SQL pia unaweza kufuta data kwenye database ama kuedit. Ila jambo hili tutajifunza katika masomo yanayofuata kwa sasa tuendelee kutumia MySQL interface kufanya haya.

 

Somo linalofuata tutajifunza namna ya kusoma data kwenye database. Kazi yako kwa sasa kablya ya kuingia somo lijalo ni kuhakikisha kuwa umeweka data nyingi zaidi kwenye table zako. Unaweza kupost posta 5 kwenye dabke ya post na menu hivyo hivyoo ama zaidi ya hapo.

 

 

Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021/11/21/Sunday - 01:30:30 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 807


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mafunzo ya database mySQl database somo la 11
huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database. Soma Zaidi...

Niambie mwanya na pengo kwa kiingereza vinaitwaje?
Give inakuwa mwajima unaitwaje kwa kiingereza. Kama hilo haji base niambie pengo linaitwaje kwa kiingereza. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)
Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi. Soma Zaidi...

Tofauti ya Trojan na virusi
Posti hii inakwenda kukupa tofauti za trojani na virusi Soma Zaidi...

WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 1
Post hii inahusu zaidi hadithi mpya na nzuri inayoitwa wakati wa Kufumbuka, ni hadithi inayohusu maisha ya kawaida ambapo watu ushindwa kudhamini watu wa karibu nao na kuona watu wa mbali ndio wenye maana ila shida zikifika ndipo wanaona umuhimu wao. Soma Zaidi...

Jinsi ya kutoa pesa ClipClaps kwa Tanzania
Njia za kutoa pesa ClipClaps Soma Zaidi...

Maanavya legacy contact katika Facebook
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya legacy contact katika facebook Soma Zaidi...

Epuka malware (virus,work)ukiwa mtandaoni
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuepuka malware ukiwa mtandaoni Soma Zaidi...

PHP level 1 somo la sita (6)
Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP Soma Zaidi...

Mafunzo ya php level 1 somo la pili (2)
hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php. Soma Zaidi...

PHP level 11 somo la kumi na moja (11)
Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form. Soma Zaidi...

Kipi kingine utafanya ukiwa Facebook
Somo hili linakwenda kukueleza Mambo mengne unayoweza kuyafanya ukiwa Facebook Soma Zaidi...