Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.
SOMO LA NANE
Katika somo lililotangulia tumejifunz namna ya kubadili jina kwenye table pia tukaona kuongeza column. Sasa katika somo hili hasa ndipo tunakwenda kuweka data kwenye table yetu, yaani kuweka data kwenye database. Katika somo hili tunakwenda kutumia ile table tulioiita post.
1. Kuweka data kwenye table kwa kutumia MySQL
Kama tulivyofanya kwenye masomo yaliyotangulia kuwa tunatumia MySQl kisha tunatumia SQL statement hivyohivyo ndivyo tutakavyofanya kwenye somo hili.Ili kuweka taarifa kwenye database yako fuata hatuwa zifuata:-
Fanya hivi kuweka posta zaidi na kwenye menu weka menu inayoitwa afya.
2. Kuweka data kwenye table kwa kutumia SQL
Sasa tunakwenda kuongeza data kwenye table yetu menu. Tujaalie tunataka kuweka menu ya afya kwenye blog yetu sasa tunakwenda kuongeza menu ya afya.
Kwanza tuedit table ya menu nayo iwena unique kama tulivyofanya kwenye post. Hivyo ingia kwenye structure, kwenye id bofya change, angalia kwenye Null kama kuna tiki ondoa, angalia kwenye A_I kama hakuna tiki weka, kisha save.
Kwenye id nenda pembeni ya change bofya more, kisha unique kisha kwenye kaujumbe utakaokuja bofya OK.
Kisha edit na hiyo title ingia change kwenye null ondoa tiki kisha save. Baada ya hapo table yetu tutakuwa tumeiandaa vyema kwa ajili ya kutumia SQL kwa urahisi kabisa. Sasa ili uweze kuweka data kwa kutumia SQl fuata hatuwa hizi:-
3. Kuedit na kufuta data kwenye table
Kuedit data kwenye MySQl rahisi sana. Kwanza bofya hiyo table mfano post. Kisha bofya browser utaona data zako.utaone katika kila row yako ya data kuna neno edit na delete. Unachotakiwa kufanya ni kubofya edit ama delete. Ukibofya delete maana yake unafuta. Na ukibofya edit maana yake utaedit.ukimaliza kuedit bofya neno GO na hapo data yako itakuwa imebadilika.
Pia MySQL inakupa fursa ya kuedit humohumo huku tunaita inline edit. Unachotakiwa kufanya kama unataka kuedit column ya conten bofya hapo, kwenye data yenyewe ya kontente yaani maandishi ambayo umesha andika. Baada ya hapo utaona kamsitari ka kuonesha sasa unaweza kuedit. Hakuna haja ya kusave ukiodoka tu hapo itasave automatik. Ama unaweza pia kubofya pembeni ambapo hapana maandishi itasave yenyewe automatiki.
4. Kufuta ama kuedit kwa kutumia SQL
Kwa kutumia SQL pia unaweza kufuta data kwenye database ama kuedit. Ila jambo hili tutajifunza katika masomo yanayofuata kwa sasa tuendelee kutumia MySQL interface kufanya haya.
Somo linalofuata tutajifunza namna ya kusoma data kwenye database. Kazi yako kwa sasa kablya ya kuingia somo lijalo ni kuhakikisha kuwa umeweka data nyingi zaidi kwenye table zako. Unaweza kupost posta 5 kwenye dabke ya post na menu hivyo hivyoo ama zaidi ya hapo.
Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email: mafunzo@bongoclass.com
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo ya html level ya 1 na hapa tutakwenda sasa kunanza somo letu rasmi, kwani katika somo la kwanza umejifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE
Soma Zaidi...Hii ni tafiti ambayo itakushangaza, kwa namna ambavyo matumizi ya AI yalivyo na athari kwenye uwezo wa kufikiri
Soma Zaidi...Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.
Soma Zaidi...hili ni somo la sita katika mfululizo wa mafunzo ya HTML level 1. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive.
Soma Zaidi...Hii ni project ya HTML ambayo imetengenezwa kulingana na mafunzo ya HTML level1. Tunatarajia project hii kuboreshwa kadiri mafunzo yanavyozidi kusonga mbele.
Soma Zaidi...Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners)
Soma Zaidi...katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment
Soma Zaidi...Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako.
Soma Zaidi...Somo la nane mafunzo ya php, katika somo hili utajifunza kuhusu array na jinsi ya kutengeneza array.
Soma Zaidi...