Mafunzo ya database mySQl database somo la 11

Mafunzo ya database mySQl database somo la 11

huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database.

Katika somo lililotangulia tumejifunza amna a kupangilia taarifa za kwenye databse. Tuliona namna ya kutumia ORDER BY. Isha tukapanga data zetu kutoka kubwa kwenda ndogo na kinyume chake. Sasa katika somo hili tutatkwenda kuendelea na nnamna ya kupangilia data hizo ila kwa kutumia WHERE .

 

Kwa nini tunatumia where ?

Tunatumia WHERE endapo tuna masharti yanatakiwa yafikiwe ili data kuonekanna. Kwa mfano unataka kusoma menu zote ambazo gharama yake ni zaidi ya 1000. hapa hili tunaita ni sharti ama condition. Sasa ili sharti hili liweze kufanya kazi kwenye SQL tunatumia where.

 

1. Mfano wa kwanza

Tunahitaji kusoma data zote ambazo price yake ni sawa na  1000.

Kufanya hivyo tutatumia alama ya = mbele ya where. Hivyocommand nzima itaonekana.

SELECT * FROM `menu` WHERE price =1000 

hapo menu itakayoonekana ni ile tu ambayo proce yake ni sawa na 1000.

 

2. Mfano wa pili

Tunataka kusoma data ambazo id yake ni 3, 4, na 8. yaani data tu zenye id hizo ndizo tunataka kuziona na si nyinginezo. Hivyo tunatarajia kuwa na row tatu tu. Kufanya hivyo tutatumia OR kwa maana au. Yaani eidha id iwe 3 au id iwe 4 au id iwe 8. Na command yote itaonekana hivi

SELECT * FROM `menu` WHERE id =3 OR id =4 OR id =8;  pia unweza kuondoa nyota na kupunguza column

SELECT name, price FROM `menu` WHERE id =3 OR id =4 OR id =8;

 

3. Mafno wa tatu

Chukulia mfano kwenye menu kuna ugali mbili. Kuna ugali nyama abayo ni 1500 na kuna ugali ng’onda ambaypo ji 1000. sasa mimi nataka kusoma ile ambayo ni ugali nyama ya 1500. kumbuka zote ni ugali na kwenye menu zitanasomeka hivyo hivyo. Ili kuona ya ugali 1500 tu tunatakiwa tutumie AND yaani tuselect ugali lakini kwa ulazima kuwa na id yake iwe 1. ambapo kwenye menu yetu id 1 ni ugali hivyo itakuwa hivi:-

SELECT * FROM menu WHERE name = 'ugali' AND id =1

 

Kuna jambo hapa unatakiwa ulijuwe. Tunapotumia string (sting ni mkusanyiko wa herufi na namba, rejea mafunzo ya php) value inatakiwa ikae ndani ya alama za kufnga na funguwa semi ‘’ kama ulivyo kwenye mfano 'ugali'.

 

4. Tofauti ya AND na OR. 

Unapotumia AND maana yake ni lazima masharti yafikiwe ili data kuonekana. Ila unapotumia OR hata shart moja likifikiwa data zitaonekana. Kwa mfano kwenye mfano namba 2 hapo hata kama kusingekuwa na id 3 data zingeonekana lakini kama tungetumia AND endapo id tatu isingekuwepo kwenye database yetu data zote zisingesoma.

 

5. Mfano wa nne

Tunahitaji kusoma menu ambazo tu majina yake yameanziwa na herufi u. chukulia mfano kuna orodha ya majina ya vyakula 50 kwenye hoteli moja kubwa sana. Sasa nataku kuona vyakula vinavyoanziwa na herufi u tu, hapo nikiwa naamini nitaona bei ua ugali kwa haraka zaidi tofauti na kuanza kusoma kutoka kwanzo hadi mwisho.

 

Kufanya hivi tutatumia LIKE kisha tutaweka hiyo heru u kikifuatiwa na alama ya asilimia %.  na ikiwa unahitaji kufatuta menu iliyoishiwa na herufi u basi alama ya asilimia % utaiweka mwanzo mfano %u. mfano huu pia utaweza kuutumia kama unataka kusearch kitu kwenye database ambacho kinaanziwa na herufi fuani. Hivyo kulingana na mfano wetu command itakuwa hivi:-

SELECT * FROM menu WHERE name LIKE 'u%'

 

Tutajifunza zaidi somo hili tutakaposoma namna ya kutafuta kitu kwenye database. Hila unaweza kutumia mfano huu pia kutafuta kitu kama mpangilio hapo unavyouona. Mfano unataka kutafuta neno supu  utaweka ‘supu%’

 

6. Mfano wa tano

Kwa kutumia SQL pia unaweza tumia mathematical operation kama >, <, !=, == na nyinginezo. Hapa nitatumia < na >. kwa ufupi > humaanisha kubwa kuliko na < humaanisha ndogo kuliko. Hapa nitatuia mifano miwili tu ya > na < .

 

A. Tunahitaji kuona menu ambazo price zake ni kubwa kuliko 1000 hapa tutatumia > .hivyo menu itakayokuja ni ile tu ambayo price yake imezidi 1000. hivyo itakuwa hivi

SELECT *  FROM menu WHERE price >1000

 

B. Tunataka kuona menu ambazo price yake ni ndogo kuliko 900. hapa tutatumia <, hivyo menu tutakazoona ni zile tu ambazo price yake haijafika 900. hivyo itakuwa hivi:-

SELECT *FROM  menu WHERE price <900

 

Tukutane somo la 12 tutajifunza kanuni kadhaa za kihesabu kwa kutumia SQL. Tafadhali usikose somo la 12 kwani ndio somo letu la mwisho wa course hii ta mafunzo ya database kwa kutumia MySQl.

 

 

Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 1248

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

PHP level 1 somo la tano (5)
PHP level 1 somo la tano (5)

Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza (basic level)
Mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza (basic level)

Huu ni utangalizi wa mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza level ya kwanza kwa lugha ya kiswahili. Haapa utapata msingi wa kuweza kutengeneza tovuti na blog.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 1  (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 1)
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 1 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 1)

hili ni somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2 html full course for beginners. Katika somo hili tutaangalia utangulizi juu ya HTML na pia utajifunza faida za HTML.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 5
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 5

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1
Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1

Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 4 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 4 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 8  (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 8)
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 8 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 8)

Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners)

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL -  DATABASE somo la 6
Mafunzo ya database MySQL - DATABASE somo la 6

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 6. Katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza table kwa kutumia MySQL na kwa kutuma SQL.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 7 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 7 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hii ni project ya HTML ambayo imetengenezwa kulingana na mafunzo ya HTML level1. Tunatarajia project hii kuboreshwa kadiri mafunzo yanavyozidi kusonga mbele.

Soma Zaidi...