picha

Fahamu dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo,dawa maalum ambayo imo kwenye kundi hili la cardiac glycoside ni digoxin, ni dawa muhimu ambayo utumika kwenye mfumo wa vidonge mara nyingi.

fahamu kuhusu dawa ya digoxin katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

1. Kama tulivyoona hapo juu ya kwamba dawa hii imo kwenye kundi la cardiac glycoside, dawa hizi mara nyingi usaidia pale kama damu imeshindwa kusambaa kwenye sehemu mbalimbali za mwili, ina uwezo wa kupanua mishipa na kueza kuruhusu damu inaweza kupita bila shida yeyote.

 

2. Pia dawa hizi inawezekana juwa na maudhi mbalimbali wakati wa kutumia ikiwemo  kutapika , kichefuchefu, kuharisha hali hizi utokea kwa sababu ya kuwepo kwa sumu ya dawa hasa kwa watumiaji wa dawa kwa mda mrefu.

 

3. Pamoja ha maudhui hayo kuna kipindi wagonjwa au watumiaji uihisi kizunguzungu au pengine kutojielewa kwa kitaalamu huitwa hallusination, hasa hasa kwa wale watu wazima ambao umri umeenda.

 

4. Na kwa walio wachache wanapata shida ya maumivu ya tumbo au pengine choo kinaweza kuwa kigumu au kuharisha mara kwa mara,

 

5. Kwa hiyo tunapaswa kufahamu watu mbalimbali wanaweza kutumia dawa hizi ya cardiac glycoside ila wale walio na presha ya kushuka hawapaswi kabisa kutumia kwa sababu dawa hizi ushusha presha iliyo juu kwa hiyo kwa wenye pressure ya kushuka wakiitumia wanaweza kupata madhara makubwa au pengine presha inashuka kabisa na kusababisha vifo.

 

6. Kwa hiyo dawa hizi tunapaswa kuzitumia kwa kufuata utaratibu wa wataalamu wa afya kwa hiyo kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba magonjwa ya moyo utofautiana kwa hiyo na tiba Nayo ni tofauti, kwa sababu hiyo dawa hizi haitumiki kiholela bali kwa utaratibu wa wataalamu wa afya.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 1637

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 web hosting     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Dawa ya maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukuletea dawa ya maumivu ya jino

Soma Zaidi...
Fahamu antibiotics ya asili.

Post hii inahusu zaidi antibiotics ya asili, ni antibiotics inayotumia vitu vya kila siku na ya kawaida na mtu akaweza kupona kabisa na kufanya kazi kama antibiotics ya vidonge vya kawaida.

Soma Zaidi...
Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.

Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya fluconazole.

Post hii inahusu zaidi dawa ya fluconazole ni dawa ya kutibu fangasi za aina au za sehemu mbalimbali,

Soma Zaidi...
Vyakula vya kusaidia katika matibabu ya kiungulia

PoPosti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo unaweza kutumia iwapo umepata tatizo la kiungulia

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza magonjwa ya akili inayoitwa Chlorpromazine

Post hii inahusu zaidi dawa zinazosaidis katika kutuliza magonjwa ya akili, dawa hii kwa kitaamu huiitwa chlorpromazine ni dawa ambayo utumiwa na watu wenye tatizo la magonjwa ya akili na kwa kiasi kikubwa huwa sawa.

Soma Zaidi...