Kazi ya Dawa ya salbutamol


image


Posti hii inahusu dawa ya salbutamol na kazi yake ya kutibu ugonjwa wa Asthma, ni dawa mojawapo ambayo imetumia na watu wengi na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwa hiyo zifuatazo ni kazi ya Dawa hii ya salbutamol katika kutibu Asthma.


Kazi za Dawa ya sulbutamol.

1. Sulbutamol ni dawa ambayo usaida katika kutibu Asthma na matatizo yote yanayohusiana na mfumo wa hewa, ufanya kazi yake kwa kwa wagonjwa wenye matatizo ya kubanwa kifua na Asthma, ufanya kazi hiyo kwa kuifanya mishipa au misuli ya kwenye mfumo wa hewa kulainika na kufanya hewa kupita kwa urahisi, tukumbuke kwamba kama mgonjwa amebakwa na kifua misuli ya kwenye kifua mara nyingi huwa imebana na kumfanya mgonjwa kuumia na kupumua kwa shida kwa hiyo kwa kutumia sulbutamol misuli ya mgonjwa ulainika naye upumua kawaida.

 

2. Pia hii dawa uwezo kuwa kwenye mifumo mbalimbali , inaweza kuwa kwenye hali ya vidonge, au kwenye mfumo wa maji ambayo utumiwa sana na watoto, na pengine inaweza kutumiwa kwa kumpulizia mgonjwa kama anaumwa kupitia mdomoni au kwa maelezo zaidi wataalamu wa afya ndio wanaweza kukupatia utaratibu kadri ya hali halisi ya mgonjwa.

 

3. Dawa hii uweza kutumiwa ila si kwa watu wote hasa wale walio na Mzio au akeji na dawa hii hawapaswi kuitumia na mtu akitumia dawa hii hapaswi kutumia dawa yoyote ya maumivu hasa hasa Asprin. Na pia dawa hii inapaswa kutumiwa kwa uangalifu kwa watu wenye matatizo ya moyo na  presha kwa sababu dawa inaweza kupandisha presha juu na mapigo ya moyo yanaweza kwenda kwa mbio, kwa hiyo kabla ya kutumia dawa hii mgonjwa anapaswa kupima presha kwanza na mapigo ya moyo ili tusije kuleta matatizo mengine zaidi.

 

4.Tunapotumia dawa hii tunategemea kupata maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda kwa mbio, maumivu ya kichwa, kupata usingizi kwa shida na pengine presha kubwa juu hii ni kwa sababu ya mishipa ya damu ambayo imeingiliwa na dawa usababisha mishipa ya damu kupitisha damu kwa haraka zaidi, kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wakiona hayo yote wasishangae ni sehemu ya kawaida ya matokeo ya dawa.

 

5 . Kwa upande wa watoto wadogo wanapaswa kupewa 0.1mg kila baada ya maasaa manne na kwa watu wazima wafuate utaratibu wa daktari  na kwa wanawake wenye mimba inabidi wapewe kwa njia ya kuvuta tu kwa sababu njia nyingine zinapelekea kuwepo kwa matatizo ya moyo hasa kwa akina mama. Kwa hiyo dawa hii ni ya muhimu sana na imewasaidia watu wengi na tusitumie kiholela Bali tusikilize ushauri wa daktari na wataalamu wengine wa afya.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Dalili za ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani
Posti hii inaonyesha dalili,Sababu,na namna ya kujikinga na ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani ambao kitaalamu hujulikana Kama orchitis. Soma Zaidi...

image Huduma kwa wanawake wenye mahitaji maalum.
Posti hii inahusu huduma kwa wanawake wenye mahitaji maalum, ni wanawake ambao wana shida ya akili, walionyanyaswa kijinsia, wakimbizi na wote wenye matatizo mbalimbali. Soma Zaidi...

image Dalili za ugonjwa wa upele
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa upele, ni dalili au mwonekano wa mgonjwa wa upele. Soma Zaidi...

image Njia za uzazi wa mpango kwa akina Mama kuanzia miezi sita baada ya kujifungua mpaka mwaka mmoja
Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango kwa mama aliyejifungua kuanzia miezi sita mpaka mwaka mmoja. Soma Zaidi...

image Dalili za mimba inayotishi kutoka
Posti hii inahusu zaidi dalili za mimba inayotaka kutoka yenyewe, Kuna wakati mwingine mama anabeba mimba na mimba hiyo I atishia kutoka na huwa inaonyesha dalili mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni dalili za mimba kutaka kutoka yenyewe. Soma Zaidi...

image Madhara ya gonorrhea endapo haitotibiwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya gonorrhea endapo haitotibiwa Soma Zaidi...

image Ambao hawapaswi kupata chanjo
Posti hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kupewa chanjo, hawa ni wale ambao wana hali tofauti na ikitokea wakapata chanjo wanaweza kupata madhara badala ya kuwasaidia. Soma Zaidi...

image Imani potofu juu ya ugonjwa wa Ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi imani potofu juu ya ugonjwa wa Ukimwi,ni Imani walizonazo watu wengi kuhusiana na ugonjwa wa Ukimwi. Soma Zaidi...

image Namna ya kusaidia mwili kupambana na maradhi
Somo hili linakwenda kukuletea namna ambavyo mwili unapambana na maradhi Soma Zaidi...

image Faida za kula bamia
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Faida ambazo anaweza kupata mwanadamu Kama akila bamia Mara kwa mara. Bamia huliwa Kama tunda au Kama mboga pia na husaidia vitu vingi mwilini. Soma Zaidi...