Kazi ya Dawa ya salbutamol

Posti hii inahusu dawa ya salbutamol na kazi yake ya kutibu ugonjwa wa Asthma, ni dawa mojawapo ambayo imetumia na watu wengi na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwa hiyo zifuatazo ni kazi ya Dawa hii ya salbutamol katika kutibu Asthma.

Kazi za Dawa ya sulbutamol.

1. Sulbutamol ni dawa ambayo usaida katika kutibu Asthma na matatizo yote yanayohusiana na mfumo wa hewa, ufanya kazi yake kwa kwa wagonjwa wenye matatizo ya kubanwa kifua na Asthma, ufanya kazi hiyo kwa kuifanya mishipa au misuli ya kwenye mfumo wa hewa kulainika na kufanya hewa kupita kwa urahisi, tukumbuke kwamba kama mgonjwa amebakwa na kifua misuli ya kwenye kifua mara nyingi huwa imebana na kumfanya mgonjwa kuumia na kupumua kwa shida kwa hiyo kwa kutumia sulbutamol misuli ya mgonjwa ulainika naye upumua kawaida.

 

2. Pia hii dawa uwezo kuwa kwenye mifumo mbalimbali , inaweza kuwa kwenye hali ya vidonge, au kwenye mfumo wa maji ambayo utumiwa sana na watoto, na pengine inaweza kutumiwa kwa kumpulizia mgonjwa kama anaumwa kupitia mdomoni au kwa maelezo zaidi wataalamu wa afya ndio wanaweza kukupatia utaratibu kadri ya hali halisi ya mgonjwa.

 

3. Dawa hii uweza kutumiwa ila si kwa watu wote hasa wale walio na Mzio au akeji na dawa hii hawapaswi kuitumia na mtu akitumia dawa hii hapaswi kutumia dawa yoyote ya maumivu hasa hasa Asprin. Na pia dawa hii inapaswa kutumiwa kwa uangalifu kwa watu wenye matatizo ya moyo na  presha kwa sababu dawa inaweza kupandisha presha juu na mapigo ya moyo yanaweza kwenda kwa mbio, kwa hiyo kabla ya kutumia dawa hii mgonjwa anapaswa kupima presha kwanza na mapigo ya moyo ili tusije kuleta matatizo mengine zaidi.

 

4.Tunapotumia dawa hii tunategemea kupata maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda kwa mbio, maumivu ya kichwa, kupata usingizi kwa shida na pengine presha kubwa juu hii ni kwa sababu ya mishipa ya damu ambayo imeingiliwa na dawa usababisha mishipa ya damu kupitisha damu kwa haraka zaidi, kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wakiona hayo yote wasishangae ni sehemu ya kawaida ya matokeo ya dawa.

 

5 . Kwa upande wa watoto wadogo wanapaswa kupewa 0.1mg kila baada ya maasaa manne na kwa watu wazima wafuate utaratibu wa daktari  na kwa wanawake wenye mimba inabidi wapewe kwa njia ya kuvuta tu kwa sababu njia nyingine zinapelekea kuwepo kwa matatizo ya moyo hasa kwa akina mama. Kwa hiyo dawa hii ni ya muhimu sana na imewasaidia watu wengi na tusitumie kiholela Bali tusikilize ushauri wa daktari na wataalamu wengine wa afya.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 7629

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa

Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili.

Soma Zaidi...
Fahamu matumizi ya Ampicillin.

Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya kutibu kikohozi inayoitwa expectorant

Post hii inahusu zaidi dawa aina ya expectorant katika matibabu ya kikohozi,ni dawa ambayo usaidia au uzuia kikohozi kuendelea kutokea.

Soma Zaidi...
Fahamu antibiotics ya asili.

Post hii inahusu zaidi antibiotics ya asili, ni antibiotics inayotumia vitu vya kila siku na ya kawaida na mtu akaweza kupona kabisa na kufanya kazi kama antibiotics ya vidonge vya kawaida.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kisukari

Post hii inahusu zaidi dawa za kisukari, kwa sababu ya kuwepo kwa ugonjwa wa kisukari vilevile kuna dawa zake ambazo utumika kurekebisha sukari kama imepanda au kushuka.

Soma Zaidi...
Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo paracetamol.

Paracetamol kwa jina kingine hujulikana kama(acetaminophen) ni dawa ya kawaida ya kutuliza maumivu ambayo hutumiwa kupunguza aina mbalimbali za maumivu. Paracetamol ndilo jina linalojulikana zaidi katika kutuliza maumivu ya kawaida. Paracetamol inajulik

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya isoniazid katika kupambana na ugonjwa wa TB

Post hii inahusu zaidi dawa ya isoniazid katika mapambano na kifua kikuu, tunafahamu kabisa kwamba kifua kikuu ni hatari katika jamii kwa hiyo dawa ya isoniazid ni mkombozi katika mapambano na kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za kifua kikuu

Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya fluoroquinolones/quinolones

Post hii inahusu dawa ya kupambana na bakteria, hili kundi la fluoroquinolones lina dawa kuu mbili ambazo ni ciprofloxin na ofloxacin.

Soma Zaidi...