picha

Kazi ya Dawa ya salbutamol

Posti hii inahusu dawa ya salbutamol na kazi yake ya kutibu ugonjwa wa Asthma, ni dawa mojawapo ambayo imetumia na watu wengi na wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa, kwa hiyo zifuatazo ni kazi ya Dawa hii ya salbutamol katika kutibu Asthma.

Kazi za Dawa ya sulbutamol.

1. Sulbutamol ni dawa ambayo usaida katika kutibu Asthma na matatizo yote yanayohusiana na mfumo wa hewa, ufanya kazi yake kwa kwa wagonjwa wenye matatizo ya kubanwa kifua na Asthma, ufanya kazi hiyo kwa kuifanya mishipa au misuli ya kwenye mfumo wa hewa kulainika na kufanya hewa kupita kwa urahisi, tukumbuke kwamba kama mgonjwa amebakwa na kifua misuli ya kwenye kifua mara nyingi huwa imebana na kumfanya mgonjwa kuumia na kupumua kwa shida kwa hiyo kwa kutumia sulbutamol misuli ya mgonjwa ulainika naye upumua kawaida.

 

2. Pia hii dawa uwezo kuwa kwenye mifumo mbalimbali , inaweza kuwa kwenye hali ya vidonge, au kwenye mfumo wa maji ambayo utumiwa sana na watoto, na pengine inaweza kutumiwa kwa kumpulizia mgonjwa kama anaumwa kupitia mdomoni au kwa maelezo zaidi wataalamu wa afya ndio wanaweza kukupatia utaratibu kadri ya hali halisi ya mgonjwa.

 

3. Dawa hii uweza kutumiwa ila si kwa watu wote hasa wale walio na Mzio au akeji na dawa hii hawapaswi kuitumia na mtu akitumia dawa hii hapaswi kutumia dawa yoyote ya maumivu hasa hasa Asprin. Na pia dawa hii inapaswa kutumiwa kwa uangalifu kwa watu wenye matatizo ya moyo na  presha kwa sababu dawa inaweza kupandisha presha juu na mapigo ya moyo yanaweza kwenda kwa mbio, kwa hiyo kabla ya kutumia dawa hii mgonjwa anapaswa kupima presha kwanza na mapigo ya moyo ili tusije kuleta matatizo mengine zaidi.

 

4.Tunapotumia dawa hii tunategemea kupata maudhi madogo madogo kama vile mapigo ya moyo kwenda kwa mbio, maumivu ya kichwa, kupata usingizi kwa shida na pengine presha kubwa juu hii ni kwa sababu ya mishipa ya damu ambayo imeingiliwa na dawa usababisha mishipa ya damu kupitisha damu kwa haraka zaidi, kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wakiona hayo yote wasishangae ni sehemu ya kawaida ya matokeo ya dawa.

 

5 . Kwa upande wa watoto wadogo wanapaswa kupewa 0.1mg kila baada ya maasaa manne na kwa watu wazima wafuate utaratibu wa daktari  na kwa wanawake wenye mimba inabidi wapewe kwa njia ya kuvuta tu kwa sababu njia nyingine zinapelekea kuwepo kwa matatizo ya moyo hasa kwa akina mama. Kwa hiyo dawa hii ni ya muhimu sana na imewasaidia watu wengi na tusitumie kiholela Bali tusikilize ushauri wa daktari na wataalamu wengine wa afya.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 8157

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Nani anapaswa kutumia vidonge vya zamiconal.

Posti hii inahusu zaidi watu ambao wana uwezo wa kutumia vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya watu au makundi yanayoweza kutumia vidonge hivi.

Soma Zaidi...
Ushauri kabla ya kubeba mimba.

Posti hii inahusu zaidi ushauri kwa akina Mama na wachumba kabla ya kubeba mimba, kabisa ya kubeba mimba akina Mama na wachumba wanapaswa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji

Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi.

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya kupunguza maumivu

Post hii inahusu dawa ya aspirin katika kupunguza maumivu,ni dawa ambayo upunguz maumivu ya Kawaida, kushusha homa na pia usaidia kwenye magonjwa ya moyo hasa kuzuia stroke kama imetokea mda ndani ya masaa ishilini na manne

Soma Zaidi...
Vyakula vya kusaidia katika matibabu ya kiungulia

PoPosti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo unaweza kutumia iwapo umepata tatizo la kiungulia

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya kaoline

Post hii inahusu dawa ya kaoline katika kutibu au kuzuia kuharisha ni dawa ambayo imependekezwa kutumiwa hasa kwa wale walioshindwa kutumia dawa ya loperamide.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya ketoconazole.

Post hii inahusu zaidi dawa aina ya ketoconazole ni dawa inayotumika kutibu fangasi za kwenye koo.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ambazo uchangia kupungua kwa nguvu za kiume

Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali ambazo uchangia katika kupunguza nguvu za kiume , hii ni kwa sababu ya wataalamu mbalimbali wanavyosema

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza aleji au mzio

Post hii inahusu zaidi dawa hydrocortisone kwa kutuliza aleji au mzio, kwa kawaida Kuna mda mtu anapotumia dawa Fulani anakuwa na mabadiliko mbalimbali kama vile kifua kubana , viupele na mambo kama hayo.

Soma Zaidi...
Dawa za maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za maumivu ya jino

Soma Zaidi...