Madhara ya kutotoa huduma kwa Mama anayevuja damu baada ya kujifungua
Posti hii inahusu zaidi Madara ya kutomsaidia mama anayetokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.
Madhara ya kutokwa dama baada ya kujifungua.
1. Kwanza kabisa tunafahamu kwamba mwili wa binadamu umejengwa na damu, damu ikipungua madhara mengi yanaweza kutokea, pia kwa akina Mama wakiwa na mimba usababisha damu kupungua kwa sababu ya matumizi ya Mama na mtoto. Kwa hiyo wakati wa kujifungua Mama upoteza damu na damu ikipotea zaidi usababisha madhara makubwa kama vile,
2. Kuwepo kwa upungufu wa damu ambapo kwa kitaalamu huitwa Anemia.
Kwa hiyo ikitokea Mama akapoteza damu nyingi anaweza kupata upungufu wa damu mwilini ni vizuri kabisa hali hii ikitokea Mama anapaswa kuongezewa damu haraka Ili kuepuka tatizo hili la upungufu wa damu. Kwa hiyo wahudumu wa afya wanapaswa kufahamu hilo na kuacha uzembe ambao usababisha kupoteza damu.
3. Mama akipoteza damu anaweza kuzimia na kuishiwa madini mwilini.
Kwa kawaida tunajua madini mbalimbali yapo kwenye damu ambayo usambazwa kutoka sehemu mbalimbali za mwili na kuweza kuupatia mwili nguvu.kwa hiyo damu ilipungua usababisha nguvu kuisha mwilini hali inayoweza kusababisha mama kuzimia baada ya kupungukiwa kwa kiwango kikubwa cha damu.
4. Kifo kinaweza kutokea ikiwa Mama hajahudumiwa ipasavyo.
Kwa wakati mwingine kama Mama ana matatizo ya kutokwa na damu kwa mda mrefu bila msaada wowote, mama anaweza kufariki.
Kwa hiyo wauguzi na wahudumu wa afya wanapaswa kufahamu hilo na kuhakikisha kuwa Mama anapata dawa zote na huduma zote ili kuweza kuokoa maisha ya Mama na mtoto.
5. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa ikiwa Mama ataonyesha dalili yoyote ya kutokwa kwa damu anapaswa kuhudumiwa kwa nguvu zote ili kuokoa maisha yake na pia kwa wale wenye sababu zinazoeleweka wanapaswa kutibiwa mapema ipasavyo
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 web hosting 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Faida za uzazi wa mpango kwa watu wenye ugonjwa wa Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.
Soma Zaidi...Namna ya kutunza uke
Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza uke, tunajua wazi kuna magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo uke hautaweza kutunzwa vizuri na pia uke ukitunzwa vizuri kuna faida ya kuepuka maradhi ya wanawake kwa njia ya kutunza uke.
Soma Zaidi...Sababu za kutokea kwa saratani ya matiti
Saratani ya matiti ji moja kati ya saratani zinazosumbuwa wqnawake wengi. Katika somo hili utajifunza chanzo cha kutokea saratani ya matiti
Soma Zaidi...Maji ya Amniotic
Posti hii inahusu zaidi maji ya Amniotic ni maji ambayo uzunguka mtoto na kufanya kazi mbalimbali kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Mbinu za kupunguza Kichefuchefu
Point hii inahusu zaidi mbinu za kupunguza Kichefuchefu hasa kwa wagonjwa na watumiaji wa madawa mbalimbali yanayoweza kusababisha kichefuchefu.
Soma Zaidi...