picha

Fahamu dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.

Fahamu dawa ya Tetracycline katika kupambana na bakteria.

1 . Tetracycline ni mojawapo ya dawa ambazo usaidia katika matibabu ya kupambana na bakteria ni  muunganiko wa dawa tatu zikiwemo penicillin na streptomycin na zikiungana ndio zinaitwa tetracycline, muunganiko wa dawa hizi tatu huwa na sifa sawa na zinazofanana na mara nyingi utolewa kwa kumezwa mdomoni na pia uingia kwenye mmengenyo wa chakula na baadae kupitia kwenye mzunguko wa damu  hatimaye  kupambana na bakteria sehemu yoyote walipo.

 

2. Kwa upande mwingine aina ya dawa ya Tetracycline hydrochloride uweza kupitia kwenye mishipa ya damu na kufanya kazi kama zile ambazo hazijapitia kwenye mishipa ya damu, dawa hizi za tetracycline zikifika kwenye mwili na kukutana na bakteria zinazuia kutengenezwaa kwa protini ndani ya bakteria kitendo ambacho ufanya bakteria huyo kushindwa kuishi kwa sababu hawezi kuishi bila kuwepo kwa protein hiyo.

 

3. Kwa kawaida dawa hizi za tetracycline utibu magonjwa mbalimbali kama vile Chlamydia, kaswende na kisonono kwenye watu walio na aleji na penicillin kwa kawaida dawa ambayo imependekezwa kutibu kaswende na kisonono ni benzyl penicillin lakini Kuna watu wenye magonjwa haya kaswende na kisonono na Wana aleji na penicillin kwa hiyo dawa yao ni tetracycline ambayo na yenyewe utibu magonjwa hayo ya kaswende na kisonono,.

 

4. Dawa hii inaweza kutumiwa na watu mbalimbali ila haipaswi kutumiwa na wote wenye aleji na tetracycline , watoto chini ya miaka minane nao hawapaswi kutumia kwa sababu Ina tabia y kuharibu meno kwa sababu uingia hata kwenye fizi,wakiona mama wenye mimba changa hawapaswi kutumia dawa hii na kwa wale wanaonyonyesha hawaruhusiwi kutumia dawa hii mpaka waache kumnyonyesha hapo wanaweza kutumia dawa hii.

 

5. Pia Kuna wale wenye matatizo ya Figo, matatizo ya moyo na pia kwa wenye matatizo ya sukari yote ya kupanda na kushuka wanapaswa kutumia dawa hii ila wawe chini ya uangalizi ikiwa mtu Hana uangalizi asitumie dawa hii kwa sababu Ina tabia ya kuongeza tatizo au ikiwezekana watumie dawa za antibiotics nyingine tofauti na hizo.

 

6. Pia dawa hii uingiliana na dawa nyingine na kumaliza dawa nyingine  nguvu kwa mfano kwa wale wanaotumia uzazi wa mpango hasa ule wenye homoni au kichocheo cha estrogen, dawa hizi za tetracycline umaliza nguvu estrogen na mama anaweza kubeba mimba huku anatumia njia ya uzazi wa mpango kwa hiyo basi kwa watumiaji wa uzazi wa mpango ni vizuri kabisa kupata ushauri wa wataalamu wa afya kabla ya kutumia dawa hii Ili kuepukana na mimba zisizotarajiwa .

 

7. Pia kwa wale watumiaji wa madawa ya kupunguza asidi mwilini hasa we ye vidonda vya tumbo pia dawa hizi uingiliana sana na kalsium pamoja na magnesium na pia kwa watumiaji wa dawa za kuongeza madini ya chuma na wenyewe dawa hizi uingiliana na dawa za tetracycline kwa hiyo kabla ya kutumia dawa hii ya tetracycline ni vizuri kabisa kupata ushauri wa wataalamu wa afya Ili kuepuka madhara zaidi au kwa wakati mwingine unaweza kutumia dawa nyingine na unatumia tetracycline unakuwa unafanya kazi Bure.

 

8. Vile vile na dawa hizi za tetracycline huwa na maudhi madogo madogo kama vile kuongeza spidi ya majimaji yaliyo kwenye ubongo na kusababisha kizunguzungu na pengine kuona maruwe ruwe, kwa sababu dawa hii uweza kupitia kwenye mmengenyo wa chakula mgonjwa uweza kuhisi kichefuchefu na kutapika, maambukizi kwenye Koo na pia mgonjwa anaweza kuwa na miwasho pamoja na kujikuna pia kwa watumiaji wa mda mrefu wanaweza kuwa na matatizo katika kuona.

 

9. Haya ni baadhi ya maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea ikiwa maudhi haya yamepita kiasi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kuweza kutafuta tiba na kuepuka matatizo zaidi, pia dawa hizi zibatibu magonjwa mengi na kwa wakati mwingine zinapatikana kwenye maduka au famasi zetu ni vizuri, ila kwa sababu Zina maudhi mengi na zinaingiliana na dawa nyingi ambazo watu wanazozitumia mara kwa mara kwa mfano uzazi wa mpango na vidonda vya tumbo ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya kabla ya kutumia dawa hii.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/12/22/Thursday - 07:33:38 pm Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 5108

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 ai web app    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.

Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo.

Soma Zaidi...
Tiba mbadala ya fangasi wa uumeni

Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala ya fangasi wa uumeni

Soma Zaidi...
Samahani naomba kuhuliza je unaweza kutokwa na maji maji ambayoa ayana rangi Wala harufu Ni dalili gani kwa mimba ya mwezi mmoja

ukiwa na ujauzito unaweza kuona mabadiliko mengi katika mwili wako yakiwemo kutokwa na majimaji. je majimaji haya yana dalili gani kwenye ujauzito?

Soma Zaidi...
Mambo yanayodhihirisha afya ya nguvu za kiume

Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali yanayodhoofisha afya za wanaume, kwa wakati mwingine wanaume ukosa kujiamini kwa sababu ya mambo ambayo yanaadhiri afya za wanaume.

Soma Zaidi...
Sababu za Kukoma hedhi (perimenopause)

Kukoma hedhi hufafanuliwa kuwa hutokea miezi 12 baada ya kipindi chako cha mwisho cha hedhi na huashiria mwisho wa mizunguko ya hedhi. Kukoma hedhi kunaweza kutokea katika miaka ya 40 au 50. Kukoma hedhi ni mchakato wa asili wa kibaolojia. Ingawa pia in

Soma Zaidi...
Kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.

Post hii inahusu zaidi kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, hali hii utokea kwa watoto wadogo wakati wa kuzaliwa kwa sababu maalum kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
SABABU ZA KUKOSA HAMU YA TENDO LANDOA

Hii ni hali inayompata mtu kukosa hamu kabisa ya kushiriki kitendo chochote kinachohusiana na kufanya tendo landoa au bunyeto.

Soma Zaidi...
Madhara ya kiafya ya kupiga punyeto

Post hii inakwenda kukutania madhara ya kuoiga punyeto kwa afya yako.

Soma Zaidi...
Fahamu madhara ya Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID

Posti hii inazungumzia kuhusiana na mathara yanayosababisha Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke

Soma Zaidi...
Vipimo muhimu wakati wa ujauzito

Post hii inahusu zaidi vipimo muhimu wakati wa ujauzito ni vipimo ambavyo vinapaswa kupimwa na Mama ili kuangalia mambo mbalimbali katika damu au sehemu yoyote, pia vipimo hivi umsaidia sana Mama kujua afya yake.

Soma Zaidi...