Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.
1 . Tetracycline ni mojawapo ya dawa ambazo usaidia katika matibabu ya kupambana na bakteria ni muunganiko wa dawa tatu zikiwemo penicillin na streptomycin na zikiungana ndio zinaitwa tetracycline, muunganiko wa dawa hizi tatu huwa na sifa sawa na zinazofanana na mara nyingi utolewa kwa kumezwa mdomoni na pia uingia kwenye mmengenyo wa chakula na baadae kupitia kwenye mzunguko wa damu hatimaye kupambana na bakteria sehemu yoyote walipo.
2. Kwa upande mwingine aina ya dawa ya Tetracycline hydrochloride uweza kupitia kwenye mishipa ya damu na kufanya kazi kama zile ambazo hazijapitia kwenye mishipa ya damu, dawa hizi za tetracycline zikifika kwenye mwili na kukutana na bakteria zinazuia kutengenezwaa kwa protini ndani ya bakteria kitendo ambacho ufanya bakteria huyo kushindwa kuishi kwa sababu hawezi kuishi bila kuwepo kwa protein hiyo.
3. Kwa kawaida dawa hizi za tetracycline utibu magonjwa mbalimbali kama vile Chlamydia, kaswende na kisonono kwenye watu walio na aleji na penicillin kwa kawaida dawa ambayo imependekezwa kutibu kaswende na kisonono ni benzyl penicillin lakini Kuna watu wenye magonjwa haya kaswende na kisonono na Wana aleji na penicillin kwa hiyo dawa yao ni tetracycline ambayo na yenyewe utibu magonjwa hayo ya kaswende na kisonono,.
4. Dawa hii inaweza kutumiwa na watu mbalimbali ila haipaswi kutumiwa na wote wenye aleji na tetracycline , watoto chini ya miaka minane nao hawapaswi kutumia kwa sababu Ina tabia y kuharibu meno kwa sababu uingia hata kwenye fizi,wakiona mama wenye mimba changa hawapaswi kutumia dawa hii na kwa wale wanaonyonyesha hawaruhusiwi kutumia dawa hii mpaka waache kumnyonyesha hapo wanaweza kutumia dawa hii.
5. Pia Kuna wale wenye matatizo ya Figo, matatizo ya moyo na pia kwa wenye matatizo ya sukari yote ya kupanda na kushuka wanapaswa kutumia dawa hii ila wawe chini ya uangalizi ikiwa mtu Hana uangalizi asitumie dawa hii kwa sababu Ina tabia ya kuongeza tatizo au ikiwezekana watumie dawa za antibiotics nyingine tofauti na hizo.
6. Pia dawa hii uingiliana na dawa nyingine na kumaliza dawa nyingine nguvu kwa mfano kwa wale wanaotumia uzazi wa mpango hasa ule wenye homoni au kichocheo cha estrogen, dawa hizi za tetracycline umaliza nguvu estrogen na mama anaweza kubeba mimba huku anatumia njia ya uzazi wa mpango kwa hiyo basi kwa watumiaji wa uzazi wa mpango ni vizuri kabisa kupata ushauri wa wataalamu wa afya kabla ya kutumia dawa hii Ili kuepukana na mimba zisizotarajiwa .
7. Pia kwa wale watumiaji wa madawa ya kupunguza asidi mwilini hasa we ye vidonda vya tumbo pia dawa hizi uingiliana sana na kalsium pamoja na magnesium na pia kwa watumiaji wa dawa za kuongeza madini ya chuma na wenyewe dawa hizi uingiliana na dawa za tetracycline kwa hiyo kabla ya kutumia dawa hii ya tetracycline ni vizuri kabisa kupata ushauri wa wataalamu wa afya Ili kuepuka madhara zaidi au kwa wakati mwingine unaweza kutumia dawa nyingine na unatumia tetracycline unakuwa unafanya kazi Bure.
8. Vile vile na dawa hizi za tetracycline huwa na maudhi madogo madogo kama vile kuongeza spidi ya majimaji yaliyo kwenye ubongo na kusababisha kizunguzungu na pengine kuona maruwe ruwe, kwa sababu dawa hii uweza kupitia kwenye mmengenyo wa chakula mgonjwa uweza kuhisi kichefuchefu na kutapika, maambukizi kwenye Koo na pia mgonjwa anaweza kuwa na miwasho pamoja na kujikuna pia kwa watumiaji wa mda mrefu wanaweza kuwa na matatizo katika kuona.
9. Haya ni baadhi ya maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kutokea ikiwa maudhi haya yamepita kiasi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya Ili kuweza kutafuta tiba na kuepuka matatizo zaidi, pia dawa hizi zibatibu magonjwa mengi na kwa wakati mwingine zinapatikana kwenye maduka au famasi zetu ni vizuri, ila kwa sababu Zina maudhi mengi na zinaingiliana na dawa nyingi ambazo watu wanazozitumia mara kwa mara kwa mfano uzazi wa mpango na vidonda vya tumbo ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya kabla ya kutumia dawa hii.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya shida ya upumuaji, ni madhara madogo madogo ambayo utokea kwa watumiaji wa matatizo ya kupumua.
Soma Zaidi...Je kutokwa na maji ukeni ambayo hayana harufu na meupe Hadi kuroanisha chupi, na je kutokwa na maji mengi wakati wa tendo la ndoa inaashilia nini?
Soma Zaidi...Kondo la nyuma ni sehemu ya mwili wa mama anapokuwa mjamziti,kondo la nyuma husaidia katika kazi mbalimbali katika ukuaji wa mtoto.
Soma Zaidi...Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali?
Soma Zaidi...Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu.
Soma Zaidi...Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaumeΒ .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia ambazo tunaweza kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili la kutanuka kwa tezi dume, kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili kwenye jamii kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Maambukizi kwenye Njia ya Uzazi kwa kifupi hujulikana Kama PID.ni Maambukizi ya mfumo wa Uzazi yanayoathiri wanawake, Maambukizi haya kwa Kawaida huhusisha sehemu Kama shingo ya uzazi,nyuma ya mfuko wa Uzazi na mirija ya uzazi.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba katika mwezi was kwanza
Soma Zaidi...