picha

Sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa.

Sababu ya mifuko ya kizazi kushindwa kisinyaa.

1. Kwa kawaida Mama akimaliza kujifungua hatua inayofuata ni kutoa kondo la nyuma  na kutoa dawa ya oxytocin Ili kuweza kusaidia  kusinyaa kwa mfuko wa kizazi wanawake wengine  mfuko wa kizazi  hausinyai kwa sababu mbalimbali kama tutakavyoziona hapo chini na mfuko wa kizazi usiposinyaa usababisha kutokwa kwa damu nyingi na kusababisha upungufu wa damu kwa akina Mama au kama hakuna matibabu kifo kinaweza kutokea.

 

 

2. Sababu ya mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa usababishwa na uchungu kuwa wa mda mrefu na mtoto hatoki tumboni, hali hii usababisha mfuko wa kizazi kuendelea kutaanuka sana na kusababisha kutosinyaa baada ya Mama kujifungua. Kwa hiyo wakunga na wahudumu wengine ni vizuri kuona dalili za mapema Ili kuweza kunisaidia Mama pale uchungu unapotumia mda mrefu kuliko kawaida.

 

3.  Kushindwa kumhudumia Mama vizuri hasa pale anapojifungua na kumchoma dawa ya oxytocin Ili kusaidia uterus iweze kusinyaa.

Kwa wakati mwingine hii sindano usahaulika au kuchomwa vibaya hali inayosababisha mfuko wa uzazi kushindwa kisinyaa na kusababisha kuendelea kuwepo kwa damu baada ya kujifungua.kwa hiyo wauguzi na wahudumu wanapaswa kujiandaa mapema Ili kuweza kuwasaidia akina Mama waweze kujifungua salama bila kutokwa na damu nyingi.

 

 

4.  Kutanuka kwa uterus.

Kwa wakati mwingine Kuna tatizo la kutanuka kwa mfuko wa uzazi hasa hasa kwa wanawake wenye matumbo makubwa wako kwenye hatari ya kupata tatizo hili kwa sababu mfuko wa uzazi unakuwa umetanuka sana hali inayosababisha mfuko wa uzazi kujirudisha kistaarabu baada ya kujifungua na kusababisha kuvuja kwa damu nyingi.

 

5. Pia sababu nyingine ni kwa akina Mama wenye tatizo na kutokwa na damu uweza kujirudia rudia kila wakati wa kujifungua kwa hiyo Mama akipata mara ya kwanza , ya pili na pengine kwa mimba zake zote.

 

6. Pia Akina Mama wenye shinikizo la damu na protein kwenye mkojo ambapo kwa kitaalamu huitwa pe eclampsia na pia wanawake wenye kifafa nao wako kwenye hatari.

 

7. Kwa hiyo baada ya kujua sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kusinyaa ni vizuri kabisa kwa wahudumu wa afya kuweza kusaidia Ili akina Mama waweze kujifungua salama na kuepukana na vifo vya akina Mama wakati wa kujifungua.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2706

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

dalili za uchungu kwa mama mjamzito

Makala hii itakwenda kukufundisha baadhi ya dalili za uchungu kwa mama mjamzito.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kwa Mama mwenye mimba

Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa Mama mwenye mimba, ni kipindi ambacho Mama uhitahi uangalizi wa karibu zaidi.

Soma Zaidi...
Zifahamu fibroids (uvimbe kwenye via vya uzazi)

Posti hii inahusu zaidi fibroids au uvimbe kwenye via vya uzazi hasa hasa utokea kwenye tumbo la uzazi ambapo kwa kitaalamu huitwa uterusi, uvimbe huu ulitokea watu wengine huwa hawawezi kutambua Dalili zake mapema kwa hiyo leo tunapaswa kujua Dalili zake

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia mimba zisiharibike.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuzuia mimba zisiharibike, kwa sababu kila mama anayebeba mimba anategemea kupata mtoto kwa hiyo na sisi hamu yetu ni kuhakikisha kwamba mtoto anazaliwa kwa kuzuia mimba kuharibik

Soma Zaidi...
Maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.

Post hii inahusu zaidi kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, hali hii utokea kwa watoto wadogo wakati wa kuzaliwa kwa sababu maalum kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...