picha

Sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa.

Sababu ya mifuko ya kizazi kushindwa kisinyaa.

1. Kwa kawaida Mama akimaliza kujifungua hatua inayofuata ni kutoa kondo la nyuma  na kutoa dawa ya oxytocin Ili kuweza kusaidia  kusinyaa kwa mfuko wa kizazi wanawake wengine  mfuko wa kizazi  hausinyai kwa sababu mbalimbali kama tutakavyoziona hapo chini na mfuko wa kizazi usiposinyaa usababisha kutokwa kwa damu nyingi na kusababisha upungufu wa damu kwa akina Mama au kama hakuna matibabu kifo kinaweza kutokea.

 

 

2. Sababu ya mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa usababishwa na uchungu kuwa wa mda mrefu na mtoto hatoki tumboni, hali hii usababisha mfuko wa kizazi kuendelea kutaanuka sana na kusababisha kutosinyaa baada ya Mama kujifungua. Kwa hiyo wakunga na wahudumu wengine ni vizuri kuona dalili za mapema Ili kuweza kunisaidia Mama pale uchungu unapotumia mda mrefu kuliko kawaida.

 

3.  Kushindwa kumhudumia Mama vizuri hasa pale anapojifungua na kumchoma dawa ya oxytocin Ili kusaidia uterus iweze kusinyaa.

Kwa wakati mwingine hii sindano usahaulika au kuchomwa vibaya hali inayosababisha mfuko wa uzazi kushindwa kisinyaa na kusababisha kuendelea kuwepo kwa damu baada ya kujifungua.kwa hiyo wauguzi na wahudumu wanapaswa kujiandaa mapema Ili kuweza kuwasaidia akina Mama waweze kujifungua salama bila kutokwa na damu nyingi.

 

 

4.  Kutanuka kwa uterus.

Kwa wakati mwingine Kuna tatizo la kutanuka kwa mfuko wa uzazi hasa hasa kwa wanawake wenye matumbo makubwa wako kwenye hatari ya kupata tatizo hili kwa sababu mfuko wa uzazi unakuwa umetanuka sana hali inayosababisha mfuko wa uzazi kujirudisha kistaarabu baada ya kujifungua na kusababisha kuvuja kwa damu nyingi.

 

5. Pia sababu nyingine ni kwa akina Mama wenye tatizo na kutokwa na damu uweza kujirudia rudia kila wakati wa kujifungua kwa hiyo Mama akipata mara ya kwanza , ya pili na pengine kwa mimba zake zote.

 

6. Pia Akina Mama wenye shinikizo la damu na protein kwenye mkojo ambapo kwa kitaalamu huitwa pe eclampsia na pia wanawake wenye kifafa nao wako kwenye hatari.

 

7. Kwa hiyo baada ya kujua sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kusinyaa ni vizuri kabisa kwa wahudumu wa afya kuweza kusaidia Ili akina Mama waweze kujifungua salama na kuepukana na vifo vya akina Mama wakati wa kujifungua.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3033

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Dalili za mimba yenye uvimbe

Mimba ya tumbo - pia inajulikana kama hydatidiform mole - ni ugumu usiyo na kansa (benign) ambayo hutokea kwenye uterasi. Mimba ya molar huanza wakati yai linaporutubishwa, lakini badala ya mimba ya kawaida, yenye uwezo wa kutokea, plasenta hukua na kuwa

Soma Zaidi...
Je siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?

Swali langu ni hili doktaJe siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisukari wakati wa ujauzito.

Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito.

Soma Zaidi...
Mimba Changa Hukaa Wiki Ngapi?

Katika lugha ya kawaida, "mimba changa" inarejelea miezi mitatu ya kwanza ya ujauzito, inayojulikana kitaalamu kama trimester ya kwanza. Kipindi hiki ni muhimu sana kwa ukuaji wa viungo vya mtoto na mabadiliko ya mwili wa mama. Makala hii inaelezea muda huu unavyohesabiwa na kile kinachotokea ndani ya kipindi hicho.

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea uvimbe kwenye kizazi.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi,kwa kawaida tumesikia akina mama wengi wanalalamika kuhusu kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na wengine hawajui sababu zake kwa hiyo sababu zifuatazo ni za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Soma Zaidi...
Madhara ya fangasi ukeni.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya fangasi ukeni, madhara mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo mtu hakutibiwa fangasi mapema.

Soma Zaidi...