picha

Zijue sababu za kutobeba mimba

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinamfanya mama au dada kutobeba mimba. Kwa hiyo tutaziona hapo chini kama ifuatavyo.

Zijue sababu za kutobeba mimba kwa akina Mama au dada.

1. Kwanza kabisa kwa wakati huu Kuna changamoto kubwa ya akina dada au mama kushindwa kubeba mimba hii ni kwa sababu mbalimbali ambazo tutaweza kuziona hapo mbeleni sababu nyingine ni nje ya uwezo wa akina dada na sababu nyingine ni wenyewe wanaosababisha kwa kushindwa kutibu magonjwa mbalimbali, kutoa mimba mara Kwa mara na matumizi ya mda mrefu ya vidonge na sindano za kuzuia kubeba mimba.

 

2. Kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na uvimbe kwenye kizazi ambao usababishwa na vitu mbalimbali kwa hiyo hata kama mimba ikitungwa haitaweza kukua kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe mpaka uvimbe utolewe ndipo mama anaweza kubeba mimba.

 

3. Kuwepo kwa hormones imbalance.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na kiwango kidogo cha aina Moja ya homoni na homoni nyingine inakuwa kubwa hali ambayo usababisha mimba kushindwa kushika kwa Sababu Ili mimba itingwe kiwango chote cha homoni kinapaswa kuwa sawa.

 

4. Kuwepo kwa uvimbe kwenye mayai.

Kuna wakati mwingine uvimbe kwenye mayai usababisha mayai kushindwa kukua na kuweza kupevuka au pengine mayai yanakosa njia ya kupanda mpaka kwenye follapian tube kwa ajili ya kuchevushwa kwa hiyo ni vigumu sana kubeba mimba.

 

5. Kukosa Ute wa uzazi.

Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa Ute wa uzazi usababisha mayai kusafiri kutoka kwenye ovaries mpaka kwenye follapian tube, kama hakuna ute wa uzazi ni vigumu sana kubeba mimba.

 

6. Kizazi kushuka.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo tatizo la kizazi kushuka au kizazi kutokuwa kwenye hali yake hali ambayo usababisha kutokushika kwa mimba.

 

7. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kupata ushauri wa daktari kama Kuna tatizo lolote lile likijitokeza Ili kuweza kuhakikisha kila mama mwenye hamu ya kupata mtoto anampata.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3239

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 web hosting     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Mbinu za kupunguza Kichefuchefu

Point hii inahusu zaidi mbinu za kupunguza Kichefuchefu hasa kwa wagonjwa na watumiaji wa madawa mbalimbali yanayoweza kusababisha kichefuchefu.

Soma Zaidi...
Je matiti kujaa na chuchu kuuma inakua ni dalili za hedhi?

Kuunda na kujaa kwa matiti ni miongoni mwa dalili za ujauzito lakini pia ni dalili za kukaribia hedhi kwa baadhi ya wanawake. Posti hii itakwenda kufafanuabutofauti wa dalili hizi na kipi ni sahihibkatibya hedhi ama ujauzito.

Soma Zaidi...
Dalili za kasoro ya moyo ya kuzaliwa kwa watu wazima

Ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa nao (kasoro ya moyo ya kuzaliwa) ni hali isiyo ya kawaida katika muundo wa moyo wako unaozaliwa nao. utu uzima. Ingawa maendeleo ya kimatibabu yameboreshwa, watu wazima wengi walio na ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa wanaweza wasip

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujikinga na maradhi ya ini

Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kujiepusha na maradhi ya ini

Soma Zaidi...
Zijue Dalili za hatari kwa Mama mjamzito

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa Mama mjamzito, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama mjamzito, hizi Dalili zisipofanyiwa kazi mapema zinaweza kuleta shida kwa Mama kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua Dalili hizi na kuchukua hatua endapo zitajio

Soma Zaidi...
Sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.

Soma Zaidi...