Zijue sababu za kutobeba  mimba

Zijue sababu za kutobeba mimba

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinamfanya mama au dada kutobeba mimba. Kwa hiyo tutaziona hapo chini kama ifuatavyo.

Zijue sababu za kutobeba mimba kwa akina Mama au dada.

1. Kwanza kabisa kwa wakati huu Kuna changamoto kubwa ya akina dada au mama kushindwa kubeba mimba hii ni kwa sababu mbalimbali ambazo tutaweza kuziona hapo mbeleni sababu nyingine ni nje ya uwezo wa akina dada na sababu nyingine ni wenyewe wanaosababisha kwa kushindwa kutibu magonjwa mbalimbali, kutoa mimba mara Kwa mara na matumizi ya mda mrefu ya vidonge na sindano za kuzuia kubeba mimba.

 

2. Kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na uvimbe kwenye kizazi ambao usababishwa na vitu mbalimbali kwa hiyo hata kama mimba ikitungwa haitaweza kukua kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe mpaka uvimbe utolewe ndipo mama anaweza kubeba mimba.

 

3. Kuwepo kwa hormones imbalance.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo na kiwango kidogo cha aina Moja ya homoni na homoni nyingine inakuwa kubwa hali ambayo usababisha mimba kushindwa kushika kwa Sababu Ili mimba itingwe kiwango chote cha homoni kinapaswa kuwa sawa.

 

4. Kuwepo kwa uvimbe kwenye mayai.

Kuna wakati mwingine uvimbe kwenye mayai usababisha mayai kushindwa kukua na kuweza kupevuka au pengine mayai yanakosa njia ya kupanda mpaka kwenye follapian tube kwa ajili ya kuchevushwa kwa hiyo ni vigumu sana kubeba mimba.

 

5. Kukosa Ute wa uzazi.

Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa Ute wa uzazi usababisha mayai kusafiri kutoka kwenye ovaries mpaka kwenye follapian tube, kama hakuna ute wa uzazi ni vigumu sana kubeba mimba.

 

6. Kizazi kushuka.

Kuna wakati mwingine kunakuwepo tatizo la kizazi kushuka au kizazi kutokuwa kwenye hali yake hali ambayo usababisha kutokushika kwa mimba.

 

7. Kwa hiyo ni vizuri kabisa kupata ushauri wa daktari kama Kuna tatizo lolote lile likijitokeza Ili kuweza kuhakikisha kila mama mwenye hamu ya kupata mtoto anampata.

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1873

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Namna ya kumpima mtoto uzito
Namna ya kumpima mtoto uzito

Posti hii inahusu namna ya kumpima mtoto uzito, ni njia ambayo utumika kujua uzito wake na maendeleo ya mtoto.

Soma Zaidi...
Je kitunguu saumu kina madhara kwa Mgonjwa wa figo?
Je kitunguu saumu kina madhara kwa Mgonjwa wa figo?

Nimesoma makala yenu, sasa nina swaliJe kitunguu saumu kina madhara kwa Mgonjwa wa figo?

Soma Zaidi...
Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto
Dalili za Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo ujitokeza kama kuna Maambukizi yoyote kwenye kitovu cha mtoto mdogo, kwa kawaida kitovu cha mtoto kama kiko vizuri kinapona kwa mda mchache na kinakauka mapema iwezekanavyo bila kuwa na tatizo lolote ila kama kuna Dal

Soma Zaidi...
Wanaopasawa kutumia PEP
Wanaopasawa kutumia PEP

PEP Ni dawa ambazo utumiwa na watu wanaojamiiana na watu wenye virus vya ukimwi ila wenyewe hawawezi kupata kwa sababu ya kutumia dawa hizo.

Soma Zaidi...
Napenda kuuliza mke wangu anamuda wa wiki moja . tumbo na maziwa vinauma je dalili hizo zinawekuwa ni ujauzito...?
Napenda kuuliza mke wangu anamuda wa wiki moja . tumbo na maziwa vinauma je dalili hizo zinawekuwa ni ujauzito...?

Maumivu ya tumbo kwa mjamzito huweza kuanaa kuonekana mwanzoni kabisa mwaujauzito, ndani ya mwezi mmoja. Ikabidi si dalili pekee ya kuwa ni mjamzito.

Soma Zaidi...
Yajue madhara ya kutoa mimba mara Kwa mara
Yajue madhara ya kutoa mimba mara Kwa mara

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa wale wenye tabia ya kutoa mimba mara Kwa mara .

Soma Zaidi...
Hatua Saba za kutibu au kuepuka uvimbe kwenye kizazi
Hatua Saba za kutibu au kuepuka uvimbe kwenye kizazi

Posti hii inahusu zaidi hatua ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kutibu uvimbe au kwa kitaalamu huitwa fibroids. Hizi hatua zikitumika uweza kusaidia kupunguza kiwango cha kupata au kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Soma Zaidi...
Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.
Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Posti hii inaelezea kiufupi kabisa kuhusiana na Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Soma Zaidi...