Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)
- Kuamini Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w).
- Kuamini vitabu vya Allah (s.w) ni lazima kwa kila muumini wa kweli kama vilivyoainishwa katika Qur’an, ambavyo baadhi ni;
- Suhufi – aliyoteremshiwa Nabii Ibrahim (a.s) na Nabii Musa (a.s).
- Taurat – aliyoteremshiwa Nabii Musa (a.s)
- Zaburi – aliyoteremshiwa Nabii Daud (a.s)
- Injili – aliyoteremshiwa Nabii Isa (a.s) na
- Qur’an – aliyoteremshiwa Nabii au Mtume Muhammad (s.a.w).
- Vitabu hivi vimeteremshwa kwa lengo la kuwaongoza wanaadamu katika njia sahihi na iliyonyooka ya maisha yao ili kufikia lengo la kuumbwa kwao.
Rejea Qur’an (57:25) na (5:46).
- Sababu ya Vitabu Vilivyotangulia kutajwa ndani ya Qur’an:
- Qur’an ndiyo Kitabu cha mwisho kilichoteremshwa kwa ajili ya kuwaongoza walimwengu wote.
- Vimetajwa ili kuwafahamisha waislamu juu ya uwiano, usahihi na upotofu wa mafundisho hayo na yale ya Qur’an.
- Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha nafasi na utata wa vitabu hivyo kutumika zama hizi kama mwongozo wa maisha.
- Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha upungufu, mabadilisho na upotofu uliofanywa ndani ya Vitabu hivyo.
Rejea Qur’an (6:92), (2:75), (4:14), (5:15), (5:48) na (16:64).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Kitau cha Fiqh
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
(c)Vipawa vya Mwanaadamu
Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine.
Soma Zaidi...