Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)
- Kuamini Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w).
- Kuamini vitabu vya Allah (s.w) ni lazima kwa kila muumini wa kweli kama vilivyoainishwa katika Qur’an, ambavyo baadhi ni;
- Suhufi – aliyoteremshiwa Nabii Ibrahim (a.s) na Nabii Musa (a.s).
- Taurat – aliyoteremshiwa Nabii Musa (a.s)
- Zaburi – aliyoteremshiwa Nabii Daud (a.s)
- Injili – aliyoteremshiwa Nabii Isa (a.s) na
- Qur’an – aliyoteremshiwa Nabii au Mtume Muhammad (s.a.w).
- Vitabu hivi vimeteremshwa kwa lengo la kuwaongoza wanaadamu katika njia sahihi na iliyonyooka ya maisha yao ili kufikia lengo la kuumbwa kwao.
Rejea Qur’an (57:25) na (5:46).
- Sababu ya Vitabu Vilivyotangulia kutajwa ndani ya Qur’an:
- Qur’an ndiyo Kitabu cha mwisho kilichoteremshwa kwa ajili ya kuwaongoza walimwengu wote.
- Vimetajwa ili kuwafahamisha waislamu juu ya uwiano, usahihi na upotofu wa mafundisho hayo na yale ya Qur’an.
- Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha nafasi na utata wa vitabu hivyo kutumika zama hizi kama mwongozo wa maisha.
- Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha upungufu, mabadilisho na upotofu uliofanywa ndani ya Vitabu hivyo.
Rejea Qur’an (6:92), (2:75), (4:14), (5:15), (5:48) na (16:64).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 ai web app 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 ai web app 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu
Soma Zaidi...Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mtazamo wa uislamu juu ya Elimu, nini maana ya elimu na nani aliye elimika.
Ni nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika? Uislamu una mtazamo gani juu ya Elimu?
Soma Zaidi...Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah
Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe).
Soma Zaidi...