Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)
- Kuamini Vitabu vya Mwenyezi Mungu (s.w).
- Kuamini vitabu vya Allah (s.w) ni lazima kwa kila muumini wa kweli kama vilivyoainishwa katika Qur’an, ambavyo baadhi ni;
- Suhufi – aliyoteremshiwa Nabii Ibrahim (a.s) na Nabii Musa (a.s).
- Taurat – aliyoteremshiwa Nabii Musa (a.s)
- Zaburi – aliyoteremshiwa Nabii Daud (a.s)
- Injili – aliyoteremshiwa Nabii Isa (a.s) na
- Qur’an – aliyoteremshiwa Nabii au Mtume Muhammad (s.a.w).
- Vitabu hivi vimeteremshwa kwa lengo la kuwaongoza wanaadamu katika njia sahihi na iliyonyooka ya maisha yao ili kufikia lengo la kuumbwa kwao.
Rejea Qur’an (57:25) na (5:46).
- Sababu ya Vitabu Vilivyotangulia kutajwa ndani ya Qur’an:
- Qur’an ndiyo Kitabu cha mwisho kilichoteremshwa kwa ajili ya kuwaongoza walimwengu wote.
- Vimetajwa ili kuwafahamisha waislamu juu ya uwiano, usahihi na upotofu wa mafundisho hayo na yale ya Qur’an.
- Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha nafasi na utata wa vitabu hivyo kutumika zama hizi kama mwongozo wa maisha.
- Mwenyezi Mungu (s.w) kutaka kuonyesha upungufu, mabadilisho na upotofu uliofanywa ndani ya Vitabu hivyo.
Rejea Qur’an (6:92), (2:75), (4:14), (5:15), (5:48) na (16:64).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
π1 ai web app π2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π3 web hosting π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Kitau cha Fiqh π6 Madrasa kiganjani
π1 ai web app π2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π3 web hosting π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Kitau cha Fiqh π6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab
Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu.
Soma Zaidi...