Menu



Zijue Athari za kuweka vitu ukeni.

Posti hii inahusu zaidi athari za kuweka vitu ukeni, tunajua kwa wakati huu kadri ya kukua kwa sayansi na teknolojia watu wanaendelea kugundua mbinu mbalimbali ili waweze kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa.

Zijue Athari za kuweka vitu ukeni .

1.wanawake walio wengi wanaweka vitu ukeni kama vile  vipipi, mawe, vikokoto, sukari na madawa mengine mengi wakiwa na malengo tofauti wengine wanaweka vitu mbalimbali ili kuweza kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa na wengine wanaweka ili kuweza kuongeza uchungu wakati wa kujifungua, pamoja na hayo kuna madhara makubwa kama ifuatavyo.

 

2.Vitu hivyo uharibu kabisa hali ya uke kwa kupunguza pH ambayo iko kwenye uke kwa sababu pH ya kwenye uke ina kiwango chake ambacho ni kati ya 3.8 hadi 4.5 ukiweka vitu kama hivyo unaweza kuipunguza au kuiongeza kwa hiyo na kusababisha kuingia kwa wadudu kwa sababu kazi ya pH ni kuweka uke kwenye hali maalum ili kuweza kupambana na magonjwa mbalimbali kwa hiyo matumizi ya vitu hivyo uharibifu kabisa hali ya uke.

 

3. Matumizi ya vitu ukeni ni chanzo cha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali, kwa sababu vitu vingine vinatolewa kwenye mazingira ya uchafu na maandalizi ya vitu hivyo pengine ni ya kimila mno hali ambayo Usababisha kuwepo kwa Magonjwa kwenye sehemu ya uke, magonjwa mengine ni kama fungusi za ukeni, Maambukizi kwenye mlango wa kizazi, Maambukizi kwenye mfuko wa kizazi na pengine mtu anaweza kupata ugumba kwa sababu ya vitu hivyo na hata kansa mbalimbali zinaweza kujitokeza.

 

4. Madhara wakati wa kujifungua.

Kwa wakati mwingine wanawake wanaweka vitu hivyo na wanafikia wakati wa kujifungua bado vipo na kwa wengine wanadhubutu kuwaamini wale waliowaweka vitu hivyo ndo wawasaidie wakati wa kujifungua hali ambayo mtoto anakuja vibaya na unakuta maarifa wanayo kidogo hali hii Usababisha vifo kwa akina Mama na watoto wao kwa sababu ya matumizi ya vitu visivyoeleweka na kuweza kujiamini.

 

5. Kuchanika na kupasuka wakati wa kujifungua.

Kwa sababu ya matumizi ya vitu hivyo ukeni kuna vingine kweli vinaongeza uchungu, kwa hiyo kuna kipindi akina Mama wanakuwa na uchungu kabla ya mda kwa sababu ya matumizi ya vitu hivyo na wakija hospitalini wanasukuna mtoto kabla njia haijafunguka vizuri kwa sababu ya kuongeza uchungu kwa hiyo wanaposukuma wanapasuka na kutokwa na damu nyingi na kama alijifungulia kwenye sehemu ambayo haina vifaa vya kutosha wanaweza kupata matatizo na hata kupoteza maisha wao na watoto wao.

 

6.Kwa hiyo akina Mama vitu hivyo havina maana yoyote kabisa kwa wale wanaovitumia kwa lengo la kufanya tendo la ndoa lipendeze jua kuwa kuna hatari ya kupata magonjwa na pia kabla ya tendo la ndoa  mjiandae vizuri ili kuweza kufanya tendo la ndoa juwa tamu sio kutumia vitu hivi vya ajabu na kumbuka wewe Mama ukipata matatizo ni wewe kwa mwanaume ni kiasi kidogo kwa hiyo akina Mama jali afya zenu na maisha yenu ni ya muhimu sana.

 

7.Na kwa wale wanaotumia vitu hivi ili kuongeza uchungu na kujifungua mapema sio kweli kwa sababu uchungu ukija ukiwa hospitalini watakusaidia wakunga kwa sababu wenyewe wanajua mda gani utajifungua na kwa wakati kwa hiyo acha kuharakisha mambo acheni short cut kwa sababu kwa kutumia vitu hivi ni kuhatarisha maisha yako na mtoto wako.

 

8.Pia jamii inapaswa kutoa elimu kwa jamii kwa ajili ya kuepukana na mila na desturi ambazo zinahatarishwa maisha ya watu na wanawake wanapaswa kuhudhuria kliniki ili kuweza kupata maelekezo muhimu kwa sababu huko kila kitu kinafundishwa huko, asilimia kubwa ya wanawake wanaokwenda kliniki mda umeenda ndio wanafanya vitu vya hivyo kwa hiyo mama maisha ni ya kwako tunapaswa kuungana kwa pamoja ili kuokoa maisha ya Mama na mtoto.

 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 2987


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

Faida za uzazi wa mpango kwa watu wenye ugonjwa wa Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi. Soma Zaidi...

Dalili za kasoro ya moyo ya kuzaliwa kwa watu wazima
Ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa nao (kasoro ya moyo ya kuzaliwa) ni hali isiyo ya kawaida katika muundo wa moyo wako unaozaliwa nao. utu uzima. Ingawa maendeleo ya kimatibabu yameboreshwa, watu wazima wengi walio na ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa wanaweza wasip Soma Zaidi...

Mabadiliko ya uzito kwa mjamzito
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya uzito kwa mjamzito, hii ni hali ya kubadilika kwa uzito kwa Mama akiwa na Mimba Soma Zaidi...

Jinsi ya kushusha homoni za kiume.
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza homoni za kiume kwa akina dada. Soma Zaidi...

Nna mimba ya miez miezi mitano 5 naruhusiwa kula papai kwa wing
Miongoni mwa matunda yenye virutubisho vingi ni pamoja na papai, nanasi, tikiti, palachichi, pera, karoti, hindi na boga. Lakini katika matunda haya yapo ambayo kwa mimba changa anatakiwa awe makini, kama papai na nanasi. Sasa vipi kuhusu mimba ya Soma Zaidi...

Sababu za wajawazito kupata Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinafanya wajawazito kupata ugonjwa wa Bawasili, kwa sababu tatizo hili linawapa wakina mama wajawazito, kwa hiyo tutaona kwa nini wajawazito wanapatwa na tatizo hili sana. Soma Zaidi...

faida za tendo ka ndoa wakati wa ujauzito
Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba Soma Zaidi...

Dalili za upungufu wa homoni ya projestron
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone. Soma Zaidi...

Dalili za kifafa cha mimba.
Posti hii inahusu zaidi Dalili za Mama mwenye kifafa cha mimba, ili kifafa cha mimba kiweze kutokea lazima kuna dalili ambazo uweza kutokea kwa Mama kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Je, wajua sababu zinazopelekea maumivu ya Matiti kwa wanawake?
Maumivu ya matiti ni malalamiko ya kawaida miongoni mwa wanawake yanaweza kujumuisha uchungu wa matiti, maumivu makali ya kuungua au kubana kwenye tishu zako za matiti. Maumivu yanaweza kuwa ya mara kwa mara au yanaweza kutokea mara kwa mara tu. Maumiv Soma Zaidi...