Posti hii inahusu zaidi athari za kuweka vitu ukeni, tunajua kwa wakati huu kadri ya kukua kwa sayansi na teknolojia watu wanaendelea kugundua mbinu mbalimbali ili waweze kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Zijue Athari za kuweka vitu ukeni .
1.wanawake walio wengi wanaweka vitu ukeni kama vile vipipi, mawe, vikokoto, sukari na madawa mengine mengi wakiwa na malengo tofauti wengine wanaweka vitu mbalimbali ili kuweza kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa na wengine wanaweka ili kuweza kuongeza uchungu wakati wa kujifungua, pamoja na hayo kuna madhara makubwa kama ifuatavyo.
2.Vitu hivyo uharibu kabisa hali ya uke kwa kupunguza pH ambayo iko kwenye uke kwa sababu pH ya kwenye uke ina kiwango chake ambacho ni kati ya 3.8 hadi 4.5 ukiweka vitu kama hivyo unaweza kuipunguza au kuiongeza kwa hiyo na kusababisha kuingia kwa wadudu kwa sababu kazi ya pH ni kuweka uke kwenye hali maalum ili kuweza kupambana na magonjwa mbalimbali kwa hiyo matumizi ya vitu hivyo uharibifu kabisa hali ya uke.
3. Matumizi ya vitu ukeni ni chanzo cha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali, kwa sababu vitu vingine vinatolewa kwenye mazingira ya uchafu na maandalizi ya vitu hivyo pengine ni ya kimila mno hali ambayo Usababisha kuwepo kwa Magonjwa kwenye sehemu ya uke, magonjwa mengine ni kama fungusi za ukeni, Maambukizi kwenye mlango wa kizazi, Maambukizi kwenye mfuko wa kizazi na pengine mtu anaweza kupata ugumba kwa sababu ya vitu hivyo na hata kansa mbalimbali zinaweza kujitokeza.
4. Madhara wakati wa kujifungua.
Kwa wakati mwingine wanawake wanaweka vitu hivyo na wanafikia wakati wa kujifungua bado vipo na kwa wengine wanadhubutu kuwaamini wale waliowaweka vitu hivyo ndo wawasaidie wakati wa kujifungua hali ambayo mtoto anakuja vibaya na unakuta maarifa wanayo kidogo hali hii Usababisha vifo kwa akina Mama na watoto wao kwa sababu ya matumizi ya vitu visivyoeleweka na kuweza kujiamini.
5. Kuchanika na kupasuka wakati wa kujifungua.
Kwa sababu ya matumizi ya vitu hivyo ukeni kuna vingine kweli vinaongeza uchungu, kwa hiyo kuna kipindi akina Mama wanakuwa na uchungu kabla ya mda kwa sababu ya matumizi ya vitu hivyo na wakija hospitalini wanasukuna mtoto kabla njia haijafunguka vizuri kwa sababu ya kuongeza uchungu kwa hiyo wanaposukuma wanapasuka na kutokwa na damu nyingi na kama alijifungulia kwenye sehemu ambayo haina vifaa vya kutosha wanaweza kupata matatizo na hata kupoteza maisha wao na watoto wao.
6.Kwa hiyo akina Mama vitu hivyo havina maana yoyote kabisa kwa wale wanaovitumia kwa lengo la kufanya tendo la ndoa lipendeze jua kuwa kuna hatari ya kupata magonjwa na pia kabla ya tendo la ndoa mjiandae vizuri ili kuweza kufanya tendo la ndoa juwa tamu sio kutumia vitu hivi vya ajabu na kumbuka wewe Mama ukipata matatizo ni wewe kwa mwanaume ni kiasi kidogo kwa hiyo akina Mama jali afya zenu na maisha yenu ni ya muhimu sana.
7.Na kwa wale wanaotumia vitu hivi ili kuongeza uchungu na kujifungua mapema sio kweli kwa sababu uchungu ukija ukiwa hospitalini watakusaidia wakunga kwa sababu wenyewe wanajua mda gani utajifungua na kwa wakati kwa hiyo acha kuharakisha mambo acheni short cut kwa sababu kwa kutumia vitu hivi ni kuhatarisha maisha yako na mtoto wako.
8.Pia jamii inapaswa kutoa elimu kwa jamii kwa ajili ya kuepukana na mila na desturi ambazo zinahatarishwa maisha ya watu na wanawake wanapaswa kuhudhuria kliniki ili kuweza kupata maelekezo muhimu kwa sababu huko kila kitu kinafundishwa huko, asilimia kubwa ya wanawake wanaokwenda kliniki mda umeenda ndio wanafanya vitu vya hivyo kwa hiyo mama maisha ni ya kwako tunapaswa kuungana kwa pamoja ili kuokoa maisha ya Mama na mtoto.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.
Soma Zaidi...Tezidume ni moja ya magonjwa hayari yanayotokea katika mwili wa mwanaume.Hapa nimekuandalia sababu za kutokea kwa tezi dume.
Soma Zaidi...Dalili za mimba pekee haziwezi kuthibitisha uwepo wa mimba. Bila vipimo kwa. Muda sahihi huwezi kuwa. Na uhakika. Je na wewe unasumbuliwa na dalili za mimba na ukapona hakuna mimba? Makala hii ni kwa ajili yako. Swali
Soma Zaidi...Post hii itakujulidha mambo ambayo hupunguza nguvu za kiume
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n
Soma Zaidi...Kupata ujauzito hufungamana na mambo mengi ikiwepo afya vya wawili yaani me na mume na mengineyo. Unaweza kushiriki sikuvhatari na usiupate mimba. Postivhii ibakwendavkukufahamisha undani wa jambo hili.
Soma Zaidi...Kuna watoto wengine huanza kucheza mapema kuliko watoto wengine. Tunapozungumzia kucheza kwa mtoto aliye tumboni yaani mimba hapa inatubidi tuangalie kwa undani zaidi, je ni muda gani mtoto ataanza kucheza?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi magonjwa madogo madogo kwa akina Mama wajawazito, ni magonjwa ambayo hayawezi kupelekea kupoteza maisha kwa Mama mjamzito, magonjwa haya upotea ikiwa Mama atajifungua.
Soma Zaidi...