Zijue Athari za kuweka vitu ukeni.

Posti hii inahusu zaidi athari za kuweka vitu ukeni, tunajua kwa wakati huu kadri ya kukua kwa sayansi na teknolojia watu wanaendelea kugundua mbinu mbalimbali ili waweze kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa.

Zijue Athari za kuweka vitu ukeni .

1.wanawake walio wengi wanaweka vitu ukeni kama vile  vipipi, mawe, vikokoto, sukari na madawa mengine mengi wakiwa na malengo tofauti wengine wanaweka vitu mbalimbali ili kuweza kuwafurahisha wapenzi wao wakati wa kufanya tendo la ndoa na wengine wanaweka ili kuweza kuongeza uchungu wakati wa kujifungua, pamoja na hayo kuna madhara makubwa kama ifuatavyo.

 

2.Vitu hivyo uharibu kabisa hali ya uke kwa kupunguza pH ambayo iko kwenye uke kwa sababu pH ya kwenye uke ina kiwango chake ambacho ni kati ya 3.8 hadi 4.5 ukiweka vitu kama hivyo unaweza kuipunguza au kuiongeza kwa hiyo na kusababisha kuingia kwa wadudu kwa sababu kazi ya pH ni kuweka uke kwenye hali maalum ili kuweza kupambana na magonjwa mbalimbali kwa hiyo matumizi ya vitu hivyo uharibifu kabisa hali ya uke.

 

3. Matumizi ya vitu ukeni ni chanzo cha kuwepo kwa magonjwa mbalimbali, kwa sababu vitu vingine vinatolewa kwenye mazingira ya uchafu na maandalizi ya vitu hivyo pengine ni ya kimila mno hali ambayo Usababisha kuwepo kwa Magonjwa kwenye sehemu ya uke, magonjwa mengine ni kama fungusi za ukeni, Maambukizi kwenye mlango wa kizazi, Maambukizi kwenye mfuko wa kizazi na pengine mtu anaweza kupata ugumba kwa sababu ya vitu hivyo na hata kansa mbalimbali zinaweza kujitokeza.

 

4. Madhara wakati wa kujifungua.

Kwa wakati mwingine wanawake wanaweka vitu hivyo na wanafikia wakati wa kujifungua bado vipo na kwa wengine wanadhubutu kuwaamini wale waliowaweka vitu hivyo ndo wawasaidie wakati wa kujifungua hali ambayo mtoto anakuja vibaya na unakuta maarifa wanayo kidogo hali hii Usababisha vifo kwa akina Mama na watoto wao kwa sababu ya matumizi ya vitu visivyoeleweka na kuweza kujiamini.

 

5. Kuchanika na kupasuka wakati wa kujifungua.

Kwa sababu ya matumizi ya vitu hivyo ukeni kuna vingine kweli vinaongeza uchungu, kwa hiyo kuna kipindi akina Mama wanakuwa na uchungu kabla ya mda kwa sababu ya matumizi ya vitu hivyo na wakija hospitalini wanasukuna mtoto kabla njia haijafunguka vizuri kwa sababu ya kuongeza uchungu kwa hiyo wanaposukuma wanapasuka na kutokwa na damu nyingi na kama alijifungulia kwenye sehemu ambayo haina vifaa vya kutosha wanaweza kupata matatizo na hata kupoteza maisha wao na watoto wao.

 

6.Kwa hiyo akina Mama vitu hivyo havina maana yoyote kabisa kwa wale wanaovitumia kwa lengo la kufanya tendo la ndoa lipendeze jua kuwa kuna hatari ya kupata magonjwa na pia kabla ya tendo la ndoa  mjiandae vizuri ili kuweza kufanya tendo la ndoa juwa tamu sio kutumia vitu hivi vya ajabu na kumbuka wewe Mama ukipata matatizo ni wewe kwa mwanaume ni kiasi kidogo kwa hiyo akina Mama jali afya zenu na maisha yenu ni ya muhimu sana.

 

7.Na kwa wale wanaotumia vitu hivi ili kuongeza uchungu na kujifungua mapema sio kweli kwa sababu uchungu ukija ukiwa hospitalini watakusaidia wakunga kwa sababu wenyewe wanajua mda gani utajifungua na kwa wakati kwa hiyo acha kuharakisha mambo acheni short cut kwa sababu kwa kutumia vitu hivi ni kuhatarisha maisha yako na mtoto wako.

 

8.Pia jamii inapaswa kutoa elimu kwa jamii kwa ajili ya kuepukana na mila na desturi ambazo zinahatarishwa maisha ya watu na wanawake wanapaswa kuhudhuria kliniki ili kuweza kupata maelekezo muhimu kwa sababu huko kila kitu kinafundishwa huko, asilimia kubwa ya wanawake wanaokwenda kliniki mda umeenda ndio wanafanya vitu vya hivyo kwa hiyo mama maisha ni ya kwako tunapaswa kuungana kwa pamoja ili kuokoa maisha ya Mama na mtoto.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 3147

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa

Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu wakati wa tendo la ndoa

Kama unapata maumivu wakati wa tendo la ndoa, suluhisho lako lipo kwenye makala hii

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha uume kutoa maji meupe bila muwasho,na tiba yake ni ipi

Je unasumbuliwa na Majimaji kwenye uume. Je unapata miwasho, ama maumivu wakati wakukojoa.

Soma Zaidi...
Niharisha siku ya pili baada ya tendo. Jana hadi leo sijapata choo inawezakua nimeshika ujauzito?

Hivi unadhani kuharisha ni katika dalili za mimba, vipi kuhusu kutopata choo pia inaweza kuwa ni ujauzito?

Soma Zaidi...
Kujaa gesi tumboni

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kujaa tmgesi tumbon

Soma Zaidi...
Ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango.

Posti hii inahusu zaidi ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango, sio kwa imani potofu ambazo Watu utumia kuelezea uzazi wa mpango.

Soma Zaidi...
Chanzo cha tezidume, dalili zake na tiba zake.

Post hii inakwenda kukufunza mambo mengi kuhusu tezi dume kama chanzo, dalili, matibabu, njia za kujikinga na mambo hatari yanayoweza kukusababishia kupata tezi dume.

Soma Zaidi...
Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni

Soma Zaidi...
Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa

Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoabkunaweza kuashiria kuwa kuna majeraha yametokea huwenda ni michubuko ilitokea ndio ikavujisha damu. Lakini kwa nini hali kama hii itokee. Posti hii itakwwnda mujibu swali hili.

Soma Zaidi...
Dr nahis kuchanganyikiwa nimetoka niliingia hedhi tar 18 mwezi wa9 lakini saivi Jana tena nmeingia dr hii imekaaje mimi?

Kamaumeshawahi kujiuliza kuhusu kutokwaba damu tofautivna siku za hedhi, base mwaka hii ni kwaajiki yako.

Soma Zaidi...