Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.
Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama.
1.Kwanza kabisa tunapaswa kupima mapigo ya moyo ya mama, kupima urefu wa Mama, kupima joto la mwili Mama, msukumo wa damu wa Mama na upumuaji wa Mama kwa kufanya hivyo tunaweza kujua kabisa maendeleo ya mtoto kama vipimo vyote viko sawa kwa Mama na kwa mtoto patakuwa hakuna shida ila kama vipimo vya mama haviko sawa na kwa mtoto huenda pakawepo na shida kwa hiyo hatua za kutibu ufuata au Mama uenda kwa daktari kwa uchunguzi zaidi.
2. Pamoja na hayo Mama anapaswa kuangaliwa kama ana damu ya kutosha kwa kuangalia macho, viganja na kama kuna dalili yoyote ya kutokuwepo kwa damu Mama anapaswa kwenda kupima kiwango cha damu na kama ni kidogo ataweza kupewa dawa na kama ni chini ya tano atapaswa kuongezewa damu.
3. Kuangalia matiti ya Mama kama kuna aina yoyote ya uvimbe na kuangalia kama matiti yana Dalili za kuwepo kwa maji maji ambayo ni ishara ya kuwepo kwa maziwa baada ya kujifungua, kama kuna dalili za uvimbe Mama anapaswa kuangaliwa kw karibu zaidi.
4.Na pia tunapaswa kuangalia kama Upumuaji wa kwenye tumbo kama ni sawa na kwenye kifua kama ni sawa hiyo ni Dalili nzuri, na pia kuangalia kama tumbo lina makovu au kama Mama amewahi kufanyiwa upasuaji au kama kuna mstari kutoka kwenye kitovu kwenda chini ambayo ni Dalili nzuri za kuwepo kwa mimba.
5.Baada ya kuangalia hayo tunapaswa kushika shika tumbo na kuangalia jinsi mtoto alivyolala kama ametanguliza kichwa au matako, kama amelala ki upande au kama kuna mapacha , Mama anapaswa kuambiwa ulalo wa mtoto ili aweze kujiandaa vizuri wakati wa kujifungua.na kama mtoto amelala vibaya Mama anasisitizwa kuzalia hospitalini ili kuepuka madhara mengine.
6.Na pia tunapaswa kujua kama mtoto anapumua kwa kusikiliza mapigo ya mtoto kwa dakika moja na kumuuliza Mama kama mtoto anacheza kama hachezi mama anapaswa kwenda kumwona daktari mara moja ili kuangalia tatizo ni nini
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Tendo la ndoa wakati wa siku za hedhi ni halia mbayo jamii nying zinakataza. Katika vitabu vya dini pia haviruhusu, hata ki saikolojia utaona kuwa sio jambo jema. Hata hivyo hapa ninakuletea madhara yake kiafya
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba imetoka moja kwa moja, aina hiyo ya mimba kwa kitaalamu huitwa complete abortion.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga shahawa nje, hii ni njia mojawapo kati ya njia za uzazi wa mpango ambapo mwanaume humwaga nje mbegu ili asimpatie Mama mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi changamoto za kwenye ndoa kwa wale waliotoa mimba mara Kwa mara,hizi ni changamoto za wakati wa kufanya tendo na mme wake au mtu mwingine kwa ajili ya kupata mtoto.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo tunaweza kuzitumia ili kuwakinga watoto dhidi ya saratani, kama tulivyotangulia kusema kwamba saratani ya watoto mara nyingi Usababishwa na akina Mama hasa kwa sababu ya mtindo wa maisha wakati wa ujauzito kwa hiyo tun
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto.
Soma Zaidi...Inashangaza sana, wakati wengine wanahangaika kutafutavijauzito kwa gharama yoyote ile, kuna wengine wanataka kutoa ujauzito kwa gharama yeyote ile. Unadhani njia za kienyeji sa kutoa mimba ni salama?
Soma Zaidi...