Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa Mama

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.

Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kupima mapigo ya moyo ya mama, kupima urefu wa Mama, kupima joto la mwili Mama, msukumo wa damu wa Mama na upumuaji wa Mama kwa kufanya hivyo tunaweza kujua kabisa maendeleo ya mtoto kama vipimo vyote viko sawa kwa Mama na kwa mtoto patakuwa hakuna shida ila kama vipimo vya mama haviko sawa na kwa mtoto huenda pakawepo na shida kwa hiyo hatua za kutibu ufuata au Mama uenda kwa daktari kwa uchunguzi zaidi.

 

2. Pamoja na hayo Mama anapaswa kuangaliwa kama ana damu ya kutosha kwa kuangalia macho, viganja na kama kuna dalili yoyote ya kutokuwepo kwa damu Mama anapaswa kwenda kupima kiwango cha damu na kama ni kidogo ataweza kupewa dawa na kama ni chini ya tano atapaswa kuongezewa damu.

 

3. Kuangalia matiti ya Mama kama kuna aina yoyote ya uvimbe na kuangalia kama matiti yana Dalili za kuwepo kwa maji maji ambayo ni ishara ya kuwepo kwa maziwa baada ya kujifungua, kama kuna dalili za uvimbe  Mama anapaswa kuangaliwa kw karibu zaidi.

 

4.Na pia tunapaswa kuangalia kama Upumuaji wa kwenye tumbo kama ni sawa na kwenye kifua kama ni sawa hiyo ni Dalili nzuri, na pia kuangalia kama tumbo lina makovu au kama Mama amewahi kufanyiwa upasuaji au kama kuna mstari kutoka kwenye kitovu kwenda chini ambayo ni Dalili nzuri za kuwepo kwa mimba.

 

5.Baada ya kuangalia hayo tunapaswa kushika shika tumbo na kuangalia jinsi mtoto alivyolala kama ametanguliza kichwa au matako, kama amelala ki upande au kama kuna mapacha , Mama anapaswa kuambiwa ulalo wa mtoto ili aweze kujiandaa vizuri wakati wa kujifungua.na kama mtoto amelala vibaya Mama anasisitizwa kuzalia hospitalini ili kuepuka madhara mengine.

 

6.Na pia tunapaswa kujua kama mtoto anapumua kwa kusikiliza mapigo ya mtoto kwa dakika moja na kumuuliza Mama kama mtoto anacheza kama hachezi mama anapaswa kwenda kumwona daktari mara moja ili kuangalia tatizo ni nini 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2091

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama.

Posti huu inahusu zaidi malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama, ni huduma muhimu ambazo zimetolewa kwa akina Mama ili kuweza kuepuka hatari mbalimbali zinazowakumba akina Mama wakati wa ujauzito, kujifu na malezi ya watoto chini ya miaka mitano.

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea uvimbe kwenye kizazi.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi,kwa kawaida tumesikia akina mama wengi wanalalamika kuhusu kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na wengine hawajui sababu zake kwa hiyo sababu zifuatazo ni za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Soma Zaidi...
Uchafu unaotoka ukeni na rangi zake.

Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.

Soma Zaidi...
Dalili za kuvimba kwa ovari.

  Posti hii inazungumzia kuhusiana na kuvimba kwa ovari kunakosababishwa na maambukizo ya bakteria na kawaida huweza kusababishwa na magonjwa sugu katika Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke.

Soma Zaidi...
Njia za kugundua kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa

Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.

Soma Zaidi...
Hatua za ukuwaji was mimba na dalili zake

Somo hili linakwenda kukuletea hatua za ukuaji mimba na dalili zake

Soma Zaidi...
DARASA LLA AFYA na afya ya uzazi na malezi bora kwa jamii

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Jinsi ya kushusha homoni za kiume.

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza homoni za kiume kwa akina dada.

Soma Zaidi...
Aina za uvimbe kwenye kizazi.

Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za uvimbe kwenye kizazi, uvimbe unatokea kwenye kizazi ila utofautiana kulingana na sehemu ambazo uvimbe huo umepata.

Soma Zaidi...
Kondomu za kike

Posti hii inaonyesha Faida na hasara za Kondomu za kike

Soma Zaidi...