Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa Mama

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.

Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kupima mapigo ya moyo ya mama, kupima urefu wa Mama, kupima joto la mwili Mama, msukumo wa damu wa Mama na upumuaji wa Mama kwa kufanya hivyo tunaweza kujua kabisa maendeleo ya mtoto kama vipimo vyote viko sawa kwa Mama na kwa mtoto patakuwa hakuna shida ila kama vipimo vya mama haviko sawa na kwa mtoto huenda pakawepo na shida kwa hiyo hatua za kutibu ufuata au Mama uenda kwa daktari kwa uchunguzi zaidi.

 

2. Pamoja na hayo Mama anapaswa kuangaliwa kama ana damu ya kutosha kwa kuangalia macho, viganja na kama kuna dalili yoyote ya kutokuwepo kwa damu Mama anapaswa kwenda kupima kiwango cha damu na kama ni kidogo ataweza kupewa dawa na kama ni chini ya tano atapaswa kuongezewa damu.

 

3. Kuangalia matiti ya Mama kama kuna aina yoyote ya uvimbe na kuangalia kama matiti yana Dalili za kuwepo kwa maji maji ambayo ni ishara ya kuwepo kwa maziwa baada ya kujifungua, kama kuna dalili za uvimbe  Mama anapaswa kuangaliwa kw karibu zaidi.

 

4.Na pia tunapaswa kuangalia kama Upumuaji wa kwenye tumbo kama ni sawa na kwenye kifua kama ni sawa hiyo ni Dalili nzuri, na pia kuangalia kama tumbo lina makovu au kama Mama amewahi kufanyiwa upasuaji au kama kuna mstari kutoka kwenye kitovu kwenda chini ambayo ni Dalili nzuri za kuwepo kwa mimba.

 

5.Baada ya kuangalia hayo tunapaswa kushika shika tumbo na kuangalia jinsi mtoto alivyolala kama ametanguliza kichwa au matako, kama amelala ki upande au kama kuna mapacha , Mama anapaswa kuambiwa ulalo wa mtoto ili aweze kujiandaa vizuri wakati wa kujifungua.na kama mtoto amelala vibaya Mama anasisitizwa kuzalia hospitalini ili kuepuka madhara mengine.

 

6.Na pia tunapaswa kujua kama mtoto anapumua kwa kusikiliza mapigo ya mtoto kwa dakika moja na kumuuliza Mama kama mtoto anacheza kama hachezi mama anapaswa kwenda kumwona daktari mara moja ili kuangalia tatizo ni nini 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1973

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dalili na sababu za Kukosa hedhi

Post hii inaongelea kuhusiana na Kukosa hedhi ambapo kitaalamu hujulikana Kama Amenorrhea ni kutokuwepo kwa hedhi - hedhi moja au zaidi ya kukosa. Wanawake ambao wamekosa angalau hedhi tatu mfululizo wana amenorrhea, kama vile wasichana ambao hawajaanz

Soma Zaidi...
Haya maji meupe hutokea wakat mimba ishatungwa au ukifanya tendo la ndoa lazima utokee?

Majimaji yanayitoka kwenye uke yanafungamana na taarifa nyingi kuhusu afya vya mwanamke. Ujauzito, maradhi, mabadiliko ya homoni na zaidi.

Soma Zaidi...
Dalili za kuvimba kwa ovari.

  Posti hii inazungumzia kuhusiana na kuvimba kwa ovari kunakosababishwa na maambukizo ya bakteria na kawaida huweza kusababishwa na magonjwa sugu katika Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke.

Soma Zaidi...
Magonjwa ya kwenye ovari na Dalili zake.

Post hii inahusu zaidi Magonjwa yanayoshambulia sana ovari na Dalili zake, haya ni magonjwa ambayo yanashambulia sana ovari ni kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Njia za kugundua kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa

Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka.

Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.

Soma Zaidi...
Mimba huonekana katka mkojo baada ya muda gan tangu itungwe

Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.

Soma Zaidi...
Niharisha siku ya pili baada ya tendo. Jana hadi leo sijapata choo inawezakua nimeshika ujauzito?

Hivi unadhani kuharisha ni katika dalili za mimba, vipi kuhusu kutopata choo pia inaweza kuwa ni ujauzito?

Soma Zaidi...
Tatizo la muingiliano wa majimaji ya Amniotic au seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito.

posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtot

Soma Zaidi...
Changamoto za ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu changamoto za ujauzito na dalili zake endelevu

Soma Zaidi...