Nguzo za uislamu


image


Katika kipengele hiki tutajifunza nguzo za uislamu.aina tano za nguzo za uislamu,dhana ya nguzo za uislamu,lengo na umuhimu wa nguzo za uislamu


6.NGUZO ZA UISLAMU.

6.1.Dhana ya Nguzo za Uislamu.

  • Nguzo za Uislamu ni tano.

Rejea Hadith ifuatayo:

Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:

“Uislamu umejengwa juu ya nguzo tano; Kushuhudia kuwa hapana Mola ila Allah na kushuhudia kuwa Muhammad ni Mtume wa Allah, Kusimamisha Swala, Kutoa Zaka, Kufunga Ramadhani na Kuhiji Makkah kwa mwenye uwezo.” (Bukhari na Muslim).

 

Kutokana na Hadith hii, nguzo za Uislamu ni:

  1. Kutoa Shahada mbili, kwa kushuhudia kuwa hapana Mola ila Allah na kushuhudia kuwa Muhammad ni Mtume wa Allah.
  2. Kusimamisha Swala.
  3. Kutoa Zakat.
  4. Kufunga mwezi wa Ramadhani.
  5. Kuhiji Makkah kwa mwenye uwezo.

 

Hadith hii inatufahamisha kuwa “Uislamu umejengwa juu ya nguzo tano” na sio “Uislamu ni nguzo tano”.

 

Hii ina maana kuwa misingi ya kusimama Uislamu ni nguzo tano lakini Uislamu hauwezi kukamilika (kusimama) kwa kusimamisha nguzo tano tu.

 

-     Nguzo tano ni nyenzo za kumuandaa muislamu kuweza kumuabudu Mola wake katika kila kipengele cha maisha yake ya kila siku.

 

-     Nguzo za Uislamu ni sehemu ndogo sana katika ibada ya muislamu ya maisha yake ya kila siku, mfano; shahada ni wastani wa 0% ya umri, swala ni 7% ya muda wa siku, zaka ni 2½ % ya mali yote ya tajiri, funga ni 5% ya saa za funga kwa mwaka na hija ni 0% ya umri wa mtu.

 

-     Jumla ya ibada ya nguzo 5 za Uislamu katika maisha ya muislamu ni wastani wa 3% tu na 97% ni nje ya ibada. 

 

-     Hivyo kutekeleza nguzo tano tu ni sawa na kufanya ibada 3% ya maisha na 97% ni nje ya ibada ambalo ndio lengo la kuumbwa mwanaadamu.

 

-     Kila nguzo ya Uislamu ina lengo maalumu na umuhimu wake katika kumuandaa mja kuweza kumuabudu na kumtumikia Mola wake ipasavyo.

 

 

 

  • Lengo na Umuhimu wa nguzo za Uislamu.

Nguzo za Uislamu zina umuhimu na malengo maalumu kama ifuatavyo:

  1. Shahada mbili.

-     Ni kiingilio (kitambulisho) cha muislamu kwa ummah wa Kiislamu anayoitoa muislamu mbele ya ummah.

 

-     Ni kutoa ahadi ya kumtii Allah (s.w) ipasavyo katika kukiendea kipengele cha maisha ya kila siku saa 24.

 

2.Kusimamisha Swala.

-     Ni nguzo ya pili na ni nguzo kuu ya Uislamu na ni amri ya Allah (s.w) kwa waislamu wote katika kuitekeleza.

 

-     Lengo kuu la kusimamisha swala ni kumtakasa mja kutokana na mambo maovu na machafu.

      Rejea Qur’an (29:45).

 

3.Zakat.

-     Ni nguzo ya tatu ya Uislamu na ni amri ya Allah (s.w) kwa waislamu matajiri kuitekeleza.

 

-     Zaka ina lengo la utakaso (kuitakasa):

  • Nafsi ya mtoaji kutokana na uchumi haramu, ubakhili, dhuluma, husuda, upupiaji wa mali, n.k.
  • Nafsi ya mpokeaji kutokana na husuda, chuki, n.k.
  • Mali ya mtoaji kutokana na uchumi haramu, dhuluma, n.k.
  • Jamii kwa kujenga huruma, mapenzi, kushirikiana na kushikamana.

         Rejea Qur’an (9:103).

 

4.Swaumu.

-     Ni nguzo ya nne ya Uislamu na ni amri ya Allah (s.w) kwa waislamu kufunga mwezi wa Ramadhani.

 

-     Swaumu ina lengo la kumuandaa mja kuwa Mcha-Mungu atakaye mtii Allah (s.w) ipasavyo katika maamrisho na makatazo yake.

Rejea Qur’an (2:183).

 

5.Hija.

-     Ni nguzo ya tano ya Uislamu na ni amri ya Mwenyezi Mungu (s.w) kwa waislamu wenye uwezo wa mali na afya.

 

-     Hija ina lengo la kumtayarisha mja kumpenda Allah (s.w) kuliko kitu chochote hata nafsi yake.

 

-     Inamuandaa mja kuwa askari aliyetayari kutumia mali na nafsi yake katika kupigania dini yake.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mali zinazojuzu kutolewa zaka, nisaab yake na viwango vyake
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Funga za kafara
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kwanini lengo la zakat na sadaqat halifikiwi katika jamii yetu
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Makundi ya dini za wanaadamu
Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu. Soma Zaidi...

image Sanda ya mtoto
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mafunzo ya hadithi zilizochaguliwa
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maswali juu ya Mambo anayopaswa kufanyiwa maiti ya muislamu
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Tofauti kati ya zakat na sadaqat
Nguzo za Imani, tofauti kati ya sadaqat na zakat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Sababu za kutokubalika kwa vitabu vilivyotumwa kuwa muongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu zama hizi
Soma Zaidi...

image Elimu yenye manufaa
Elimu yenye manufaa Ni ipi? (EDK form 1:elimu yenye manufaa) Soma Zaidi...