picha

Kutoa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

4.3. Kutoa Zakat.

Umuhimu wa Zakat na Sadakat katika Uislamu.

Zakat ni nguzo ya tatu ya Uislamu.

Baada ya shahada mbili na kusimamisha swala nguzo muhimu sana katika uislamu ni kutoa zakat kama ilivyoainishwa katika hadithi.

Kutoa zakat na Sadaka ni amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Kutoa zaka na vile tulivyoruzukiwa katika mali na huduma au misaada mbali mbali ni wajibu kwa waislamu wanaovimudu.

Rejea Quran (14:31) na (2:254).

 

Kutoa Zakat ndio kitambulisho cha Uislamu na Ucha-Mungu wa mtu.

Muislamu akiacha au kukataa kutoa zakat kwa makusudi ni ishara ya kuritadi na kutoka katika Uislamu.

Rejea Quran (9:11) na (2:2-3).

 

Kutoa Zakat na sadaka ni sababu ya mtu kufaulu Duniani na Akhera.

Miongoni mwa sifa za waumini na wacha-Mungu ni kutoa katika vile walivyoruzukiwa na muumba wao.

Rejea Quran (2:2-3), (23:1-4), (22:34-45) na (2:262,274).

 

Kutotoa Zakat na Sadaka ni sababu ya kuangamia mtu Duniani na Akhera.

Kutotoa katika vile tulivyoruzukiwa hupelekea mtu kustahiki adhabu hapa Duniani na Akhera pia.

Rejea Quran (9:34-35), (92:8-10) na (3:180).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/18/Tuesday - 04:37:18 pm Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2101

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 web hosting    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango

Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.

Soma Zaidi...
Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani

Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku.

Soma Zaidi...
Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu

Kuchunga au kutekeleza ahadi ni miongoni mwa vipengele muhimu vya tabia ya muumini wa kweli.

Soma Zaidi...
Sunnah za funga ya ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...