image

Kutoa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

4.3. Kutoa Zakat.

Umuhimu wa Zakat na Sadakat katika Uislamu.

Zakat ni nguzo ya tatu ya Uislamu.

Baada ya shahada mbili na kusimamisha swala nguzo muhimu sana katika uislamu ni kutoa zakat kama ilivyoainishwa katika hadithi.

Kutoa zakat na Sadaka ni amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Kutoa zaka na vile tulivyoruzukiwa katika mali na huduma au misaada mbali mbali ni wajibu kwa waislamu wanaovimudu.

Rejea Quran (14:31) na (2:254).

 

Kutoa Zakat ndio kitambulisho cha Uislamu na Ucha-Mungu wa mtu.

Muislamu akiacha au kukataa kutoa zakat kwa makusudi ni ishara ya kuritadi na kutoka katika Uislamu.

Rejea Quran (9:11) na (2:2-3).

 

Kutoa Zakat na sadaka ni sababu ya mtu kufaulu Duniani na Akhera.

Miongoni mwa sifa za waumini na wacha-Mungu ni kutoa katika vile walivyoruzukiwa na muumba wao.

Rejea Quran (2:2-3), (23:1-4), (22:34-45) na (2:262,274).

 

Kutotoa Zakat na Sadaka ni sababu ya kuangamia mtu Duniani na Akhera.

Kutotoa katika vile tulivyoruzukiwa hupelekea mtu kustahiki adhabu hapa Duniani na Akhera pia.

Rejea Quran (9:34-35), (92:8-10) na (3:180).





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1486


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

Masharti ya swala
Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali. Soma Zaidi...

Sera ya uchumi katika Uislamu
4. Soma Zaidi...

IBADA YA HIJA NA NAMNA YA KUITEKELEZA
Soma Zaidi...

Ni wakina nani ni lazima kwao kufunga ramadhani?
Soma Zaidi...

Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu. Soma Zaidi...

Namna ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.
Post hii inakwenda kukugundisha jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

Nguzo za kufunga ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Twahara na namna ya kujitwaharisha, nguzo zake na sunna zake
Soma Zaidi...

Mambo yanayotenguwa udhu
Post hiibinakwenda kukufundisha mambo ambayo yanaharibu udhu. Soma Zaidi...

Swala ya maiti, namna ya kuiswali, nguzo zake, sharti zake na suna zake, hatua kwa hatua
Soma Zaidi...

Kupanga uzazi na uzazi wa mpango katika uislamu
Soma Zaidi...

darasa la funga
Soma Zaidi...