Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)
4.3. Kutoa Zakat.
Umuhimu wa Zakat na Sadakat katika Uislamu.
Zakat ni nguzo ya tatu ya Uislamu.
Baada ya shahada mbili na kusimamisha swala nguzo muhimu sana katika uislamu ni kutoa zakat kama ilivyoainishwa katika hadithi.
Kutoa zakat na Sadaka ni amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).
Kutoa zaka na vile tulivyoruzukiwa katika mali na huduma au misaada mbali mbali ni wajibu kwa waislamu wanaovimudu.
Rejea Quran (14:31) na (2:254).
Kutoa Zakat ndio kitambulisho cha Uislamu na Ucha-Mungu wa mtu.
Muislamu akiacha au kukataa kutoa zakat kwa makusudi ni ishara ya kuritadi na kutoka katika Uislamu.
Rejea Quran (9:11) na (2:2-3).
Kutoa Zakat na sadaka ni sababu ya mtu kufaulu Duniani na Akhera.
Miongoni mwa sifa za waumini na wacha-Mungu ni kutoa katika vile walivyoruzukiwa na muumba wao.
Rejea Quran (2:2-3), (23:1-4), (22:34-45) na (2:262,274).
Kutotoa Zakat na Sadaka ni sababu ya kuangamia mtu Duniani na Akhera.
Kutotoa katika vile tulivyoruzukiwa hupelekea mtu kustahiki adhabu hapa Duniani na Akhera pia.
Rejea Quran (9:34-35), (92:8-10) na (3:180).
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Hapa utajifunza taratibu za kumkafini maiti wa kiislamu. Yaani kushona sanda yake na kumvisha.
Soma Zaidi...Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kuzijuwa aina za twahara katika uislamu. Utaviona vigawanyo vya twahara kulingana na maulamaa wa Fiqh
Soma Zaidi...