Haki za nafsi

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Haki za Nafsi.

Haki za nafsi imekokotezwa kuanzia binafsi, familia, wazazi, n.k kama ifuatavyo;

Mtu Binafsi.

Haki za msingi ni chakula, makazi, malezi, elimu, mavazi, matibabu na kufanyia kazi vipaji na neema alizonazo inavyostahiki ikiwemo;

Haki ya Macho.

Ni kutazama yaliyoamrishwa na kuyaepusha na yaliyoharamishwa.

 Rejea Quran (17:36), (41:20), (24:30-31) na (20:131).

 

Haki ya Masikio.

Ni kusikiliza yaliyoamrishwa na kutosikiliza yaliyoharamishwa pia.

Rejea Quran (8:22) na (6:25).

 

Haki ya Midomo na Ulimi.

Ni kula, kunywa na kuzungumza yaliyohalalishwa na sio yaliyoharamu.

Rejea Quran (16:114), (17:26-29), (17:53), (41:33) na (31:6).

 

Haki ya Mikono na Miguu.

Ni kushika na kuendea vyote vilivyoamrishwa na kuacha vilivyokatazwa.

Rejea Quran (25:72) na (31:18).

 

                     (b)  Haki za Familia.

Ni kusimamia malezi, elimu, uadilifu na wajibu wa kila mmoja katika familia    kwa muongozo wa Quran na Sunnah ili kuleta kufikia lengo la kuumbwa.

Rejea Quran (52:21).

 

                    (c)  Haki za Watoto.

Watoto wana haki ya kupata malezi na makuzi bora kulingana na mahitaji yao kwa mujibu wa mafundisho ya Quran na Sunnah katika sehemu zifuatazo;

 

Haki ya Uhai.

Uhai wa mtoto ni haki itokayo kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kupitia malezi na makuzi ya wazazi. 

 

Haki ya Nasaba.

Mtoto kupata nasaba ni haki kisheria ili kuwa mwanafamilia halali.

Rejea Quran (33:4).

 

Haki ya Makuzi na Malezi bora.

Makuzi na malezi bora ya mtoto ni kupata haki zake za msingi na elimu inayomuwezesha kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) ipasavyo.

Rejea Quran (66:6).

 

                    (d)  Haki za Wazazi.

Ni kuwahurumia, kuwaheshimu, kuwafanyia wema, kuwahudumia na      kuwalea ipasavyo.

Rejea Quran (31:14), (17:23-24), (4:36), (6:151), (19:14) na (19:32).

 

                    (e)  Haki za Jamaa na Majirani.

Ni kutunza uhusiano na kusaidiana pale inapohitajika kwa kuzingatia mipaka.

Rejea Quran (2:215).

 

                     (f)  Haki za Mayatima, Wajane na Masikini.

Ni kuwahifadhi na kuwasaidia wanapokuwa na shida na mahitaji ya kimaisha.

Rejea Quran (2:220), (4:2), (4:10), (2:262) na (2:267).

                    (g)  Haki za Udugu wa Kiimani na za Watu wengine.

Udugu wa kiimani ni haki na bora zaidi kuliko udugu wa damu au nasaba.

Rejea Quran (49:10), (49:13), (7:172-173), (4:7) na (5:8). 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2233

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kutekeleza funga za sunnah

Hapa utajifunza muda wa kutia jia katika funga za sunnah. Pia utajifunza kuhusu uhuru ulio nao

Soma Zaidi...
Sura zinazosomwa katika Swala ya Dhuha

Swala ya Dhuha ni swala ya sunna inayosaliwa wakati wa asubuhi baada ya jua kuchomoza na kupanda angalau kiasi cha mkuki (takribani dakika 15 baada ya jua kuchomoza) mpaka kabla ya adhuhuri. Ingawa hakuna sura maalum zilizowekwa kisheria, Mtume ï·º alisoma baadhi ya sura zenye maana ya kuhimiza kheri na shukrani.

Soma Zaidi...
Maana ya zakat

Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Adhabu ya mzinifu katika jamii ya kiislamu

(iii) Adhabu ya UzinifuKatika Sheria ya Kiislamu mtu haadhibiwi mpaka atende kwa uwazi matendo yenye kuvuruga utaratibu na amani ya jamii.

Soma Zaidi...
Nini kifanyike baada ya mazishi ya kiislamu

Huu ni utaratibu unaotakiwa kufanyika baada ya kuzika.

Soma Zaidi...
Nguzo za uislamu:Shahada

Nguzo za uislamu: Shahada (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...