Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Haki za Nafsi.
Haki za nafsi imekokotezwa kuanzia binafsi, familia, wazazi, n.k kama ifuatavyo;
Mtu Binafsi.
Haki za msingi ni chakula, makazi, malezi, elimu, mavazi, matibabu na kufanyia kazi vipaji na neema alizonazo inavyostahiki ikiwemo;
Haki ya Macho.
Ni kutazama yaliyoamrishwa na kuyaepusha na yaliyoharamishwa.
Rejea Quran (17:36), (41:20), (24:30-31) na (20:131).
Haki ya Masikio.
Ni kusikiliza yaliyoamrishwa na kutosikiliza yaliyoharamishwa pia.
Rejea Quran (8:22) na (6:25).
Haki ya Midomo na Ulimi.
Ni kula, kunywa na kuzungumza yaliyohalalishwa na sio yaliyoharamu.
Rejea Quran (16:114), (17:26-29), (17:53), (41:33) na (31:6).
Haki ya Mikono na Miguu.
Ni kushika na kuendea vyote vilivyoamrishwa na kuacha vilivyokatazwa.
Rejea Quran (25:72) na (31:18).
(b) Haki za Familia.
Ni kusimamia malezi, elimu, uadilifu na wajibu wa kila mmoja katika familia kwa muongozo wa Quran na Sunnah ili kuleta kufikia lengo la kuumbwa.
Rejea Quran (52:21).
(c) Haki za Watoto.
Watoto wana haki ya kupata malezi na makuzi bora kulingana na mahitaji yao kwa mujibu wa mafundisho ya Quran na Sunnah katika sehemu zifuatazo;
Haki ya Uhai.
Uhai wa mtoto ni haki itokayo kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kupitia malezi na makuzi ya wazazi.
Haki ya Nasaba.
Mtoto kupata nasaba ni haki kisheria ili kuwa mwanafamilia halali.
Rejea Quran (33:4).
Haki ya Makuzi na Malezi bora.
Makuzi na malezi bora ya mtoto ni kupata haki zake za msingi na elimu inayomuwezesha kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) ipasavyo.
Rejea Quran (66:6).
(d) Haki za Wazazi.
Ni kuwahurumia, kuwaheshimu, kuwafanyia wema, kuwahudumia na kuwalea ipasavyo.
Rejea Quran (31:14), (17:23-24), (4:36), (6:151), (19:14) na (19:32).
(e) Haki za Jamaa na Majirani.
Ni kutunza uhusiano na kusaidiana pale inapohitajika kwa kuzingatia mipaka.
Rejea Quran (2:215).
(f) Haki za Mayatima, Wajane na Masikini.
Ni kuwahifadhi na kuwasaidia wanapokuwa na shida na mahitaji ya kimaisha.
Rejea Quran (2:220), (4:2), (4:10), (2:262) na (2:267).
(g) Haki za Udugu wa Kiimani na za Watu wengine.
Udugu wa kiimani ni haki na bora zaidi kuliko udugu wa damu au nasaba.
Rejea Quran (49:10), (49:13), (7:172-173), (4:7) na (5:8).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 1779
Sponsored links
๐1
Simulizi za Hadithi Audio
๐2
Kitabu cha Afya
๐3
Madrasa kiganjani
๐4
kitabu cha Simulizi
๐5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
๐6
Kitau cha Fiqh
JIFUNZE FIQH
Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka. Soma Zaidi...
Mwenendo wa Mtu aliyetoa Shahada
Muislamu aliyetoa shahada ya kweli hanabudiย kumfanya Mtume (s. Soma Zaidi...
Namna ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.
Post hii inakwenda kukugundisha jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...
Vipi utapata uchamungu kupitia funga
Vipi lengo la funga litafikiwa na kumfanya mfungaji awe mchamungu. Soma Zaidi...
Msimamo wa uislamu juu ya utumwa
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf Soma Zaidi...
MTAZAMO NA HUKUMU YA KUPANGA UZAZI WA MPANGO KWENYE UISLAMU
Atika uislamu swala la kupanga uzazi linaruhusiwa endapo kutakuwa na sababu maalumu za kisheria. Soma Zaidi...
Sunnah za siku ya idi na utaratibu wa kusherehekea
Hapa utajifunza utaratibu wa kusherekea ifil fitir. Pia utajifunza sunnah zinazoambatsns na idil fitir Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi
Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu. Soma Zaidi...
Umuhimu wa uchumi katika uislamu
Post hii itakufundisha faida na umuhimu wa kijenga uchumi katika jamii ya kiislamu. Soma Zaidi...