Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Haki za Nafsi.
Haki za nafsi imekokotezwa kuanzia binafsi, familia, wazazi, n.k kama ifuatavyo;
Mtu Binafsi.
Haki za msingi ni chakula, makazi, malezi, elimu, mavazi, matibabu na kufanyia kazi vipaji na neema alizonazo inavyostahiki ikiwemo;
Haki ya Macho.
Ni kutazama yaliyoamrishwa na kuyaepusha na yaliyoharamishwa.
Rejea Quran (17:36), (41:20), (24:30-31) na (20:131).
Haki ya Masikio.
Ni kusikiliza yaliyoamrishwa na kutosikiliza yaliyoharamishwa pia.
Rejea Quran (8:22) na (6:25).
Haki ya Midomo na Ulimi.
Ni kula, kunywa na kuzungumza yaliyohalalishwa na sio yaliyoharamu.
Rejea Quran (16:114), (17:26-29), (17:53), (41:33) na (31:6).
Haki ya Mikono na Miguu.
Ni kushika na kuendea vyote vilivyoamrishwa na kuacha vilivyokatazwa.
Rejea Quran (25:72) na (31:18).
(b) Haki za Familia.
Ni kusimamia malezi, elimu, uadilifu na wajibu wa kila mmoja katika familia kwa muongozo wa Quran na Sunnah ili kuleta kufikia lengo la kuumbwa.
Rejea Quran (52:21).
(c) Haki za Watoto.
Watoto wana haki ya kupata malezi na makuzi bora kulingana na mahitaji yao kwa mujibu wa mafundisho ya Quran na Sunnah katika sehemu zifuatazo;
Haki ya Uhai.
Uhai wa mtoto ni haki itokayo kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kupitia malezi na makuzi ya wazazi.
Haki ya Nasaba.
Mtoto kupata nasaba ni haki kisheria ili kuwa mwanafamilia halali.
Rejea Quran (33:4).
Haki ya Makuzi na Malezi bora.
Makuzi na malezi bora ya mtoto ni kupata haki zake za msingi na elimu inayomuwezesha kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) ipasavyo.
Rejea Quran (66:6).
(d) Haki za Wazazi.
Ni kuwahurumia, kuwaheshimu, kuwafanyia wema, kuwahudumia na kuwalea ipasavyo.
Rejea Quran (31:14), (17:23-24), (4:36), (6:151), (19:14) na (19:32).
(e) Haki za Jamaa na Majirani.
Ni kutunza uhusiano na kusaidiana pale inapohitajika kwa kuzingatia mipaka.
Rejea Quran (2:215).
(f) Haki za Mayatima, Wajane na Masikini.
Ni kuwahifadhi na kuwasaidia wanapokuwa na shida na mahitaji ya kimaisha.
Rejea Quran (2:220), (4:2), (4:10), (2:262) na (2:267).
(g) Haki za Udugu wa Kiimani na za Watu wengine.
Udugu wa kiimani ni haki na bora zaidi kuliko udugu wa damu au nasaba.
Rejea Quran (49:10), (49:13), (7:172-173), (4:7) na (5:8).
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.
Soma Zaidi...(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu.
Soma Zaidi...Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.
Soma Zaidi...