Haki za nafsi

Haki za nafsi

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Haki za Nafsi.

Haki za nafsi imekokotezwa kuanzia binafsi, familia, wazazi, n.k kama ifuatavyo;

Mtu Binafsi.

Haki za msingi ni chakula, makazi, malezi, elimu, mavazi, matibabu na kufanyia kazi vipaji na neema alizonazo inavyostahiki ikiwemo;

Haki ya Macho.

Ni kutazama yaliyoamrishwa na kuyaepusha na yaliyoharamishwa.

 Rejea Quran (17:36), (41:20), (24:30-31) na (20:131).

 

Haki ya Masikio.

Ni kusikiliza yaliyoamrishwa na kutosikiliza yaliyoharamishwa pia.

Rejea Quran (8:22) na (6:25).

 

Haki ya Midomo na Ulimi.

Ni kula, kunywa na kuzungumza yaliyohalalishwa na sio yaliyoharamu.

Rejea Quran (16:114), (17:26-29), (17:53), (41:33) na (31:6).

 

Haki ya Mikono na Miguu.

Ni kushika na kuendea vyote vilivyoamrishwa na kuacha vilivyokatazwa.

Rejea Quran (25:72) na (31:18).

 

                     (b)  Haki za Familia.

Ni kusimamia malezi, elimu, uadilifu na wajibu wa kila mmoja katika familia    kwa muongozo wa Quran na Sunnah ili kuleta kufikia lengo la kuumbwa.

Rejea Quran (52:21).

 

                    (c)  Haki za Watoto.

Watoto wana haki ya kupata malezi na makuzi bora kulingana na mahitaji yao kwa mujibu wa mafundisho ya Quran na Sunnah katika sehemu zifuatazo;

 

Haki ya Uhai.

Uhai wa mtoto ni haki itokayo kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kupitia malezi na makuzi ya wazazi. 

 

Haki ya Nasaba.

Mtoto kupata nasaba ni haki kisheria ili kuwa mwanafamilia halali.

Rejea Quran (33:4).

 

Haki ya Makuzi na Malezi bora.

Makuzi na malezi bora ya mtoto ni kupata haki zake za msingi na elimu inayomuwezesha kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) ipasavyo.

Rejea Quran (66:6).

 

                    (d)  Haki za Wazazi.

Ni kuwahurumia, kuwaheshimu, kuwafanyia wema, kuwahudumia na      kuwalea ipasavyo.

Rejea Quran (31:14), (17:23-24), (4:36), (6:151), (19:14) na (19:32).

 

                    (e)  Haki za Jamaa na Majirani.

Ni kutunza uhusiano na kusaidiana pale inapohitajika kwa kuzingatia mipaka.

Rejea Quran (2:215).

 

                     (f)  Haki za Mayatima, Wajane na Masikini.

Ni kuwahifadhi na kuwasaidia wanapokuwa na shida na mahitaji ya kimaisha.

Rejea Quran (2:220), (4:2), (4:10), (2:262) na (2:267).

                    (g)  Haki za Udugu wa Kiimani na za Watu wengine.

Udugu wa kiimani ni haki na bora zaidi kuliko udugu wa damu au nasaba.

Rejea Quran (49:10), (49:13), (7:172-173), (4:7) na (5:8). 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1948

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu
Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu

- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.

Soma Zaidi...
MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA
MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA

*Suala la kumilikiwa binaadam (utumwa), japokuwa linaendelea kutajwa kwenye Sharia (katika vitabu), ni suala ambalo haliko.

Soma Zaidi...
maana ya uchumi kiislamu
maana ya uchumi kiislamu

Maana ya UchumiMfumo wa maisha wa Kiislamu humuelekeza binaadamu kujenga na kudumisha uhusiano wake na Al-lah (s.

Soma Zaidi...
Usawa na uhuru wa kuchuma mali katika uislamu
Usawa na uhuru wa kuchuma mali katika uislamu

Uchumi wa uislamu umeweka taratibu mbalimbali katika kuchuma mali.

Soma Zaidi...
Maana ya talaka na kuacha ama kuachwa
Maana ya talaka na kuacha ama kuachwa

Maana ya TalakaTalaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili.

Soma Zaidi...