Haki za nafsi


image


Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)


Haki za Nafsi.

Haki za nafsi imekokotezwa kuanzia binafsi, familia, wazazi, n.k kama ifuatavyo;

Mtu Binafsi.

Haki za msingi ni chakula, makazi, malezi, elimu, mavazi, matibabu na kufanyia kazi vipaji na neema alizonazo inavyostahiki ikiwemo;

Haki ya Macho.

Ni kutazama yaliyoamrishwa na kuyaepusha na yaliyoharamishwa.

 Rejea Quran (17:36), (41:20), (24:30-31) na (20:131).

 

Haki ya Masikio.

Ni kusikiliza yaliyoamrishwa na kutosikiliza yaliyoharamishwa pia.

Rejea Quran (8:22) na (6:25).

 

Haki ya Midomo na Ulimi.

Ni kula, kunywa na kuzungumza yaliyohalalishwa na sio yaliyoharamu.

Rejea Quran (16:114), (17:26-29), (17:53), (41:33) na (31:6).

 

Haki ya Mikono na Miguu.

Ni kushika na kuendea vyote vilivyoamrishwa na kuacha vilivyokatazwa.

Rejea Quran (25:72) na (31:18).

 

                     (b)  Haki za Familia.

Ni kusimamia malezi, elimu, uadilifu na wajibu wa kila mmoja katika familia    kwa muongozo wa Quran na Sunnah ili kuleta kufikia lengo la kuumbwa.

Rejea Quran (52:21).

 

                    (c)  Haki za Watoto.

Watoto wana haki ya kupata malezi na makuzi bora kulingana na mahitaji yao kwa mujibu wa mafundisho ya Quran na Sunnah katika sehemu zifuatazo;

 

Haki ya Uhai.

Uhai wa mtoto ni haki itokayo kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kupitia malezi na makuzi ya wazazi. 

 

Haki ya Nasaba.

Mtoto kupata nasaba ni haki kisheria ili kuwa mwanafamilia halali.

Rejea Quran (33:4).

 

Haki ya Makuzi na Malezi bora.

Makuzi na malezi bora ya mtoto ni kupata haki zake za msingi na elimu inayomuwezesha kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) ipasavyo.

Rejea Quran (66:6).

 

                    (d)  Haki za Wazazi.

Ni kuwahurumia, kuwaheshimu, kuwafanyia wema, kuwahudumia na      kuwalea ipasavyo.

Rejea Quran (31:14), (17:23-24), (4:36), (6:151), (19:14) na (19:32).

 

                    (e)  Haki za Jamaa na Majirani.

Ni kutunza uhusiano na kusaidiana pale inapohitajika kwa kuzingatia mipaka.

Rejea Quran (2:215).

 

                     (f)  Haki za Mayatima, Wajane na Masikini.

Ni kuwahifadhi na kuwasaidia wanapokuwa na shida na mahitaji ya kimaisha.

Rejea Quran (2:220), (4:2), (4:10), (2:262) na (2:267).

                    (g)  Haki za Udugu wa Kiimani na za Watu wengine.

Udugu wa kiimani ni haki na bora zaidi kuliko udugu wa damu au nasaba.

Rejea Quran (49:10), (49:13), (7:172-173), (4:7) na (5:8). 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Funga za kafara
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Zoezi
Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira. Soma Zaidi...

image Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)
Nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Vita vya uhudi
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Shahada mbili
Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku. Soma Zaidi...

image Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Faida za funga
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kuamini mitume wa mwenyezi Mungu
Nguzo za Imani (EDK form 2:. Dhana ya elimu ya uislamu Soma Zaidi...

image Aina za hijjah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mambo yanayodhaniwa kuwa yanaharibu funga lakini hayaharibu
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...