Kulinda account yako ya Facebook dhidi ya waharifu wa kimtandao

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kulinda account yako ya Facebook dhidi ya waharifu wa kimtandao

KULINDA AKAUNT YAKO YA FACEBOOK DHIDI YA WAHALIFU WA KIMTANDAO

Watu wengi wanalalamika kuwa akaunti zao za facebook zimehakiwa, yaani zimeshambuliwa na wahalifu wa kimtandano. Akaunti kuhakiwa inamaana kuna mtu amelogin kwenye akaunti yako bila ya ruhusa yako ama bila ya kumpatia neno la siri. Facebook imeweka njia kadhaa kuhakikisha kuwa akaunti za watu zipo salama muda wowote.

 

Two-factor authentication ni katika njia mujarabu ambazo facebook wameweka ili kulinda akaunti za watumiaji wake. Kwa kutumia njia hii hata kama mtu anaijuwa password yako (neno la siri) hataweza kuingia kwenye akaunti yako ya facebook mpaka awe na laini yako ambayo namba yeke umeisajili facebook.

 

Njia hii inaongeza tabaka lingine la usalama wa akaunti yako ya facebook. Baada ya kuingiza neno la siri kwenye akaunti yako ya facebook, facebook watakutumia code (namba sita) kwenye laini yako ulioisajili facebook. Namba hizo utaziingiza kwenye kibox na ndipo utaruhusiwa kuingia kwenye akaunti.

 

Kuanza kutumia  njia hii ingia kwenye setting, kisha security and login kisha Two-Factor Authentication. Utatakiwa kuingiza namba ya simu na maelekezo machache yatafuata. Utalogout kisha utalogin tena ili kuthibitisha huduma kama ipo tayari.

 

Njia hii itasaidia sana kwa wale ambao tayari password zao kuna watu wanazifahamu. Hata kama mtu anaijua password TROJAN) yako katu hataweza kuingia kwenye akaunti yako mpaka awe na laini yako. Karibia mitandao mingi inatumia njia hii ikiwemo google, linkedin, github na mingine mingi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Teknolojia Main: Jifunze File: Download PDF Views 1072

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kutuma sms ndefu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kutuma sms ndefu

Soma Zaidi...
Utajuaje Kama simu au kompyuta yako Ina virus

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kujua Kama simu yako ina virus

Soma Zaidi...
yanayoathiri betri ya kifaa chako

makala hii itakuelezea mambo makuu ambayo ni hatari kwa usalama wa betri ya kifaa chako

Soma Zaidi...
Simu au Kompyuta inastak? (inasumbua)

Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta..

Soma Zaidi...
Utunzaji wa betri la kifaa chako

Posti hii inakwenda kukupa elimu kuhusu utunzaji wa betri la kifaa chako

Soma Zaidi...
Kufungua program nyingi kwa wakati mmoja

Posti hii inakwenda kukuelekeza njia za kufungua program nyingi kwa wakati mmoja

Soma Zaidi...
Muda wa kuchaji simu yako

Posti hii itakwenda kukujuza juu ya kuda mzuri wa kuchaji simu yako

Soma Zaidi...
Kipi kingine utafanya ukiwa Facebook

Somo hili linakwenda kukueleza Mambo mengne unayoweza kuyafanya ukiwa Facebook

Soma Zaidi...
Sababu za simu kusumbua mtandao

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sabau za simu kusumbua mtandao

Soma Zaidi...