NJIA RAHISI YA KUDOWNLOAD VIDEO YOUTUBE Teknolojia ya mawasiliano ni muhimu katika kuhakikisha kuwa ulimwengu unafikika kama kijiji kimoja na hapa ndipo unapata maana halisi ya neno UTANDAWAZA yaani kwa lugha ya kimombo ni globalization.
NJIA RAHISI YA KUDOWNLOAD VIDEO YOUTUBE
Teknolojia ya mawasiliano ni muhimu katika kuhakikisha kuwa ulimwengu unafikika kama kijiji kimoja na hapa ndipo unapata maana halisi ya neno UTANDAWAZA yaani kwa lugha ya kimombo ni globalization. Kuweza kulifanikisha hili tunahitaji kuwa na teknolojia uliyo madhubuti na rafiki kwa watumiaji. Tunahitaji pia teknolojia kwa ajili ya kuburudika, na hapa ninazungumzia mtandao mkubwa duniani kwa kuonyesha video nao ni youtube.
Youtube ni kitengo katika kampuni itambulikayo kama google iliyo chini ya kampuni mama inayoitwa Alphabet. Youtube ni mtandao mkuu wa kurusha na kushiriki video. Hapa utaweza kupata fursa ya kushiriki video yako kwenye hadhara (public) ama na watu maalumu uwapendao. Video hii inaweza pia kuwa live yaani mubashara moja kwa moja
Changamoto inayowakumbwa watu wengi leo wanashindwa kudownload video za kwenye youtube. Usijali, katika makala hii nitakuletea njia rahisi na nyepesi ya kudownload video ya youtube. Baada ya kuidownload video hiyo unaweza kuweka kwenye flash, memori ana CD na kuitazama kwenye vifaa vyako vingine kama TV, SABUFA N.K
Zipo njia nyingi ambazo unaweza kuzitumia kudownload video ya youtube zipo nyingine za kuzunguruka sana kama kutumia tubemate. Ama kutumia youtube go ambapo utawza kuangalia video ya bila ya kuhitaji intanet yaani offline. Nitazungumzia njia hizi kwa ufupi kisha nitakuletea njia iliyo rahisi zaidi katika hizo:-
1.tubemate ni muda mrefu toka watumiaji wa simu za smartphone waanze kulalamika kuwa wanahitaji kudownload video za youtube. Tubemate ikaja kwa lengo la kutatua tatizo hili. App hii haipatikani playstore kwa hiyo usalama wake ni mdogo kwa taarifa zako za siri.
Kwa kutumia tubemate unaweza kudownload video na ikabakia kwenye simu yako. Video hii pia unaweza kuihamisha kutoka kwenye simu yako na kuipeleka kwingine ukutakako. App hii utaidownload kwenye tovuti ya tubemate kisha utaruhusu kuinstall APK kutoka unknown source. Baada ya hapo unaweza kuingia youtube ukiwa kwenye App hii. Utachangua ama kutafuta video unayoitaka na utabofya kitufe cha kudownload. Video yako itakuwa tayari kwa kudownload na kuifadhiwa kwenye simu yako.
App hii pia ni maarufu sana kwa hiyo unaweza kuipata kwenye tovuti kama updown. Tubemate ni msaada mkubwa kwa watumiaji wa simu. Kwani unaweza pia kudownload video zaidi ya moja kwa wakati mmoja na kuchagua format uitakayo kama mp3, mp4, n.k
2.YOUTUBE GO hii ni App nyingine inayopatikana youtube go pia unaweza kuipata App hii playstore. App hii ni salama kama utaidownload kutoka playstore ama kwenye tovuti mama ya youtube go. hapo mwanzoni App hii haikuwa ikipatikana nchi zote, ilikuwa ikipatikana india na maeneo yenye mtandao hafifu usiofikia 3g.
Lengo hasa la App hii ya youtube go ni kuwezesha kuangalia video hata ukiwa na mtandao mdogo ama maeneo ambayo netweki inazumbua. Kwa kutumia unaweza kudownload video na kuzitazama kwenye kifaa chako ukiwa kwenye App ya youtube go. Unachotakiwa ni kuinstall App kutoka playstore google play store baada ya hapo unafungua App kisha unatafuta video unayoitaka, ukisha bofya kuitazama itakuja meseji kama unavyoona kwenye picha hapo juu.
Kama unataka kuitazama bila ya kudownload utachagua ubora kulingana na MB ukizo nazo kwa mfano vide ya hapo juu ina MB 48 ukiiangalia kwa ubora mkubwa na kwa ubora mdogo ni MB 6. Kama unataka kuidownload utabofya neno download. Baada ya hapo utaona sehemu imeandikwa Download hapo utaziona video zote ulizo download.
Utatazama video hizo bila ya kuhitaji intanet wala mb. Pia unaweza kushiriki na mwenzio ambaye ana App hii kwenye simu yake. Youtube go imekuwa ni msaada mkubwa kwa watu wanaoishi kwenye maeneo yemye mtandao mdogo.
3.https://www.y2mate.com/en4 hii ni njia nyingine na iliyo rahisi kuitumia. Kwa kupitia njia hii utaweza kuidownload video kwa usalama zaidi, kisha utaiweza kwenye kifaa chako. Video hii utaweza kuitazama kwa kutumia njia yeyote unayoitaka.
Unachotakiwa kufanya ni kuingia kwenye tovuti ya youtube kisha unatafuta video unayoitaka. Baada ya hapo utakopi link ya video kama inavyoonyeshwa kwenye picha hapo chini. Ukitoka hapo utaingia kwenye tovuti ya y2mate hapo utapest link. Chini utaiona video yako na utaona batani za kudownload kama inavyoonyeshwa kwenye picha hapo chini.
1. HATUA YA KWANZA: INGIA YOUTUBE NA KISHA KOPI LINK YA VIDEO
2. HATUA YA PILI PEST LINK YAKO KWENYE TOVUTI YA Y2MATE, au bofya hapa kuingia
3. HATUA YA TATU CHAGUA FOMATI YA VIDEO YA KUDOWNLOAD
4. HATUA YA NNE DOWNLOAD VIDEO YAKO KWA KUBOFYA BATANI ILIYOANDIKWA DOWNLOAD
Zipo njia nyingi tuu za kudownload video youtube kwa mfamo cyberspaceandtime hiini tovuti inayoonyesha video zilizopo youtube pamoja na kutoa chaguzi za kuweza kudownload video bila hata ya kutazama matangazo.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Teknolojia Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 3221
Sponsored links
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Kitabu cha Afya
👉3
Kitau cha Fiqh
👉4
Madrasa kiganjani
👉5
kitabu cha Simulizi
👉6
Simulizi za Hadithi Audio
Maana ya legacy contact katika Facebook
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya legacy contact katika facebook Soma Zaidi...
JE NITUMIE SIMU YANGU WAKATI INACHAJI?
Watu wengi wamekuwa wakijiuliza swali hili. Soma Zaidi...
Jinsi ya kufanya simu yako iwe fasta
Posti hii inakwenda kukuelekeza njia za kufanya simu yako iwe fasta Soma Zaidi...
Kufungua program nyingi kwa wakati mmoja
Posti hii inakwenda kukuelekeza njia za kufungua program nyingi kwa wakati mmoja Soma Zaidi...
Muda wa kuchaji simu yako
Posti hii itakwenda kukujuza juu ya kuda mzuri wa kuchaji simu yako Soma Zaidi...
Chanzo cha matatiza ya simu/kompyuta
Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta.. Soma Zaidi...
Jinsi ya kutuma sms ndefu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kutuma sms ndefu Soma Zaidi...
TEKNOLOJIA, HABARI NA MAWASILIANO
Soma Zaidi...
Utunzaji wa betri la kifaa chako
Posti hii inakwenda kukupa elimu kuhusu utunzaji wa betri la kifaa chako Soma Zaidi...
Matatizo katika hard disk
Posti hii inakwenda kukupa baadhi ya matatizo katika hard disk Soma Zaidi...