KOTLIN somo la 7: Jinsi ya kutumia If na ifelse kwenye Kotlin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement
Ili uweze kwanza kuelewa somo hili nitakupa case hapa mbili.
Case 1: umetkiwa ktengeneza program kwa ajili ya menyu ya chakula chuleni. Unatakiwa program hiyo inapofika muda wa kula asubuhi saa 4 iseme chakula cha asubuhi kipo tayari na wakati wa mchana saa 7 iseme chakula cha mchana kipo tayari na inapofika jioni saa 1 usiku iseme chakula cha usiku kipo tayari mwisho inapofika saa 4 usiku iseme mlale salama.
Kwa hiyo hapo utaona tumeweka masharti kulingana na saa. Shari la kwanza ifike saa 4 asubuhi ndipo iseme chakula cha subuhi kipo tayari… na kuendelea masharti mengine. Hii ndio tunaita descision making
Case 2: umetakiwa kutengeneza table (zile tabo za kuzidisha katika somo la hesabu) ya 2 kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la tatu. Sasa badala ya kuandika moja moja utahitaji program yako iandike yenyewe. Hapa ndio tunaita loop .mfano mzui wa loop ni music player, kwamba unawez akuchaguwa mziki ujirudie rudie mara ngapii.
Flow statemenet zimegawanyika katika makundi makuu matatu ambayo ni:-
- Descision making: hapa program inafanya maamuzi kulingana na masharti atakayoweka. Hizi ni kama
- If
- Ifelse
- If else if
- when case
- Looping: hapa program inarudia rudia ku run code zaidi ya mara moja kulingana na masharti yatakayowekwa.. Hizi ni kama :-
- For loop
- For in loop
- While loop
- Do while loop
- Jumping: hapa program ita run kisha itawacha baadhi ya block za code na kuendelea tena kulingana na masharti yatakayowekwa.
- If statement:
Hii ni sawa na neno la kiswahiki ikiwa. Kwa mfano tunasema ikiwa umri wa mtoto ni miaka 7 program iseme aende shule. Sawa ngoja tuone jinsi ya kufanya program yetu itumie sharti hili.
Jinsi ya kuandika descision making statemen
If ( weka sharti) {
Weka code
}
Kama unavyoona hapo kwanza utaanza na keyword if likifuatiwa na na mabano () ndani ya mabano hayo weka charti lako. Ambapo ni umri wa mtoto iwe miaka 7. Kisha utaweka mabano {} ambapo ndani ya mabani hayo utaweka nini kitokee kama sharti limefikiwa. Kwa mujibu wa mfano wetu hap tunataka program iseme aende shule. Sasa wacha tuone jinsi ya kuandika hizo code.
Kwanza tutaanz akuweka variable yetu ambayoiabeba umri wa mtoto. Kisha tutaweka charti letu .
fun main() {
val umri = 7;
if(umri == 7){
print("aende shule");
}
}
Sasa tunataka kusema ikiwa umri wa mtoto ni zaidi ama sawasawa na miaka 7 iseme aende shule.
fun main() {
val umri = 7;
if(umri >= 7){
print("aende shule");
}
}
Unaweza kutumia naoperator nyingine kama <, 1=, <= na nyinginezo kufanya mazoezi zadi.
Sasa hapo kuna tatizo kama umriutakuwa ni chini ya saba hakuna chochote program itasema . hapa sasa tutahitaji else satatement, ambayo itaangalia ...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
KOTLIN somo la 17: method na properties za namba
Katika somo hili tutajifunza kuhusu method na properties za Kotlin zinazofanya kazi kwenye namba.
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 12: Jinsi ya kupata user input
Jinsi ya kuchukuwa user input kwenye Kotlin kwa ajili ya kuongeza user interaction kwenye program.
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 6: string kwenye Kotlin
Katika somo hili tutakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na string kwenye Kotlin.
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 13: Jinsi ya kuandika function na kuweka parameter
Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function na kuweka parameter kwenye function
Soma Zaidi...Kotlin somo la 22: Package kenye kotlin
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu nadharia ya package, kazi zake, aina zake na jinsi zinavyotumika
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 19: method na properties zinazotumika kwenye set
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu set data type pamoja na method ambazo hufanya kazi kwenye set.
Soma Zaidi...