picha

KOTLIN somo la 7: Jinsi ya kutumia If na ifelse kwenye Kotlin

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement

Ili uweze kwanza kuelewa somo hili nitakupa case hapa mbili. 

Case 1: umetkiwa ktengeneza program kwa ajili ya menyu ya chakula chuleni. Unatakiwa program hiyo inapofika muda wa kula asubuhi saa 4 iseme chakula cha asubuhi kipo tayari na wakati wa mchana saa 7 iseme chakula cha mchana kipo tayari na inapofika jioni saa 1 usiku iseme  chakula cha usiku kipo tayari mwisho inapofika saa 4 usiku iseme  mlale salama.  

 

Kwa hiyo hapo utaona tumeweka masharti kulingana na saa. Shari la kwanza ifike saa 4 asubuhi ndipo iseme chakula cha subuhi kipo tayari… na kuendelea masharti mengine. Hii ndio tunaita descision making

 

Case 2: umetakiwa kutengeneza  table (zile tabo za kuzidisha katika somo la hesabu) ya 2 kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la tatu. Sasa badala ya kuandika moja moja utahitaji program yako iandike yenyewe. Hapa ndio tunaita  loop .mfano mzui wa loop ni music player, kwamba unawez akuchaguwa mziki ujirudie rudie mara ngapii.


 

Flow statemenet zimegawanyika katika makundi makuu matatu ambayo ni:-

  1. Descision making: hapa program inafanya maamuzi kulingana na masharti atakayoweka. Hizi ni kama
    1. If
    2. Ifelse
    3. If else if
    4. when case
  2. Looping: hapa program inarudia rudia ku run code zaidi ya mara moja kulingana na masharti yatakayowekwa.. Hizi ni kama :-
    1. For loop
    2. For in loop
    3. While loop
    4. Do while loop
  3. Jumping: hapa program ita run kisha itawacha baadhi ya block za code na kuendelea tena kulingana na masharti yatakayowekwa.

 

  1. If statement:

Hii ni sawa na neno la kiswahiki ikiwa. Kwa mfano tunasema ikiwa umri wa mtoto ni miaka 7 program iseme aende shule. Sawa ngoja tuone jinsi ya kufanya program yetu itumie sharti hili.

 

Jinsi ya kuandika descision making statemen

If ( weka sharti) {

Weka code

}

Kama unavyoona hapo kwanza utaanza na keyword if likifuatiwa na na mabano ()  ndani ya mabano hayo weka charti lako. Ambapo ni umri wa mtoto iwe miaka 7. Kisha utaweka mabano {} ambapo ndani ya mabani hayo utaweka nini kitokee kama sharti limefikiwa. Kwa mujibu wa mfano wetu hap tunataka program iseme aende shule. Sasa wacha tuone jinsi ya kuandika hizo code.

 

Kwanza tutaanz akuweka variable yetu ambayoiabeba umri wa mtoto. Kisha tutaweka charti letu .

fun main() {

  val umri = 7;

  if(umri == 7){

     print("aende shule");

  }

}

 Sasa tunataka kusema ikiwa umri wa mtoto ni zaidi ama sawasawa na miaka 7 iseme aende shule.

fun main() {

  val umri = 7;

  if(umri >= 7){

     print("aende shule");

  }

}

Unaweza kutumia naoperator nyingine kama <, 1=, <= na nyinginezo kufanya mazoezi zadi.


 

Sasa hapo kuna tatizo kama umriutakuwa ni chini ya saba hakuna chochote program itasema . hapa sasa tutahitaji else satatement, ambayo itaangalia ikiwa umri ni miaka 7 iseme aende shule lakini ikiwa ni tofauti na miaka 7 iseme hajafikia umri. Kufanya hivi tutafuata formla hii

If (sharti) {

Code

">...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-02-01 Topic: Kotlin Main: ICT File: Download PDF Views 725

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 ai web app   

Post zinazofanana:

Kotlin somo la 22: Package kenye kotlin

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu nadharia ya package, kazi zake, aina zake na jinsi zinavyotumika

Soma Zaidi...
Kotlin Somo la 28: Abstraction na Interfaces

Somo hili linaelezea dhana ya abstraction na interfaces katika Kotlin — namna zinavyosaidia kuficha undani wa utekelezaji na kuweka miongozo ya kazi. Tutafahamu tofauti kati ya abstract class na interface, na tutaandika mifano halisi ya kila moja.

Soma Zaidi...
KOTLIN somo la 2: sheria na kanuni za uandishi wa code za Kotlin

Katika somo hili unakwenda kujifunza kuhusu sheria na kanuni za undishi wa code za Kotlin yaani syntax za kotlin.

Soma Zaidi...
KOTLIN somo la 21: Jinsi ta kutengeneza library

Katika somo hili utajifunza kuhusu Kotlin library. Pia tutakwenda kutengeneza library yetu wenyewe kwa ajili ya kufanya mazoezi zaidi.

Soma Zaidi...
KOTLIN somo la 18: string na method zinazotumika kwenye list data type.

Katika somo hili tutajifunza method zinazofanya kazi kwenye list data type kwenye Kotlin.

Soma Zaidi...
KOTLIN somo la 8: Jinsi ya kutumia when

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu when case na jinsi inavyofanya kazi kwenye Kotlin.

Soma Zaidi...
Kotlin Somo la 26: Inheritance (Urithi)

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ambavyo class moja inaweza kuriti method na properties kutoka kwenye class nyingine.

Soma Zaidi...
Kotlin somo la 26: Dhana ya class, object na method kwenye kotlin

Katika soomo hili utakwenda kujifunza kuhusu class, maana yake, na jinsi ya kuitengeneza

Soma Zaidi...
Kotlin Somo la 30: Data Classes

Somo hili linaeleza maana ya data classes katika Kotlin, kwa nini zipo, jinsi ya kuzitumia, sifa zake, pamoja na mifano ya vitendo. Pia tutajifunza tofauti kati ya class ya kawaida na data class.

Soma Zaidi...
Kotlin Somo la 31: Objects na Companion Objects

Somo hili linaeleza matumizi ya objects na companion objects katika Kotlin. Tutajifunza tofauti kati ya object na class ya kawaida, faida za singleton pattern, na jinsi ya kutumia companion kama mbadala wa static members katika Java.

Soma Zaidi...