KOTLIN somo la 6: string kwenye Kotlin
Katika somo hili tutakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na string kwenye Kotlin.
Tulisha jifunza kuhusu string katika somo la aina za data. Pia tulijifunza mambo kadhaa khusu string kama interpolation na concatnate. Katika somo hili tutaingia ndani zaidi.
String indexing
Katika programming unaweza kuitumia character yeyote kwenye string husika. Kwa mfano katika string bongoclass hapo naweza kusoma herufi moja moja. Tunapohesabu index ya string tunaanza na 0. Hivyo katika string Bongoclass kama tunataka kusoma herufi ya mwanzo tu hapo tutatumia index ya 0
Mfano:
fun main() {
val text = "Bongoclass"
print(text[0])
}
Hapo utaona imeleta B
fun main() {
val text = "Bongoclass"
print(text[6])
}
Hapa itakuletea l
Sas kwa mfano unataka kujuwa kwenye string yetu ya bongoclass neno class linapatikana kuandia index ya ngapi. Kufanya hivi tutatumia indexOf .
fun main() {
val text = "bongoclass"
print(text.indexOf("class"))
}
Hapo itakupa jibu 5 kumaanisha kuwa neno class kwenye string ya bongoclass hupatikana kuandia index ya 5, kumbuka tunahesabu index kuanzi 0.
Kujuwa idadi y character kwenye string (string length)
Kwa mfabo tunataka kujuwa katika string bongoclass kuna character ngapi. Hapo tutatumia length property.
Mfano:
fun main() {
val text = "Bongoclass"
print(text.length)
}
Hapo itakuletea jibu 10 kumaanisha kuwa kuna character 10.
Kubadili string kuwa katika herufi kubwa na ndogo
Kama unataka kubadili string case kutoka herufi kubwa kwenye ndogo utatumia lowercase() na kama unataka kubadili kutoka ndogo kuwa kubwa utatumia uppercase()
Mfano:
fun main() {
val text = "bongoclass"
val text2 = "BONGOCLASS"
println(text.uppercase())
print(text2.lowercase())
}
Kulinganisha string mbili:
Wakati mwingine utahitaji kulinganisha string mwili. Kama zipo sawa. Kufanya hivi utatumia compareTo. Ikiwa itakupa jibu 0 ujuwe zipo sawa, na ikikupa jibu tofauti ujuwe hazipo sawa.
Mfano:
fun main() {
val text = "bongoclass"
val text2 = "bongoclass...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 web hosting 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Kotlin Somo la 30: Data Classes
Somo hili linaeleza maana ya data classes katika Kotlin, kwa nini zipo, jinsi ya kuzitumia, sifa zake, pamoja na mifano ya vitendo. Pia tutajifunza tofauti kati ya class ya kawaida na data class.
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 10: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Kotlin.
Soma Zaidi...Kotlin Somo la 26: Inheritance (Urithi)
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ambavyo class moja inaweza kuriti method na properties kutoka kwenye class nyingine.
Soma Zaidi...Kotlin somo la 22: Package kenye kotlin
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu nadharia ya package, kazi zake, aina zake na jinsi zinavyotumika
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 13: Jinsi ya kuandika function na kuweka parameter
Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function na kuweka parameter kwenye function
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 7: Jinsi ya kutumia If na ifelse kwenye Kotlin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement
Soma Zaidi...