KOTLIN somo la 13: Jinsi ya kuandika function na kuweka parameter
Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function na kuweka parameter kwenye function
Function ni nini?
Function ni kifungu cha code (block of code) ambacho hufanya kazi maalumu. Function inaweza kufanya kazi kwa kujirudia rudia bila ya kikomo kila itakapoitwa. Function husaidia kutokurudiarudia kuandika code.
Mambo ya kuzingatia:
- Function hutumika zaidi ya mara moja
- Function haifanyikazi mpaka iitwe
- Function inakuwa na parameter
Jinsi ya kuandika function
fun name (){
Code
}
Kwanza utaanza keyword fun kisha utaweka jina la hiyo function (name yaani jina la hiyo function), kisha utaweka mabano () ndani ya haya mabano tutakuja kuweka parameter. Kisha utaweka mabano {} ndani ya haya mabano ndipo utaweka code ambazo unataka zifanye kazi. Wacha tuone mifano huwenda ukaelewa zaidi:-
Mfano 1:
Tunatengeneza program ya kuandika neno bongoclass mara 10. Kwanza tuatatengeneza hiyo fnction ambayo ita print nrno bongoclass
fun main() {
fun bongo() {
print("Bongoclass")
}
}
Kisha tutaiita (call) hiyo funcyion kwenye main().
fun main() {
fun bongo() {
print("Bongoclass")
}
bongo()
}
Sasa kama tutaiita mara 10 itaprint hilo neno mara 10
fun main() {
fun bongo() {
println("Bongoclass")
}
for (x in 1..10) {
bongo()
}
}
Jinsi ya kuweka parameter kwenye function
Tuchukulie mfano kama huu wa mwanzo. Tunataka mtumiaji aweze kuandika mwenyewe anataka neno bongoclass litokee mara ngapi. Kwa mfano akitaka litokee mara 6 ataandika 6 kwenye user input kisha function yetu itafanya kazi husika.
Sasa katika hali hiyo tutahitaji kuweka variable ambayo itawakilisha hiyo 6 atakayowekamtu. Hiyo variable ndio parameter kwa mfano tutaiita idadi. Na hiyo namba 6 atakayoinginza mtu huitwa argument. Kwa ufup tunasema parameter ni jina ila argument ni value yenyewe.
Unapoweka parameter zingatia kuweka na aina ya data ambayo hiyo parameter inakwenda kutumia. Kwa mfano kama parameter itabeba namba tunatweka Int kama ni string tutaweka String unaweza kurejea aina za data. Sasa kuweka aina ya data kwana utaana za alama ya (:) kisha utaruka nafasi moja kisha utaandika aina ya data. Angalia hapo chini.
fun main() {
fun bongo(idadi: Int) {
for (x in 0 until idadi) {
println("Bongoclass")
}
}
println("ANDIKA IDADI")
val idadi = readLine()?.toInt()
bongo(idadi !!)
}
Ukicheki hizo code kuna alama ya (!!) hiyo huitwa double-bang operator au not-null operator. Hii hutumika kuieleza kompyuta kuwa hizo data sio tupu yaani notnull. Hivyo kama ni tupu utapata error. Ni vyema kutumia if kutest kama ni null nini kifanyike tofauti na kuleta error.
fun main() {
fun bongo(idadi: Int) {
println("Bongoclass")
}
println("ANDIKA IDADI")
val idadi = readLine()?.toIntOrNull()
if (idadi != null) {
bongo(idadi)
} else {
println("Invalid input. Please enter a valid number.")
}
}
Function yenye parameter zaidi ya moja.
Parameter zinaweza kuwa zaidi ya moja. Wacha tuone mfano mwingine wa kujumlisha namba mbili. Hapa sitatumia user input. Tutaweka wenyewe namba hizo. Kwa mfano tutaweka 5 na 7 ili program izijumlishe. Ikiwa parameter ni zaidi ya moja zote utatenganisha kwa alama ya koma ( , ).
fun jumlisha(x: Int, y: Int) {
println(x + y)
}
fun main() {
jumlisha(5, 6)
}
Ngoja tutengeneze program ya calculator ambapo itakuwa na parameter 3, ya kwanz ani namba ya kwanza, ya pili ni tendo la hesabu na ya tatu ni namba ya tatu.
Kwa kutumia if
fun jumlisha(x: Int, y: String, z: Int): Int {
val result: Int
if (y == "+") {
result = x + z
} else if (y == "-") {
result = x - z
} else if (y == "*") {
result = x * z
} else if (y ...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
KOTLIN somo la 12: Jinsi ya kupata user input
Jinsi ya kuchukuwa user input kwenye Kotlin kwa ajili ya kuongeza user interaction kwenye program.
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 17: method na properties za namba
Katika somo hili tutajifunza kuhusu method na properties za Kotlin zinazofanya kazi kwenye namba.
Soma Zaidi...Kotlin somo la 26: Dhana ya class, object na method kwenye kotlin
Katika soomo hili utakwenda kujifunza kuhusu class, maana yake, na jinsi ya kuitengeneza
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 16:baadhi ya method na properies zinazofanya kazi kwenye string
Katika somo hili tutajifunza kuhusu method za String zinazotumika kwenye Kotlin.
Soma Zaidi...Kotlin somo la 24: Dhana ya Module katika kotlin
Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu dhana ya module. Hata ivyo tutakwenda kuisoma zaidi kwenye android App
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 15: ainza za parameter kwenye function
Katika somo hili tutakwenda kuzungumzia kuhusu parameter kwenye Kotlin function. Pia tutakwenda kuona mambo mengine yanayohusu function
Soma Zaidi...