Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function na kuweka parameter kwenye function
Function ni nini?
Function ni kifungu cha code (block of code) ambacho hufanya kazi maalumu. Function inaweza kufanya kazi kwa kujirudia rudia bila ya kikomo kila itakapoitwa. Function husaidia kutokurudiarudia kuandika code.
Mambo ya kuzingatia:
Jinsi ya kuandika function
fun name (){
Code
}
Kwanza utaanza keyword fun kisha utaweka jina la hiyo function (name yaani jina la hiyo function), kisha utaweka mabano () ndani ya haya mabano tutakuja kuweka parameter. Kisha utaweka mabano {} ndani ya haya mabano ndipo utaweka code ambazo unataka zifanye kazi. Wacha tuone mifano huwenda ukaelewa zaidi:-
Mfano 1:
Tunatengeneza program ya kuandika neno bongoclass mara 10. Kwanza tuatatengeneza hiyo fnction ambayo ita print nrno bongoclass
fun main() {
fun bongo() {
print("Bongoclass")
}
}
Kisha tutaiita (call) hiyo funcyion kwenye main().
fun main() {
fun bongo() {
print("Bongoclass")
}
bongo()
}
Sasa kama tutaiita mara 10 itaprint hilo neno mara 10
fun main() {
fun bongo() {
println("Bongoclass")
}
for (x in 1..10) {
bongo()
}
}
Jinsi ya kuweka parameter kwenye function
Tuchukulie mfano kama huu wa mwanzo. Tunataka mtumiaji aweze kuandika mwenyewe anataka neno bongoclass litokee mara ngapi. Kwa mfano akitaka litokee mara 6 ataandika 6 kwenye user input kisha function yetu itafanya kazi husika.
Sasa katika hali hiyo tutahitaji kuweka variable ambayo itawakilisha hiyo 6 atakayowekamtu. Hiyo variable ndio parameter kwa mfano tutaiita idadi. Na hiyo namba 6 atakayoinginza mtu huitwa argument. Kwa ufup tunasema parameter ni jina ila argument ni value yenyewe.
Unapoweka parameter zingatia kuweka na aina ya data ambayo hiyo parameter inakwenda kutumia. Kwa mfano kama parameter itabeba namba tunatweka Int kama ni string tutaweka String unaweza kurejea aina za data. Sasa kuweka aina ya data kwana utaana za alama ya (:) kisha utaruka nafasi moja kisha utaandika aina ya data. Angalia hapo chini.
fun main() {
fun bongo(idadi: Int) {
for (x in 0 until idadi) {
println("Bongoclass")
}
}
println("ANDIKA IDADI")
val idadi = readLine()?.toInt()
bongo(idadi !!)
}
Ukicheki hizo code kuna alama ya (!!) hiyo huitwa double-bang operator au not-null operator. Hii hutumika kuieleza kompyuta kuwa hizo data sio tupu yaani notnull. Hivyo kama ni tupu utapata error. Ni vyema kutumia if kutest kama ni null nini kifanyike tofauti na kuleta error.
fun main() {
fun bongo(idadi: Int) {
println("Bongoclass")
}
println("ANDIKA IDADI")
val idadi = readLine()?.toIntOrNull()
if (idadi != null) {
bongo(idadi)
} else {
println("Invalid input. Please enter a valid number.")
}
}
Function yenye parameter zaidi ya moja.
Parameter zinaweza kuwa zaidi ya moja. Wacha tuone mfano mwingine wa kujumlisha namba mbili. Hapa sitatumia user input. Tutaweka wenyewe namba hizo. Kwa mfano tutaweka 5 na 7 ili program izijumlishe. Ikiwa parameter ni zaidi ya moja zote utatenganisha kwa alama ya koma ( , ).
fun jumlisha(x: Int, y: Int) {
println(x + y)
}
fun main() {
jumlisha(5, 6)
}
Ngoja tutengeneze program ya calculator ambapo itakuwa na parameter 3, ya kwanz ani namba ya kwanza, ya pili ni tendo la hesabu na ya tatu ni namba ya tatu.
Kwa kutumia if
fun jumlisha(x: Int, y: String, z: Int): Int {
val result: Int
if (y == "+") {
result = x + z
} else if (y == "-") {
result = x - z
} else if (y == "*") {
result = x * z
} else if (y == "/") {
result = x / z
} else {
println("Invalid oper">...
Je! umeipenda hii post?
Rajabu
Sponsored links
KOTLIN somo la 7: Jinsi ya kutumia If na ifelse kwenye Kotlin
KOTLIN somo la 15: ainza za parameter kwenye function
KOTLIN somo la 8: Jinsi ya kutumia when
KOTLIN somo la 3: Jinsi ya kuandika variable
KOTLIN somo la 5: operator na aina zake kwenye Kotlin
HOTLIN somo la 9: Jinsi ya kutumia for loop
KOTLIN somo la 4: Aina za Data kwenye Kotlin
KOTLIN somo la 14: Aina za function kwenye Kotlin
KOTLIN somo la 16:baadhi ya method na properies zinazofanya kazi kwenye string
KOTLIN somo la 18: string na method zinazotumika kwenye list data type.
KOTLIN somo la 13: Jinsi ya kuandika function na kuweka parameter
KOTLIN somo la 11:Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop
Nicheki WhatsApp kwa maswali
Ndio Hapana Save post
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Kotlin
Main: Masomo
File: Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 376
👉1 Kitau cha Fiqh
👉2 kitabu cha Simulizi
👉3 Kitabu cha Afya
👉4 Madrasa kiganjani
👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zifazofanana:-
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement Soma Zaidi...
Katika somo hili tutakwenda kuzungumzia kuhusu parameter kwenye Kotlin function. Pia tutakwenda kuona mambo mengine yanayohusu function Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu when case na jinsi inavyofanya kazi kwenye Kotlin. Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika variable kweye Kotlin. pia utakwenda kujifunza kuhusu concatnation na interpolation Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu operator na aina zake. Soma Zaidi...
Katika somo hli utakwend akujifunza kuhusu loop kwenye kOTLIN. Loop zimegawanyika katika makundi mnne ambayo ni for loop, while loop, for in loop na do while loop. Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data zinazotumika kwenye Kotlin. Soma Zaidi...
Katika somo hili tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye somo la function. Hapa tutakwenda kuona aina za function. Soma Zaidi...
Katika somo hili tutajifunza kuhusu method za String zinazotumika kwenye Kotlin. Soma Zaidi...
Katika somo hili tutajifunza method zinazofanya kazi kwenye list data type kwenye Kotlin. Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function na kuweka parameter kwenye function Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu break na continue kwenye Kotlin loop za for loop na while loop. Soma Zaidi...