Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function na kuweka parameter kwenye function
Function ni nini?
Function ni kifungu cha code (block of code) ambacho hufanya kazi maalumu. Function inaweza kufanya kazi kwa kujirudia rudia bila ya kikomo kila itakapoitwa. Function husaidia kutokurudiarudia kuandika code.
Mambo ya kuzingatia:
Jinsi ya kuandika function
fun name (){
Code
}
Kwanza utaanza keyword fun kisha utaweka jina la hiyo function (name yaani jina la hiyo function), kisha utaweka mabano () ndani ya haya mabano tutakuja kuweka parameter. Kisha utaweka mabano {} ndani ya haya mabano ndipo utaweka code ambazo unataka zifanye kazi. Wacha tuone mifano huwenda ukaelewa zaidi:-
Mfano 1:
Tunatengeneza program ya kuandika neno bongoclass mara 10. Kwanza tuatatengeneza hiyo fnction ambayo ita print nrno bongoclass
fun main() {
fun bongo() {
print("Bongoclass")
}
}
Kisha tutaiita (call) hiyo funcyion kwenye main().
fun main() {
fun bongo() {
print("Bongoclass")
}
bongo()
}
Sasa kama tutaiita mara 10 itaprint hilo neno mara 10
fun main() {
fun bongo() {
println("Bongoclass")
}
for (x in 1..10) {
bongo()
}
}
Jinsi ya kuweka parameter kwenye function
Tuchukulie mfano kama huu wa mwanzo. Tunataka mtumiaji aweze kuandika mwenyewe anataka neno bongoclass litokee mara ngapi. Kwa mfano akitaka litokee mara 6 ataandika 6 kwenye user input kisha function yetu itafanya kazi husika.
Sasa katika hali hiyo tutahitaji kuweka variable ambayo itawakilisha hiyo 6 atakayowekamtu. Hiyo variable ndio parameter kwa mfano tutaiita idadi. Na hiyo namba 6 atakayoinginza mtu huitwa argument. Kwa ufup tunasema parameter ni jina ila argument ni value yenyewe.
Unapoweka parameter zingatia kuweka na aina ya data ambayo hiyo parameter inakwenda kutumia. Kwa mfano kama parameter itabeba namba tunatweka Int kama ni string tutaweka String unaweza kurejea aina za data. Sasa kuweka aina ya data kwana utaana za alama ya (:) kisha utaruka nafasi moja kisha utaandika aina ya data. Angalia hapo chini.
fun main() {
fun bongo(idadi: Int) {
for (x in 0 until idadi) {
println("Bongoclass")
}
}
println("ANDIKA IDADI")
val idadi = readLine()?.toInt()
bongo(idadi !!)
}
Ukicheki hizo code kuna alama ya (!!) hiyo huitwa double-bang operator au not-null operator. Hii hutumika kuieleza kompyuta kuwa hizo data sio tupu yaani notnull. Hivyo kama ni tupu utapata error. Ni vyema kutumia if kutest kama ni null nini kifanyike tofauti na kuleta error.
fun main() {
fun bongo(idadi: Int) {
println("Bongoclass")
}
println("ANDIKA IDADI")
val idadi = readLine()?.toIntOrNull()
if (idadi != null) {
bongo(idadi)
} else {
println("Invalid input. Please enter a valid number.")
}
}
Function yenye parameter zaidi ya moja.
Parameter zinaweza kuwa zaidi ya moja. Wacha tuone mfano mwingine wa kujumlisha namba mbili. Hapa sitatumia user input. Tutaweka wenyewe namba hizo. Kwa mfano tutaweka 5 na 7 ili program izijumlishe. Ikiwa parameter ni zaidi ya moja zote utatenganisha kwa alama ya koma ( , ).
fun jumlisha(x: Int, y: Int) {
println(x + y)
}
fun main() {
jumlisha(5, 6)
}
Ngoja tutengeneze program ya calculator ambapo itakuwa na parameter 3, ya kwanz ani namba ya kwanza, ya pili ni tendo la hesabu na ya tatu ni namba ya tatu.
Kwa kutumia if
fun jumlisha(x: Int, y: String, z: Int): Int {
val result: Int
if (y == "+") {
result = x + z
} else if (y == "-") {
result = x - z
} else if (y == "*") {
result = x * z
} else if (y == "/") {
result = x / z
} else {
println(">...
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu break na continue kwenye Kotlin loop za for loop na while loop.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu nadharia ya package, kazi zake, aina zake na jinsi zinavyotumika
Soma Zaidi...Somo hili linafafanua dhana ya Encapsulation katika OOP, matumizi yake ndani ya Kotlin, pamoja na modifiers mbalimbali (private, protected, internal, public). Pia tutajifunza kwa mifano jinsi encapsulation inavyosaidia kulinda data na kudhibiti ufikivu.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na string kwenye Kotlin.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kuzungumzia kuhusu parameter kwenye Kotlin function. Pia tutakwenda kuona mambo mengine yanayohusu function
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye somo la function. Hapa tutakwenda kuona aina za function.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu method za String zinazotumika kwenye Kotlin.
Soma Zaidi...Katika somo hili unakwenda kujifunza kuhusu sheria na kanuni za undishi wa code za Kotlin yaani syntax za kotlin.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza method zinazofanya kazi kwenye list data type kwenye Kotlin.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuchukuwa user input kwenye Kotlin kwa ajili ya kuongeza user interaction kwenye program.
Soma Zaidi...