image

KOTLIN somo la 13: Jinsi ya kuandika function na kuweka parameter

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function na kuweka parameter kwenye function

Function ni nini?

Function ni kifungu cha code (block of code) ambacho hufanya kazi maalumu. Function inaweza kufanya kazi kwa kujirudia rudia bila ya kikomo kila itakapoitwa. Function husaidia kutokurudiarudia kuandika code.

 

Mambo ya kuzingatia:

  1. Function hutumika zaidi ya mara moja
  2. Function haifanyikazi mpaka iitwe
  3. Function inakuwa na parameter

 

Jinsi ya kuandika function

fun name (){

Code

}

 

Kwanza utaanza keyword fun kisha utaweka jina la hiyo function (name yaani  jina la hiyo function), kisha utaweka mabano () ndani ya haya mabano tutakuja kuweka parameter. Kisha utaweka mabano {} ndani ya haya mabano ndipo utaweka code ambazo unataka zifanye kazi. Wacha tuone mifano huwenda ukaelewa zaidi:-

 

Mfano 1: 

Tunatengeneza program ya kuandika neno bongoclass mara 10. Kwanza tuatatengeneza hiyo fnction ambayo ita print nrno bongoclass

fun main() {

   fun bongo() {

       print("Bongoclass")

   }

}

 

Kisha tutaiita (call) hiyo funcyion kwenye main().

fun main() {

   fun bongo() {

       print("Bongoclass")

   }

   bongo()

}

 

Sasa kama tutaiita mara 10 itaprint hilo neno mara 10

fun main() {

   fun bongo() {

       println("Bongoclass")

   }

   for (x in 1..10) {

       bongo()

   }

}

 

 

Jinsi ya kuweka parameter kwenye function

Tuchukulie mfano kama huu wa mwanzo. Tunataka mtumiaji aweze kuandika mwenyewe anataka neno bongoclass litokee mara ngapi. Kwa mfano akitaka litokee mara 6 ataandika 6 kwenye user input kisha function yetu itafanya kazi husika.

 

Sasa katika hali hiyo tutahitaji kuweka variable ambayo itawakilisha hiyo 6 atakayowekamtu. Hiyo variable ndio parameter kwa mfano tutaiita idadi. Na hiyo namba 6 atakayoinginza mtu huitwa argument. Kwa ufup tunasema parameter ni jina ila argument ni value yenyewe.

 

Unapoweka parameter zingatia kuweka na aina ya data ambayo hiyo parameter inakwenda kutumia. Kwa mfano kama parameter itabeba namba tunatweka Int kama ni string tutaweka String unaweza kurejea aina za data. Sasa kuweka aina ya data kwana utaana za alama ya (:) kisha utaruka nafasi moja kisha utaandika aina ya data. Angalia hapo chini.

 fun main() {

   fun bongo(idadi: Int) {

       for (x in 0 until idadi) {

           println("Bongoclass")

       }

   }

 

   println("ANDIKA IDADI")

   val idadi = readLine()?.toInt()

   bongo(idadi !!)

}


 

 

Ukicheki hizo code kuna alama ya (!!) hiyo huitwa double-bang operator au not-null operator. Hii hutumika kuieleza kompyuta kuwa hizo data sio tupu yaani notnull. Hivyo kama ni tupu utapata error. Ni vyema kutumia if kutest kama ni null nini kifanyike tofauti na kuleta error.

 

fun main() {

   fun bongo(idadi: Int) {

           println("Bongoclass")

   }

 

   println("ANDIKA IDADI")

   val idadi = readLine()?.toIntOrNull()

 

   if (idadi != null) {

       bongo(idadi)

   } else {

       println("Invalid input. Please enter a valid number.")

   }

}

 

 

Function yenye parameter zaidi ya moja.

Parameter zinaweza kuwa zaidi ya moja. Wacha tuone mfano mwingine wa kujumlisha namba mbili. Hapa sitatumia user input. Tutaweka wenyewe namba hizo. Kwa mfano tutaweka 5 na 7 ili program izijumlishe. Ikiwa parameter ni zaidi ya moja zote utatenganisha kwa alama ya koma ( , ).

fun jumlisha(x: Int, y: Int) {

    println(x + y)

}

 

fun main() {

    jumlisha(5, 6)

}

 

 

 

 

Ngoja tutengeneze program ya calculator ambapo itakuwa na parameter 3, ya kwanz ani namba ya kwanza, ya pili ni tendo la hesabu na ya tatu ni namba ya tatu. 

 

Kwa kutumia if

fun jumlisha(x: Int, y: String, z: Int): Int {

   val result: Int

 

   if (y == "+") {

       result = x + z

   } else if (y == "-") {

       result = x - z

   } else if (y == "*") {

       result = x * z

   } else if (y == "/") {

       result = x / z

   } else {

       println("Invalid operator&">...



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 223


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

KOTLIN somo la 10: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Kotlin. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 16:baadhi ya method na properies zinazofanya kazi kwenye string
Katika somo hili tutajifunza kuhusu method za String zinazotumika kwenye Kotlin. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 4: Aina za Data kwenye Kotlin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data zinazotumika kwenye Kotlin. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 1: Historia ya kotlin na kazi zake
Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya Kotlin pamoja na kazi za kotlin. Pia utakwenda kujifunza kuhusu uhusiano wake na java. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 21: Jinsi ta kutengeneza library
Katika somo hili utajifunza kuhusu Kotlin library. Pia tutakwenda kutengeneza library yetu wenyewe kwa ajili ya kufanya mazoezi zaidi. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 17: method na properties za namba
Katika somo hili tutajifunza kuhusu method na properties za Kotlin zinazofanya kazi kwenye namba. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 6: string kwenye Kotlin
Katika somo hili tutakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na string kwenye Kotlin. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 5: operator na aina zake kwenye Kotlin
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu operator na aina zake. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 2: sheria na kanuni za uandishi wa code za Kotlin
Katika somo hili unakwenda kujifunza kuhusu sheria na kanuni za undishi wa code za Kotlin yaani syntax za kotlin. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 3: Jinsi ya kuandika variable
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika variable kweye Kotlin. pia utakwenda kujifunza kuhusu concatnation na interpolation Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 14: Aina za function kwenye Kotlin
Katika somo hili tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye somo la function. Hapa tutakwenda kuona aina za function. Soma Zaidi...

KOTLIN somo la 7: Jinsi ya kutumia If na ifelse kwenye Kotlin
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement Soma Zaidi...