KOTLIN somo la 2: sheria na kanuni za uandishi wa code za Kotlin
Katika somo hili unakwenda kujifunza kuhusu sheria na kanuni za undishi wa code za Kotlin yaani syntax za kotlin.
Somo leu moja kwa moja linakwenda kuanzia kwenye code za hello world. Copi code hizo hapo chini kisha pest kwenye text editor unayotumia.
fun main() {
println("Hello World")
}
1. Kotlin file extension
Format ya faili ya Kotlin ni kt. Mfano faili linaloitwa mafunzo litaandikwa hivi mafunzo.kt .kwa wale ambao mnatumia jetbrain faili lako utaliona kwenye folda linaloitwa kotlin. Angalia upande wa kushoto kuna palipoandikwa scr bofya hapo kisha bofya main kisha bofya kotlin hapo utalikuta faili lako. Kuanzi hapo ndipo tunapoendelea kufanyia mazoezi.
2. Mwanzo wa program
Kama ukiangalia ode hizo hapo juu utaona program yetu imeanza na keyword fun, hii keyword ama hili neno hutumika katika kuandika function. Funnction ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kufanya kazi fulani. Tunajifunza zaidi huko mbele.
Kisha utaona kuna keyword nyingine main() hii ndio function yenyewe. Hii huonyesha mwanzo wa program ya kotlin. Function hii code zake zipo ndani ya {}. Kwa mfano utaona hapo kuna println(“hello world”). Hapo kuna function nyingine ya println() hii hutumika ku print matokeo ya code kwenye screen.
Sasa ili kuona matokeo bofya batani ya kijani iliyofanana na batani ya kuplay mziki, inapatikana kwa juu katikati hii ni kwa wanaotumia kompyuta na software ya jetbrain. Kwa wale wanaotumia simu bofya batani ya ku play ama fuata maelekezo ya App unayotuia. Na kama unatumia online compiler weka code kusha bofya run.
Kisha angalia kwa chini itakuwa inaonyesha kama ina run. Ikimaliza unaona neno hello world kwenye ubao mweusi kwa chini. Huo unao ndio unaitwa console angalia picha hapo chini namba 3. Namba 1 inaonyesha neno java hapa nataka utambuwe kuwa kotlin yenyewe inafanyakazi kwenye java environment na hapo kwenye namba 2 utaona kuna 0. Hiyo inaonyesha kuwa code zime run bila hata ya matatizo.
Kama unatumia software nyingine maelekezo hayo hapo juu unaweza kuwa tofauti.
Katika matoleo ya zamani ya Kotlin ulihitajika kuweka parameter kwenye main function ambapo mfano wa hapo juu utaandikwa hivi
fun main(args : Array<String>) {
println("Hello World")
}
3. String na nmba
String ni mkusanyiko wa herufi, namba, na alama nyinginezo. Mfano mafunzo_55@bongoclass.com . Sasa unapoandika string utatakiwa kutumia alama ya (“) yaani quotation mark ama alama za kunukuu. Hivyo itaandikwa “mafunzo_55@bongoclass.com” kam...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 ai web app 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Kotlin somo la 24: Dhana ya Module katika kotlin
Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu dhana ya module. Hata ivyo tutakwenda kuisoma zaidi kwenye android App
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 20: method na properties za map
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu method ambazo hutumika kwenye map data type
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 16:baadhi ya method na properies zinazofanya kazi kwenye string
Katika somo hili tutajifunza kuhusu method za String zinazotumika kwenye Kotlin.
Soma Zaidi...Kotlin somo la 26: Dhana ya class, object na method kwenye kotlin
Katika soomo hili utakwenda kujifunza kuhusu class, maana yake, na jinsi ya kuitengeneza
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 21: Jinsi ta kutengeneza library
Katika somo hili utajifunza kuhusu Kotlin library. Pia tutakwenda kutengeneza library yetu wenyewe kwa ajili ya kufanya mazoezi zaidi.
Soma Zaidi...Kotlin Somo la 28: Abstraction na Interfaces
Somo hili linaelezea dhana ya abstraction na interfaces katika Kotlin — namna zinavyosaidia kuficha undani wa utekelezaji na kuweka miongozo ya kazi. Tutafahamu tofauti kati ya abstract class na interface, na tutaandika mifano halisi ya kila moja.
Soma Zaidi...