KOTLIN somo la 2: sheria na kanuni za uandishi wa code za Kotlin
Katika somo hili unakwenda kujifunza kuhusu sheria na kanuni za undishi wa code za Kotlin yaani syntax za kotlin.
Somo leu moja kwa moja linakwenda kuanzia kwenye code za hello world. Copi code hizo hapo chini kisha pest kwenye text editor unayotumia.
fun main() {
println("Hello World")
}
1. Kotlin file extension
Format ya faili ya Kotlin ni kt. Mfano faili linaloitwa mafunzo litaandikwa hivi mafunzo.kt .kwa wale ambao mnatumia jetbrain faili lako utaliona kwenye folda linaloitwa kotlin. Angalia upande wa kushoto kuna palipoandikwa scr bofya hapo kisha bofya main kisha bofya kotlin hapo utalikuta faili lako. Kuanzi hapo ndipo tunapoendelea kufanyia mazoezi.
2. Mwanzo wa program
Kama ukiangalia ode hizo hapo juu utaona program yetu imeanza na keyword fun, hii keyword ama hili neno hutumika katika kuandika function. Funnction ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kufanya kazi fulani. Tunajifunza zaidi huko mbele.
Kisha utaona kuna keyword nyingine main() hii ndio function yenyewe. Hii huonyesha mwanzo wa program ya kotlin. Function hii code zake zipo ndani ya {}. Kwa mfano utaona hapo kuna println(“hello world”). Hapo kuna function nyingine ya println() hii hutumika ku print matokeo ya code kwenye screen.
Sasa ili kuona matokeo bofya batani ya kijani iliyofanana na batani ya kuplay mziki, inapatikana kwa juu katikati hii ni kwa wanaotumia kompyuta na software ya jetbrain. Kwa wale wanaotumia simu bofya batani ya ku play ama fuata maelekezo ya App unayotuia. Na kama unatumia online compiler weka code kusha bofya run.
Kisha angalia kwa chini itakuwa inaonyesha kama ina run. Ikimaliza unaona neno hello world kwenye ubao mweusi kwa chini. Huo unao ndio unaitwa console angalia picha hapo chini namba 3. Namba 1 inaonyesha neno java hapa nataka utambuwe kuwa kotlin yenyewe inafanyakazi kwenye java environment na hapo kwenye namba 2 utaona kuna 0. Hiyo inaonyesha kuwa code zime run bila hata ya matatizo.
Kama unatumia software nyingine maelekezo hayo hapo juu unaweza kuwa tofauti.
Katika matoleo ya zamani ya Kotlin ulihitajika kuweka parameter kwenye main function ambapo mfano wa hapo juu utaandikwa hivi
fun main(args : Array<String>) {
println("Hello World")
}
3. String na nmba
String ni mkusanyiko wa herufi, namba, na alama nyinginezo. Mfano mafunzo_55@bongoclass.com . Sasa unapoandika string utatakiwa kutumia alama ya (“) yaani quotation mark ama alama za kunukuu. Hivyo itaandikwa “mafunzo_55@bongoclass.com” kam...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 web hosting 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Kotlin somo la 25: Nadharia ya Object Oriented Programming
Katika somo hili utakwenda kujifunza maana na features za object oriented Programming
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 19: method na properties zinazotumika kwenye set
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu set data type pamoja na method ambazo hufanya kazi kwenye set.
Soma Zaidi...Kotlin Somo la 29: Encapsulation
Somo hili linafafanua dhana ya Encapsulation katika OOP, matumizi yake ndani ya Kotlin, pamoja na modifiers mbalimbali (private, protected, internal, public). Pia tutajifunza kwa mifano jinsi encapsulation inavyosaidia kulinda data na kudhibiti ufikivu.
Soma Zaidi...KOTLIN somo la 1: Historia ya kotlin na kazi zake
Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya Kotlin pamoja na kazi za kotlin. Pia utakwenda kujifunza kuhusu uhusiano wake na java.
Soma Zaidi...HOTLIN somo la 9: Jinsi ya kutumia for loop
Katika somo hli utakwend akujifunza kuhusu loop kwenye kOTLIN. Loop zimegawanyika katika makundi mnne ambayo ni for loop, while loop, for in loop na do while loop.
Soma Zaidi...Kotlin somo la 23: Utofauti wa package na library
Katika somo hili utakwenda kujifunza tofauti wa library na package
Soma Zaidi...