Katika somo hili tutajifunza kuhusu method za String zinazotumika kwenye Kotlin.
Method ni nini?
Method ni kama function, lakini tofauti ni kuwa method zina uhusiano mkubwa na object. Hapa nitakuletea baadhi ya method za String:-
String length
Hii hutumika kujuwa je, string ina herufi ngapi.
fun main() {
val text = "haloo bongoclass"
println(text.length)
}
Hii itakupa jibu 16, kumaanisha hapo kuna herufi (character) 16.
Kubadili herufi kuwa ndogo au kubwa
Kubadilisha kuwa herufi ndogo utatumia toLowerCase na kubadilisha kuwa kubwa utatumia toUpperCase.
fun main() {
val text1 = "haloo bongoclass"
val text2 = "HALOO BONGOCLASS"
println(text1.toUpperCase())
println(text2.toLowerCase())
}
HALOO BONGOCLASS
haloo bongoclass
Kuigawa string kwenye (substring)
Kwa mfano, katika neno "bongoclass," tunataka kuchapisha neno "bongo" tu.
fun main() {
val text = "bongoclass"
println(text.substring(0, 5))
}
bongo
Kuchuja string (contains)
Kwa mfano, unahitaji kuangalia kama neno fulani lipo au halipo kwenye string.
Kama lipo, utapata jibu true, na kama halipo, jibu ni false. Wacha tuangalie je neno "class" lipo kwenye neno "bongoclass"?
fun main() {
val text = "bongoclass"
println(text.contains("class"))
}
true
Kubadili string kuwa list data type (split)
Hapa tutakwenda kuigawa string kwenye mafungu. Kwa mfano, neno "haloo karibu bongo class." Tutagawa kwa kila neno.
fun main(">...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Somo hili linaeleza msingi wa database, kwa nini tunazitumia, aina za database, na utangulizi wa MySQL. Pia tutaona jinsi Kotlin inaweza kuunganishwa na MySQL kwa ajili ya kutekeleza CRUD operations (Create, Read, Update, Delete).
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye somo la function. Hapa tutakwenda kuona aina za function.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Kotlin.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana na features za object oriented Programming
Soma Zaidi...Katika soomo hili utakwenda kujifunza kuhusu class, maana yake, na jinsi ya kuitengeneza
Soma Zaidi...Somo hili linafafanua dhana ya Encapsulation katika OOP, matumizi yake ndani ya Kotlin, pamoja na modifiers mbalimbali (private, protected, internal, public). Pia tutajifunza kwa mifano jinsi encapsulation inavyosaidia kulinda data na kudhibiti ufikivu.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu method na properties za Kotlin zinazofanya kazi kwenye namba.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza tofauti wa library na package
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ambavyo class moja inaweza kuriti method na properties kutoka kwenye class nyingine.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu operator na aina zake.
Soma Zaidi...