Katika somo hili tutajifunza kuhusu method za String zinazotumika kwenye Kotlin.
Method ni nini?
Method ni kama function, lakini tofauti ni kuwa method zina uhusiano mkubwa na object. Hapa nitakuletea baadhi ya method za String:-
String length
Hii hutumika kujuwa je, string ina herufi ngapi.
fun main() {
val text = "haloo bongoclass"
println(text.length)
}
Hii itakupa jibu 16, kumaanisha hapo kuna herufi (character) 16.
Kubadili herufi kuwa ndogo au kubwa
Kubadilisha kuwa herufi ndogo utatumia toLowerCase na kubadilisha kuwa kubwa utatumia toUpperCase.
fun main() {
val text1 = "haloo bongoclass"
val text2 = "HALOO BONGOCLASS"
println(text1.toUpperCase())
println(text2.toLowerCase())
}
HALOO BONGOCLASS
haloo bongoclass
Kuigawa string kwenye (substring)
Kwa mfano, katika neno "bongoclass," tunataka kuchapisha neno "bongo" tu.
fun main() {
val text = "bongoclass"
println(text.substring(0, 5))
}
bongo
Kuchuja string (contains)
Kwa mfano, unahitaji kuangalia kama neno fulani lipo au halipo kwenye string.
Kama lipo, utapata jibu true, na kama halipo, jibu ni false. Wacha tuangalie je neno "class" lipo kwenye neno "bongoclass"?
fun main() {
val text = "bongoclass"
println(text.contains("class"))
}
true
Kubadili string kuwa list data type (split)
Hapa tutakwenda kuigawa string kwenye mafungu. Kwa mfano, neno "haloo karibu bongo class." Tutagawa kwa kila neno.
fun main(">...
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye somo la function. Hapa tutakwenda kuona aina za function.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza kufanya maamuzi kulingana na mashart fulani.ama namna ambavyo program inaweza ku run code zaii ya mara moja kulingana na mashart. Hapa tutazingumzia flow of control statement
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data zinazotumika kwenye Kotlin.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu Kotlin library. Pia tutakwenda kutengeneza library yetu wenyewe kwa ajili ya kufanya mazoezi zaidi.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na string kwenye Kotlin.
Soma Zaidi...Katika soomo hili utakwenda kujifunza kuhusu class, maana yake, na jinsi ya kuitengeneza
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza tofauti wa library na package
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu operator na aina zake.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do while loop zinavyofanya kazi katika Kotlin.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu break na continue kwenye Kotlin loop za for loop na while loop.
Soma Zaidi...