Katika somo hili tutajifunza kuhusu method za String zinazotumika kwenye Kotlin.
Method ni nini?
Method ni kama function, lakini tofauti ni kuwa method zina uhusiano mkubwa na object. Hapa nitakuletea baadhi ya method za String:-
String length
Hii hutumika kujuwa je, string ina herufi ngapi.
fun main() {
val text = "haloo bongoclass"
println(text.length)
}
Hii itakupa jibu 16, kumaanisha hapo kuna herufi (character) 16.
Kubadili herufi kuwa ndogo au kubwa
Kubadilisha kuwa herufi ndogo utatumia toLowerCase na kubadilisha kuwa kubwa utatumia toUpperCase.
fun main() {
val text1 = "haloo bongoclass"
val text2 = "HALOO BONGOCLASS"
println(text1.toUpperCase())
println(text2.toLowerCase())
}
HALOO BONGOCLASS
haloo bongoclass
Kuigawa string kwenye (substring)
Kwa mfano, katika neno "bongoclass," tunataka kuchapisha neno "bongo" tu.
fun main() {
val text = "bongoclass"
println(text.substring(0, 5))
}
bongo
Kuchuja string (contains)
Kwa mfano, unahitaji kuangalia kama neno fulani lipo au halipo kwenye string.
Kama lipo, utapata jibu true, na kama halipo, jibu ni false. Wacha tuangalie je neno "class" lipo kwenye neno "bongoclass"?
fun main() {
val text = "bongoclass"
println(text.contains("class"))
}
true
Kubadili string kuwa list data type (split)
Hapa tutakwenda kuigawa string kwenye mafungu. Kwa mfano, neno "haloo karibu bongo class." Tutagawa kwa kila neno.
fun main(">...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Somo hili linaelezea dhana ya abstraction na interfaces katika Kotlin β namna zinavyosaidia kuficha undani wa utekelezaji na kuweka miongozo ya kazi. Tutafahamu tofauti kati ya abstract class na interface, na tutaandika mifano halisi ya kila moja.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu set data type pamoja na method ambazo hufanya kazi kwenye set.
Soma Zaidi...Somo hili linaeleza dhana ya polymorphism katika OOP ya Kotlinβuwezo wa kutumia method au object moja kufanya kazi tofauti kulingana na muktadha wake. Tutajifunza aina kuu za polymorphism, jinsi ya kuandika code inayotumia override, open, super, pamoja na mifano hai.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu dhana ya module. Hata ivyo tutakwenda kuisoma zaidi kwenye android App
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu Kotlin library. Pia tutakwenda kutengeneza library yetu wenyewe kwa ajili ya kufanya mazoezi zaidi.
Soma Zaidi...Katika somo hli utakwend akujifunza kuhusu loop kwenye kOTLIN. Loop zimegawanyika katika makundi mnne ambayo ni for loop, while loop, for in loop na do while loop.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu operator na aina zake.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu method na properties za Kotlin zinazofanya kazi kwenye namba.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuchukuwa user input kwenye Kotlin kwa ajili ya kuongeza user interaction kwenye program.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na string kwenye Kotlin.
Soma Zaidi...