picha

Kazi ya chanjo ya Surua

Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya Surua kwa watoto, ni Aina ya chanjo ambayo utolewa kwa watoto na kufanya kazi mbalimbali mwilini ambazo ni kumkinga mtoto asipatwe na magonjwa.

Kazi ya chanjo ya Surua.

1. Hii ni chanjo ambayo upewa na watoto Ili kuwakinga na magonjwa mbalimbali kwenye mwili, chanjo hii huwa Iko kwenye mfumo wa poda na uweza kuchanganya Ili iweze kufanya kazi, na wakati wa poda kuchanganya na maji inabidi vyote vinapaswa kutoka kwenye sehemu kiwanda kimoja Ili kuepuka hali ya kuchanganya madawa ambayo yanaweza kuleta madhara makubwa kwa mtoto kwa sababu mtoto mdogo anahitaji uangalizi wa hali ya juu.

 

2. Kama mtoto hasipopota chanjo hii anaweza kuwa na utapiamlo kwa sababu sura usababisha utapiamlo kwa mtoto na makuzi ya mtoto yanakuwa kwa shida kwa hiyo mtoto anakuwa dhaifu hali inayopelekea mtoto kupata magonjwa nyemelezi kama vile upungufu wa damu, kubanwa kifua, kushindwa kupumua hali hii ujitokeza kwa Sababu ya utapiamlo kwa hiyo watoto wanapaswa kupewa chanjo hii Ili waweze kuwa na afya nzuri na pia kuepuka utapiamlo kwa watoto.

 

3. Ugonjwa wa Surua usababisha ubongo wa Mtoto kuwa na matatizo ambapo mtoto anakuwa na matatizo katika kufikilia na hatimaye mtoto anakuwa na upungufu wa akili na anaweza hasieleweke katika jamii na hatimaye kupoteza taiga la kesho, kwa hiyo tunapaswa kuwapatia watoto wetu chanjo ya kuzuia Surua Ili kupunguza watu wasio na akili timamu kwenye jamii na watoto wajisikie vizuri kwenye jamii. Na wazazi wapewe elimu kuhusu kukosa kwa chanjo hiii kwa watoto

 

4. Pengine mtoto hasipopata chanjo hii ya kuzuia Surua anaweza kuwa  bubu au kiziwi na kusababisha madhara mengine ambayo hayakutarajiwa kwa sababu ya hali ya kutojali au kushindwa kumpatia mtoto chanjo akiwa bado mdogo kwa hiyo basi tunapaswa kutimiza wajibu katika kuwashughulikia watoto.

 

5. Pengine mtoto anaweza hasipate chanjo hii ya Surua kwa hiyo mtoto utamtambua kwa dalili zifuatazo kama vile joto la mwili kupanda Mara kwa mara, mtoto anaweza akawa na upele kwenye mwili mzima au sehemu nyingine za mwili, kikohozi ambacho hakikatiki, Macho ya mtoto kuwa mwekundu kwa mda wote, mtoto hasipopata huduma mapema kifo kinaweza kutokea kwa mtoto.kwa hiyo jamii nzima kwa ujumla wanapaswa kuchukua hatua kuhakikisha kuwa watoto wanakata chanjo kwa Sababu magonjwa nyemelezi kwa watoto ni mengi mno.

 

6. Hii chanjo ya Surua inabidi mtoto apewa kwenye miezi tisa naa miezi ya Kumi na nane baada ya mtoto kuzaliwa, kwa hiyo dozi hii utolewa mara mbili tu yaani mwezi wa tisa baada ya kuzaliwa na mwezi wa Kumi na nane baada ya mtoto kuzaliwa kwa hiyo kila mzazi anapaswa kujua hilo na kulitendea kazi .kwa hiyo jamii yote inapaswa kutis maanani chanjo hii Ili kuondoa hali ya kuleta madhara kwenye jamii.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 2657

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 ai web app     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Zijue faida za maji ya uvuguvugu.

Posti hii inahusu zaidi faida za maji ya uvuguvugu, hasa hasa maji haya ni vizuri kabisa kuyatumia hasa wakati wa asubuhi na pia wakati tumbo likiwa halina kitu, kwa hiyo zifuatazo ni faida za maji ya uvuguvugu.

Soma Zaidi...
Aina kuu tatu za mvunjiko wa viuno vya mwilini na mifupa

Posti hii inahusu zaidi Aina kuu tatu za mvunjiko ni Aina za kuvunjika ambazo uwakumba watu mbalimbali na watu ushindwa kutambua hizi Aina tatu za mvunjiko, zifuatazo ni Aina za mvunjiko.

Soma Zaidi...
Upungufu was fati

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu was fati

Soma Zaidi...
Mzunguko wa mwezi kwa mwanamke

Posti hii inahusu zaidi mzunguko wa mwezi kwa mwanamke, ni mzunguko ambao huchukua siku ishilini na nane kwa kawaida Ila lla ubadilika kulingana na mtu, Ila ngoja tuangalie siku ishilini na nane tu.

Soma Zaidi...
Uvimbe kwenye utandu laini uliopo tumboni (peritonitis)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Uvimbe au mashambulizi ya bacteria kwenye utando laini uliopo tumboni ambao kitaalamu hujulikana Kama peritonitis.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa asidi iliyokwenye tumbo( kwa kitaalamu huitwa HCL)

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa asidi iliyo kwenye tumbo kwa kitaalamu huitwa HCL, ni asidi inayofanya kazi nyingi hasa wakati wa kumengenya chakula.

Soma Zaidi...