Navigation Menu



Zijue kazi za chanjo ya DTP au DPT (Donda Koo,Pepopunda, na kifaduro))

Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya DTP au DPT ambayo Inazuia magonjwa ya Donda Koo, Pepopunda na kifaduro.

Kazi ya chanjo ya DTP.

1. Aina hii ya chanjo uzuia Magonjwa mengi miongoni mwao ni kifaduro, Pepopunda na  Dondakoo haya ni baadhi ya magonjwa ambayo uzuiwa na Aina hii ya chanjo, tunaona kwamba hii chanjo Ina nguvu sana hasa kwa watoto kwa hiyo akina Mama na walezi wanapaswa kuhimizwa kuwapeleka watoto kwenye chanjo Ili waweze kuepuka haya magonjwa hatarishi kwa watoto.

 

2. Kwa kuwa hii chanjo ina mchanganyiko na ukinga  magonjwa mbalimbali kama vile Pepopunda ambayo usaidia au kuzuia kukakamaa kwa misuli kwa sababu misuli ikikajamaa usababisha maumivu makali kwa mtoto, kwa hiyo mtoto akipata chanjo ya Pepopunda misuli inakuwa kwenye hali ya kawaida na mtoto anaweza kuishi vizuri tu na kuendelea na maisha yake kama kawaida, kwa hiyo akina Mama na walezi wanapaswa kuwapeleka watoto wao Ili kupata chanjo ya kuzuia Pepopunda Ili kuepuka matatizo kwa mtoto.

 

3. Chanjo hii Inazuia na kifaduro, kwa sababu kifaduro uharibifu mfumo wa hewa  na kusababisha kikohozi kwa mtoto kwa ambacho uchukua wiki nne mpaka nane tunaona hii ni hatari kwa mtoto kupata kikohozi kwa mda mrefu wa Aina hii, kwa hiyo hii chanjo utolewa pia kwa watoto na wachanga na wanawake wenye mimba Ili kuweza kuwakinga dhidi ya matatizo makubwa yanayoweza kujitokeza kama mtoto hajapata chanjo ya namna hii kwa hiyo tunapaswa kuhimiza akina Mama na walezi wahakikishe kuwa watoto wao wanapata chanjo ya Aina hii.

 

4. Pia chanjo hii isipotolewa inaweza kusababisha maambukizi kwenye Koo la hewa na kusababisha mgonjwa hashindwe kupumua na hatimaye na kifo kinaweza kutokea, kwa hiyo ugonjwa huu unaitwa Donda Koo. Kwa hiyo tunapaswa kuwapatia watoto wetu chanjo ya namna hii Ili kuepuka madhara makubwa zaidi.

 

5. Mtoto Upata chanjo hii akiwa na miezi sita baada ya kuzaliwa na baadae kila baada ya wiki nne mpaka pale anapofikisha miezi mitatu, kwa hiyo siku hizi zinapaswa kuzingatiwa kwa akina Mama na kwa walezi wa watoto.

 

6. Kwa sababu hii chanjo utolewa kwa watoto inaweza kuleta matokeo kwa mtoto ambayo yanaweza kumfanya mama akawa na wasiwasi juu ya mtoto kama vile kidonda kidogo kwenye sehemu ambayo wamepitishia dawa, wakati mwingine sehemu hiyo inaweza kuwa nyekundu,au sehemu hiyo inaweza kuvimba kwa hiyo mama inabidi hasiogope Bali ajue ni kawaida kwa mtoto mdogo kuwa hivyo baada ya kupata Aina hii ya chanjo.

 

 

 

 

 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1398


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Huduma ya Kwanza kwa mtu anayetokwa na damu ya pua
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu anayetokwa na damu ya pua Soma Zaidi...

Zijue kazi za ini
Post hii inahusu zaidi kazi za ini, ni kiungo muhimu kwenye mwili ambacho Kina umuhimu sana, bila ini maisha ya mwanadamu yanaweza kuishia pabaya Soma Zaidi...

Uvutaji wa sigara
Somo Hili linakwenda me kuhusu madhara ya uvutaji wa sigara Soma Zaidi...

Dalili za sumu ya pombe
hatari matokeo ya kunywa kiasi kikubwa cha pombe kwa muda mfupi. Kunywa pombe haraka kupita kiasi kunaweza kuathiri kupumua kwako, mapigo ya moyo, halijoto ya mwili na kunaweza kusababisha Coma na kifo. Soma Zaidi...

Njia za kujikinga na vidonda vya tumbo
Kama unahitaji kujuwa namna ya kuweza kujikinga na vidonda vya tumbo, basi makala hii ni kwa ajili yako. Hapa utaweza kuzijuwa hatuwa zote za kujikinga na kupata vidonda vya tumbo. Soma Zaidi...

Jifunze namna ya kutoa huduma ya kwanza
Soma Zaidi...

Namna ya kujikinga na kifua kikuu
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia au kujikinga na kifua kikuu, hizi ni njia ambazo utumika ili kujikinga na kifua kikuu Soma Zaidi...

Mkojo mchafu na Rangi za mikojo na maana zake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Rangi za mkojo na maana zake na mkojo mchafu Soma Zaidi...

Faida za tumbo katika mwili wa binadamu
Posti hii inahusu zaidi faida za tumbo,tumbo ni sehemu ya mwili ambayo ushughilika na kutunza chakula, Soma Zaidi...

Imani potofu juu ya ugonjwa wa Ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi imani potofu juu ya ugonjwa wa Ukimwi,ni Imani walizonazo watu wengi kuhusiana na ugonjwa wa Ukimwi. Soma Zaidi...