picha

Zijue kazi za chanjo ya DTP au DPT (Donda Koo,Pepopunda, na kifaduro))

Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya DTP au DPT ambayo Inazuia magonjwa ya Donda Koo, Pepopunda na kifaduro.

Kazi ya chanjo ya DTP.

1. Aina hii ya chanjo uzuia Magonjwa mengi miongoni mwao ni kifaduro, Pepopunda na  Dondakoo haya ni baadhi ya magonjwa ambayo uzuiwa na Aina hii ya chanjo, tunaona kwamba hii chanjo Ina nguvu sana hasa kwa watoto kwa hiyo akina Mama na walezi wanapaswa kuhimizwa kuwapeleka watoto kwenye chanjo Ili waweze kuepuka haya magonjwa hatarishi kwa watoto.

 

2. Kwa kuwa hii chanjo ina mchanganyiko na ukinga  magonjwa mbalimbali kama vile Pepopunda ambayo usaidia au kuzuia kukakamaa kwa misuli kwa sababu misuli ikikajamaa usababisha maumivu makali kwa mtoto, kwa hiyo mtoto akipata chanjo ya Pepopunda misuli inakuwa kwenye hali ya kawaida na mtoto anaweza kuishi vizuri tu na kuendelea na maisha yake kama kawaida, kwa hiyo akina Mama na walezi wanapaswa kuwapeleka watoto wao Ili kupata chanjo ya kuzuia Pepopunda Ili kuepuka matatizo kwa mtoto.

 

3. Chanjo hii Inazuia na kifaduro, kwa sababu kifaduro uharibifu mfumo wa hewa  na kusababisha kikohozi kwa mtoto kwa ambacho uchukua wiki nne mpaka nane tunaona hii ni hatari kwa mtoto kupata kikohozi kwa mda mrefu wa Aina hii, kwa hiyo hii chanjo utolewa pia kwa watoto na wachanga na wanawake wenye mimba Ili kuweza kuwakinga dhidi ya matatizo makubwa yanayoweza kujitokeza kama mtoto hajapata chanjo ya namna hii kwa hiyo tunapaswa kuhimiza akina Mama na walezi wahakikishe kuwa watoto wao wanapata chanjo ya Aina hii.

 

4. Pia chanjo hii isipotolewa inaweza kusababisha maambukizi kwenye Koo la hewa na kusababisha mgonjwa hashindwe kupumua na hatimaye na kifo kinaweza kutokea, kwa hiyo ugonjwa huu unaitwa Donda Koo. Kwa hiyo tunapaswa kuwapatia watoto wetu chanjo ya namna hii Ili kuepuka madhara makubwa zaidi.

 

5. Mtoto Upata chanjo hii akiwa na miezi sita baada ya kuzaliwa na baadae kila baada ya wiki nne mpaka pale anapofikisha miezi mitatu, kwa hiyo siku hizi zinapaswa kuzingatiwa kwa akina Mama na kwa walezi wa watoto.

 

6. Kwa sababu hii chanjo utolewa kwa watoto inaweza kuleta matokeo kwa mtoto ambayo yanaweza kumfanya mama akawa na wasiwasi juu ya mtoto kama vile kidonda kidogo kwenye sehemu ambayo wamepitishia dawa, wakati mwingine sehemu hiyo inaweza kuwa nyekundu,au sehemu hiyo inaweza kuvimba kwa hiyo mama inabidi hasiogope Bali ajue ni kawaida kwa mtoto mdogo kuwa hivyo baada ya kupata Aina hii ya chanjo.

 

 

 

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 2429

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 ai web app     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Mambo yanayosababisha kupona kwa vidonda.

Posti hii inahusu mambo yanayochangia katika kupona kwa kidonda, ni mambo ambayo yapo kwa mgonjwa mwenyewe kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu michubuko kwa watoto wakati wa kuzaliwa

Post hii inahusu zaidi michubuko ambayo mara nyingi utokea kwa watoto wakati wa kuzaliwa,na mara nyingi uweza kupona baada ya masaa ishilini na manne au ndani ya masaa ishilini na manne.

Soma Zaidi...
Ntajilinda vipi na magonjwa ya meno

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujilinda na magonjwa ya meno

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyekunywa sumu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyekunywa sumu

Soma Zaidi...
Madhara ya chakula kutosagwa vizuri tumboni.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya chakula kushindwa kumengenywa vizuri tumboni, haya ni madhara ambayo utokea kwa sababu ya chakula kushindwa kumengenywa vizuri tumboni.

Soma Zaidi...
Upungufu wa vitamin

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vitamin

Soma Zaidi...