picha

Zijue kazi za chanjo ya DTP au DPT (Donda Koo,Pepopunda, na kifaduro))

Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya DTP au DPT ambayo Inazuia magonjwa ya Donda Koo, Pepopunda na kifaduro.

Kazi ya chanjo ya DTP.

1. Aina hii ya chanjo uzuia Magonjwa mengi miongoni mwao ni kifaduro, Pepopunda na  Dondakoo haya ni baadhi ya magonjwa ambayo uzuiwa na Aina hii ya chanjo, tunaona kwamba hii chanjo Ina nguvu sana hasa kwa watoto kwa hiyo akina Mama na walezi wanapaswa kuhimizwa kuwapeleka watoto kwenye chanjo Ili waweze kuepuka haya magonjwa hatarishi kwa watoto.

 

2. Kwa kuwa hii chanjo ina mchanganyiko na ukinga  magonjwa mbalimbali kama vile Pepopunda ambayo usaidia au kuzuia kukakamaa kwa misuli kwa sababu misuli ikikajamaa usababisha maumivu makali kwa mtoto, kwa hiyo mtoto akipata chanjo ya Pepopunda misuli inakuwa kwenye hali ya kawaida na mtoto anaweza kuishi vizuri tu na kuendelea na maisha yake kama kawaida, kwa hiyo akina Mama na walezi wanapaswa kuwapeleka watoto wao Ili kupata chanjo ya kuzuia Pepopunda Ili kuepuka matatizo kwa mtoto.

 

3. Chanjo hii Inazuia na kifaduro, kwa sababu kifaduro uharibifu mfumo wa hewa  na kusababisha kikohozi kwa mtoto kwa ambacho uchukua wiki nne mpaka nane tunaona hii ni hatari kwa mtoto kupata kikohozi kwa mda mrefu wa Aina hii, kwa hiyo hii chanjo utolewa pia kwa watoto na wachanga na wanawake wenye mimba Ili kuweza kuwakinga dhidi ya matatizo makubwa yanayoweza kujitokeza kama mtoto hajapata chanjo ya namna hii kwa hiyo tunapaswa kuhimiza akina Mama na walezi wahakikishe kuwa watoto wao wanapata chanjo ya Aina hii.

 

4. Pia chanjo hii isipotolewa inaweza kusababisha maambukizi kwenye Koo la hewa na kusababisha mgonjwa hashindwe kupumua na hatimaye na kifo kinaweza kutokea, kwa hiyo ugonjwa huu unaitwa Donda Koo. Kwa hiyo tunapaswa kuwapatia watoto wetu chanjo ya namna hii Ili kuepuka madhara makubwa zaidi.

 

5. Mtoto Upata chanjo hii akiwa na miezi sita baada ya kuzaliwa na baadae kila baada ya wiki nne mpaka pale anapofikisha miezi mitatu, kwa hiyo siku hizi zinapaswa kuzingatiwa kwa akina Mama na kwa walezi wa watoto.

 

6. Kwa sababu hii chanjo utolewa kwa watoto inaweza kuleta matokeo kwa mtoto ambayo yanaweza kumfanya mama akawa na wasiwasi juu ya mtoto kama vile kidonda kidogo kwenye sehemu ambayo wamepitishia dawa, wakati mwingine sehemu hiyo inaweza kuwa nyekundu,au sehemu hiyo inaweza kuvimba kwa hiyo mama inabidi hasiogope Bali ajue ni kawaida kwa mtoto mdogo kuwa hivyo baada ya kupata Aina hii ya chanjo.

 

 

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 2110

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 web hosting    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyezimia

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyezimia

Soma Zaidi...
Dalili za shambulio la hofu

Shambulio la hofu ni tukio la ghafla la hofu kali ambayo husababisha athari kali za kimwili wakati hakuna hatari halisi au sababu inayoonekana. Mashambulizi ya hofu yanaweza kuwa ya kutisha sana. Mashambulizi ya hofu yanapotokea, unaweza kufikiri kwamba

Soma Zaidi...
Faida za kusafisha vidonda.

Posti hii inahusu zaidi faida za kusafisha vidonda, ni faida ambazo Mgonjwa mwenye vidonge uzipata kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa asidi iliyokwenye tumbo( kwa kitaalamu huitwa HCL)

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa asidi iliyo kwenye tumbo kwa kitaalamu huitwa HCL, ni asidi inayofanya kazi nyingi hasa wakati wa kumengenya chakula.

Soma Zaidi...
Sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa

Posti hii inahusu zaidi sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa, Mgonjwa akiwa anaumwa na pia anakula chakula ni lazima asafishwe kinywa Ili kuweza kuepuka madhara mengine yanayoweza kujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kinywani.

Soma Zaidi...
Nini husababisha kibofu cha mkojo kuuma na baadae kutoka damu

Katika post hii utajifunza sababu zinazowezabkuorlekea kibofu kuuma upande mmoja

Soma Zaidi...
Makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika

Post hii inahusu zaidi umuhimu wa makundi manne ya damu na jinsi yanavyotumika, Ni magroup manne ya damu ambayo husaidia kuongeza damu kwa mtu ambaye amepungukiwa damu

Soma Zaidi...
Namna ya kumwosha Mgonjwa vidonda

Posti hii inahusu zaidi njia za kutumia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda, ni njia muhimu ambazo ni lazima kuzipitia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda.

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia ugonjwa wa kipindupindu,

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kipindupindu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria kwa kitaalamu huitwa vibrio cholera.

Soma Zaidi...
Utaratibu wa maisha kwa aliye athirika

Somo hili linakwenda kukuletea utaratibu wa maisha kwa aliye athirika

Soma Zaidi...