picha

JAVASCRIPT - somo la 15: Jinsi ya kukusanya user input

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu user input. Somo hili litaangalia html form na attribute zake na jinsi zinavyohusiana na user input. Mwisho wa somo hili utaweza kutengeneza simple Calculator kwa kutumia javascript.

User input ni nini? 

Tunasema user input tunaangalia taarifa ambazo mtumiaji ataziinguza kwenye system kwa ajili ya kukamilisha ufanyajivwakazi ama kwa ajili ya kuoatavout put fulani. 

 

Hivyo basi hapa tunazungumzia user interaction yaani muingiliano wake na hiyo system. 

 

Mfano wa uzee input ni kama unapojisajili,  ama unapojaza madodoso kwenye mitandao. Hata unapoandika meseji ama unapo upload faili hizo zote ni user input. 

 

Njia ambazo mtumiaji ataweka input kwenye javascript program. 

Zipo njia kadhaa ambazo utatumia ili kuweka input kwenye javascript program. Kwa mfano: -

  1. Kwa kutumia prompt() function

  2. Kwa kutumia html form

  3. Kwa kutumia batani

Katika somo hili tutakwenda kuzitumia njia zote hizo tatu. 

 

  1. Kwa kutumia prompt()

Hii ni javascript finction ambayo hutumika pale ambapo mtumiaji anatakiwa kuweka input. 

 

Function hii inabeba parameta 2 ambazo ni,  string na default. Kwenye string mtumiaji atajaza hicho anachotakiwa kujaza. Sasa unaweza kuweka defaul yaani unaijaza kwanza. Ili endapo mtumiaji hatajaza basi value ulizojaza wewe zitumike. 

 

Hiyo string hapo hutumika kama ile placeholder kwenye html form. Hapo unaweza kuandika je ni nini mtumiaje ajaze. 

 

Hiyo parameter ya default sio ya lazima. Inamaana unaweza kuiwacha .

 

Mfano 1:

<script>

  let h = prompt("Jina");

  document.write("Haloo"+ " "+ h);

</script>

Hapo sijatumia default. Sasa wacha tuone jinsi default inavyifanya kazi. Kwenye default mtumiaji atakuta tayari pameshajazwa hivyo ataamuwa abadili aweke majibu yake ama aache hivyo hivyo. 

 

 Mfano 2:

<script>

  let h = prompt("Jina", "Bongoclass");

  document.write("Haloo"+ " "+ h);

</script>

Kwa kutumia prompt pia tunaweza kufanya mahesabu. Kwa mfano tunaweza kutumia function ya eval() tulisha jifunza hapo awali. Unaweza kuingiza hesabu na kukupatia majibu. 

 

Mfano 3:

<script>

  let namba = prompt("weka hesabu");

  document.write("Jibu ni:-"+ " "+ eval(namba));

</script>

Sasa endapo mtumiaji hatajaza kitu basibitakupa majibu indefined. Angalia mfano hapo chini

 

Mfano 4: 

 

Kwa ufupi hivyo ndivyo tunavyoweza kuingiza usiwe input kwa kutumia javascript. Baada ya hapo utaweza kuzifanyia kazi hizo input kwa namna unavyotaka.

 

2.Kwa kutumia batani

Batani inaweza kutumika ku input data kwenye element za html. Kwa mfano kwenye paragraph, kwenye section element kama div, na kwenye textarea na zaidi ya hapo. 

 

Ili kuweza kupata data zilizopo kwenye batani tutatumia finction ndani ya batani. Kisha tutapata thamani ama input kwa kutumia .value ili kupata id ya hiyo batani tutatumia .id na ili kupata name attribute tutatumia .name na kujua type ya hiyo batani utatumia .type.  Wacha tuone mifano. 

 

Katika mfano wa hapo chini. Nimeweka maneno haloo Bongoclass kwenye batani kama value. Sasa tunataka kuyaingiza maneno hayo kwenye textarea element. Hivyo basi kwanza tutatengeneza function ya ambayo tutakwenda kwenye onclick event. Function yetu tutaiita myFunc. Kisha tutatengeneza variable kwa ajili ya kuwakilisha value yetu. 

 

Mfano 5:

<title>User input</title>

<textarea id="demo" name="txt"></textarea>

<br><button id="btn" name="myBtn" onclick="myFnc()" value="Haloo Bongoclass" type="submit">Bofya</button>

 

<script>

  function myFnc(){

    var btnId = document.getElementById("btn").value;

    

    document.getElementById("demo").innerHTML = btnId;

  }

</script>

 

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-20 Topic: JavaScript Main: ICT File: Download PDF Views 889

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 web hosting    👉3 ai web app    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 16: Jinsi ya kutumia html form kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku dili na html form kwenye javascript. Javascript inaweza kufanya mengi kwenye html form.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 13: Function zinazofanya kazi kwenye array.

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array pamoja na method zinazohusiana na array. Pia nitakujuza tena kuhusu array ni nini. Utajifunza pia jinsi ya kutengeneza array.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 11: function maalumu zinazotumika kwenye string yaani string method

Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function maaumu zinazotumika kwenye string yaani string method.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 5: Jinsi ya kupangilia maandishi wakati wa ku output kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa maandishi (text) wakati wa ku out put matokeo ya code

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 18: Jinsi ya kutumia switch case kwenye javascript

Kwa kutumia mfano huu na iliyotangulia unaweza kuweka masharti kadiri uwezavyo. Tukutane somo linalofuata tutajifunza kuhusu switch statement.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 4: Jinsi ya kuandika variable kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika variable. Hapa utajifunza sheria zinazohusu variable katika javascript

Soma Zaidi...
Game 2: Jinsi ya kutengeneza tic toc game ya single player kwa kutumia javascript, html na css

Katika post hii utakwenda kujifunza kutengeneza game ya tic toc ya mchezaji mmoja na kompyuta yaani single player

Soma Zaidi...