JAVASCRIPT - somo la 3: sheria za uandishi wa code za javascript yaani syntax za javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria ama syntax za kuandika javascript. Hii itakuwezesha kuelwa zaidi code za javascript.
Katika somo hili utajifunza kanuni za kuandika code za javascript ama javascript statement.Lamda kwanza nianze kukujuza maana ya hili neno statement. Ni kuwa kwenye program ya kikompyuta kuna code amabazo ni maelekezo ambayo kompyuta hupewa ili kufanya jambo fulani. Sasa hizi code ama haya maelekezo ndio huitwa statement.
Katika somo hili utajifunza kanuni za kuandika hizi statement. Kanuni hizi zitaweza kukuongoza kwa ufupi uweze kugunduwa kama kwenye code zako kuna tatizo. Na kama lipo nini kimesababisha. Hivyo tutajifunza syntax ya javascript.
Kabla hujasonga mbele zaidi na somo hili, nikujuze kuwa javascript statement inaweza kuwa na vitu hivi Values, Operators, Expressions, Keywords, na Comments. Value ni thamani ambazo zinaweza kuwa ni thamani za variable, operator ni alama za kihesabu kama + kumaanisha jumlisha, Expression ni mkusanyiko wa variable, value na operator, na comment hapa ni sehemu ambayo programmer ama mtu anayeandika hizo code kuweka kumbukumbu zake, ili baadaye aweze kukumbuka.
Kanuni za kuandika javascript:
-
Matumizi ya semicolon (;)
Weka alama hii ya semicoloni mwishoni mwa ststement yako. kwa mfano:
Mfano: 1
<!DOCTYPE html>
<html>
<body>
<p id="demo"></p>
<script>
let x, y, z;
x = 5;
y = 6;
z = x + y;
document.getElementById("demo").innerHTML =
"The value of z is " + z + ".";
</script>
</body>
</html>
Hapo juu utaona mwishoni mwa kila msitari kuna alama ya semicolon. Pia unaweza kuunganisha statement nyingi katika msitari mmoja na kutenganisha kwa semicoloni.
Mfano 2
<!DOCTYPE html>
<html>
<body>
<p id="demo"></p>
<script>
let x, y, z; x = 5; y = 6; z = x + y; document.getElementById("demo").innerHTML = "The value of z is " + z + ".";
</script>
</body>
</html>
Matokeo ya statement ya kwanza, na ya pili ni sawa, ijapokuwa hii ya pili ina mistari kidogo ya code, ni kwa saabu imeunganishwa pamoja na kutengenishwa kwa alama ya semicolon kwa kila statement.
-
Kuruka nafasi wakati wa uandishi (White Space):
Ni kuwa wakati unaandika huwa tunaruka nafasi, huwenda zikawa nyingi ama moja. Sasa katika javascript nafasi ambayo itahisabika kwenye code ni moja tu, hizo ambazo umeongeza javascript hazita zitambuwa na hasita athiri matokeo ya code zako.
Hivyo unaweza kuruka nafasi kadiri uwezavyo, ili kuweza kuboresha muonekano wa code zako. Angalia mifano ya code hizo hapo chini majibu yake ni sawa.
Mfano 3
<!DOCTYPE html>
<html>
<body>
<p id="demo"></p>
<script>
document.getElementById("demo").innerHTML = "haloo javascript";
</script>
</body>
</html>
Mfano wa 4
<!DOCTYPE html>
<html>
<body>
<p id="demo"></p>
<script>
document.getElementById ("demo"). innerHTML = "haloo javascript";
</script>
</body>
</html>
-
Urefu wa msitari wa code
urefu wa msitari wa code hauwezi kuathiri matokeo ya code. Hata hivyo inashauriwa usizindi character 80. Inashauriwa pia kupunguza urefu wa msitari wa code kwa kuukata msitari (line break) baada ya semicoloni (;) kama ilivyo kwenye mfano wa kwanza huko juu.
-
Uandishi wa code block
Hiki ni kifungu ch...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 web hosting 👉3 ai web app 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 21: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop
Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 6: Jinsi ya kufanya mahesabu kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 20 Jinsi ya kutumia foOfloop kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia forOfLoop. Hii ni aina ya loop ambayo yenyewe inahusisha item zote kwenye array.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT -somo la 1: Kwa nini ni muhimu kujifunza javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya javacsript pamoja na kazi za javascript. Pia utayajuwa makampuni makubwa yanayotumia javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.
Soma Zaidi...