Katika somo hili utakwenda kujifunza baadhi ya function maaumu zinazotumika kwenye string yaani string method.
Katika somo hili utajifunza kutumia method (function) kwenye string. Tulisha jifunza kwenye aina za data kuhusu string. Hapa tutakwenda kuangalia zaidi jinsi ya kuitumia string.
Tulipokuwa tunasoma object nilikueleza kuwa object ni variable. Katika javascript karibia variable zote utakazozitengeneza zinaweza kuwa ni object. Kwa mfano var web ="bongoclass". katika mfano huu variable web hapo ni object. Hivyo variable yetu itakuwa tayari kupokea method mbalimbali zinazohusu string object.
Kujuwa idadi ya character
Kujuwa idadi ya maneno tutatumia lenth kama built in property ya string. kwabnfano katika variable yetu web hapo tutasema web.length kumaanisha kuwa variable web ni object name na length ni object property ambayo value yake nibidadi ya character.
Ukihesabu neno Bongoclass utapata kuwa lina idadi yabherufi 10. Hivyo hiyo 10 itakuwa ndio property value.
<script>
var web="Bongoclass";
document.write(web.length)
</script>
Ku retrive string
Ku retrive string ni sawa na kusema kujuwa kila character ipo nafasi gani kwenye hiyo string. Na kumbuka kuwa kuhesabu tunaanza kwenye 0. Mfano kwenye string yetu Bongoclass tunataka kuangalia je character namba 4 inawakilisha herufi gani kwenye hiyovstrong?
<script>
var web="Bongoclass";
document.write(web[4])
</script>
Kujuwa nafasi ya neno
Hapa tunataka kujuwa je neno hili kwa mara ya kwanza limetokea kwenye nafasi ya ngapi. Yaani unapita character ngapi kutoka mwanzo wa string mpaka kulikuta hilo neno kwa mara ya kwanza.
Chukulia mfano wa hii string "Haloo karibu Bongoclass upate kujifunza bure, karibu sana" sasa hapa tunataka kujuwa neno karibu kwa mara ya kwanza limeonekana kuanzia character ya ngapi. Kama utahesabu hapo utaona neno karibu kwa mara ya kwanza linapatikana kuanzia character ya 6. Endapo hilo neno halijatokea utapata jibu -1.
<script>
var web="Haloo karibu Bongoclass upate kujifunza bure, karibu sana";
document.write(web.indexOf("karibu"))
</script>
Sasa endapo unataka kujuwa nafasi ya hilo neno lililotokea mara ya mwisho hapa tutatumia lastIndexOf hii ni method ambayo itatupa majibu tunayoyataka. Angalia hiyo string yetu hapo juu neno karibu limejitokeza mara mbili. Sasa tunataka tujuwe hiyo ya mwisho limejitokeza katika nafasi ha ngapi.
<script>
var web="Haloo karibu Bongoclass upate kujifunza bure, karibu sana";
document.write(web.lastIndexOf("karibu"))
</script>
Utaona hapo jibu ni 46, inamaana kuwa kwa mara ya mwisho neno karibu limejitokeza kuanzia character ya 46.
Katika indexOf na lastIndexOf hizi huangalia neno kama lilivyo yaani KaRibu na karibu ni maneno mawili tofauti. Hivyo kama hayatafanana haiwezi kukupa majibu. Sasa endapo utahitaji kutafuta neno bila kujali uandishi kama limechanganja herufi lakjni linasomeka sawa hapa tunatumia method ya search()
Mfano we.search("karibu") hii ni sawa na hizo method mbili tulojifunza kwani majibu yake ni sawa. Sasa angalia string hii "Haloo KariBu Bongoclass upate kujifunza bure, karibu sana." utaona hapo neno KariBU lipo mwanzo na neno karibu lipo mwisho.
<script>
var web="Haloo KariBu Bongoclass upate kujifunza bure, karibu sana.";
document.write(web.search("karibu"))
</script>
Utaona hapo umepata jibu 47 kwa maana karibu ya kwanza imeonekana haipo sawa na neno lililopo kwenye method yetu. Ili kufanya karibu ya kwanza itambulike tutatumia alama za back lash yaani /. Mfano search(/karibu/i) kisha tutaweka i kumaanisha insensitivity higyobkuifanya isijali uandishi ila izingatie kuwa neno linasomeka sawa.
<script>
var web="Haloo KariBu Bongoclass upate kujifunza bure, karibu sana.";
document.write(web.search(/karibu/i))
</script>
Tofauti kuu iliyopo kati ya indexOf na lastIndexOf na search ni kuwa hii ya search inakubali matumizi yavregular expression. Regular expression ni javascript expression ambayo inakuwa na paten maalumu. Inaweza kuwa na special character, herufi, namba, symbol na space character.
Kunyofoa maneno
Hapa tutakwenda kujifunza namna ya kunyofoa maneno kwenye string ka namna tunavyotaka.
Kwa mfano una string hii hapa "Bonhoclass ni tovuti inayokua fursa ya kujifunza elimu ya TEHEMA" sasa tunataka kunyofoa herufi kuanzia character ya 13 hadi ya 20 ili tupate nono jipya ambalo litatengenezwa kupitia character hizo.
Kufanya hivyo tutatumia method inayoitwa slice(). Itakachofanya hapo ni kukusanya hizo character na kupata neno moja. Kwa mujibubwa character yetu hapo tutapata tovuti
<script>
var web="Bonhoclass ni tovuti inayokua fursa ya kujifunza elimu ya TEHEMA";
document.write(web.slice(13, 20))
</script>
Pia method ya slice inaweza kuchukuwa negative hivyo kuanza kuhesabu kutoka mwisho kujabmwanzo. Kwa mfano hapo kwenye string yetu neno tovuti tutalipata kwenye -50 hadi -44 kama ukihesabu kutoka mwisho.
<script>
var web="Bonhoclass ni tovuti inayokua fursa ya kujifunza elimu ya TEHEMA";
document.write(web.slice(-50, -44))
</script>
...
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowKatika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu condition statemant. Darasa hili ni moja katika madarasa muhimu programming. Katika somo hili tutajifunza kwa vitendo zaidi. Tutatumia mifano ya somo lililo tangulia.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za data ambazo hutumika kwenye javascript
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu matendo ya hesabu ambayo ni kugawanya, kujumlisha, kuzidisha na kutoa
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kutumia javascript kutengeneza kikokotoo cha hesabu yaani calculator
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunz kuhusu baadhi ya function ambazo hutumika kwenye namba
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa maandishi (text) wakati wa ku out put matokeo ya code
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria ama syntax za kuandika javascript. Hii itakuwezesha kuelwa zaidi code za javascript.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya javacsript pamoja na kazi za javascript. Pia utayajuwa makampuni makubwa yanayotumia javascript.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.
Soma Zaidi...