JAVASCRIPT - somo la 12: Function zinazotumika kwenye namba

Katika somo hili utajifunz kuhusu baadhi ya function ambazo hutumika kwenye namba

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu method ambazo hutumika kwenye namba na mahesabu yaani Math property na Number property. Kama ambavyo somo lililotangulia ulijifunza method zinazofanya kazi kwenye string. 

 

 

isInteger()

Hii hutumika katika kuthibitisha kama hiyo taarifa ni namba ama sio namba. Kama itakuwa ni namba itakupa jibu true na kama sio namba itakupa jibu la false

 

<script>

  var a=3, b="haloo";

document.write(Number.isInteger(a) +"<br>");

  document.write(Number.isInteger(b))

</script>

 

Utaona hapo variable a ni namba hivyo imekuja true na hiyo variable b imeleta false kwa kuwa sio namba.

 

 

isNaN()

Hii hutumika huthibitisha kuwa hiyo taarifa ilioingizwa sio namba. Huleta majibu ya true kama sio namba na false kama ni namba. 

<script>

  var a=3, b="haloo";

  document.write(isNaN(a) +"<br>");

  document.write(isNaN(b))

</script>

 

 

parseInt()

Hii hutumika kuchukuwa namba kutoka kwenye data iliyoingizwa. Kwa mfano unahitaji mtu aingize mwaka wake wa kuzaliwa kwenye program ambayo inauliza umri. Sasa unakuta ameandika hivi 26 ndio miaka yangu wakati alichotakiwa kuandika ni 26 tu. Hivyo Method hii itanyakuwa hiyo 26 na kuacha hizo zisizo husika. 

 

Medhod hii itachukuwa namba yeyote itakayokuwa mwanza. Kwa mfano ameandika 4 miezi na miaka 26 hapa itakayichukuliwa ni hiyo 4 hivyo program itatambuwa kuwa ana miaka 4.

 

Pia endapo ataandika hivi miaka 26 program haitatambuwa kitu. Kwa kuwa yenyewe inachukuwa character ya kwanza hivyo itakupa jibu NaN Angalia mfano hapo chini nimekuekea mitindo yotebhiyo. 

 

<script>

 

document.write(parseInt("26 ndio maka yangu")+"<br>");

  document.write(parseInt("4 miezi nabmiaka 26")+"<br>");

  document.write(parseInt("miaka yangu ni 26"))

</script>

 

parse    Float()

Hii hutumika kuchukuwa namba zenye viwango vya desimali kutoka kwenye string. Inafanana na hiyo ya hapo juu parseInt kuwa huchukuwa character ya kwanza, na huketa NaN kama imeanza na hefuri.

<script>

 

  document.write(parseFloat("56.6 kg")+"<br>");

  document.write(parseFloat("4.7 cm na futi 5")+"<br>");

  document.write(parseFloat("kilogram thelathini"))

</script>

 

toFixed()

Hii hutumika katika kukadiria viwango maalumu kwenye desimali. Kwa mfano namba hii 2.63698 tunataka kuiandika kwenye viwango viwili vya desimali hivyo itakuwa 2.64 utaona hapo imekuwa 4 baada ya kuikadiria na endapo tutaiandika kwenye kiwango kimoja itakuwa 2.6 kufanya hivi utatumia toFixed()

 

<script>

  var a=0.63698, b=2.63698, c=2.47290;

  document.write(a.toFixed(0) +"<br>");

  document.write(b.toFixed(1) +"<br>");

  document.write(c.toFixed(2))

</script>

 

toExponential()

Hii hutumika kubadili namba iliyo katika viwango vya desimali kwa katika exponent. Hivyo kuiandika namba ki sayansi zaidi. 

 

<script>

  var a=32.63698, b=2.63698, c=2432.47290;

  document.write(a.toExponential(1) +"<br>");

  document.write(b.toExponential(2) +"<br>");

  document.write(c.toExponential(3))

</script>

 

 

toString()

Hii hutumika katika kubadili namba kuwa string. Kwa mfano ukiweka namba hii 24 program itatambuwa hii namba kama string hivyo itaichakata hii namba kama "24" kisha kuirudisha matokeo yake kama 24 ila utofauti ni kuwa hatambuliki tena kuwa ni namba ila ni string .

 

<script>

  var a=32, b=24, c=243;

  document.write(a.toString()+"<br>");

  document.write(b.toString()+"<br>");

  document.write(c.toString())

</script>

 

 

ceil()

Hii hutumika katika kukadiria viwango vya desimali round up kwa maana kuwa bila kujali kwamba ni kubwa kuliko 5 yenyewe itaongeza moja kwenye namba husika. 

<script>

   document.write(Math.ceil(3.76353)+"<br>");

  document.write(Math.ceil(1.239)+"<br>");

  document.write(Math.ceil(0.13))

</script>

Katika matumizi ya kawaida chukulia kuwa unakokotoa ni watu wangapi wanaweza kupita kwenye daraja husika kwa wakati mmoja. Sasa unapata jibu kuwa ni watu 2.3 kiuhalisia hapo inamaana watu 2 na kidogo. Sasa ni vyema kitaalamu useme ni watu watatu ndio wanapita hapo.  Hivyo tunapuuzia desimali zilizopo na kuweka 3. Ina maana kuwa hatuna shaka kabisa kuwa watu watatu watapita. 

 

floor()

Hii hutumika kukadiria namba kwa kupuuza viwango vyote vya desimali vilivyopo na kulibakisha nmab yenyewe. Kwa mfano 6.9 hii itasomeka 6 bila kujali viwango vya desimali. Hii ndio kitaalamu huitwa roun down

<script>

  document.write(Math.floor(3.76353)+"<br>");

  document.write(Math.floor(1.239)+"<br>");

  document.write(Math.floor(0.13))

</script>

 

Katika matumizi ya kawaida mfano unataka kulipa wafanyakazi lakini katika mahesabu yako mfanyakazi atatakiwa kulipwa Tsh 424900.28 hivyo hapa tutatumia floor na kuondoa hizo .28 na kwa mahesabu haya mfanyakazi atapokea 424900

 

round()

Hii sasa ndio ile n">...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: JavaScript Main: ICT File: Download PDF Views 484

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

JAVASCRIPT - somo la 5: Jinsi ya kupangilia maandishi wakati wa ku output kwenye javascript

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa maandishi (text) wakati wa ku out put matokeo ya code

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 9: Jinsi ya kuandika function kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 23: Jinsi ya kutengeneza calculator yaani kikokotoo cha hesabu kwa kutumia javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kutumia javascript kutengeneza kikokotoo cha hesabu yaani calculator

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 15: Jinsi ya kukusanya user input

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu user input. Somo hili litaangalia html form na attribute zake na jinsi zinavyohusiana na user input. Mwisho wa somo hili utaweza kutengeneza simple Calculator kwa kutumia javascript.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 22: Jinsi ya ku set time na tarehe

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu ku set time. Yaani tutaweka muda ambao code zinatakiwa ndio zilete matokeo.

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 19: Jinsi ya kutumia loop kwenye javascript

Katika somo hilibtutakwenda kujifunza kuhusu loop. Katika programming tunaposema loop tunamaanisha ile hali ya program ku excute code zaidi na zaidi. Tofauti na kurudia rudia kuandika statement moja kwa ajili ya kupata matokeoa hayohayo basi unapotumia lo

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 21: Jinsi ya kutumia while loop na do while loop

Katika somo hili tutakwenda kujifunza khusu while loop na do while loop.

Soma Zaidi...
Game 1: Jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawili kwa kutumia html, css na javascript

Katika post hii utakwenda kujifundisha jinsi ya kutengeneza game ya tic toc ya wachezaji wawii kwa utumia html, css na javascript

Soma Zaidi...
JAVASCRIPT - somo la 16: Jinsi ya kutumia html form kwenye javascript

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku dili na html form kwenye javascript. Javascript inaweza kufanya mengi kwenye html form.

Soma Zaidi...