JAVASCRIPT - somo la 17: condition statement za if else, else if kwenye javascript
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu condition statemant. Darasa hili ni moja katika madarasa muhimu programming. Katika somo hili tutajifunza kwa vitendo zaidi. Tutatumia mifano ya somo lililo tangulia.
Ili uelewe vyema somo hili soma kwanza habari hii. Umetakiwa kusajili wanafunzi katika darasa la kwanza. Sharti mwanafunzi awe na umri kati ya miaka 6 hadi 8. Program itasema umefanikiwa kumsajili mwanafunzi Endapo mwanafunzi atakuwa na umri wa miaka chini ya 6 program inatakiwa iseme anatakiwa kurudi darasa la chekechea na endapo umri utakuwa zaidi ya miaka 8 basi program imwambie anatakiwa asome memkwa . Darasa letu litakuwa linachezea kwenye habari hiyo.
Condition statement ni nini?
Neno statement ni neno la kiingereza lenye maana maelezo na neno condition lina maana ya masharti. Hivyo kwa ujumla tunasema kuwa condition statement ni maelekezo ambayo yanakuwa na masharti. Maelekezo haya yanaweza kubeba pande mbili pande yabkwanza itabeba maelezo na pande ya lili itatupa matokeo.
Mfano: "endapo umri ea mtoto ni miaka 5". Haya ni maelekezo na matokeo yake anatakiwa kurudi darasa la chekechea. Hivyo shart hapa la kusajiliwa ni kuwa na umri kuanzia miaka 6.
Aina za condition statement:
Condition statement zipo katika aina kuu 3 ambazo ni:-
- if……else
- switch
- loop
Katika somo hili tutaona aina kwanza. Kisha switch na loop tutaisoma kwenye somo linalofuata.
- if…else
Tunataka tuanze kuona endapo umri wa mtoto utakuwa chinivya miaka 6.
Kwanza tutatiloa prompy() kwa ajili ya kudaka user input. Rejea somo la 15 tumezungumzia sana habari hii.
Pili tutatumia variable kwa ajili ya ku store user input kutoka kwenye prompt(). Variable yetu tutaiita umri. Hivyo code itasomeka hivi
let umri = prompt("Weka umri wa mtoto");
Tatu tutakwenda kutengeneza condition statement. Jinsfi ya kutengeneza condition statemen
- Utaanza na neno if
- Litafuatiwa na mabano ()
- Ndani ya hayo mabano ndipo kunakaa mashart
- Kisha utaweka mabano mengine haya {} yanayifahamikabkwa jina la curl au brace
- Ndani ya jayo mabano {} utaweka maelekezo. Maelekezo haya yataonyesha nini kifanyike endapo sharti litatimizwa ama laa.
Kwa mujibu wa mfano wetu, shart amavcondition ni kuwa na umri kuanzia miaka 6. Ikiwa ni chini ya hapo program itatoa maelekezo.
Kanuni ya kuandika if… else
if(weka sharti hapa){
weka maelekezo hapa
}
Kumbuka tayari tunayo vatiable yabkukusanya data ambazo zitajazwa. Variable hiyo ni umri rejea hapo juu.
Sasa tunakwenda kusema kwenye shart ikiwa umri ni chini ya miaka sita. Kama tulivyoona hapo juu kuwa shart huwekwa ndanibya mabano (). Kumbuka alama hizi ambazo tulishasomaga masomo ya mwanzoni: -
> Kubwa kuliko
< Ndogo kuliko
== Sawa sawa na
=> Kubwa kuliko au sawa sawa na
<= Ndogo kuliko au sawa sawa na
& and au na hutumika kuunganisha mfano Juma na Ali
! hii hutumika katika kukanusha
|| hii hutumika kumaanisha au
Hivyo itaandikwa hivi: -
if(umri ) sas kwa kuwa umri tunaujuwa nibchini yabmiaka 6 tutasema if(umri < 6) hapo sharti limekamilika.
Hatuwa inayofuata ni kuandika statement na kama nilivyotangulia kusema kuwa statement huandikwa ndani ya {} hivyo itakuwa hivi
if(umri <6){"Anatakiwa kurudi darasa la chekechea"} sasa kumbuka ili statement yetu ionekane tunatakiwa tutumie zile njia za ku onyesha matokeobya code kama document.write(). Hivyo code zetu zitasomeka hivi: -
if(umri <6){
document.write("Anatakiwa kurudi darasabla chekechea");}
Pia unaweza kitia rangi maandishi kwa kitumia html. Kwa mfano hapo tutatumia <b style='color:blue'> Anatakiwa arudi darasa la chekechea</b>
Hivyo code nzima zitakuwa hivi: -
<html>
<head>
<title>Mafunzo ya javascript</title>
</head>
<body>
<script>
let umri = prompt("Weka umri wa mtoto");
if(umri < 6){
document.write("<b style='color:blue'> Anatakiwa arudi darasa la chekechea</b>");
}
</script>
</body>
</html>
Sasa hapo utaona nimeweka namba 4 ambayo ni ndogo kuliko 6. Ukibonyeza ok utapata majibu haya.
Kwa mfano huo huo sasa utaona kama utajaza umri kuanzia 6 na kuendelea haitaonyesha chochote. Sasa itatakiwa tuseme else yaani ukiwa umri ni zaidi ya mika 6 ama zsidi program iseme umefanikiwa kumsajili mwanagunzi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
JAVASCRIPT - somo la 14: Jifunze kuhusu event kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu javascript events. Event ni neno la Kiingereza lenye maana tukio wingi wake events kumaanisha matukio. Natumia ni kila ambacho kinatokea kwenye javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 9: Jinsi ya kuandika function kwenye javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function kwenye javascript. Utajifunz apia namna ya kuitumia function hiyo
Soma Zaidi...JAVASCRIPT -somo la 1: Kwa nini ni muhimu kujifunza javascript
Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya javacsript pamoja na kazi za javascript. Pia utayajuwa makampuni makubwa yanayotumia javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 2: Jisi ya ku print output ya code za javascript.
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza ku display matokeo ya code za javascript.
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 5: Jinsi ya kupangilia maandishi wakati wa ku output kwenye javascript
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kupangilia muonekano wa maandishi (text) wakati wa ku out put matokeo ya code
Soma Zaidi...JAVASCRIPT - somo la 23: Jinsi ya kutengeneza calculator yaani kikokotoo cha hesabu kwa kutumia javascript
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kutumia javascript kutengeneza kikokotoo cha hesabu yaani calculator
Soma Zaidi...