Inakuwaje unafanya ngono na aliyeathirika na usipate UKIMWI?

Watu wengi wamekuwa na mawazo kuwa ili nipate ukimwi ninatakiwa nishiriki ngono zembe na aliyeathirika mara ngapi? Majibu ya swali hili ni mafupi tu, ni kuwa unaweza kuathirika kwa ngono zembe ya siku moja tu ndani ya dakika chache. Lakini jambo la kuzing

Inakuwaje unafanya ngono na aliyeathirika na usipate UKIMWI?

Njia ambazo virusi huingia mwilini:

Kabala ya kuingia ndani zaidi kwenye somo letu, kwanza tujuwe namna ambavyo virusi vya ukimwi vinavyoingia ndani ya miili yetu. Mara tu virusi vinapokutana na mwili wa mtu unaanza kutafuta njia za kuingilia mwilini hadi kufikia kwenye damu. Njia hizo ni kupitia kwenye majeraha, michubuko, matundu yaliyo wazi kwenye vidonda, upele, majibu ama sehemu za mwili zilizo wazi kupitia mikato kama mtu alikatwa na kitu cha ncha kali, ama alichomwa kwa sindano ama kitu cha ncha kali.

 

Michubuko inaweza kuwa kwenye sehemu za siri yaani uke na uume kutokana na kufanya tendo la ndoa, ama michubuko inaweza kuwa kwenye maeneo mengine ya mwili kutokana na majeraha, mikato ama mikwaruzo. Majeraha na vidonda huweza kupatikana kwenye mdomo ama maeneo mengine ya mwili kutokana na majeraha ama mikato na mikwaruzo. Pia wakati wa kunyoa sehemu za siri huwenda mtu akajikata hivyo kusababisha majeraha madogomadogo.

 

Nini hutokea baada ya virusi kuipata njia ya kuingia mwilini?

Kitu cha kwanza virusi huhitaji kuingia kwenye damu. Vinapofika kwenye damu vinatafuta seli zinazofahamika kwa jina la CD4. Katika damu aina zisizopunguwatatu za seli. Kuna seli hai nyekundu za damu, kuna seli hai nyeupe za dam na pia kuna seli sahani. Seli hai nyekundu kaziyake kuu ni kusafirisha hewa ya okksijeni kwenda maeneo mengine ya mwili. Kazi kuu ya seli hai nyeupe ni kulinda mwili na kukinga dhidi ya vijidudu vya maradhi kwa kuviuwa vijidudu hivi.

 

Sasa virusi vya virusi vya ukimwi vinapoingia kwenye damu moja kwa moja hutafuta seli hai nyeupe inayofahamika kwa jina la CD4 na kuingia ndani. Lengo lake ni kweda kuzaliana humo. Hivyo virusi vinapoingia kwenye seli hizi vinaanza kuzaliana na vikijaa kwenye seli seli hupasuka na kumwaga maelfu ya virusi kwenye damu, kisha mchakato huendelea kwenye seli nyingine. Kwa njia hii virusi vinajaa mwilini na kuathiri seli nyingi Zaidi na kila seli inapojaa virusi hupasuka na kufa. Kadiri seli zinapokufa ndipo kinga ya mwili hupunguwa na hatimaye kupata upungufu wa kinga mwilini.

 

Sasa inakuwaje inakuwaje mtu anashiriki tendo la ndoa na mtu aliyeathirikabila ya kuathirika?

Ok, sasa turudi kwenye swali letu la msingi. Bila shaka umejifunza hapo juu njia ambazo virusi huingia mwilini. Wapo watu wengi walioishi miaka kadhaa na waathirika bila ya wao kuathirika na hali wanazaa watoto n ahata hawatumii kinga. Unadhani ni kitu gani hapa hutokea. Zifuatazo ni baadhi tu ya sababu:-

 

 

 

Je nawezaje kuzuia kutopata michubuko wakati wa tendola ndoa?

Hili ni swali zuri, ila kabla ya kulijuwa uzuri wa swali hili, nakupa swali jingine. Je kuna umuhimu gani wa kujizuia kutopata michubuko wakati wat endo la ndoa? Kwa ufupi wa majawabu ni kuwa, michubuko ndio njia ambazo virusi huweza kuingia mwilii, sasa kama hatuna michubuko si rahisi kwa virusi kuingia mwilini. Sasa wacha tuone njia ambazo unaweza kutumia kuzuia michubuko wakati wat endo la ndoa:-

 

 

 

 

Inakuwaje idadi ya virusi ikawa 0 kwenye damu na mtu akawa ni muathirika?

Vipimo vya virusi vya ukimwi vipo vya aina nyingi. Kuna ambavyo hupima idadi ya virusi kwenye damu na kuna ambavyo hupima antibody zinazotolewa na virusi. Kitaalamu idadi ya virusi kwenye damu hufahamika kama viral load. Sasa hutokea wakati kwa yule anayetumia dawa za VVU ikafikia idadi ya virusi kwenye damu yake inawa ni sifuri. 

 

Hii hutokea kama ametuma dawa kwa muda mrefu usiopunguwa miezi 6, na akawa anafuata masharti yote. Sasa endapo atadumu na hali hii kwa muda wa miezi 6 hawezi kumuambukiza mtu. Sasa lamda tuone hali hii inatokeaje. Kawaida kama mtu ameanza mapema kutumia ARV basi dawa hizi huzuia uzalishaji wa virusi hivi ama hupunguza visizaliane ama hupunguza visisathiri seli nyingine. Kama mtu atatumia vema dawa virusi vinakwenda kujificha maeneo mengine ya mwili na vinaondoka kwenye damu, na hapa ndipo hufikia mtu anawa hana kabisa virusi kwenye damu.

 

Sasa kwa kuwa virusi hivi bado vipo mwilini ila vimejificha tuu, vitaendelea kuzalisha kemikali zinazofahamika kama antibody, kemikali hizi ndizo hutuonyehsa kuwa bado vipo mwilini ila vimejificha. Endao mtu ataacha kutumia dawa vitarudi tena kwa kasi kubwa na kwa nguvu mpya na kuathiri wili kwa haraka Zaidi. Ikifikia hali hii mtu huambiwa kitaalamu ana viral resistance yaani virusi vyeke vimetengeneza usugu.

 

 

Tukutane Makala ijayo tutakapozungumzia watu walio hatarini kupata maambukizi na dawa wanazopaswa kutumia kama tahadhari kwao.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 12092

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Dalili za mawe kwenye kibofu Cha mkono

Mawe ya kibofu ni mkusanyiko mgumu wa madini kwenye kibofu chako. Mawe kwenye kibofu hukua wakati mkojo kwenye kibofu chako unapokolea, na kusababisha madini katika mkojo wako kung'aa.

Soma Zaidi...
Dalili za VVU/UKIMWI Ni zipi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI

Soma Zaidi...
Sababu za Maumivu ya shingo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na maumivu ya shingo na ndani yake kunasababu zinazopelekea shingo kupata maumivu.

Soma Zaidi...
Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo

Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa degedege na dalili zake

Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo

Soma Zaidi...
Dalili za gonorrhea - gonoria

Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume

Soma Zaidi...
Dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za Ugonjwa wa akili.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa akili .

Soma Zaidi...
Huduma kwa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa

Posti hii inahusu zaidi msaada kwa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa, ni huduma anayopewa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa.

Soma Zaidi...