Inakuwaje unafanya ngono na aliyeathirika na usipate UKIMWI?

Inakuwaje unafanya ngono na aliyeathirika na usipate UKIMWI?

Watu wengi wamekuwa na mawazo kuwa ili nipate ukimwi ninatakiwa nishiriki ngono zembe na aliyeathirika mara ngapi? Majibu ya swali hili ni mafupi tu, ni kuwa unaweza kuathirika kwa ngono zembe ya siku moja tu ndani ya dakika chache. Lakini jambo la kuzing

Download Post hii hapa

Inakuwaje unafanya ngono na aliyeathirika na usipate UKIMWI?

Njia ambazo virusi huingia mwilini:

Kabala ya kuingia ndani zaidi kwenye somo letu, kwanza tujuwe namna ambavyo virusi vya ukimwi vinavyoingia ndani ya miili yetu. Mara tu virusi vinapokutana na mwili wa mtu unaanza kutafuta njia za kuingilia mwilini hadi kufikia kwenye damu. Njia hizo ni kupitia kwenye majeraha, michubuko, matundu yaliyo wazi kwenye vidonda, upele, majibu ama sehemu za mwili zilizo wazi kupitia mikato kama mtu alikatwa na kitu cha ncha kali, ama alichomwa kwa sindano ama kitu cha ncha kali.

 

Michubuko inaweza kuwa kwenye sehemu za siri yaani uke na uume kutokana na kufanya tendo la ndoa, ama michubuko inaweza kuwa kwenye maeneo mengine ya mwili kutokana na majeraha, mikato ama mikwaruzo. Majeraha na vidonda huweza kupatikana kwenye mdomo ama maeneo mengine ya mwili kutokana na majeraha ama mikato na mikwaruzo. Pia wakati wa kunyoa sehemu za siri huwenda mtu akajikata hivyo kusababisha majeraha madogomadogo.

 

Nini hutokea baada ya virusi kuipata njia ya kuingia mwilini?

Kitu cha kwanza virusi huhitaji kuingia kwenye damu. Vinapofika kwenye damu vinatafuta seli zinazofahamika kwa jina la CD4. Katika damu aina zisizopunguwatatu za seli. Kuna seli hai nyekundu za damu, kuna seli hai nyeupe za dam na pia kuna seli sahani. Seli hai nyekundu kaziyake kuu ni kusafirisha hewa ya okksijeni kwenda maeneo mengine ya mwili. Kazi kuu ya seli hai nyeupe ni kulinda mwili na kukinga dhidi ya vijidudu vya maradhi kwa kuviuwa vijidudu hivi.

 

Sasa virusi vya virusi vya ukimwi vinapoingia kwenye damu moja kwa moja hutafuta seli hai nyeupe inayofahamika kwa jina la CD4 na kuingia ndani. Lengo lake ni kweda kuzaliana humo. Hivyo virusi vinapoingia kwenye seli hizi vinaanza kuzaliana na vikijaa kwenye seli seli hupasuka na kumwaga maelfu ya virusi kwenye damu, kisha mchakato huendelea kwenye seli nyingine. Kwa njia hii virusi vinajaa mwilini na kuathiri seli nyingi Zaidi na kila seli inapojaa virusi hupasuka na kufa. Kadiri seli zinapokufa ndipo kinga ya mwili hupunguwa na hatimaye kupata upungufu wa kinga mwilini.

 

Sasa inakuwaje inakuwaje mtu anashiriki tendo la ndoa na mtu aliyeathirikabila ya kuathirika?

Ok, sasa turudi kwenye swali letu la msingi. Bila shaka umejifunza hapo juu njia ambazo virusi huingia mwilini. Wapo watu wengi walioishi miaka kadhaa na waathirika bila ya wao kuathirika na hali wanazaa watoto n ahata hawatumii kinga. Unadhani ni kitu gani hapa hutokea. Zifuatazo ni baadhi tu ya sababu:-

 

 

 

Je nawezaje kuzuia kutopata michubuko wakati wa tendola ndoa?

Hili ni swali zuri, ila kabla ya kulijuwa uzuri wa swali hili, nakupa swali jingine. Je kuna umuhimu gani wa kujizuia kutopata michubuko wakati wat endo la ndoa? Kwa ufupi wa majawabu ni kuwa, michubuko ndio njia ambazo virusi huweza kuingia mwilii, sasa kama hatuna michubuko si rahisi kwa virusi kuingia mwilini. Sasa wacha tuone njia ambazo unaweza kutumia kuzuia michubuko wakati wat endo la ndoa:-

 

 

 

 

Inakuwaje idadi ya virusi ikawa 0 kwenye damu na mtu akawa ni muathirika?

Vipimo vya virusi vya ukimwi vipo vya aina nyingi. Kuna ambavyo hupima idadi ya virusi kwenye damu na kuna ambavyo hupima antibody zinazotolewa na virusi. Kitaalamu idadi ya virusi kwenye damu hufahamika kama viral load. Sasa hutokea wakati kwa yule anayetumia dawa za VVU ikafikia idadi ya virusi kwenye damu yake inawa ni sifuri. 

 

Hii hutokea kama ametuma dawa kwa muda mrefu usiopunguwa miezi 6, na akawa anafuata masharti yote. Sasa endapo atadumu na hali hii kwa muda wa miezi 6 hawezi kumuambukiza mtu. Sasa lamda tuone hali hii inatokeaje. Kawaida kama mtu ameanza mapema kutumia ARV basi dawa hizi huzuia uzalishaji wa virusi hivi ama hupunguza visizaliane ama hupunguza visisathiri seli nyingine. Kama mtu atatumia vema dawa virusi vinakwenda kujificha maeneo mengine ya mwili na vinaondoka kwenye damu, na hapa ndipo hufikia mtu anawa hana kabisa virusi kwenye damu.

 

Sasa kwa kuwa virusi hivi bado vipo mwilini ila vimejificha tuu, vitaendelea kuzalisha kemikali zinazofahamika kama antibody, kemikali hizi ndizo hutuonyehsa kuwa bado vipo mwilini ila vimejificha. Endao mtu ataacha kutumia dawa vitarudi tena kwa kasi kubwa na kwa nguvu mpya na kuathiri wili kwa haraka Zaidi. Ikifikia hali hii mtu huambiwa kitaalamu ana viral resistance yaani virusi vyeke vimetengeneza usugu.

 

 

Tukutane Makala ijayo tutakapozungumzia watu walio hatarini kupata maambukizi na dawa wanazopaswa kutumia kama tahadhari kwao.

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 12341

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma

Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa ukoma ni Ugonjwa unaosababishwa na bacteria anayejulika kama mycobacterium leprae.

Soma Zaidi...
  Dalili za Uvimbe kwenye mfuko wa uzazi (uterine fibroid)
Dalili za Uvimbe kwenye mfuko wa uzazi (uterine fibroid)

Uvimbe kwenye mfuko wa uzazi hukua kutoka kwenye tishu laini za misuli ya uterasi. Fibroids nyingi ambazo zimekuwepo wakati wa ujauzito hupungua au kutoweka baada ya ujauzito, kwani uterasi inarudi kwenye ukubwa wa kawaida.

Soma Zaidi...
Je kwa mfano mimi nmeupata ukimwi leo na sihitaji kwenda kupima yaaan uanza kujionyesha baada ya muda gani
Je kwa mfano mimi nmeupata ukimwi leo na sihitaji kwenda kupima yaaan uanza kujionyesha baada ya muda gani

Watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuwa ukimwi huonekana baada ya muda gani toka kuathirika?

Soma Zaidi...
SABABU ZINAZOPELEKEA KUJAA KWA MATE MDOMONI NA MATIBABU YAKE
SABABU ZINAZOPELEKEA KUJAA KWA MATE MDOMONI NA MATIBABU YAKE

Kutokwa na mate mengi mdomoni si ugojwa ni hali inayoweza kutokea kwa mtu yeyote. Mara nyingi hali hii haihitaji matibabu wa dawa, na huondoka yenyewe. Lakini hutokea baadhi ya nyakati ikawa mate yanatoka zaidi mdomoni. Je na wewe ni miongoni mwao? Makala

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa ngiri
Dalili za ugonjwa wa ngiri

Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo mgonjwa wa ngiri anaweza kuzipata, kwa hiyo baada ya kusoma na kuelewa dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospitali mapema kwa ajili ya kupata matibabu.

Soma Zaidi...
Tufanyeje ili kuepuka kuaribika kwa figo?
Tufanyeje ili kuepuka kuaribika kwa figo?

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia kuaribika kwa figo, hizi ni njia zinazotumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuaribika kwa figo na hasa wale ambao hawajapata tatizo hili wazitumie ili tuone kama tutaweza kupunguza tatizo hili.

Soma Zaidi...
Matibabu ya maumivu chini ya kitovu
Matibabu ya maumivu chini ya kitovu

Post hii inahusu zaidi matibabu ya kutibu ugonjwa wa maumivu chini ya kitovu.

Soma Zaidi...
Sababu za kuumwa na tumbo, chini ya kitomvu ama upande wa kulia
Sababu za kuumwa na tumbo, chini ya kitomvu ama upande wa kulia

Post hii inakwenda kukutajia baadhi tu ya sababu zinazopelekea kuumwa na tumbo. Hali hizi zinawweza kuwapata watu wa jinsia zote katika umri wowote ule. Ijapokuwa nyingine si kwa wote ni kwa baadhi ya watu. hapa nitakuletea sababu 5 tu.

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya kibofu Cha nyongo
Dalili za saratani ya kibofu Cha nyongo

Saratani ya kibofu cha nyongo ni Saratani inayoanzia kwenye kibofu cha nyongo. Nyongo yako ni kiungo kidogo, chenye umbo la peari upande wa kulia wa tumbo lako, chini ya ini lako. Kibofu cha nyongo huhifadhi nyongo, Kioevu cha usaga

Soma Zaidi...