Inakuwaje unafanya ngono na aliyeathirika na usipate UKIMWI?
Watu wengi wamekuwa na mawazo kuwa ili nipate ukimwi ninatakiwa nishiriki ngono zembe na aliyeathirika mara ngapi? Majibu ya swali hili ni mafupi tu, ni kuwa unaweza kuathirika kwa ngono zembe ya siku moja tu ndani ya dakika chache. Lakini jambo la kuzing
Inakuwaje unafanya ngono na aliyeathirika na usipate UKIMWI?
Njia ambazo virusi huingia mwilini:
Kabala ya kuingia ndani zaidi kwenye somo letu, kwanza tujuwe namna ambavyo virusi vya ukimwi vinavyoingia ndani ya miili yetu. Mara tu virusi vinapokutana na mwili wa mtu unaanza kutafuta njia za kuingilia mwilini hadi kufikia kwenye damu. Njia hizo ni kupitia kwenye majeraha, michubuko, matundu yaliyo wazi kwenye vidonda, upele, majibu ama sehemu za mwili zilizo wazi kupitia mikato kama mtu alikatwa na kitu cha ncha kali, ama alichomwa kwa sindano ama kitu cha ncha kali.
Michubuko inaweza kuwa kwenye sehemu za siri yaani uke na uume kutokana na kufanya tendo la ndoa, ama michubuko inaweza kuwa kwenye maeneo mengine ya mwili kutokana na majeraha, mikato ama mikwaruzo. Majeraha na vidonda huweza kupatikana kwenye mdomo ama maeneo mengine ya mwili kutokana na majeraha ama mikato na mikwaruzo. Pia wakati wa kunyoa sehemu za siri huwenda mtu akajikata hivyo kusababisha majeraha madogomadogo.
Nini hutokea baada ya virusi kuipata njia ya kuingia mwilini?
Kitu cha kwanza virusi huhitaji kuingia kwenye damu. Vinapofika kwenye damu vinatafuta seli zinazofahamika kwa jina la CD4. Katika damu aina zisizopunguwatatu za seli. Kuna seli hai nyekundu za damu, kuna seli hai nyeupe za dam na pia kuna seli sahani. Seli hai nyekundu kaziyake kuu ni kusafirisha hewa ya okksijeni kwenda maeneo mengine ya mwili. Kazi kuu ya seli hai nyeupe ni kulinda mwili na kukinga dhidi ya vijidudu vya maradhi kwa kuviuwa vijidudu hivi.
Sasa virusi vya virusi vya ukimwi vinapoingia kwenye damu moja kwa moja hutafuta seli hai nyeupe inayofahamika kwa jina la CD4 na kuingia ndani. Lengo lake ni kweda kuzaliana humo. Hivyo virusi vinapoingia kwenye seli hizi vinaanza kuzaliana na vikijaa kwenye seli seli hupasuka na kumwaga maelfu ya virusi kwenye damu, kisha mchakato huendelea kwenye seli nyingine. Kwa njia hii virusi vinajaa mwilini na kuathiri seli nyingi Zaidi na kila seli inapojaa virusi hupasuka na kufa. Kadiri seli zinapokufa ndipo kinga ya mwili hupunguwa na hatimaye kupata upungufu wa kinga mwilini.
Sasa inakuwaje inakuwaje mtu anashiriki tendo la ndoa na mtu aliyeathirikabila ya kuathirika?
Ok, sasa turudi kwenye swali letu la msingi. Bila shaka umejifunza hapo juu njia ambazo virusi huingia mwilini. Wapo watu wengi walioishi miaka kadhaa na waathirika bila ya wao kuathirika na hali wanazaa watoto n ahata hawatumii kinga. Unadhani ni kitu gani hapa hutokea. Zifuatazo ni baadhi tu ya sababu:-
- 1. Kama wameshiriki ngono kwa kutumia kinga kifasaha na kujilinda na hatari zinazoweza kutokea wakati wat endo kama kupasuka kwa kondom. Kama wamechukuwa thadhali vyema hawawezi kuambukizana.
- 2. Kama hakuna michubuko yeyote iliyotokea wakati wat endo.maambukizi ya VVU kupitia ngono mara nyingi hutokea kama kumetokea michubuko kwenye sehemu za siri uume ama uke wakati wat endo. Michubuko hii ni midogo kiasi kwambu unaweza usihisi chochote. Sasa kama tendo lilifanyika kistarabu, kipole na kwa utaratibu mzuri ni vigumu kutokea kwa michubuko hivyo si rahisi mtu kuathirika hata kama alishiriki na muathirika.
- 3. Kama muathirika alikuwa ni mtumiaji wa dozi ya ARV kwa ufasaha kwa mda mrefu hata akafikia idadi ya virusi kwenye kipimo cha damu ni 0, akifikia hatuwa hii hawezi kumuambukiza mtu mwingine hata kama hawakutumia kinga.
Je nawezaje kuzuia kutopata michubuko wakati wa tendola ndoa?
Hili ni swali zuri, ila kabla ya kulijuwa uzuri wa swali hili, nakupa swali jingine. Je kuna umuhimu gani wa kujizuia kutopata michubuko wakati wat endo la ndoa? Kwa ufupi wa majawabu ni kuwa, michubuko ndio njia ambazo virusi huweza kuingia mwilii, sasa kama hatuna michubuko si rahisi kwa virusi kuingia mwilini. Sasa wacha tuone njia ambazo unaweza kutumia kuzuia michubuko wakati wat endo la ndoa:-
- 1. Kwa kutumia vilainishi. Vilainishi hivi vinaweza kuwa mafuta ama vilainishi vingine vya asili. Kawaida mwili wa mwanamke una vilainishi ambavyo hupunguza msuguano na kuzuia michubuko ila si kila wakati vilainishi hivi vitakuwepo kwa muda wote.
- 2. Kuandaa mwili wa mwanamke hata kabla ya kuanza kwa tendo. Maandalizi haya ni muhimu katika kuhakikisha kuwa mwili wa mwanamke unatowa majimaji ambayo ndio vilainishi vya asili.
- 3. Tendo lifanyike kwa upole na kwa ustaarabu na kwa hisia. Endapo hisia za mwanamke zitakata ni vyema kustop hadi zirudi ili kuwepo kwa majimaji, kwani endapo zitakata hatoweza kuwa na majimaji ambayo ndio vilainishi vya asili vinginevyo mafuta yatumike kama vilainishi mbadala.
- 4. Tendolisifanyike kwa muda mrefu sana, kawaida kama tendo litafanyika kwa muda mrefu ni vigumu kwa mwili wa mwanamke kuendelea kuzalisha vilainishi muda wote, hivyo uwezekano wa kupata michubuko ni mkubwa sana.
Inakuwaje idadi ya virusi ikawa 0 kwenye damu na mtu akawa ni muathirika?
Vipimo vya virusi vya ukimwi vipo vya aina nyingi. Kuna ambavyo hupima idadi ya virusi kwenye damu na kuna ambavyo hupima antibody zinazotolewa na virusi. Kitaalamu idadi ya virusi kwenye damu hufahamika kama viral load. Sasa hutokea wakati kwa yule anayetumia dawa za VVU ikafikia idadi ya virusi kwenye damu yake inawa ni sifuri.
Hii hutokea kama ametuma dawa kwa muda mrefu usiopunguwa miezi 6, na akawa anafuata masharti yote. Sasa endapo atadumu na hali hii kwa muda wa miezi 6 hawezi kumuambukiza mtu. Sasa lamda tuone hali hii inatokeaje. Kawaida kama mtu ameanza mapema kutumia ARV basi dawa hizi huzuia uzalishaji wa virusi hivi ama hupunguza visizaliane ama hupunguza visisathiri seli nyingine. Kama mtu atatumia vema dawa virusi vinakwenda kujificha maeneo mengine ya mwili na vinaondoka kwenye damu, na hapa ndipo hufikia mtu anawa hana kabisa virusi kwenye damu.
Sasa kwa kuwa virusi hivi bado vipo mwilini ila vimejificha tuu, vitaendelea kuzalisha kemikali zinazofahamika kama antibody, kemikali hizi ndizo hutuonyehsa kuwa bado vipo mwilini ila vimejificha. Endao mtu ataacha kutumia dawa vitarudi tena kwa kasi kubwa na kwa nguvu mpya na kuathiri wili kwa haraka Zaidi. Ikifikia hali hii mtu huambiwa kitaalamu ana viral resistance yaani virusi vyeke vimetengeneza usugu.
Tukutane Makala ijayo tutakapozungumzia watu walio hatarini kupata maambukizi na dawa wanazopaswa kutumia kama tahadhari kwao.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 kitabu cha Simulizi ๐2 web hosting ๐3 Bongolite - Game zone - Play free game ๐4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐5 Dua za Mitume na Manabii ๐6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Bipolar disorders
Bipolar disorder ni hali ya afya ya akili inayohusisha mabadiliko makubwa katika hisia, nishati, na shughuli za kila siku za mtu. Dalili za bipolar disorder zinaweza kuwa kwenye kipindi cha mania na kipindi cha unyogovu, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa bipolar.
Soma Zaidi...Dalilili za kukosa oksijeni
Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalilili za kukosa oksijeni ambalo kitaalamu hujulikana Kama apnea.kukosa oksijeni ni tatizo ambapo kupumua kwako hukoma na kuanza unapolala.
Soma Zaidi...Mambo yanayosababisha kiuno au mgongo kuwa na maumivu
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kusababishwa mgongo wAko au kiuno kwa na maumivu, Mgongo ukiwa na maumivu makali Sana yanaweza kusababishwa shida kubwa ata utakapokaa au ukilala au ukitumia bado maumivu yanakuwepo.
Soma Zaidi...Nini chanzo cha malaria
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu chanzo cha ugonjwa wa malaria
Soma Zaidi...NJIA YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA VIRUSI VYA VYA UKIMWI NA ATHARI ZAKE
Posti hii inahusisha maambukizi ya virusi vya ukimwi .piaย tutangaliaย njia za kujikinga naย ugonjwa wa UKIMWI
Soma Zaidi...