Dalili kuu za minyoo

Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen

DALILI ZA MINYOO

Aina za minyoo:

Kuna aina za minyoo ziatazo 300000 na kati ya hozo 300 tu ndio ambazo husababisha maradhi kwa binadamu. Minyoo imegawanyika katika aina kadhaa kulingana na tabia zao, jinsi wanavyozaliana na maeneo wanayoishi, pia na maumbile yako. Aina hizo za minyoo ni kama:-

 

  1. Trichinosis hawa tunaweza kuwapata kutoka kwa wanyama
  2. Pinworm (thread worm) hawa ni wadogo sana na unaweza kuwapata kwa kuyala mayai yao kutoka pale yalipo. Kama utakuwa unanawa mikono mara kwa mara, kabla ya kula na huna tabia ya kula vidole ni ngumu kuwapata hawa minyoo
  3. Hookworm (roundworm) minyoo hawa husambazwa kupitia udongo na kinyesi
  4. Fluke; (flatworm) hawa wanaishi kwenye utumbo mdogo na meneo mengine. Tunaweza kuwapata kwenye vyakula na mboga zisizooshwa vyema.
  5. Tapeworm (flatworm)  unaweza kuwapata hawa kwenye maji machafu na kwenye vyakula.

 

Je ni wapi naweza kupata minyoo?

Minyoo tunaweza kuipata maeneo mengi. Na katika miili yetu pia inaweza kuingia kupitia njia nyingi. Njia kuu ni kwa kupitia mdomoni kwa njia ya chakula, ama kinywaji. Lakini pia inaweza kupitia kwenye ngozi. Hebu tuyaone maeneo ambayo monyoo ipo sana.

 

  1. Kwenye majimaji
  2. Ndani ya maji
  3. Kwenye udongo
  4. Kwenye nyama
  5. Kwenye chakula kisichopikwa kama matunda
  6. Kwenye mbog za majani

 

Ni kivipi naweza pata minyoo?

  1. kwa kugusa kitu chenye mayai ya minyoo, kisha ukapeleka mkono mdomoni bila ya kuosha
  2. Kunywa maji yenye mayai ya minyoo
  3. Kula chakula chenye mayai ya minyoo
  4. Kula udongo wenye mayai ya minyoo
  5. Unapotembea bila ya viatu maeneo machafu
  6. Unapokula vyakula visivyopikwa ama vilivyopikwa kwa uchache kama nyama ya ngurue

 

Ni ziipi dalili za minyoo?

  1. Maumivu ya tumbo
  2. Kuharisha, kutapika na kupata kichefuchefu
  3. Tumbo kujaa gesi ama kuunguruma
  4. Uchofu wa mara kwa mara
  5. Kupunguwa uzito bila ya sababu maalimu
  6. Tumbo kujaa na kuwa gumu

 

Ni vipi naweza kuepuka kupata minyoo?

  1. Osha mikono kabla ya kula ama kuingiza mdomoni
  2. Kula chakula kilichopikwa vyema
  3. Usile matunda bila ya kuosha
  4. Unapotembea kwenye ardhi chafu usitembee bila ya viatu
  5. Kama unaishi na paka ama mbwa hakikisha yupo salama
  6. Vinyesi vya wanyama kama paka, mbwa, na wanyama wafugwo wa nyama vihifadhiwe vyema.
  7. Kuwa makini na nyama ya nguruwe.

 

JE minyoo inatibika?

Ndio mimnyoo inatibika tena kwa muda mchache tu. Kama unasumbuliwa fika kituo cha afya kwa vipimo zaidi. Makala inayofata tutazungumzia kuhusu matibabu ya minyoo.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2810

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dalili za saratani ya tishu (leukemia)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na saratani za tishu ambazo kitaalamu hujulikana Kama Leukemia kawaida huhusisha seli nyeupe za damu. Seli zako nyeupe za damu ni wapiganaji hodari wa maambukizo - kwa kawaida hukua na kugawanyika kwa utaratibu, kadri mwi

Soma Zaidi...
Ni zipi dalili za Ukimwi na ni zipi dalili za VVU

Ijuwe historia ya VVu, Dalili zake, tiba na vipimo vyake pia njia za kueneza VVU na UKIMWI

Soma Zaidi...
Dalili na sababu za mawe kwenye in yaani liver stone au intrahepatic stones

Katika post hii utakwend akujifunza kuhusu tatizo la kuwa na vijiwe kwenye ini vijiwe hivi hufahamika kama intrahepatic stones.

Soma Zaidi...
NINI SABABU YA VIDONDA VYA TUMBO

NENO LA AWALI Hapa utaweza kujifunza mambo mengi kuhusu vidonda vyatumbo.

Soma Zaidi...
MARADHI MENGINE 10 YANAYOTOKANA NA MBU ( matende, ngirimaji, homa ya manjano, n.k

Tofauti na maradhi yaliyotajwa hapo juu pia tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwepo kwa maradhi mengine hatari yanayosambazwa na mbu, kama vile ngirimaji pamoja na matende.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa misuli kuwa dhaifu.

hali ambayo misuli unayotumia kwa hotuba ni dhaifu au unapata shida kuidhibiti mara nyingi inaonyeshwa na usemi wa kufifia au polepole ambao unaweza kuwa mgumu kuelewa. Sababu za kawaida za Ugonjwa huu ni pamoja na matatizo ya mfumo wa neva (neurolojia

Soma Zaidi...
Watu walio hatarini kupata fangasi

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya watu walio hatarini kupata fangasi

Soma Zaidi...
Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia

Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia

Soma Zaidi...
Je utaweza kuambukiza HIV ukiwa unatumia PrEP?

Swali hili limeulizwa na mdau mmoja. Kuwa endapo mtu atafanya ngono zembe na akapata virusi je ataweza kuambukiza.

Soma Zaidi...
Dalilili za saratani ya utumbo

Saratani ya Utumbo ni Saratani ya utumbo mpana (koloni), sehemu ya chini ya mfumo wako wa usagaji chakula. Kwa pamoja, mara nyingi hujulikana kama Saratani ya utumbo mpana. Visa vingi vya Saratani ya utumbo mpana huanza

Soma Zaidi...