picha

Dalili kuu za minyoo

Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen

DALILI ZA MINYOO

Aina za minyoo:

Kuna aina za minyoo ziatazo 300000 na kati ya hozo 300 tu ndio ambazo husababisha maradhi kwa binadamu. Minyoo imegawanyika katika aina kadhaa kulingana na tabia zao, jinsi wanavyozaliana na maeneo wanayoishi, pia na maumbile yako. Aina hizo za minyoo ni kama:-

 

  1. Trichinosis hawa tunaweza kuwapata kutoka kwa wanyama
  2. Pinworm (thread worm) hawa ni wadogo sana na unaweza kuwapata kwa kuyala mayai yao kutoka pale yalipo. Kama utakuwa unanawa mikono mara kwa mara, kabla ya kula na huna tabia ya kula vidole ni ngumu kuwapata hawa minyoo
  3. Hookworm (roundworm) minyoo hawa husambazwa kupitia udongo na kinyesi
  4. Fluke; (flatworm) hawa wanaishi kwenye utumbo mdogo na meneo mengine. Tunaweza kuwapata kwenye vyakula na mboga zisizooshwa vyema.
  5. Tapeworm (flatworm)  unaweza kuwapata hawa kwenye maji machafu na kwenye vyakula.

 

Je ni wapi naweza kupata minyoo?

Minyoo tunaweza kuipata maeneo mengi. Na katika miili yetu pia inaweza kuingia kupitia njia nyingi. Njia kuu ni kwa kupitia mdomoni kwa njia ya chakula, ama kinywaji. Lakini pia inaweza kupitia kwenye ngozi. Hebu tuyaone maeneo ambayo monyoo ipo sana.

 

  1. Kwenye majimaji
  2. Ndani ya maji
  3. Kwenye udongo
  4. Kwenye nyama
  5. Kwenye chakula kisichopikwa kama matunda
  6. Kwenye mbog za majani

 

Ni kivipi naweza pata minyoo?

  1. kwa kugusa kitu chenye mayai ya minyoo, kisha ukapeleka mkono mdomoni bila ya kuosha
  2. Kunywa maji yenye mayai ya minyoo
  3. Kula chakula chenye mayai ya minyoo
  4. Kula udongo wenye mayai ya minyoo
  5. Unapotembea bila ya viatu maeneo machafu
  6. Unapokula vyakula visivyopikwa ama vilivyopikwa kwa uchache kama nyama ya ngurue

 

Ni ziipi dalili za minyoo?

  1. Maumivu ya tumbo
  2. Kuharisha, kutapika na kupata kichefuchefu
  3. Tumbo kujaa gesi ama kuunguruma
  4. Uchofu wa mara kwa mara
  5. Kupunguwa uzito bila ya sababu maalimu
  6. Tumbo kujaa na kuwa gumu

 

Ni vipi naweza kuepuka kupata minyoo?

  1. Osha mikono kabla ya kula ama kuingiza mdomoni
  2. Kula chakula kilichopikwa vyema
  3. Usile matunda bila ya kuosha
  4. Unapotembea kwenye ardhi chafu usitembee bila ya viatu
  5. Kama unaishi na paka ama mbwa hakikisha yupo salama
  6. Vinyesi vya wanyama kama paka, mbwa, na wanyama wafugwo wa nyama vihifadhiwe vyema.
  7. Kuwa makini na nyama ya nguruwe.

 

JE minyoo inatibika?

Ndio mimnyoo inatibika tena kwa muda mchache tu. Kama unasumbuliwa fika kituo cha afya kwa vipimo zaidi. Makala inayofata tutazungumzia kuhusu matibabu ya minyoo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 4462

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

WAJUE FANGASI, AINA ZAKE, DALILI ZAKE NA MATIBABU YAKE

Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili.

Soma Zaidi...
Yajue mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi (cellulitis)

Mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi hujitokeza sehemu yenye jeraha pia huonyesha wekundu wenye upele,Uvimbe na malengelenge.

Soma Zaidi...
Uwepo wa asidi nyingi mwilini

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kuwepo kwa asidi nyingi mwilini hali uwasumbua watu wengi na kufikia kiasi cha kusababisha madhara mengine mawilini ikiwamo pamoja na kansa ya koo, ili kujua kama una wingi wa asildi mwilini unapaswa kujua dalili kama ifu

Soma Zaidi...
Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa

Soma Zaidi...
Ni nini husababisha kuziba kwa Njia ya machozi

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na sababu zinazopelekea Ugonjwa wa kuziba kwa Njia ya machozi yaani kukosa machozi ambayo husababishwa na maambukizi.

Soma Zaidi...