Imam Malik Ibn Anas

Imam Malik Ibn Anas

Imam Malik bin Anas



Kwa mujibu wa “Kitab al-Ansab na Dhahabi, Tadhkirah al- Huffaz” juzuu ya kwanza, Imam Malik alizaliwa mwaka 93 A.H. Baadhi ya vitabu vimetaja pia mwaka 94 na 95 A.H. Wazazi wa Imam Malik walitoka katika familia ya kifalme ya Kiarabu toka Yemen ambayo ilihamia Madinah. Wakati anazaliwa Imam Malik dola ya Kiislamu ilikuwa chini ya uongozi wa Khalifa Walid bin Abd- al-Malik na japo makao makuu ya dola yalikuwa yamehamishiwa Damascus, Syria, lakini mji wa Madinah ulibakia mashuhuri na kitovu cha elimu ya Uislamu. Familia ya Imam Malik ilizungukwa na ndugu na jamaa wa karibu waliokuwa na elimu ya kutosha.


Hivyo alianza kupata elimu yake katika mazingira ya nyumbani. Zaidi ya hapo alisoma kwa waalimu wengine saba mashuhuri wa fani mbalimbali, miongoni mwao alikuwa Jafar al-Sadiq, kitukuu cha Imam Hussein. Pamoja na kujikusanyia elimu nyingi, umaarufu wa Imam Malik ulizidi kuvuma kutokana na unyenyekevu na ucha Mungu wake. Watu walitoka masafa ya mbali kuja Madina kuhudhuria darsa za Imam Malik.


Sehemu kubwa ya muda wake aliitoa kwa kufundisha na akiifurahia kazi hii. Japo Imam Malik alikuwa mtaalam mzuri wa Hadith, lakini alikuwa dhaifu kidogo katika mambo ya sheria na kutoa fa-twa za kifiqh. Hata hivyo alikuwa mtu madhubuti na mwenye msimamo. Hakukubali kutolewa katika haki kwa hali yoyote iwayo. Wakati fulani alitoa fa’twa ambayo ilikuwa kinyume na matakwa ya Gavana wa Madinah. Gavana alimuonya asitoe fa’twa hiyo hadharani, lakini kwa kuridhika kuwa ndio haki, Imam Malik alitoa maoni yake hadharani na akachapwa viboko hadharani kwa tendo hilo. Katika kazi muhimu alizoziacha Imam Malik ni kitabu chake al-Muwatta chenye mjumuiko wa Hadith na mafundisho ya Mtume(s.a.w) ya ibada na mas’ala mbalimbali ya Kiislamu. Imam Malik alitawafu mwaka 179A.H.Madinah.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 3194

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu

KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.

Soma Zaidi...
Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)

Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Makubaliano ya Mkataba wa Al Fudhul

Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 13. Hapa utajifunza historia ya Mkataba wa al fudhul na makubaliano yake.

Soma Zaidi...
Ni nani alikuwa sahaba wa mwisho kufariki

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu nani alikuwa wamwisho kufariki katika masahaba wa Mtume kwa mujibu wa historia

Soma Zaidi...