Navigation Menu



Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba

Mtume (s.

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba

Mtume (s.a.w) alivyoandaa Ummah wa Kiislamu Makkah.
- Mtume (s.a.w) alitumia kila aina ya fursa iliyopatikana katika kuufikisha
ujumbe Uislamu kwa watu wengine.



- Mtume (s.a.w) alifikisha ujumbe wa Uislamu kwa watu na makabila mbali
mbali kwa siri na dhahiri kutokana na uadui wa Maquraish dhidi yake.



- Mtume (s.a.w) alitumia mikataba kwa kuandaa ummah wa kiislamu kutoka
sehemu mbali mbali hasa mji wa Madinah (Yathrib) kama ifuatavyo;




Mikataba ya ‘Aqabah.
- Hii ilikuwa ni baina ya Mtume (s.a.w) na watu wanaotoka nje ya mji wa
Makkah hasa waliokuja kuhiji msimu wa Hija.



- Mtume (s.a.w) alikutana na kikosi cha kwanza kabisa cha watu sita (6)
kutoka Madinah (Yathrib) wa kabila la Khazraj, baada ya kuwafikishia
ujumbe wa Uislamu, walisilimu na wakaahidi kuufikisha kwao Madina.



- Mwaka uliofuata, 621 A.D, kikundi kingine cha waislamu 12 (2 Aus na
10 Khazraj) walikutana na Mtume (s.a.w) kwa siri eneo la ‘Jaratul
‘Aqabah’ na kuweka mkataba wa kwanza wa ‘Aqaba na kukubaliana
yafuatatayo;


i.Hawataabudu chochote isipokuwa Allah (s.w) pekee.
ii.Hawataiba wala hawatapokonya misafara ya biashara njiani.
iii.Hawatazini.
iv.Hawatawaua watoto wao tena.
v.Hawatasema uongo wala hawatawasingizia wengine uovu.


vi.Hawatamuasi Mtume kwa kila atakalowaamrisha na watakuwa waaminifu kwake kwa hali yeyote iwayo.

- Mtume (s.a.w) aliwapa mwalimu wa kuwafundisha Uislamu, ‘Mus’ab bin
Umair.
- Mwaka uliofuata, 622 A.D.walimjia Mtume (s.a.w) waislamu 75
(wanawake 2) wakiongozwa na mwalimu wao, ‘Mus’ab na kufunga
Mkataba wa pili wa ‘Aqabah sehemu ile ile kwa kukubaliana kuwa;



oMtume na Waislamu wote wa Makka wahamie Madinah (Yathrib) na wao watawapokea na kuwahifadhi dhidi ya maadui wao.

- Mtume (s.a.w) aliwachagulia viongozi 12 (9 Khazraj na 3 Aus) na watu
watakaokuwa chini ya kila kiongozi, na wanaume wote walimpa Mtume
(s.a.w) mkono wa bai’at kwa maana ya utii wao kwake.



- Baada ya kikundi hicho kurejea na kufika Madinah salama, ndipo Mtume
(s.a.w) aliwatangazia waislamu wote wa Makkah kuhamia Madinah.



- Na takriban baada ya miezi miwili hivi, Waislamu wote wenye uwezo wa
kuhama walishahamia Yathrib (Madinah) kwenda kujiimarisha zaidi.



Mafunzo yatokanayo na Mikataba ya ‘Aqabah katika kuandaa ummah.
i.Waislamu hawana budi kupanga mikakati na mambo yao kwa siri ili kutojulikana na maadui wa Uislamu na waislamu.



ii.Waislamu hawanabudi kutotangaza mikakati yao kwa maadui kabla ya kuitekeleza ili kuepukana na njama ya kukwamishwa.



iii.Waislamu hawanabudi kuwa na mipango na mikakati (long and short term strategies) ya muda mrefu na mfupi katika kuandaa Ummah.



iv.Uongozi bora na makini ni jambo la msingi sana la mwanzo katika kuusimamisha na kuuendeleza Uislamu katika jamii.



v.Waislamu wanaharakati wanapoazimia jambo lolote katika kuusimamisha na kuuendeleza Uislamu, hawana budi kujifunga nalo na kupeana kiapo cha utekelezaji.



vi.Waislamu hawana budi kutumia kila aina ya fursa itakayojitokeza katika kuusimamisha na kuuendeleza Uislamu katika jamii.



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1595


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

HISTORIA NA SIRA YA UISLAMU NA MTUME MUHAMMAD KUTOKA KUZALIWA MPAKA KUFARIKI NA HARAKATI ZAKE
Soma Zaidi...

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu
Musa(a. Soma Zaidi...

Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋 Soma Zaidi...

tarekh
MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU). Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika Surat Ar-Raad (13:19-26)
Soma Zaidi...

Hitimisho juu ya Historia ya maimam wanne
Soma Zaidi...

Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake
Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri. Soma Zaidi...

KAZI ALIZOFANYA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KABLA YA UTUME
KAZI ALIZOKUWA AKIFANYA MUHAMMAD (S. Soma Zaidi...

MAMA YAKE MTUME MUHAMMAD (S.A.W) ANAMLEA MTUME MUHAMAD AKIWA NA UMRI WA MIAKA MINNE (4)
KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s. Soma Zaidi...

tarekh 02
FAMILIA YA MTUME (S. Soma Zaidi...