Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba

Mtume (s.

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba

Mtume (s.a.w) alivyoandaa Ummah wa Kiislamu Makkah.
- Mtume (s.a.w) alitumia kila aina ya fursa iliyopatikana katika kuufikisha
ujumbe Uislamu kwa watu wengine.



- Mtume (s.a.w) alifikisha ujumbe wa Uislamu kwa watu na makabila mbali
mbali kwa siri na dhahiri kutokana na uadui wa Maquraish dhidi yake.



- Mtume (s.a.w) alitumia mikataba kwa kuandaa ummah wa kiislamu kutoka
sehemu mbali mbali hasa mji wa Madinah (Yathrib) kama ifuatavyo;




Mikataba ya ‘Aqabah.
- Hii ilikuwa ni baina ya Mtume (s.a.w) na watu wanaotoka nje ya mji wa
Makkah hasa waliokuja kuhiji msimu wa Hija.



- Mtume (s.a.w) alikutana na kikosi cha kwanza kabisa cha watu sita (6)
kutoka Madinah (Yathrib) wa kabila la Khazraj, baada ya kuwafikishia
ujumbe wa Uislamu, walisilimu na wakaahidi kuufikisha kwao Madina.



- Mwaka uliofuata, 621 A.D, kikundi kingine cha waislamu 12 (2 Aus na
10 Khazraj) walikutana na Mtume (s.a.w) kwa siri eneo la ‘Jaratul
‘Aqabah’ na kuweka mkataba wa kwanza wa ‘Aqaba na kukubaliana
yafuatatayo;


i.Hawataabudu chochote isipokuwa Allah (s.w) pekee.
ii.Hawataiba wala hawatapokonya misafara ya biashara njiani.
iii.Hawatazini.
iv.Hawatawaua watoto wao tena.
v.Hawatasema uongo wala hawatawasingizia wengine uovu.


vi.Hawatamuasi Mtume kwa kila atakalowaamrisha na watakuwa waaminifu kwake kwa hali yeyote iwayo.

- Mtume (s.a.w) aliwapa mwalimu wa kuwafundisha Uislamu, ‘Mus’ab bin
Umair.
- Mwaka uliofuata, 622 A.D.walimjia Mtume (s.a.w) waislamu 75
(wanawake 2) wakiongozwa na mwalimu wao, ‘Mus’ab na kufunga
Mkataba wa pili wa ‘Aqabah sehemu ile ile kwa kukubaliana kuwa;



oMtume na Waislamu wote wa Makka wahamie Madinah (Yathrib) na wao watawapokea na kuwahifadhi dhidi ya maadui wao.

- Mtume (s.a.w) aliwachagulia viongozi 12 (9 Khazraj na 3 Aus) na watu
watakaokuwa chini ya kila kiongozi, na wanaume wote walimpa Mtume
(s.a.w) mkono wa bai’at kwa maana ya utii wao kwake.



- Baada ya kikundi hicho kurejea na kufika Madinah salama, ndipo Mtume
(s.a.w) aliwatangazia waislamu wote wa Makkah kuhamia Madinah.



- Na takriban baada ya miezi miwili hivi, Waislamu wote wenye uwezo wa
kuhama walishahamia Yathrib (Madinah) kwenda kujiimarisha zaidi.



Mafunzo yatokanayo na Mikataba ya ‘Aqabah katika kuandaa ummah.
i.Waislamu hawana budi kupanga mikakati na mambo yao kwa siri ili kutojulikana na maadui wa Uislamu na waislamu.



ii.Waislamu hawanabudi kutotangaza mikakati yao kwa maadui kabla ya kuitekeleza ili kuepukana na njama ya kukwamishwa.



iii.Waislamu hawanabudi kuwa na mipango na mikakati (long and short term strategies) ya muda mrefu na mfupi katika kuandaa Ummah.



iv.Uongozi bora na makini ni jambo la msingi sana la mwanzo katika kuusimamisha na kuuendeleza Uislamu katika jamii.



v.Waislamu wanaharakati wanapoazimia jambo lolote katika kuusimamisha na kuuendeleza Uislamu, hawana budi kujifunga nalo na kupeana kiapo cha utekelezaji.



vi.Waislamu hawana budi kutumia kila aina ya fursa itakayojitokeza katika kuusimamisha na kuuendeleza Uislamu katika jamii.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2188

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)

Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s.

Soma Zaidi...
tarekh 01

NASABA YA MTUME (S.

Soma Zaidi...
Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.

Soma Zaidi...
tarekh 3

KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba.

Soma Zaidi...
HISTORIA YA BANI ISRAIL

Nabii Musa na Harun walikuwa na kazi kubwa mbili; kwanza, kuwakomboa Bani Israil kutokana na dhuluma waliyokuwa wakifanyiwa na Firaun na Serikali yake, na pili, kuwarudisha kwenye nchi yao takatifu ya Palestina.

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...