Mkewe Al-Aziz hakumkatia tamaa Yusufu(a.
Mkewe Al-Aziz hakumkatia tamaa Yusufu(a.s). Uovu wake ulimchochea kuzidi kumuandama Yusufu(a.s). Alimpa Yusufu chaguzi mbili: Ama akubali kuzini naye au amfanyie hila atiwe gerezani.
................Na kama hatafanya ninalomuarisha, hakika atafungwa gerezani na atakuwa miongoni mwa madhalili(12:32)
Kwa kumukhofu Allah(s.w) na kuchukia tendo chafu la zinaa, Yusufu akasema Ee Mola wangu! Nastahabu zaidi gereza kuliko haya wanayoniitia........(12:33)
Yusufu(a.s) alijikuta yupo gerezani, si kama mhalifu bali aliyeonewa kwa uadilifu na uaminifu wake. Lakini pia hakusononeneka kwa dhulma ile aliyofanyiwa kwani kuwepo gerezani kulimtenga na watu waovu waliotaka kumtia kwenye uchafu.
Uadilifu na sifa zake njema zilikuwa zimezagaa kila mahali. Hata alipoingia gerezani wafungwa wenzake walimpa heshima ya pekee. Walikiri kwamba Yusufu(a.s) ni miongoni mwa watu wazuri.
Ilitokea kule gerezani wafungwa wenzake wakaota ndoto na kumtaka Yusufu(a.s) awape tafsiri yake.
Na wakaingia pamoja naye gerezani vijana wawili. Mmoja wao akasema: Hakika nimeona (katika ndoto) nakamua ulevi”; na mwingine akasema: Hakika nimeona(katika) ndoto nabeba mikate juu ya kichwa changu ambayo ndege wanaila. Tuambie tafsiri yake; kwa yakini sisi tunakuona wewe ni miongoni mwa watu wazuri(12:36)
Yusufu(a.s) aliwakubalia ombi lao lakini kabla ya kuwatafsiria ndoto zao aliwalingania kwa Allah(s.w) kwakuwauliza:
“Enyi wafungwa wenzangu wawili! Je, waungu wengi wanaofarikiana ndio bora (kuabudiwa) au Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu (juu ya kila kitu?)” (12:39).
Hamuabudu badala yake (Mwenyezi Mungu) ila majina (matupu) mliyopanga nyinyi wenyewe na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuteremsha dalili kwa hayo. Haikuwa hukumu ila hii ya Mwenyezi Mungu tu; ameamrisha msimuabudu yoyote isipokuwa Yeye tu. Hiyo ndiyo Dini iliyonyooka lakini watu wengi hawajui.” (12:40).
Baada ya kuwafikishia ujumbe huu muhimu, Nabii Yusufu (a.s) akaanza kuwaeleza taawili ya ndoto zao kuwa:
Enyi wafungwa wenzangu wawili! Mmoja katika ninyi atarejeshwa kazini kwake akamnyweshe bwana wake ulevi. na yule mwingine atauawa kwa kusulubiwa, na ndege watamla kichwa chake. Limekwishakatwa (huko kwa Firaun) hili jambo mlilokuwa mkiuliza (12:41)
Kisha Yusufu(a.s) akamuomba yule atakayetolewa gerezani:
“...........Unikumbuke mbele ya bwana wako;(umwambie kuwa nimeonewa nimefungwa bure); Lakini shetani alimsahaulisha kumkumbusha bwana wake. kwa hivyo akakaa gerezani (Nabii Yusufu) baadhi ya miaka (baada ya hapa)(12:42)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowKULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s.
Soma Zaidi...KAZI ALIZOKUWA AKIFANYA MUHAMMAD (S.
Soma Zaidi...KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji.
Soma Zaidi...Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a.
Soma Zaidi...Katika zama za kale Mayahudi walikatazwa kufanya kazi siku ya Jumamosi.
Soma Zaidi...Fat-h Makkah (Kukombolewa Makkah).
Soma Zaidi...