Ijue dawa ya sulphadoxine na pyrimethamine (sp)

Post hii inahusu zaidi dawa ya Sp , kirefu cha dawa hii ni sulphadoxine na pyrimethamine hii dawa ilitumika kutibu malaria kwa kipindi fulani lakini sasa hivi imebaki kutumiwa na wajawazito kama kinga ya kuwazuia kupata malaria.

Ijue dawa ya  Sp.

1. Kama tulivyotangulia kusema kwamba ni dawa ambayo ina majina mawili ambayo ni sulphadoxine na pyrimethamine ambayo uunda dawa hii ya Sp, dawa hii iko kwenye mfumo wa vidonge ambapo kila sehemu ina milligrams zake ambapo sulphadoxine ina milligrams miatano na pyrimethamine ina miilgram ishirini na tano jumla kuu ufanya miligramu mia tano ishirini na tano.

 

2. Dawa hii utumika sana kwa wanawake wajawazito na haipendekezwi kama mojawapo ya dawa za kutibu malaria kwa sasa, ila kwa wajawazito ikitokea wakapata malaria ingawa wanatumia sp matibabu yao wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya ili wawaeleze cha kufanya.

 

3. Kwa akina Mama wajawazito wanapaswa kutumia vidonge hivi vya sp pindi wanapogundua kwamba ni wajawazito kwa sababu vidonge hivi vikimezwa uenda moja kwa moja mpaka kwenye sehemu ya mwanzo ya kondo la nyuma na kuweza kuzuia wadudu wanaosababisha malaria kutoingia kwenye kondo la nyuma na kusababisha madhara mbalimbali kama vile mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, mtoto kutokuwa na afya nzuri akiwa tumboni, au mimba kutoka.

 

4. Kwa hiyo akina mama wanapaswa kujua kabisa kwamba hizi dawa ni za muhimu sana wakati wa ujauzito kwa sababu bila matumizi ya dawa hizi madhara makubwa yanaweza kutokea ambayo usababisha kukosa mtoto, au mimba kutoka, mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, haya matatizo utokea kwa sababu ya kuwepo kwa wadudu wa malaria kwenye kondo la nyuma na kusababisha uharibifu kwenye sehemu hiyo.

 

5. Akina mama wote wanapaswa kutumia dawa hizi isipokuwa wale wenye aleji na sulphur , au wanaotumia dawa ambazo kwa kitaalamu huitwa cotrimoxazole au wale wamama ambao wamegundulika na malaria kwa hiyo wanapaswa kufuata kawaida ya matibabu ya ugonjwa wa malaria kadri ya wataalamu wa afya.

 

6. Kwa hiyo akina mama wenye imani potovu kuhusu dawa hizi wanapaswa kujua kwamba dawa hizi ni za muhimu sana na kutotumia dawa hizi ni hatari sana hasa kwa afya ya mtoto.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 5252

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 web hosting    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya sulfonamide dawa inayopambana na maambukizi ya bakteria mwilini.

Post hii inahusu zaidi dawa ya sulphonamide ni mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria ni dawa au antibiotics ya mda mrefu na pia matumizi yake sio makubwa sana kwa sababu ya kuwepo kwa antibiotics zenye ngu

Soma Zaidi...
Fahamu aina ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu

Post hii inahusu zaidi aina mojawapo ya dawa ya penicillin ambayo ufanya kazi kwa mda mrefu, dawa hii kwa kitaamu huiitwa procaine benzyl penicillin.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza aleji au mzio

Post hii inahusu zaidi dawa hydrocortisone kwa kutuliza aleji au mzio, kwa kawaida Kuna mda mtu anapotumia dawa Fulani anakuwa na mabadiliko mbalimbali kama vile kifua kubana , viupele na mambo kama hayo.

Soma Zaidi...
Tiba mbadala za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Njia ya kupitisha dawa kwenye mdomo na vipengele vyake

Posti hii inahusu zaidi njia ya kupitisha dawa kwenye mdomo na vipengele vyake, hii njia dawa umengenywa kwenye tumbo na kupitia kwenye utumbo mdogo na baadae kwenye damu,

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya kaoline

Post hii inahusu dawa ya kaoline katika kutibu au kuzuia kuharisha ni dawa ambayo imependekezwa kutumiwa hasa kwa wale walioshindwa kutumia dawa ya loperamide.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa tiba ya kifua kikuu

Post hii inahusu zaidi mgawanyiko wa tiba ya kifua kikuu, kwa kawaida tiba hii imegawanyika katika sehemu kuu mbili.

Soma Zaidi...
Dawa za Anesthesia katika kutuliza maumivu.

Unapotaka kufanyiwa baadhi ya matibabu unatakiwa kupewa ganzi ama nusu kaput ili kulifanyia usihisi maumivu. Dawa hizi zinajulikana na Anesthesia.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu maumivu ya jino

Utaijuwa Dawa ya maumivu ya jino, sababu za maumivu ya jino na njia za kujikinga na maumivu ya jino

Soma Zaidi...