IJUE DAWA YA SULPHADOXINE NA PYRIMETHAMINE (SP)


image


Post hii inahusu zaidi dawa ya Sp , kirefu cha dawa hii ni sulphadoxine na pyrimethamine hii dawa ilitumika kutibu malaria kwa kipindi fulani lakini sasa hivi imebaki kutumiwa na wajawazito kama kinga ya kuwazuia kupata malaria.


Ijue dawa ya  Sp.

1. Kama tulivyotangulia kusema kwamba ni dawa ambayo ina majina mawili ambayo ni sulphadoxine na pyrimethamine ambayo uunda dawa hii ya Sp, dawa hii iko kwenye mfumo wa vidonge ambapo kila sehemu ina milligrams zake ambapo sulphadoxine ina milligrams miatano na pyrimethamine ina miilgram ishirini na tano jumla kuu ufanya miligramu mia tano ishirini na tano.

 

2. Dawa hii utumika sana kwa wanawake wajawazito na haipendekezwi kama mojawapo ya dawa za kutibu malaria kwa sasa, ila kwa wajawazito ikitokea wakapata malaria ingawa wanatumia sp matibabu yao wanapaswa kuwaona wataalamu wa afya ili wawaeleze cha kufanya.

 

3. Kwa akina Mama wajawazito wanapaswa kutumia vidonge hivi vya sp pindi wanapogundua kwamba ni wajawazito kwa sababu vidonge hivi vikimezwa uenda moja kwa moja mpaka kwenye sehemu ya mwanzo ya kondo la nyuma na kuweza kuzuia wadudu wanaosababisha malaria kutoingia kwenye kondo la nyuma na kusababisha madhara mbalimbali kama vile mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, mtoto kutokuwa na afya nzuri akiwa tumboni, au mimba kutoka.

 

4. Kwa hiyo akina mama wanapaswa kujua kabisa kwamba hizi dawa ni za muhimu sana wakati wa ujauzito kwa sababu bila matumizi ya dawa hizi madhara makubwa yanaweza kutokea ambayo usababisha kukosa mtoto, au mimba kutoka, mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, haya matatizo utokea kwa sababu ya kuwepo kwa wadudu wa malaria kwenye kondo la nyuma na kusababisha uharibifu kwenye sehemu hiyo.

 

5. Akina mama wote wanapaswa kutumia dawa hizi isipokuwa wale wenye aleji na sulphur , au wanaotumia dawa ambazo kwa kitaalamu huitwa cotrimoxazole au wale wamama ambao wamegundulika na malaria kwa hiyo wanapaswa kufuata kawaida ya matibabu ya ugonjwa wa malaria kadri ya wataalamu wa afya.

 

6. Kwa hiyo akina mama wenye imani potovu kuhusu dawa hizi wanapaswa kujua kwamba dawa hizi ni za muhimu sana na kutotumia dawa hizi ni hatari sana hasa kwa afya ya mtoto.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    2 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    3 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    4 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    5 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    6 Magonjwa na afya    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Wanaopasawa kutumia PEP
PEP Ni dawa ambazo utumiwa na watu wanaojamiiana na watu wenye virus vya ukimwi ila wenyewe hawawezi kupata kwa sababu ya kutumia dawa hizo. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya sulfonamide dawa inayopambana na maambukizi ya bakteria mwilini.
Post hii inahusu zaidi dawa ya sulphonamide ni mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria ni dawa au antibiotics ya mda mrefu na pia matumizi yake sio makubwa sana kwa sababu ya kuwepo kwa antibiotics zenye nguvu zaidi kuliko yenyewe,lakina dawa nyingine zikishindikana yenyewe bado inatumika na watu wanapona. Soma Zaidi...

image Ifahamu dawa ya furosemide.
Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu dawa ya loperamide dawa ya kuzuia kuharusha
Post hii inahusu zaidi dawa ya loperamide ni dawa ambayo inazuia kuharisha ni dawa inayofanya kazi kuanzia kwenye utumbo na pia usaidia kutuliza maumivu ya tumbo Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ambazo uchangia kupungua kwa nguvu za kiume
Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali ambazo uchangia katika kupunguza nguvu za kiume , hii ni kwa sababu ya wataalamu mbalimbali wanavyosema Soma Zaidi...

image Fahamau madhara ya flagyl (Metronidazole)
Flagyl ni nini? Flagyl (metronidazole) ni antibiotic. Inapigana na bakteria katika mwili wako. Flagyl hutumiwa kutibu maambukizo ya bakteria ya uke, tumbo, ngozi, viungo na njia ya upumuaji. Soma Zaidi...

image Fahamu Dawa inayotibu minyoo iitwayo albenza (albendazole)
Albenza (albendazole) hutumika kutibu magonjwa ya minyoo ya ndani ikiwa ni pamoja na maambukizi ya minyoo ya tegu. Albenza inafanya kazi kukomesha kuenea kwa maambukizo ya minyoo kwenye chanzo, na kukata chanzo chao cha nishati, na hivyo kuzuia kuenea kwa uvamizi zaidi. Ondoa minyoo hatari haraka na bila maumivu kwa kutumia albenza (albendazole) Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya kuzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya cloxacillin ambayo Iko kwenye kundi mojawapo la penicillin ambalo uzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria. Soma Zaidi...

image Fahamu Dawa inayotumika kupunguza maumivu (ibuprofen)
Ibuprofen ni mojawapo ya dawa zinazotumiwa sana duniani kote! Ili kupunguza maumivu na kuvimba, agiza Ibuprofen leo na upate afya bora! Ni kiungo amilifu katika dawa za jina kama vile Motrin na zaidi. Ibuprofen pia inaweza kuuzwa kama: Advil Motrin, Nuprin. Soma Zaidi...

image Fahamu dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa
Post hii inahusu zaidi dawa ya diazepam katika kutuliza kifafa, ni dawa ambayo matumizi yake yanaweza kuingilia pote kwenye kutuliza kifafa na pia kwa wagonjwa wa akili. Soma Zaidi...