image

Fahamu kuhusu dawa ya streptomycin

Post hii inahusu zaidi dawa ya streptomycin ni dawa mojawapo ya kupambana na bakteria hasa wanaoshambulia mfumo wa hewa.

Fahamu dawa ya streptomycin kama dawa inayopambana na bakteria wanaoshambulia mfumo wa hewa .

1. Streptomycin ni mojawapo wa dawa ya kupambana na bakteria hasa bakteria ambao ushambulia mfumo wa hewa , bakteria hao kwa kitaamu huiitwa mycobacterium ni bakteria ambao ueneza kifua kikuu kwa kutumia dawa hii pamoja na dawa nyingine kifua kikuu uweza kutibika kwa kufuata kanuni na utaratibu wa matibabu.

 

2. Dawa hii ya streptomycin inafanya kazi kwa kupitia kwenye mzunguko wa damu na ikifika kwa bakteria inashambulia Ganda la juu ambalo kwa kitaamu huiitwa cell wall na kuingia kwa Ganda la ndani kwa kitaamu huiitwa cell membrane na kujibanza kwenye protein kwa hiyo uzuia protini ya bakteria kuendelea kuzalishwa na kuzuia kuendelea kukua na kusababisha kuharibu kwa bakteria na ugonjwa hauwezi kuendelea kuwepo tena, na mafanikio ya kupona utokea kulingana na udumifu na maelekezo katika matumizi ya dawa.

 

3. Katika kufanya kazi dawa hii upitia sehemu mbalimbali na kuweza kufanikisha uponyaji kwa hiyo dawa hiyo inapoingia mwilini na ikishasambaa uweza kupitia kwenye maji maji mbalimbali kwenye mwili ambayo Kwa kitaamu huiitwa extracellular fluids, na inapiita kwenye plasenta au kwa lugha nyepesi kwenye kondo la nyuma kama mama ana mimba, pia zinaweza kupitia hata kwenye maziwa ya mama kama ananyonyesha na kwenda kwenye maji maji ambayo yamo kwenye ubongo kwa kitaamu huiitwa cerebral Spinal fluids.

 

4. Kwa hiyo kama mama ana mimba anaweza kumkinga mtoto dhidi ya maambukizi ya kifua kikuu,na kama mama ananyonyesha pia anaweza kumsaidia mtoto asipate kama hajapata kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wanaweza kusaidia hata vichanga na wanaonyonya .

 

5. Kwa matumizi ya dawa hii Kuna wale ambao hawapaswi kutumia dawa hii kwa mfano wenye aleji na streptomycin,wale wenye upungufu wa damu hawapaswi kutumia, watoto chini ya miezi miwili hawapaswi kutumia na wale wenye matatizo ya Figo wanapaswa kutumia dawa hii kwa kiwango kidogo na kwa wakati mwingine wanawapunguzia dozi.

 

6. Pia dawa hii nayo Ina mahudhi madogo madogo kama maumivu ya kichwa, kuwepo kwa ndoto za kutisha kwa baadhi ya wagonjwa au pengine mgonjwa anaweza kuwa na magonjwa ya akili kama vile kuwa mkimya sana au pengine kuchangamka sana ila ni kwa watu wachache mno, kwa sababu dawa hii upitia kwenye mmengenyo wa chakula Kuna hatari ya kupata kichefuchefu na kutapika, kuharisha pia utokea kukiambatatana na maumivu ya tumbo.

 

7. Kwa watumiaji wa mda mrefu wanaweza kuwa na matatizo ya macho au kuona kwa shida na pia mwili unaweza kuwa na vi upele pamoja na kujikuna kwa mda mrefu na pia dawa hizi zina tabia ya kupunguza damu mwilini wakati wa kutumia ni vizuri kuwa makini kwa wale wenye tatizo la upungufu wa damu wakati wa kutumia dawa hizi, kwa hiyo maudhi haya madogo madogo yakizidi na kuwa kama ugonjwa ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya Ili kubadilishiwaa dawa au kutoa huduma yoyote inayofaa.

 

8. Vile vile dawa hizi uweza kuingiliana na dawa nyingine na kumaliza nguvu dawa hizo na kufanya uponyaji kuwa wa shida, kwa hiyo kwa watumiaji wa penicillin na cephalosporin , dawa hii ya streptomycin uweza kumaliza nguvu dawa hizo na kufanya uponyaji wa kutumia penicillin na cephalosporin kushindwa kufanikiwa, kwa hiyo ni vizuri kuongea na mgonjwa ipasavyo Ili kuweza kuwa na uhakika wa dawa anazozitimia na kuweza kuwepo kwa tiba ya kweli na inayofaa.

 

9. Kwa hiyo katika matibabu au kutumia dawa hii ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya na sio kutumia dawa hii kiholela kwa sababu Zina matokeo mengine ni ya kuhitaji uangalizi na pia dawa hii uingiliana na dawa nyingine ni vizuri kabisa kabla ya kutumia dawa hii kuwaona wataalamu wa afya Ili kuweza kutumia dawa kwa umakinu Zaidi na kuepuka matatizo ambayo yanaweza kutokea.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 693


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Fahamu kundi la veta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo.
Post hii inahusu zaidi kundi la beta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo,hili kundi lina dawa mbalimbali ambazo utumika katika matibabu ya magonjwa ya moyo na kila dawa tutaiongelea tofauti tofauti ili kuweza kujua kazi zake. Soma Zaidi...

Ifahamu dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji
Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi. Soma Zaidi...

Faida za vidonge vya zamiconal
Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya faida ambazo upatikana kutokana na vidonge vya zamiconal,ni vidonge ambavyo utibu au kusaidia kwenye matatizo ya viungo vya uzazi. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya parental Artusnate dawa ya kutibu malaria sugu
Post hii inahusu zaidi dawa ya Parental Artusnate ni dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria sugu kama tutakavyoona hapo baadaye. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya mucolytic dawa ya kutibu kikohozi
Post hii inahusu zaidi dawa ya mucolytic katika kutibu kikohozi kwa watu wazima na watoto. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa za magonjwa ya moyo
Post hii inahusu zaidi dawa za magonjwa ya moyo, ni dawa ambazo utumika kusaidia pale moyo kama umeshindwa kufanya kazi ipasavyo. Soma Zaidi...

Ifahamu dawa ya furosemide.
Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix Soma Zaidi...

Dawa ya Carvedilol na kazi yake.
Posti hii inahusu zaidi dawa ya Carvedilol na kazi yake, ni dawa inayotibu au kuzuia mapigo ya moyo ambayo yako juu na kusababisha kulegeza kwa mishipa ya moyo. Soma Zaidi...

Dawa za kutibu kiungulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za kutibu kiungulia Soma Zaidi...

IJUE DAWA YA AMOXLINE (antibiotic) NA MATUMIZI YAKE
Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake. Soma Zaidi...

Fahamu kazi za homoni katika kupamba na kansa.
Post hii inahusu zaidi homoni mbalimbali ambazo upambana na kansa, hizi homoni zikitumika vizuri matokeo yake huwa na mazuri pia kwa wagonjwa wa kansa. Soma Zaidi...

Matibabu ya Fangasi ukeni na dawa za fangasi wanaoshambulia uke.
Fangasi wanaweza kushambulia uke, kwa juu kwenye mashhav ya uke ama kwa ndani. Hali hii inaweza kusababisha miwasho na maumivu pia. Inaweza kusababisha michubuko na kutofurahia tendo la ndoa. Makala hii inakwenda kukujuza dawa na matibabu ya fangasi ukeni Soma Zaidi...