picha

Fahamu kuhusu dawa ya streptomycin

Post hii inahusu zaidi dawa ya streptomycin ni dawa mojawapo ya kupambana na bakteria hasa wanaoshambulia mfumo wa hewa.

Fahamu dawa ya streptomycin kama dawa inayopambana na bakteria wanaoshambulia mfumo wa hewa .

1. Streptomycin ni mojawapo wa dawa ya kupambana na bakteria hasa bakteria ambao ushambulia mfumo wa hewa , bakteria hao kwa kitaamu huiitwa mycobacterium ni bakteria ambao ueneza kifua kikuu kwa kutumia dawa hii pamoja na dawa nyingine kifua kikuu uweza kutibika kwa kufuata kanuni na utaratibu wa matibabu.

 

2. Dawa hii ya streptomycin inafanya kazi kwa kupitia kwenye mzunguko wa damu na ikifika kwa bakteria inashambulia Ganda la juu ambalo kwa kitaamu huiitwa cell wall na kuingia kwa Ganda la ndani kwa kitaamu huiitwa cell membrane na kujibanza kwenye protein kwa hiyo uzuia protini ya bakteria kuendelea kuzalishwa na kuzuia kuendelea kukua na kusababisha kuharibu kwa bakteria na ugonjwa hauwezi kuendelea kuwepo tena, na mafanikio ya kupona utokea kulingana na udumifu na maelekezo katika matumizi ya dawa.

 

3. Katika kufanya kazi dawa hii upitia sehemu mbalimbali na kuweza kufanikisha uponyaji kwa hiyo dawa hiyo inapoingia mwilini na ikishasambaa uweza kupitia kwenye maji maji mbalimbali kwenye mwili ambayo Kwa kitaamu huiitwa extracellular fluids, na inapiita kwenye plasenta au kwa lugha nyepesi kwenye kondo la nyuma kama mama ana mimba, pia zinaweza kupitia hata kwenye maziwa ya mama kama ananyonyesha na kwenda kwenye maji maji ambayo yamo kwenye ubongo kwa kitaamu huiitwa cerebral Spinal fluids.

 

4. Kwa hiyo kama mama ana mimba anaweza kumkinga mtoto dhidi ya maambukizi ya kifua kikuu,na kama mama ananyonyesha pia anaweza kumsaidia mtoto asipate kama hajapata kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wanaweza kusaidia hata vichanga na wanaonyonya .

 

5. Kwa matumizi ya dawa hii Kuna wale ambao hawapaswi kutumia dawa hii kwa mfano wenye aleji na streptomycin,wale wenye upungufu wa damu hawapaswi kutumia, watoto chini ya miezi miwili hawapaswi kutumia na wale wenye matatizo ya Figo wanapaswa kutumia dawa hii kwa kiwango kidogo na kwa wakati mwingine wanawapunguzia dozi.

 

6. Pia dawa hii nayo Ina mahudhi madogo madogo kama maumivu ya kichwa, kuwepo kwa ndoto za kutisha kwa baadhi ya wagonjwa au pengine mgonjwa anaweza kuwa na magonjwa ya akili kama vile kuwa mkimya sana au pengine kuchangamka sana ila ni kwa watu wachache mno, kwa sababu dawa hii upitia kwenye mmengenyo wa chakula Kuna hatari ya kupata kichefuchefu na kutapika, kuharisha pia utokea kukiambatatana na maumivu ya tumbo.

 

7. Kwa watumiaji wa mda mrefu wanaweza kuwa na matatizo ya macho au kuona kwa shida na pia mwili unaweza kuwa na vi upele pamoja na kujikuna kwa mda mrefu na pia dawa hizi zina tabia ya kupunguza damu mwilini wakati wa kutumia ni vizuri kuwa makini kwa wale wenye tatizo la upungufu wa damu wakati wa kutumia dawa hizi, kwa hiyo maudhi haya madogo madogo yakizidi na kuwa kama ugonjwa ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya Ili kubadilishiwaa dawa au kutoa huduma yoyote inayofaa.

 

8. Vile vile dawa hizi uweza kuingiliana na dawa nyingine na kumaliza nguvu dawa hizo na kufanya uponyaji kuwa wa shida, kwa hiyo kwa watumiaji wa penicillin na cephalosporin , dawa hii ya streptomycin uweza kumaliza nguvu dawa hizo na kufanya uponyaji wa kutumia penicillin na cephalosporin kushindwa kufanikiwa, kwa hiyo ni vizuri kuongea na mgonjwa ipasavyo Ili kuweza kuwa na uhakika wa dawa anazozitimia na kuweza kuwepo kwa tiba ya kweli na inayofaa.

 

9. Kwa hiyo katika matibabu au kutumia dawa hii ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya na sio kutumia dawa hii kiholela kwa sababu Zina matokeo mengine ni ya kuhitaji uangalizi na pia dawa hii uingiliana na dawa nyingine ni vizuri kabisa kabla ya kutumia dawa hii kuwaona wataalamu wa afya Ili kuweza kutumia dawa kwa umakinu Zaidi na kuepuka matatizo ambayo yanaweza kutokea.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/12/22/Thursday - 08:13:30 pm Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 1603

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 web hosting    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Fahamu dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa ya captopril katika matibabu ya magonjwa ya moyo, ni dawa ambayo imo kwenye kundi la vasodilators na ufanya Kazi mbalimbali zinazousu magonjwa ya moyo.

Soma Zaidi...
Dawa ya UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa ya UTI

Soma Zaidi...
dawa ya kutibu infection kwenye kizazi nisaidie doctor

Je unasumbuliwa na maambukizi na mashambulizi ya virusi na bakteria kwenye sehemu za siri ama via vya uzazi?. Posti hii inakwenda kuupa ushauri.

Soma Zaidi...
Dawa ya Rifampicin na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya sulfonamide dawa inayopambana na maambukizi ya bakteria mwilini.

Post hii inahusu zaidi dawa ya sulphonamide ni mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria ni dawa au antibiotics ya mda mrefu na pia matumizi yake sio makubwa sana kwa sababu ya kuwepo kwa antibiotics zenye ngu

Soma Zaidi...
Dawa za fangasi ukeni

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za fangasi ukeni

Soma Zaidi...
Tiba mbadala za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya hydralazine katika matibabu ya magonjwa ya moyo

Post hii inahusu zaidi dawa ya hydralazine katika matibabu ya magonjwa ya moyo, dawa hii imetoka kwenye kundi la vasodilators, na pia usaidia sana kwenye matibabu ya magonjwa ya moyo.

Soma Zaidi...
Dawa inaitwa koflame ukitumia inashida kwa mama mjamzito? Maumivu ya mgongo na nyonga zinasumbua

Maumivu ya mgongo hutokea sana kwa wajawazito. Ijapokuwa ni hali ya usumbufu sana ila hakikisha hautumii madawa kiholela kutoka maduka ya dawa ama miti shamba. Kwani ukikisea kidogobinawezabhatarisha afya ya mtoto

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza kifafa inayoitwa phenobarbital

Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa.

Soma Zaidi...