Post hii inahusu zaidi dawa ya Parental Artusnate ni dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria sugu kama tutakavyoona hapo baadaye.
1.Ni aina ya dawa ambayo inatumika kutibu malaria sugu, tunahita malaria sugu kwa sababu ya dalili zake ambazo ujitokeza kwa mgonjwa, dalili hizo ni kama ifuatavyo, mgonjwa anakuwa amechoka sana, mgonjwa anakuwa amezimia au hana fahamu, pia kunakuwepo na upungufu wa damu kwa sababu ya kuharibikiwa kwa chembe chembe za seli, tabia ya mgonjwa ubadirika na pengine kuna wagonjwa ambao malaria uwaingia kichwani na kutaka kukimbia kwa kitaalamu huitwa cerebral malaria au malaria iliyomuingia mtu kichwani.
2. Pia dalili nyingine mgonjwa anakuwa anapumua vibaya mpaka anawekewa mashine ya kumsaidia kupumua, na kwa wakati mwingine mgonjwa anakuwa anatokwa damu kwenye fizi na kwenye pua, na dalili nyingine mgonjwa anakuwa na njano au akitapika utafika njano tu kwa sababu ya kuharibikiwa kwa chembe chembe ndogo za seli,au dalili nyingine mgonjwa anaweza kuwa na degedege hata kama ni mtoto au mtu mzima kwa malaria sugu degedege uwapata wote.pia mgonjwa anashindwa kula kabisa au ikitokea akala anatapika kila kitu.
3. Baada ya kuona dalili kama hizi moja kwa moja hizi ni dalili za malaria sugu kwa hiyo Parental Artusnate utumika kutibu malaria ya aina hizi, na pia vipimo upima kama vile damu ni kuthibitisha kuwepo kwa malaria, kwa kawaida dawa hii upitishwa kwenye damu dozi ya kwanza mgonjwa hupata na baada ya kuipata atapata nyingine baada ya masaa kumi na mawili na pia anasubiri baada ya masaa mengine kumi na mawili kwa kawaida dozi ambayo utokea ni dozi tatu na hapo mgonjwa anakuwa ameshapata nafuu na kama hali haijakaa sawa anaweza kuongezewa kwa kufuatana na utaratibu wa wataalamu wa afya.
4. Kwa kawaida baada ya kutumia dawa ya Parental Artusnate ni vizuri na ni lazima mgonjwa amalize kwa kutumia vidonge vya ALU ili kumalizia malaria iliyobaki, kwa kawaida dawa hizi iko kwenye muundo wa Poda na pia ina vibox viwili moja ni ndogo ambayo kwa kitaalamu kuna aina ya dawa ambayo uchanganyikana na dawa ambayo imo kwenye ka kopo kakubwa na baadae Poda uchanganyawa na ile dawa mpaka inakuwa clealy kwa ajili ya alivyo agiziwa Mgonja .
5. Kwa hiyo dawa hizi inapaswa kutumiwa na watu kwa kufuata utaratibu na kuomba ushauri kwa waty mbalimbali kuhusu dawa hizi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Ibuprofen ni mojawapo ya dawa zinazotumiwa sana duniani kote! Ili kupunguza maumivu na kuvimba, agiza Ibuprofen leo na upate afya bora! Ni kiungo amilifu katika dawa za jina kama vile Motrin na zaidi. Ibuprofen pia inaweza kuuzwa kama: Advil Motrin,
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.
Soma Zaidi...Nitakujuza dawa ya kutibu vidonda vya tumbo, na kutibu vidonda vya tumbo sugu
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa mbadala za vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia kuu nne ambazo utumika kumpatia mgonjwa dawa, Ili kumpatia mgonjwa dawa Kuna njia za kutumia kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...