Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba hii ni dawa ambayo usaidia kutibu maambukizi ya bakteria na pia ni dawa ambayo imo kwenye makundi ya penicillin kama tulivyoona hapo kwenye utangulizi na pia dawa hii inaweza kusaidia pia kupambana na bakteria ambao utoa asidi Ili kuweza kuzuia kazi ya dawa, kama dawa husika haipo ampicillin inaweza kutumika.
2. Kwa kawaida ampicillin usaidia katika matibabu ya maambukizi ya bakteria kwenye Koo,sikio,mkojo na pia usaidia katika matibabu ya nimonia, dawa hii huwa na container lake kila container Ina milligrams mia mbili hamsini na na nyingine huwa na miigram mia tano na pia milligrams utolewa kulingana na wataalamu wa afya na pia dawa hii utolewa kila baada ya masaa sita , kabla ya kutumia dawa hii ni vizuri kutumiwa dakika thelathini kabla ya kula chakula.
3. Dawa pia IPO kwenye mfumo wa unga au poda na huwa na maji maalumu yametengwa kwa ajili ya kuchanganya poda hiyo na maji, maji hayo kwa kitaamu huiitwa water for injection, kwa hiyo dawa hiyo uchanganywa na maji na utikiswa na kuhakikisha kwamba poda haionekani tena na pia mgonjwa uweza kupewa dawa hiyo, kwa upande wa dozi utegemea umri na uzito wa mgonjwa. Pia dawa hiyo inawezekana kutolewa kwenye paja au Tako na pia kwenye mishipa ya damu.
Tunapaswa kufahamu kwamba mchanganyiko wa dawa inayopitia kwenye damu na kwenye paja au Tako ni tofauti kwa sababu ya kwenye mishipa inaenda Moja kwa moja kwenye damu kwa hiyo tunaongeza maji zaidi ya Ile inayopitia kwenye nyama ( Tako na paja).
4. Kwa wakati mwingine kuna syrup hizi ni kwa upande hasa wa watoto, mchanganyiko ni kutumia milligrams mia ishilini na tano kwenye mills tano na pia mtoto anapewa, mara nyingi hizi dawa zinakuja zimechanganywa Moja kwa moja na chupa Huwa na maagizo namna ya kutumia, kwa hiyo wazazi wa mtoto uweza kupewa maagizo na jinsi ya kumpatia mtoto dawa hiyo.
5. Dawa hii ya ampicillin na yenyewe Ina tabia kama dawa zote au makundi ya penicillin kwa hiyo kila mtu anaweza kutumia dawa hii ila kwa wale ambao Wana aleji na ampicillin hawapaswi kutumia dawa hii na pia wale wenye aleji ya penicillin hawapaswi kutumia kwa sababu dawa hii imo miongoni mwa makundi ya penicillin na pia kwa wale wenye tatizo la upungufu wa damu wanapaswa kuitumia kwa taahadhari au waitumie kwenye uangalizi maalumu Ili wasije kuleta tatizo kubwa zaidi kwa sababu dawa hii Ina tabia ya kupunguza damu hasa kwa watumiaji wa mara kwa mara.
6. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kujitokeza wakati wa kuitumia maudhi hayo ni pamoja na maumivu kwenye joint, kichefuchefu na kutapika, maumivu ya tumbo , kizunguzungu na upungu wa damu au kama Kuna mtu ana kidonda au sehemu inayotoa damu anaweza kuendelea kutoa damu kwa mda mrefu wakati akiwa anatumia dawa hii. Kwa hiyo haya maudhi madogo madogo yakitokea ni kawaida wakati wa kutumia dawa hii ila yakiongezeka na kuleta madhara zaidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya na kubadilishiwaa dawa.
7. Pia ni vizuri kutumia dawa hii kwa ushauri wa wataalamu wa afya sio kutumia dawa hii kiholela kwa sababu matokeo yake yanaweza kuwa mabaya hasa kwa watu wenye damu kidogo wakitumia dawa hii wakiwa nyumbani wanaweza kuleta tatizo juu ya tatizo na pia kwa wale wenye sickle cell yaani wenye matatizo ya kuishiwa damu wanapaswa kuitumia dawa hii wakiwa kwenye uangalizi maalumu au wapime wingi wa damu kabla ya kutumia ai tatizo kama litakuwa kubwa zaidi na kuleta madhara ni Bora wabadilidhiwe na kupewa dawa ambazo hazitaleta madhara kwao.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi dawa ya epinephrine kwa kutuliza aleji ni dawa ambayo imependekezwa kutuliza aleji kama dawa ya hydrocortisone, Prednisone hazipo au zimeshindwa kufanya kazi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya cephalosporin katika kupambana na bakteria, ni mojawapo ya kundi kati ya makundi ya kupambana na bakteria ambalo ufanya Kazi kama penicillin.
Soma Zaidi...Nitakujuza dawa ya kutibu vidonda vya tumbo, na kutibu vidonda vya tumbo sugu
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi imani potofu kuhusu madawa yanayotolewa hospitalini, ni imani waliyonayo Watu hasa Watu wa bi vijijini na hata wa mjini nao wameanza kutumia madawa ya miti shamba kwa wingi.
Soma Zaidi...Je unasumbuliwa na maambukizi na mashambulizi ya virusi na bakteria kwenye sehemu za siri ama via vya uzazi?. Posti hii inakwenda kuupa ushauri.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za fangasi na matumizi yake kwa kutumia dawa ya fluconazole kama dawa mojawapo ya fangasi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi madhara ya Tiba mionzi kwa wagonjwa wa saratani, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wanaotumia mionzi katika matibabu ya saratani.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya ALU ila kwa jina jingine huitwa dawa ya mseto,ni aina ya dawa inayotumika kutibu ugonjwa wa malaria ya kawaida.
Soma Zaidi...PoPosti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo unaweza kutumia iwapo umepata tatizo la kiungulia
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya back bone pain kwa matibabu ya mgongo, ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa kutuliza maumivu ya mgongo.
Soma Zaidi...