image

Fahamu kazi ya dawa ya ampicillin inayopambana na maambukizi ya bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya ampicillin, ni mojawapo ya dawa za kutibu maambukizi ya bakteria kwenye mwili wa binadamu ba pia ni dawa ambayo IPO kwenye kundi la penicillin kundi hili kwa kitaa huitwa broad spectrum penicillin

Fahamu dawa ya ampicillin.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba hii ni dawa ambayo usaidia kutibu maambukizi ya bakteria na pia ni dawa ambayo imo kwenye makundi ya penicillin kama tulivyoona hapo kwenye utangulizi na pia dawa hii inaweza kusaidia pia kupambana na bakteria ambao utoa asidi Ili kuweza kuzuia kazi ya dawa, kama dawa husika haipo ampicillin inaweza kutumika.

 

2. Kwa kawaida ampicillin usaidia katika matibabu ya maambukizi ya bakteria kwenye Koo,sikio,mkojo na pia usaidia katika matibabu ya nimonia, dawa hii huwa na container lake kila container Ina milligrams mia mbili hamsini na na nyingine huwa na miigram mia tano na pia milligrams utolewa kulingana na wataalamu wa afya na pia dawa hii utolewa kila baada ya masaa sita , kabla ya kutumia dawa hii ni vizuri kutumiwa dakika thelathini kabla ya kula chakula.

 

3. Dawa pia IPO kwenye mfumo wa unga au poda na huwa na maji maalumu yametengwa kwa ajili ya kuchanganya poda hiyo na maji, maji hayo kwa kitaamu huiitwa water for injection, kwa hiyo dawa hiyo uchanganywa na maji na utikiswa na kuhakikisha kwamba poda haionekani tena na pia mgonjwa uweza kupewa dawa hiyo, kwa upande wa dozi utegemea umri na uzito wa mgonjwa. Pia dawa hiyo inawezekana kutolewa kwenye paja au Tako na pia kwenye mishipa ya damu.

 

Tunapaswa kufahamu kwamba mchanganyiko wa dawa inayopitia kwenye damu na kwenye paja au Tako ni tofauti kwa sababu ya kwenye mishipa inaenda Moja kwa moja kwenye damu kwa hiyo tunaongeza maji zaidi ya Ile inayopitia kwenye nyama ( Tako na paja).

 

4. Kwa wakati mwingine kuna syrup hizi ni kwa upande hasa wa watoto, mchanganyiko  ni kutumia milligrams mia ishilini na tano kwenye mills tano na pia mtoto anapewa, mara nyingi hizi dawa zinakuja zimechanganywa Moja kwa moja na chupa  Huwa na maagizo namna ya kutumia, kwa hiyo wazazi wa mtoto uweza kupewa maagizo na jinsi ya kumpatia mtoto dawa hiyo.

 

5. Dawa hii ya ampicillin na yenyewe Ina tabia kama dawa zote au makundi ya penicillin kwa hiyo kila mtu anaweza kutumia dawa hii ila kwa wale ambao Wana aleji na ampicillin hawapaswi kutumia dawa hii na pia wale wenye aleji ya penicillin hawapaswi kutumia kwa sababu dawa hii imo miongoni mwa makundi ya penicillin na pia kwa wale wenye tatizo la upungufu wa damu wanapaswa kuitumia kwa taahadhari au waitumie kwenye uangalizi maalumu Ili wasije kuleta tatizo kubwa zaidi kwa sababu dawa hii Ina tabia ya kupunguza damu hasa kwa watumiaji wa mara kwa mara.

 

6. Vile vile dawa hii Ina maudhi madogo madogo ambayo yanaweza kujitokeza wakati wa kuitumia maudhi hayo ni pamoja na maumivu kwenye joint, kichefuchefu na kutapika, maumivu ya tumbo , kizunguzungu na upungu wa damu au kama Kuna mtu ana kidonda au sehemu inayotoa damu anaweza kuendelea kutoa damu kwa mda mrefu wakati akiwa anatumia dawa hii. Kwa hiyo haya maudhi madogo madogo yakitokea ni kawaida wakati wa kutumia dawa hii ila yakiongezeka na kuleta madhara zaidi ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya na kubadilishiwaa dawa.

 

7. Pia ni vizuri kutumia dawa hii kwa ushauri wa wataalamu wa afya sio kutumia dawa hii kiholela kwa sababu matokeo yake yanaweza kuwa mabaya hasa kwa watu wenye damu kidogo wakitumia dawa hii wakiwa nyumbani wanaweza kuleta tatizo juu ya tatizo na pia kwa wale wenye sickle cell yaani wenye matatizo ya kuishiwa damu wanapaswa kuitumia dawa hii wakiwa kwenye uangalizi maalumu au wapime wingi wa damu kabla ya kutumia ai tatizo kama litakuwa kubwa zaidi na kuleta madhara ni Bora wabadilidhiwe na kupewa dawa ambazo hazitaleta madhara kwao.

 

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2926


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Fahamu kuhusu dawa ya streptomycin
Post hii inahusu zaidi dawa ya streptomycin ni dawa mojawapo ya kupambana na bakteria hasa wanaoshambulia mfumo wa hewa. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu dawa ya Nystatin
Post hii inahusu zaidi dawa ya Nystatin ni mojawapo ya dawa ambayo utumika kwenye ngozi. Soma Zaidi...

Kazi za Dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria
Posti hii inahusu zaidi kazi za dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria kali, ni dawa ambayo inatumika sana kutibu Malaria kali. Soma Zaidi...

Mebendazole kama dawa ya kutibu Minyoo.
Post hii inahusu zaidi dawa ya Mebendazole kama Dawa ya kutibu Minyoo, ni dawa inayotumiwa na watu wengi pale wanapokuwa na minyoo, walio wengi wamefanikiwa kupona kwa kutumia Dawa hii. Soma Zaidi...

Fahamu matumizi ya Dawa iitwayo Aspirin.
Aspirini Ni dawa ya kutuliza maumivu.Majina yanayoaminika zaidi katika kutuliza maumivu sasa yanapatikana kwa njia mbadala inayookoa gharama kwa kutumia Aspirini. Aspirini inayopendwa na familia kwa miongo kadhaa, mara nyingi hutumiwa kupunguza maumivu y Soma Zaidi...

Dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo.
Posti hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo, ni Aina mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu Minyoo inayosababishwa na bakteria mbalimbali. Soma Zaidi...

dawa ya minyoo, dalili za minyoo na sababu na vyanzo vya minyoo
MWISHO Mwisho tunapenda kusema kuwa unapohisi una minyoo kutokana na dalili ambazo tumezitaja humu, nenda kituo cha afya ukapate ushauri zaidi. Soma Zaidi...

Fahamu tiba ya jino
Post hii inahusu zaidi tiba ya jino,ni tiba ya kawaida kwa watu walio na matatizo ya meno, kwa kawaida tunafahamu kwamba jino huwa halina dawa ila dawa yake huwa ni kungoa lakini Leo nawaletea habari njema kwamba jino sio kungoa tena ila Kuna tiba ambayo Soma Zaidi...

Dawa ya kutibu macho
Hizi ndio dawa za macho yenye ukavu, kuwasha ama kutoa machozi Soma Zaidi...

Dawa ya Carvedilol na kazi yake.
Posti hii inahusu zaidi dawa ya Carvedilol na kazi yake, ni dawa inayotibu au kuzuia mapigo ya moyo ambayo yako juu na kusababisha kulegeza kwa mishipa ya moyo. Soma Zaidi...

Dawa ya fangasi ukeni
Makala hii itakueleza dawa ya kutibu fangasi wa ukeni Soma Zaidi...

Fahamu dawa za kutuliza kifafa inayoitwa phenobarbital
Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa. Soma Zaidi...