Dawa ya Rifampicin na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.
Dawa ya Rifampicin na kazi zake.
1.Dawa ya Rifampicin ni dawa ambayo utumika katika kipindi cha kwanza na cha pili katika vipindi vikuu viwili vya matibabu ya kifua kikuu, hii dawa usaidia kuuua bakteria wanaosababisha kifua kikuu na pia kuzuia protein ya bakteria isizalishwe kwa hiyo bakteria hao hawawezi kuishi na kuzaliana kwa sababu ya kuwepo kwa dawa ya Rifampicin.
2.Pia hii dawa usaidia kuua bakteria anayeitwa TB bacill na pia dawa hiii uweza kuua bakteria ambao wameshaene kwenye mwili wa binadamu na pia uua bakteria wale ambao wamekaa mda mrefu kwenye mwili wa binadamu, kwa hiyo tunaona faida kubwa ya dawa hii tunapaswa kuitumia kwa maelekezo ya wataalamu wa afya, pia dawa hii haiwezi kutumika ikiwa yenyewe bali huwa na mchanganyiko wa madawa mengine.
3.Dawa hii ya Rifampicin utumiwa na watu wenye kifua kikuu lakini sio wote wenye kifua kikuu wanaweza kutumia kwa sababu mbalimbali kwa mfano wale wanaotumia uzazi wa mpango na wana Ugonjwa wa kifua kikuu wanapaswa kuona madaktari ili waweze kupata njia za uzazi wa mpango hambazo haziingilian na dawa ya Rifampicin kwa sababu kuna njia za uzazi wa mpango ukizitumia pamoja na dawa ya Rifampicin dawa hii uweza kumaliza dawa za njia ya mpango nguvu na mtu akapata mimba.
4.Pamoja na kutumia njia hii kuna maudhi mbalimbali ambayo yanaweza kujitokeza katika kutumia dawa hizi ni kama kichefuchefu, kutapika na hata kuharisha kwa wagonjwa wengine, na maumivu ya kichwa yanaweza kutokea pia pamoja na homa, kwa hiyo hizi Dalili zikitokea mgonjwa hasiogope ni kawaida ila kwa wanaoanza maudhi haya yakiendelea wanapaswa kwenda hospitalini ili kuangalia labda kuna tatizo fulani.
5.Kwa kubwa ugonjwa huu unatibika tunapaswa kuwapeleka wagonjwa wetu hospitali ikiwa wataonesha Dalili za kifua kikuu ambazo ni pamoja na homa za mara kwa mara, kupungua uzito , kukohoa kwa wiki mbili na kukonda hizi ni baadhi ya Dalili tunapaswa kuwahi mapema kwa sababu Ugonjwa huu usambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kama mgonjwa hajatumia dawa akishatumia dawa kwa wiki mbili hawezi kuambukiza wengine.
6.Kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii ili kuwaleta wagonjwa wao hospitalini wasiwafiche na kuna imani potovu ambayo utokea kubwa mgonjwa wa kifua kikuu ufuchwa ndani wakidai kuwa ana Maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi kumbe ni kifua kikuu kwa sababu ya kufanana kwa baadhi ya Dalili, kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa ili kuweza kutokomeza kabisa janga hili
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Mebendazole kama dawa ya kutibu Minyoo.
Post hii inahusu zaidi dawa ya Mebendazole kama Dawa ya kutibu Minyoo, ni dawa inayotumiwa na watu wengi pale wanapokuwa na minyoo, walio wengi wamefanikiwa kupona kwa kutumia Dawa hii.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya kutuliza mishutuko.
Post hii inahusu zaidi dawa ya phenytoin,ni dawa inayotuliza mishutuko mbalimbali inayoweza kutokea kwenye mwili na kutokana na mishutuko hiyo tunaweza kupata kifafa.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya kuzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya cloxacillin ambayo Iko kwenye kundi mojawapo la penicillin ambalo uzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria.
Soma Zaidi...Dawa za Anesthesia katika kutuliza maumivu.
Unapotaka kufanyiwa baadhi ya matibabu unatakiwa kupewa ganzi ama nusu kaput ili kulifanyia usihisi maumivu. Dawa hizi zinajulikana na Anesthesia.
Soma Zaidi...Dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Soma Zaidi...Umuhimu wa kutumia dawa za ARV
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za ARV kwa wathirika wa virusi vya ukimwi .pia tutangalia kwa undani mambo ya kuzingatia kwa wathirika wanaotumia ARV .pamoja na kujali watu wanaotumia dawa hizo .
Soma Zaidi...