picha

Dawa ya Rifampicin na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.

Dawa ya Rifampicin na kazi zake.

1.Dawa ya Rifampicin ni dawa ambayo utumika katika kipindi cha kwanza na cha pili katika vipindi vikuu viwili vya matibabu ya kifua kikuu, hii dawa usaidia kuuua bakteria wanaosababisha kifua kikuu na pia kuzuia protein ya bakteria isizalishwe kwa hiyo bakteria hao hawawezi kuishi na kuzaliana kwa sababu ya kuwepo kwa dawa ya Rifampicin.

 

2.Pia hii dawa usaidia kuua bakteria anayeitwa TB bacill  na pia dawa hiii uweza kuua bakteria ambao wameshaene kwenye mwili wa binadamu na pia uua bakteria wale ambao wamekaa mda mrefu kwenye mwili wa binadamu, kwa hiyo tunaona faida kubwa ya dawa hii tunapaswa kuitumia kwa maelekezo ya wataalamu wa afya, pia dawa hii haiwezi kutumika ikiwa yenyewe bali huwa na mchanganyiko wa madawa mengine.

 

3.Dawa hii ya Rifampicin utumiwa na watu wenye kifua kikuu lakini sio wote wenye kifua kikuu wanaweza kutumia kwa sababu mbalimbali kwa mfano wale wanaotumia uzazi wa mpango na wana Ugonjwa wa kifua kikuu wanapaswa kuona madaktari ili waweze kupata njia za uzazi wa mpango hambazo haziingilian na dawa ya Rifampicin kwa sababu kuna njia za uzazi wa mpango ukizitumia pamoja na dawa ya Rifampicin dawa hii uweza kumaliza dawa za njia ya mpango nguvu na mtu akapata mimba.

 

4.Pamoja na kutumia njia hii kuna maudhi mbalimbali ambayo yanaweza kujitokeza katika kutumia dawa hizi ni kama kichefuchefu, kutapika na hata kuharisha kwa wagonjwa wengine, na maumivu ya kichwa yanaweza kutokea pia pamoja na homa, kwa hiyo hizi Dalili zikitokea mgonjwa hasiogope ni kawaida ila kwa wanaoanza maudhi haya yakiendelea wanapaswa kwenda hospitalini ili kuangalia labda kuna tatizo fulani.

 

5.Kwa kubwa ugonjwa huu unatibika tunapaswa kuwapeleka wagonjwa wetu hospitali ikiwa wataonesha Dalili za kifua kikuu ambazo ni pamoja na homa za mara kwa mara, kupungua uzito , kukohoa kwa wiki mbili na kukonda hizi ni baadhi ya Dalili tunapaswa kuwahi mapema kwa sababu Ugonjwa huu usambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kama mgonjwa hajatumia dawa akishatumia dawa kwa wiki mbili hawezi kuambukiza wengine.

 

6.Kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii ili kuwaleta wagonjwa wao hospitalini wasiwafiche na kuna imani potovu ambayo utokea kubwa mgonjwa wa kifua kikuu ufuchwa ndani wakidai kuwa ana Maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi kumbe ni kifua kikuu kwa sababu ya kufanana kwa baadhi ya Dalili, kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa ili kuweza kutokomeza kabisa janga hili

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/02/16/Wednesday - 07:14:09 am Topic: Dawa Main: Afya File: Download PDF Views 3366

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Dawa na matibabu ya presha ya kushuka

Hapa utajifuanza dalili za presha ya kushuka, na dawa ya presha ya kushuka na nJia za kuzuiaama kudhibiti presha ya kushuka

Soma Zaidi...
Fahamu dawa zinazotumika kwenye matibabu ya kansa

Post hii inahusu zaidi dawa ambazo zinatumika kwenye matibabu ya kansa, dawa hizi usaidia kuharibu seli ambazo ambazo hazistahili kwa kitaalamu huitwa malignant seli.

Soma Zaidi...
Tiba mbadala za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Faida za vidonge vya zamiconal

Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya faida ambazo upatikana kutokana na vidonge vya zamiconal,ni vidonge ambavyo utibu au kusaidia kwenye matatizo ya viungo vya uzazi.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya Theophylline katika kutibi mfumo wa upumuaji

Post hii inahusu zaidi dawa ya theophylline ni dawa inayofanya kazi kwenye mfumo wa upumuaji.

Soma Zaidi...
Fahamu zaidi kuhusiana na Dawa inayotibu shinikizo la damu. iitwayo LASIX

Lasix (Furosemide) iko katika kundi la dawa zinazoitwa vidonge vya maji (loop diuretics) vidonge vya maji. Lasix hutumiwa kupunguza uvimbe mwilini unaosababishwa na kushindwa kwa moyo, ugonjwa wa ini, au ugonjwa wa figo. Kwa matibabu ya dalili nyingi.La

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya potassium sparing

Post hii inahusu zaidi dawa ya potassium sparing katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

Soma Zaidi...
dawa ya minyoo, dalili za minyoo na sababu na vyanzo vya minyoo

MWISHO Mwisho tunapenda kusema kuwa unapohisi una minyoo kutokana na dalili ambazo tumezitaja humu, nenda kituo cha afya ukapate ushauri zaidi.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji

Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.

Soma Zaidi...
Dawa ya Panadol au paracetamol katika kutuliza maumivu

Posti hii inahusu zaidi kazi ya paracetamol katika kutuliza maumivu, ni Aina ya dawa ambayo utumiwa sana katika kutuliza maumivu kwa wagonjwa.

Soma Zaidi...