Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.
Dawa ya Rifampicin na kazi zake.
1.Dawa ya Rifampicin ni dawa ambayo utumika katika kipindi cha kwanza na cha pili katika vipindi vikuu viwili vya matibabu ya kifua kikuu, hii dawa usaidia kuuua bakteria wanaosababisha kifua kikuu na pia kuzuia protein ya bakteria isizalishwe kwa hiyo bakteria hao hawawezi kuishi na kuzaliana kwa sababu ya kuwepo kwa dawa ya Rifampicin.
2.Pia hii dawa usaidia kuua bakteria anayeitwa TB bacill na pia dawa hiii uweza kuua bakteria ambao wameshaene kwenye mwili wa binadamu na pia uua bakteria wale ambao wamekaa mda mrefu kwenye mwili wa binadamu, kwa hiyo tunaona faida kubwa ya dawa hii tunapaswa kuitumia kwa maelekezo ya wataalamu wa afya, pia dawa hii haiwezi kutumika ikiwa yenyewe bali huwa na mchanganyiko wa madawa mengine.
3.Dawa hii ya Rifampicin utumiwa na watu wenye kifua kikuu lakini sio wote wenye kifua kikuu wanaweza kutumia kwa sababu mbalimbali kwa mfano wale wanaotumia uzazi wa mpango na wana Ugonjwa wa kifua kikuu wanapaswa kuona madaktari ili waweze kupata njia za uzazi wa mpango hambazo haziingilian na dawa ya Rifampicin kwa sababu kuna njia za uzazi wa mpango ukizitumia pamoja na dawa ya Rifampicin dawa hii uweza kumaliza dawa za njia ya mpango nguvu na mtu akapata mimba.
4.Pamoja na kutumia njia hii kuna maudhi mbalimbali ambayo yanaweza kujitokeza katika kutumia dawa hizi ni kama kichefuchefu, kutapika na hata kuharisha kwa wagonjwa wengine, na maumivu ya kichwa yanaweza kutokea pia pamoja na homa, kwa hiyo hizi Dalili zikitokea mgonjwa hasiogope ni kawaida ila kwa wanaoanza maudhi haya yakiendelea wanapaswa kwenda hospitalini ili kuangalia labda kuna tatizo fulani.
5.Kwa kubwa ugonjwa huu unatibika tunapaswa kuwapeleka wagonjwa wetu hospitali ikiwa wataonesha Dalili za kifua kikuu ambazo ni pamoja na homa za mara kwa mara, kupungua uzito , kukohoa kwa wiki mbili na kukonda hizi ni baadhi ya Dalili tunapaswa kuwahi mapema kwa sababu Ugonjwa huu usambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kama mgonjwa hajatumia dawa akishatumia dawa kwa wiki mbili hawezi kuambukiza wengine.
6.Kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa kwa jamii ili kuwaleta wagonjwa wao hospitalini wasiwafiche na kuna imani potovu ambayo utokea kubwa mgonjwa wa kifua kikuu ufuchwa ndani wakidai kuwa ana Maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi kumbe ni kifua kikuu kwa sababu ya kufanana kwa baadhi ya Dalili, kwa hiyo elimu inapaswa kutolewa ili kuweza kutokomeza kabisa janga hili
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole katika kutibu Minyoo, ni Aina mojawapo ya dawa ambayo usaidia kutibu Minyoo inayosababishwa na bakteria mbalimbali.
Soma Zaidi...Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ,ni dawa ambayo utumiwa na watu wengi kwa matibabu ya ugonjwa wa Malaria.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa zinazosaidis katika kutuliza magonjwa ya akili, dawa hii kwa kitaamu huiitwa chlorpromazine ni dawa ambayo utumiwa na watu wenye tatizo la magonjwa ya akili na kwa kiasi kikubwa huwa sawa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi antibiotics ya asili, ni antibiotics inayotumia vitu vya kila siku na ya kawaida na mtu akaweza kupona kabisa na kufanya kazi kama antibiotics ya vidonge vya kawaida.
Soma Zaidi...hapa utajifunza dalili za fangasi, dawa ya fangasi na aina za fangasi, pia nitakujuza njia za kukabiliana na fangasi
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya macrolide ni mojawapo ya dawa ya kutibu au kupambana na bakteria na upambana na bakteria wafuatao streptococcus pyogenes, staphylococcus aureus na haihusiki na haemophilia influenza ambao usababisha maambukizi kwenye mfumo w
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za kisukari, kwa sababu ya kuwepo kwa ugonjwa wa kisukari vilevile kuna dawa zake ambazo utumika kurekebisha sukari kama imepanda au kushuka.
Soma Zaidi...Zijuwe aina za minyoo na tiba yake. Dawa 5 za kutibu minyoo ya aina zote
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kundi la beta blockers katika matibabu ya magonjwa ya moyo,hili kundi lina dawa mbalimbali ambazo utumika katika matibabu ya magonjwa ya moyo na kila dawa tutaiongelea tofauti tofauti ili kuweza kujua kazi zake.
Soma Zaidi...