image

HUKUMU ZA MADD YAANI KUVUTA HERUFI KWENYE USOMAJI WA QURAN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

HUKUMU ZA MADD YAANI KUVUTA HERUFI KWENYE USOMAJI WA QURAN

SURA YA KUMI
MADD-Madd-Twab'iy
MADD
Katika hukmu ya Tajwiyd ni urefushaji au uongezaji wa sauti, kwa maana kuivuta sauti ya herufi wakati inapokutana na moja ya herufi za madd kuifanya iwe ndefu.
Herufi za madd ni tatu:
ا • Alif saakinah iliyotanguliwa na fat-hah: قَالَ
ي • Yaa saakinah iliyotanguliwa na kasrah: قِيلَ
و • Waaw saakinah iliyotanguliwa na dhwammah: يَقُولُ

Madd imegawanyika sehemu mbili kuu:
الْمَدُّ الطَبِيعي • Al-Maddutw-Twabiy’iy pia huitwa: الْمدّ الأصْلي - Al-Maddul-Aswliy
الْمَدّ الْفَرْعي • - Al-Maddul-Far-’iy

1.Maddu-twabiy’y
Hii ni madd ya asili ambayo madd zote zimepatikana kutoka hapa. Maddd hii ni ya haraka 2 na haijuzu kuzipunguza wala kuzizidisha na ni makosa kufanya vinginevyo. Madd hii itavutwa katika hali zote ima katika hali ya kuunganisha maneno au katika hali ya kusimama. Ili itokee madd hii haihitaji sababu zingine ila ni asili ya neno tu ni lazima liwe na madd hiyo.
MADD

Halikadhalika madd hii kuna maeneo saba ambayo haipatikani wakati wa kuunga maneno ila itapatikana tu pale msomaji anaposimama. Na sehemu hizi zipo saba tu na zinapatikana kwa kuwepo alif na hii huitwa jina la الْفات السبع (Alifaatus-Sab-‘iy - Alif Saba).
MADD

(maddutw-twabiy’iy) nyinginezo ni:
مَدُّ الصِّلَّةِ الصُّغْرى . 1 - Maddusw-Swillatis-Sughraa
2 مَدُّ الْعِوَضِ . - Maddul-‘Iwadhw
مَدُّ الْبَدَل . 3 – Maddul-Badl
مَدُّ التَّمْكِين . 4 – Maddut-Tamkiyn
ألِفَات حَيُّ طَهْر . 5 – Alifaatu Hayyun Twahr

. 1 Maddusw-Swillatis-Sughraa:
Swillah ni kuunganisha herufi ya ه (haa) ya kiwakilishi1 na herufi ya madd yenye kunasibiyana na i’raab yake (dhwammah au kasrah) kitakapokuwa hicho kiwakilishi cha ه ni chenye i’raab na kipo baina ya herufi mbili zenye i’raab. Swillah hii imegawanyika sehemu mbili mojawapo ni hii ya assughraa (ndogo) na ya pili yake ni ya al-kubraa (kubwa) itakayokuja maelezo yake katika Maddul-Far-’iy.
Shart zake:
i) Kuweko na i’raab (sio sukuwn au herufi ya madd) kabla ya ه (haa)
ii) Kuweko na i’raab ifuatie katika neno la pili.
iii) Haifuatwi na hamzah.
MADD


Hukumu hii haizingatiwi katika maeneo mawili kwenye qurani. Aya hizi moja wapo huvutwa (Al-Furqaan (25: 69) ) ijapokuwa haina sifa za kuvutwa na nyingine haivutwi (Az-Zumar (39 : 7)) ijapokuwa ina sifa za kuvutwa. Na hii ni kutokana kuwa hivyo ndivyo inavyosomwa. Maeneo hayo ni haya;-
MADD

(Az-Zumar (39 : 7) Al-Furqaan (25: 69)

. 2 Maddul-Badal
Kanuni ya badal: ni kuja kwa hamzah mbili zenye kufuatana moja baada ya nyengine, ya kwanza ikawa na i’raab na ya pili ikawa saakin katika neno moja, hivyo hubadilishwa hamzah ya pili saakinah na kuwa herufi ya madd yenye kuwiana na i’raab ya hamzah ya kwanza. Hukmu yake ni kuvutwa harakah mbili.
MADD


Maddul-‘Iwadhw
Ni madd inayotokea wakati wa kusimama msomaji katika neno lenye fathataan (tanwiyn fat-hah). Hukmu yake ni huvutwa kwa harakah mbili. Kusimama kwenye ة (taa marbuwtwah ya kike iliyofungwa) kunapelekea kutokuwepo hukmu hii ya مَدُّ الْعِوَض (maddul-‘iwadhw) kwani wakati huo huondoka tanwiyn na kusimamiwa kwa ه (haa) saakinah.

4.Maddut-Tamkiyn
Ni madd inayotokea wakati ي mbili zimekutana, ya kwanza ina shaddah na kasrah na ya pili ina sukuwn. Imeitwa مَدُّ التَّمْكِين kwa sababu inatamkwa ikiwa imethibitika kwa sababu ya shaddah. ي ya pili ambayo ina sukuwn inavutwa kwa harakah mbili.
MADD


5 - Alifaatu-Hayyin-Twahur
Ni مَدُ الطَّبِيعي (maddutw-twabiy’iy) inayotokana katika kutamkwa baadhi ya الحروف المتقاطعة (Al-Huruwf Al-Mutaqatw-twa’ah)1 zinazoanzia baadhi ya
Suwrah, kwa vile herufi hizo zinatamkwa kama herufi za hijaaiyah طا حا
ها را . Nazo zimeundwa katika ibara ya حيّ طهر (hayyun twahur) kwa jina
jingine huitwa ألِفَاتُ حَيٍّ طَهُ ر (Alifaatu hayyin twahur).
MADD


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1339


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake
Soma Zaidi...

Kutokea Kweli Matukio yaliyotabiriwa katika Qur-an
Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr
Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii Soma Zaidi...

HUKUMU ZA IDGHAM
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MADD
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MADD YAANI KUVUTA HERUFI KWENYE USOMAJI WA QURAN
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Mpangilio wa quran ni wa kipekee na uliotumia ujuzi mkubwa
Soma Zaidi...

DARSA ZA QURAN
Soma Zaidi...

Madai ya makafiri dhidi ya quran na hoja zao
Soma Zaidi...

Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid
Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo. Soma Zaidi...

quran na sayansi
QURANI KATIKA ZAMA ZA SAYANSI NA TEKNOLOJIAAsalaalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh. Soma Zaidi...

Maana ya Quran na Majina ya quran n amaana zao
Soma Zaidi...