Muhammad hakufundishwa quran na padri Bahira

Muhammad hakufundishwa quran na padri Bahira

(a)Dai la Kufundishwa na Padri Bahira:



Baadhi ya makafiri wanadai kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) alijifunza Uyahudi na Ukristo katika safari zake mbili za biashara alizofanya Sham (Syria), hasa katika safari yake ya kwanza alipokutana na Padri Bahirah, alipokuwa na umri wa miaka 12. Tunavyojifunza katika historia ni kuwa Bahirah alikutana na Mtume (s.a.w) njiani na kuashiria kwa Ami yake Abutwalib, kuwa anamkisia kijana wake (Muhammad) ana sifa za yule mtume aliyetabiriwa katika Injili (Rejea Qur-an 61:6).


Je, inamkinika kuwa mazungumzo haya ya njiani ya muda mfupi yawe ndiyo yaliyompelekea Mtume (s.a.w) kuandika Qur-an miaka 28 baada ya makutano hayo? Ikumbukwe kuwa Mtume (s.a.w) alianza kushushiwa wahy wa Quran alipokuwa na umri wa miaka arobaini ambapo alikutana na Bahirah akiwa na umri wa miaka kumi na mbili.



Safari ya pili ya Mtume (s.a.w) kwenda Syria kwa biashara ni pale alipokodiwa na Bibi Khadijah alipokuwa na umri miaka ishirini na tano. Katika kumbukumbu za historia, Mtume (s.a.w) hakufanya mkutano wowote na Wakristo wala Mayahudi kabla ya Utume.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1613

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.

Soma Zaidi...
Nini maana ya Quran

Post hii inakwenda kukuambia maana ya Quran

Soma Zaidi...
Fadhila za kusoma surat al Baqarah

Surat al Baqarah ni katika sura ambazo tunapaswa tuwe tunasoma mara kwa mara. Post hii itakufundisha kuhusu fadhila za sura hii.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii

Soma Zaidi...
Asbab nuzul surat at Tin, Sababu za kushuka surat at Tin (watin wazaitun)

Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun).

Soma Zaidi...