picha

Muhammad hakufundishwa quran na padri Bahira

Muhammad hakufundishwa quran na padri Bahira

(a)Dai la Kufundishwa na Padri Bahira:



Baadhi ya makafiri wanadai kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) alijifunza Uyahudi na Ukristo katika safari zake mbili za biashara alizofanya Sham (Syria), hasa katika safari yake ya kwanza alipokutana na Padri Bahirah, alipokuwa na umri wa miaka 12. Tunavyojifunza katika historia ni kuwa Bahirah alikutana na Mtume (s.a.w) njiani na kuashiria kwa Ami yake Abutwalib, kuwa anamkisia kijana wake (Muhammad) ana sifa za yule mtume aliyetabiriwa katika Injili (Rejea Qur-an 61:6).


Je, inamkinika kuwa mazungumzo haya ya njiani ya muda mfupi yawe ndiyo yaliyompelekea Mtume (s.a.w) kuandika Qur-an miaka 28 baada ya makutano hayo? Ikumbukwe kuwa Mtume (s.a.w) alianza kushushiwa wahy wa Quran alipokuwa na umri wa miaka arobaini ambapo alikutana na Bahirah akiwa na umri wa miaka kumi na mbili.



Safari ya pili ya Mtume (s.a.w) kwenda Syria kwa biashara ni pale alipokodiwa na Bibi Khadijah alipokuwa na umri miaka ishirini na tano. Katika kumbukumbu za historia, Mtume (s.a.w) hakufanya mkutano wowote na Wakristo wala Mayahudi kabla ya Utume.




                   


Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF Views 2522

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 ai web app     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

IDGHAAM KATIKA LAAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Quran Tafsiri kwa Kiswahili

Tafsiri ya quran kw akiswahili, imeandikw ana Shekh Ali Muhsin al-Barwani

Soma Zaidi...
Saratul-humaza

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
fadhila za sura kwenye quran

FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.

Soma Zaidi...