HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYUKI

Kung’atwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYUKI

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYUKI


Kung’atwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki. Utamjuaje kama ana aleji na nyuki?. ni pale utakapomuona aliyeng’atwa na nyuki akivimba mwili, na anaweza pia kupoteza fahamu. Pia hali hizi zinategemea ni kiasi gani cha nyuki wamemg’ata mtu.



Utakapomuona mtu ameng’atwa na nyuki usimkimbie, kwanza msaidie, kuhakikisha kuwa nyuki hawamng’ati tena. Unaweza kuchukuwa blanketi ama shuka uakmfunika vyema. Hakikisha na wewe umefunika pua, mgomo na masikio. Kama nyuki wanaendelea kuja mmwagie maji mgonjwa ili kupoteza harufu ya nyuki.



Hakikisha kabla hujaanza kutoa huduma ya kwanza, kwanza unaangalia hali ya aliyeng’atwa, kama hali ni ya kawaida na hahitaji kwenda hospitali. Kama anahitaji kwenda hospitali haraka wasiliana na kituo kilicho jirani ama tafuta msaada, kwa watu walio karibu. Hakikisha maamuzi haya hayaathiri hali ya mgonjwa. Ili kumpa huduma ya kwanza aliyeng’atwa na nyuki:-


1.kwa upole tumia kitu chenye wembamba kisha toa miiba ya nyuki kwenye ngozi ya mgonjwa. Katu usitukie kucha zako, maana zitaipasua miipa na sumu itaingia ndani na katu hutaweza kuitoa tena.


2.Unaweza kutuia kisu, ama kituchenye ncha, ila hakikisha kuwa miiba ya nyuki haikatiki kwa ndani. Kwa mfano unapotumia kiwembe kuna uwezekano mkubwa ukaikata miib kwa ndani.


3.Muweke mgonjwa mahali pa ubaridi kama inawezekana


4.Osha maeneo aliyong’atwa kwa sabuni na maji


5.Unaweza kutumia dawa za kutuliza maumivu.


6.Zipo dawa kama losheni (calamine lotion) ila ni maalumu kwa aliyeng’atwa na nyuki, kama zipo mgonjwa apakwe.


7.Hakikisha unamtuliza moyo mgonjwa.


8.Kama hali ni mbaya bado mgonjwa apelekwe kituo cha afya.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 6146

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Aina za vidonda.

Posti hii inahusu zaidi aina kuu za vidonda,kuna aina kuu tatu za vidonda ambapo kila aina utumiwa kwa njia yake kama tutakavyoona hapo chini.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kulingana na tatizo

Posti hii inahusu sana mambo ya huduma ya kwanza ambayo huduma ya kwanza inapatikana au inatolewa na mtu yeyote katika jamii .

Soma Zaidi...
Visababishi vya magonjwa.

Posti huu inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya magonjwa, tunajua wazi kuwa ugonjwa ni hali ya kutokuwa kawaida kwa ogani mbalimbali kwenye mwili na kusababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.

Soma Zaidi...
Madhara ya kuchelewa kutibu tatizo la kiafya

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea endapo tatizo halijatibiwa.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa

Soma Zaidi...
Huwezi kuambukizwa Ukimwi kwa mambo yafuatayo

Posti hii inahusu zaidi au inapinga Imani potofu ambayo utokea kwenye jamii kwamba unaweza kuambukizwa Ukimwi kwa vitu ambavyo haviusiani na namna mtu anavyoweza kuambukizwa Ukimwi,Ila mapendekezo kuwa watu wanapaswa kujua kuwa huwezi kuambukizwa Ukimwi k

Soma Zaidi...
Upungufu wa maji

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa maji mwilini

Soma Zaidi...
Namna ya kumfanyia usafi Mgonjwa kwa mwili mzima.

Posti hii inahusu namna ya kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima, ni njia ambazo utumika kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima au kumwosha Mgonjwa hasa wale walio mahututi na hawawezi kuamka kitandani.

Soma Zaidi...