picha

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA

Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu.

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA


Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu. Ni vigumu kuwatofautisha wenye sumu na wasio na sumu kwani wakati mwengine wanafanana sifa. Wataalamu wameweka njia kadhaa za kuweza kuwajuwa weenye sumu. Nyoka mwenye sumu ana sifa zifuatazo


1.kichwa chake kipo katika pembe tatu


2.Rangi zake zinameremeta sana


3.Mboni ya Macho yao yamefanana na macho ya paka


4.Wanapoogelea kwenye maji miili yao inaelea juu



Tmbua kuwa sifa hizi hata nyoka wasio na sumu wamaweza kuwa nazo. Kuwa makini na kaa mbali na nyoka wa aina yeyote kama huna ujuzi na utambuzi huu. Mtu aliyengatwa na nyka mwenye sumu ataonyesha dalili zifuatazo:-


1.Uchovu

2.Kizunguzungu

3.Anaweza kuzimia

4.Kichefuchefu

5.Kuharisha

6.Kutapika

7.Mapigo ya moyo kuongezeka kwa kasi

8.Misuli kukosa uweze wa kutanuka na kusinyaa

9.Kuvimba eneo alipong’atwa.



Ukiona mtu ameng’atwa na nyoka na akaonyesha dalili hizi, wahi kuomba msaada ili awahishwe ituo cha afya kwa haraka. Hakikisha unampatia huduma ya kwanza ili kupunguza athari za kusambaa kwa sumu mwilini. Huduma ya kwanza kwa mtu aliyeng’atwa na nyoka inaweza kuwa kwa nama zifuata zo:-




1.mtulize mgonjwa nafsi yake, mpe maneno matamu na ya kutuliza. Hii itasaidia moyo kupunguza kazi ya kusambaza damu mwilini, hivyo sumu haita sambaa kwa kasi.


2.Muweke mgonjwa chini, na katu usimtembeze, mlaze chini kwa namna ambayo sehemu alipong’atwa itakuwa chini. Kwa mfano kama ameng’atwa mguuni, unaweza kumuwekea kitu kichwani akaegemea kwa mto ili sehemu ya mguuni iwe chini.


3.Ondoa mengo ya nyoka kwa uangalifu na katu usimishe eneo alilongatwa na nyoka.


4.Kama mgonjwa ana kizunguzungu, ama baridi mfunike kwa nguo ili kumuongezea joto


5.Chukuwa maelezo kuhusu aina ya nyoka, hii itasaidia wataalamu wa afya kujuwa tiba sahihi.


6.Osha eneo kwa kupitishia maji kwa juu na katu usisugue ama kuminya jeraha.



Usifanye vitu hivi:
1.Usinyonye sumu kwa mdomo wako
2.Usimpe mgonjwa chakula wala maji
3.Usimtembeze mgojwa
4.Usitumie barafu sehemu yenye jeraha
5.Usifunge kwenye jeraha eti kuzuia mzunguo wa damu.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 4909

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 web hosting    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Zijue kazi za uke (vagina)

Uke ni sehemu ambayo imo ndani ya mwili wa mwanamke, sehemu hii ufanya kazi mbalimbali hasa wakati wa kujamiiana, kubarehe na kujifungua kwa mama.

Soma Zaidi...
Jifunze kuhusu msukumo wa damu kwa kitaalamu huitwa pressure

Kupanda kwa msukumo wa damu ni ktendo ambapo moyo husukuma damu kwa nguvu kuliko kawaida ambapo hupelekea matatizo mengi kwenye mwili

Soma Zaidi...
Upungufu wa vyakula vya madini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula vya madini

Soma Zaidi...
Faida za tumbo katika mwili wa binadamu

Posti hii inahusu zaidi faida za tumbo,tumbo ni sehemu ya mwili ambayo ushughilika na kutunza chakula,

Soma Zaidi...
Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa Damu kwenye moyo.

 Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye misuli ya moyo, kitaalamu huitwa Angina ni dalili ya Ugonjwa wa ateri ya Coronary. Ugonjwa huu kawaida hufafanuliwa kama kufinya, shinikizo, uzito, kubana au maumivu kwenye

Soma Zaidi...
Kazi ya madini mwilini

Posti hii inakwenda kukueleza kuhusu kazi za madini mwilini

Soma Zaidi...
Upungufu wa vyakula na madhara yake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu protini na kazi zake mwilini

Tunahitaji kuwa na protini mwilini. Kuna baadhi ya makundi ya watu wanahitaji protini zaidi. Je unawajuwa hao ni kina nana?, na je unauwa kazi za protini mwilini na athari za upungufu wake? endelea na makala hii.

Soma Zaidi...
Upungufu wa damu mwilini

Post inaenda kuzungumzia kuhusiana na upungufu wa damu mwilini ambapo tutaona SABABU na dalili zake lakin upungufu wa damu mwilini hujulikana Kama ANEMIA.

Soma Zaidi...
Aina mbalimbali za maumivu ya mwili.

Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali ya maumivu ya mwili, Maumivu ya mwili utokea kwa aina mbalimbali kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...