HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA

Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu.

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA


Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu. Ni vigumu kuwatofautisha wenye sumu na wasio na sumu kwani wakati mwengine wanafanana sifa. Wataalamu wameweka njia kadhaa za kuweza kuwajuwa weenye sumu. Nyoka mwenye sumu ana sifa zifuatazo


1.kichwa chake kipo katika pembe tatu


2.Rangi zake zinameremeta sana


3.Mboni ya Macho yao yamefanana na macho ya paka


4.Wanapoogelea kwenye maji miili yao inaelea juu



Tmbua kuwa sifa hizi hata nyoka wasio na sumu wamaweza kuwa nazo. Kuwa makini na kaa mbali na nyoka wa aina yeyote kama huna ujuzi na utambuzi huu. Mtu aliyengatwa na nyka mwenye sumu ataonyesha dalili zifuatazo:-


1.Uchovu

2.Kizunguzungu

3.Anaweza kuzimia

4.Kichefuchefu

5.Kuharisha

6.Kutapika

7.Mapigo ya moyo kuongezeka kwa kasi

8.Misuli kukosa uweze wa kutanuka na kusinyaa

9.Kuvimba eneo alipong’atwa.



Ukiona mtu ameng’atwa na nyoka na akaonyesha dalili hizi, wahi kuomba msaada ili awahishwe ituo cha afya kwa haraka. Hakikisha unampatia huduma ya kwanza ili kupunguza athari za kusambaa kwa sumu mwilini. Huduma ya kwanza kwa mtu aliyeng’atwa na nyoka inaweza kuwa kwa nama zifuata zo:-




1.mtulize mgonjwa nafsi yake, mpe maneno matamu na ya kutuliza. Hii itasaidia moyo kupunguza kazi ya kusambaza damu mwilini, hivyo sumu haita sambaa kwa kasi.


2.Muweke mgonjwa chini, na katu usimtembeze, mlaze chini kwa namna ambayo sehemu alipong’atwa itakuwa chini. Kwa mfano kama ameng’atwa mguuni, unaweza kumuwekea kitu kichwani akaegemea kwa mto ili sehemu ya mguuni iwe chini.


3.Ondoa mengo ya nyoka kwa uangalifu na katu usimishe eneo alilongatwa na nyoka.


4.Kama mgonjwa ana kizunguzungu, ama baridi mfunike kwa nguo ili kumuongezea joto


5.Chukuwa maelezo kuhusu aina ya nyoka, hii itasaidia wataalamu wa afya kujuwa tiba sahihi.


6.Osha eneo kwa kupitishia maji kwa juu na katu usisugue ama kuminya jeraha.



Usifanye vitu hivi:
1.Usinyonye sumu kwa mdomo wako
2.Usimpe mgonjwa chakula wala maji
3.Usimtembeze mgojwa
4.Usitumie barafu sehemu yenye jeraha
5.Usifunge kwenye jeraha eti kuzuia mzunguo wa damu.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 3863

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Aliyepaliwa na maji huduma ya kwanza itakuwaje

Vipi utamsaidia mti ambaye amepaliwa na maji? Post hii itakwenda kukifundisha jambo hili.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYUKI

Kung’atwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.

Soma Zaidi...
Nyanja sita za afya

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu nyanja sita za afya

Soma Zaidi...
Kwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?

Swali languKwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?

Soma Zaidi...
Uvimbe kwenye utandu laini uliopo tumboni (peritonitis)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Uvimbe au mashambulizi ya bacteria kwenye utando laini uliopo tumboni ambao kitaalamu hujulikana Kama peritonitis.

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa vitamini C mwilini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za upungufu wa vitamini C mwilini

Soma Zaidi...
Njia za kuongeza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya njia za kuongeza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Kawaida Mtu anatakiwa na kiwango gani Cha presha

Nimeambiwa presha yangu umeshuka iko 90/60 na Nina umri wa miaka 26 KawaidaMtu anatakiwa na kiwango gani Cha presha

Soma Zaidi...
Huduma ya kwanza kwa aliye ungua na Moto.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa aliyeungua na Moto.

Soma Zaidi...
Utaratibu wa lishe kwa wagonjwa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wagonjwa

Soma Zaidi...