Huduma kwa mama mwenye mimba Inayotishia kutoka.

Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka.

Huduma kwa mama mwenye dalili za mimba Inayotishia kutoka .

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujikumbushia kidogo kuhusu mimba Inayotishia kutoka , mimba ya aina hii utokea pale ambapo mjamzito utokwa na damu kidogo kidogo zinaweza kuwa kama za hedhi ila zinaweza kuwa kidogo lakini ni za mwendelezo au za mara kwa mara na hazikati na pengine Mama anakuwa Hana maumivu hata kidogo au pengine maumivu yanakuwepo ila ni kwa kiasi kidogo sana kwa hiyo mama baada ya kuona hayo anapaswa kuwahi hospital Ili kupata matibabu na kuokoa mimba isitoke. Kwa mjamzito wa namna hii tunapaswa kumpatia huduma zifuatazo.

 

 

 

 

2. Kwa kwaida Mama akiwa katika hali hii mara nyingi huwa na wasiwasi kwa hiyo anapaswa kutiwa moyo na kumhakikishia usalama na kumwambia ni shida gani iliyompata pia mama anapaswa kulala kitandani kwa wiki Moja bila kutembea huko na huku bila sababu , mjamzito anashauliwa kulala kwa Sababu kama Kuna sehemu yoyote imeachia ni rahisi kabisa kujirudia na kuwa kawaida kabisa na pia mjamzito kama amefuata mashariti haya kitu cha kwanza kabisa damu ambazo zilikuwa zinatoka zinakoma na kama mjamzito amefuata mashariti anakuwa vizuri ndani ya wiki Moja ,na pia mama kama ameambiwa kulala anapaswa kuelezwa wazi kwa nini amelala na pia aambiwe wazi kwamba akikosea mashariti anaweza kupoteza mtoto.

 

 

 

 

3. Pia Mama anapaswa kushauliwa au kuambiwa kabisa kuachana na tendo la ndoa anapopatwa na tatizo la namna hii,

Mama anapaswa kuachana na tendo la ndoa kwa sababu inawezekana kwenye sehemu ya mlango wa kizazi Kuna sehemu iliyolegea kwa hiyo mama akiendelea kufanya tendo la ndoa anasababisha sehemu Ile kulegea na kuendelea kuleta matatizo zaidi au kwa wakati mwingine baba akitoa mbegu na mbegu hizo mara nyingi Zina kichocheo ambacho kikichanganyika na kichocheo cha uchungu cha mama uweza kuanzisha uchungu na kusababisha mlango wa kizazi kufunguka na mtoto anaweza kutoka, kwa hiyo Mama mwenye tatizo hili anapaswa kuacha tendo la ndoa mpaka hapo atakapomaliza kujifungua. Pia na baba anapaswa kuelezwa wazi hali ya mke wake.

 

 

 

 

 

4. Pia kwa Kipindi hiki kwa sababu mama anaweza kuwa na mawazo au kwa sababu ya kulala kwa mda mrefu anaweza kukosa usingizi na kuwa na kishawishi cha kutembea akiwa amejificha na kusababisha madhara zaidi kwa hiyo ni vizuri mjamzito akionekana na wasiwasi na kutotulia apewe dawa za usingizi, na pia pengine mimba inawezekana kutishia kutoka kwa sababu ya kukosekana kwa baadhi ya vichocheo ambavyo usaidia kukua kwa mimba kwa hiyo mama anapaswa kupewa vichocheo mbalimbali,kwa kitaamu huiitwa progesterone hasa hasa kama Kuna ushaidi kwamba imepungua kwenye mwili wa mama 

 

 

 

 

 

5. Ikitokea damu ikaacha kutoka hiyo ni dalili kubwa ya kwamba tatizo limepona na mama anaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani lakina kwamashariti makubwa kati ya mtoa huduma za afya, mama na ndugu wa karibu hasa mme wake , kwa hiyo mama atapaswa kurudi klinic mara kwa mara Ili kuendelea kuangalia afya ya mama na mtoto, na kabla mama hajaondoka anapaswa kabisa kuangalia kama damu imeacha kutoka na watoa huduma wajihajikishie kwa sababu Kuna akina Mama ambao wamechoka kuishi hospital, na akina Mama wanapaswa kuwa wakweli na wawazi kuhusu afya zao na za watoto pia.

 

 

 

 

 

 

6. Pia tatizo likipona ni vizuri kutoa elimu ya kutosha kwa mama na ndugu Ili kuepuka Mila potofu ambazo zinaweza kuleta matatizo zaidi

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 9748

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Kutokwa maji yan seminal swhemu za siri kwa mwanamke nidalili ya ugojwa gan?

Kutokwa Majimaji sehemu za siri kwa mwanamke sio jambo la kushangaza na kuhisivunaumwa. Majimajivhaya ndio huboresha afya ya uzazi kwa kusafisha na kulinda via vya uzazi. Lakini majimajivhaya yakiwa mengi, ama yanawasha ama yanaharufu haa ndipo kwenye tat

Soma Zaidi...
Hatua Saba za kutibu au kuepuka uvimbe kwenye kizazi

Posti hii inahusu zaidi hatua ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kutibu uvimbe au kwa kitaalamu huitwa fibroids. Hizi hatua zikitumika uweza kusaidia kupunguza kiwango cha kupata au kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Soma Zaidi...
Njia za kuongeza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuongeza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Faida na hasara za kutumia kondomu kama njia ya uzazi wa mpango

Kondomu ni mpira ambao uwekwa kwenye uke au uume kwa ajili ya kuzuia mimba wakati wa kujamiiana

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa?

Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Faida na hasara za kutumia uzazi wa mpango

Tunaposema uzazi wa mpango, tunamaanisha ile hali ya kuachanisha muda kutoka mtoto hadi mwingine. Inatakiwa angalau mtoto na mtoto wapishane miaka miwili. Uzazi wa mpango ni maamuzi kati ya mama na baba.

Soma Zaidi...
Mimba huonekana katka mkojo baada ya muda gan tangu itungwe

Kipimo cha mimba kwa mkojo kimekuwa kikitumika sana kuangalia ujauzito. Kipimo hiki kinapotumika vibaya kinaweza kukupa majibu ya uongo. Kuwa makini na ujue muda sahihi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuacha kupiga punyeto.

Post hii inakwenda kukupa njia za kukusaidia kuacha punyeto.

Soma Zaidi...