Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujikumbushia kidogo kuhusu mimba Inayotishia kutoka , mimba ya aina hii utokea pale ambapo mjamzito utokwa na damu kidogo kidogo zinaweza kuwa kama za hedhi ila zinaweza kuwa kidogo lakini ni za mwendelezo au za mara kwa mara na hazikati na pengine Mama anakuwa Hana maumivu hata kidogo au pengine maumivu yanakuwepo ila ni kwa kiasi kidogo sana kwa hiyo mama baada ya kuona hayo anapaswa kuwahi hospital Ili kupata matibabu na kuokoa mimba isitoke. Kwa mjamzito wa namna hii tunapaswa kumpatia huduma zifuatazo.
2. Kwa kwaida Mama akiwa katika hali hii mara nyingi huwa na wasiwasi kwa hiyo anapaswa kutiwa moyo na kumhakikishia usalama na kumwambia ni shida gani iliyompata pia mama anapaswa kulala kitandani kwa wiki Moja bila kutembea huko na huku bila sababu , mjamzito anashauliwa kulala kwa Sababu kama Kuna sehemu yoyote imeachia ni rahisi kabisa kujirudia na kuwa kawaida kabisa na pia mjamzito kama amefuata mashariti haya kitu cha kwanza kabisa damu ambazo zilikuwa zinatoka zinakoma na kama mjamzito amefuata mashariti anakuwa vizuri ndani ya wiki Moja ,na pia mama kama ameambiwa kulala anapaswa kuelezwa wazi kwa nini amelala na pia aambiwe wazi kwamba akikosea mashariti anaweza kupoteza mtoto.
3. Pia Mama anapaswa kushauliwa au kuambiwa kabisa kuachana na tendo la ndoa anapopatwa na tatizo la namna hii,
Mama anapaswa kuachana na tendo la ndoa kwa sababu inawezekana kwenye sehemu ya mlango wa kizazi Kuna sehemu iliyolegea kwa hiyo mama akiendelea kufanya tendo la ndoa anasababisha sehemu Ile kulegea na kuendelea kuleta matatizo zaidi au kwa wakati mwingine baba akitoa mbegu na mbegu hizo mara nyingi Zina kichocheo ambacho kikichanganyika na kichocheo cha uchungu cha mama uweza kuanzisha uchungu na kusababisha mlango wa kizazi kufunguka na mtoto anaweza kutoka, kwa hiyo Mama mwenye tatizo hili anapaswa kuacha tendo la ndoa mpaka hapo atakapomaliza kujifungua. Pia na baba anapaswa kuelezwa wazi hali ya mke wake.
4. Pia kwa Kipindi hiki kwa sababu mama anaweza kuwa na mawazo au kwa sababu ya kulala kwa mda mrefu anaweza kukosa usingizi na kuwa na kishawishi cha kutembea akiwa amejificha na kusababisha madhara zaidi kwa hiyo ni vizuri mjamzito akionekana na wasiwasi na kutotulia apewe dawa za usingizi, na pia pengine mimba inawezekana kutishia kutoka kwa sababu ya kukosekana kwa baadhi ya vichocheo ambavyo usaidia kukua kwa mimba kwa hiyo mama anapaswa kupewa vichocheo mbalimbali,kwa kitaamu huiitwa progesterone hasa hasa kama Kuna ushaidi kwamba imepungua kwenye mwili wa mama
5. Ikitokea damu ikaacha kutoka hiyo ni dalili kubwa ya kwamba tatizo limepona na mama anaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani lakina kwamashariti makubwa kati ya mtoa huduma za afya, mama na ndugu wa karibu hasa mme wake , kwa hiyo mama atapaswa kurudi klinic mara kwa mara Ili kuendelea kuangalia afya ya mama na mtoto, na kabla mama hajaondoka anapaswa kabisa kuangalia kama damu imeacha kutoka na watoa huduma wajihajikishie kwa sababu Kuna akina Mama ambao wamechoka kuishi hospital, na akina Mama wanapaswa kuwa wakweli na wawazi kuhusu afya zao na za watoto pia.
6. Pia tatizo likipona ni vizuri kutoa elimu ya kutosha kwa mama na ndugu Ili kuepuka Mila potofu ambazo zinaweza kuleta matatizo zaidi
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutumia mara kwa mara vidonge vya P2,
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu kwa mama au mlezi wa mtoto mgonjwa. Ni maelekezo muhimu hasa wakati wa kutoa dawa kwa mtoto.
Soma Zaidi...Ni mida gani njamzito ananza kuhisi kuwa tumboni anebeba mtoto.
Soma Zaidi...Hii ni hali inayompata mtu kukosa hamu kabisa ya kushiriki kitendo chochote kinachohusiana na kufanya tendo landoa au bunyeto.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za PID maana yake ni maambukizi kwenye pelvic kwa kitaalamu huitwa pelvic infection disease, ni ugonjwa unaoshambulia sana wanawake na wasichana
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba , tunapaswa kujua hivi Ili kuweza kupanga uzazi na kuepuka njia ambazo ni hatarishi kwa afya zetu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia Faida za Uzazi wa mpango kwa watoto, mama, wanandoa, na jamii au JUMUIYA.
Soma Zaidi...Kukoma hedhi hufafanuliwa kuwa hutokea miezi 12 baada ya kipindi chako cha mwisho cha hedhi na huashiria mwisho wa mizunguko ya hedhi. Kukoma hedhi kunaweza kutokea katika miaka ya 40 au 50. Kukoma hedhi ni mchakato wa asili wa kibaolojia. Ingawa pia in
Soma Zaidi...