picha

Huduma kwa mama mwenye mimba Inayotishia kutoka.

Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka.

Huduma kwa mama mwenye dalili za mimba Inayotishia kutoka .

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujikumbushia kidogo kuhusu mimba Inayotishia kutoka , mimba ya aina hii utokea pale ambapo mjamzito utokwa na damu kidogo kidogo zinaweza kuwa kama za hedhi ila zinaweza kuwa kidogo lakini ni za mwendelezo au za mara kwa mara na hazikati na pengine Mama anakuwa Hana maumivu hata kidogo au pengine maumivu yanakuwepo ila ni kwa kiasi kidogo sana kwa hiyo mama baada ya kuona hayo anapaswa kuwahi hospital Ili kupata matibabu na kuokoa mimba isitoke. Kwa mjamzito wa namna hii tunapaswa kumpatia huduma zifuatazo.

 

 

 

 

2. Kwa kwaida Mama akiwa katika hali hii mara nyingi huwa na wasiwasi kwa hiyo anapaswa kutiwa moyo na kumhakikishia usalama na kumwambia ni shida gani iliyompata pia mama anapaswa kulala kitandani kwa wiki Moja bila kutembea huko na huku bila sababu , mjamzito anashauliwa kulala kwa Sababu kama Kuna sehemu yoyote imeachia ni rahisi kabisa kujirudia na kuwa kawaida kabisa na pia mjamzito kama amefuata mashariti haya kitu cha kwanza kabisa damu ambazo zilikuwa zinatoka zinakoma na kama mjamzito amefuata mashariti anakuwa vizuri ndani ya wiki Moja ,na pia mama kama ameambiwa kulala anapaswa kuelezwa wazi kwa nini amelala na pia aambiwe wazi kwamba akikosea mashariti anaweza kupoteza mtoto.

 

 

 

 

3. Pia Mama anapaswa kushauliwa au kuambiwa kabisa kuachana na tendo la ndoa anapopatwa na tatizo la namna hii,

Mama anapaswa kuachana na tendo la ndoa kwa sababu inawezekana kwenye sehemu ya mlango wa kizazi Kuna sehemu iliyolegea kwa hiyo mama akiendelea kufanya tendo la ndoa anasababisha sehemu Ile kulegea na kuendelea kuleta matatizo zaidi au kwa wakati mwingine baba akitoa mbegu na mbegu hizo mara nyingi Zina kichocheo ambacho kikichanganyika na kichocheo cha uchungu cha mama uweza kuanzisha uchungu na kusababisha mlango wa kizazi kufunguka na mtoto anaweza kutoka, kwa hiyo Mama mwenye tatizo hili anapaswa kuacha tendo la ndoa mpaka hapo atakapomaliza kujifungua. Pia na baba anapaswa kuelezwa wazi hali ya mke wake.

 

 

 

 

 

4. Pia kwa Kipindi hiki kwa sababu mama anaweza kuwa na mawazo au kwa sababu ya kulala kwa mda mrefu anaweza kukosa usingizi na kuwa na kishawishi cha kutembea akiwa amejificha na kusababisha madhara zaidi kwa hiyo ni vizuri mjamzito akionekana na wasiwasi na kutotulia apewe dawa za usingizi, na pia pengine mimba inawezekana kutishia kutoka kwa sababu ya kukosekana kwa baadhi ya vichocheo ambavyo usaidia kukua kwa mimba kwa hiyo mama anapaswa kupewa vichocheo mbalimbali,kwa kitaamu huiitwa progesterone hasa hasa kama Kuna ushaidi kwamba imepungua kwenye mwili wa mama 

 

 

 

 

 

5. Ikitokea damu ikaacha kutoka hiyo ni dalili kubwa ya kwamba tatizo limepona na mama anaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani lakina kwamashariti makubwa kati ya mtoa huduma za afya, mama na ndugu wa karibu hasa mme wake , kwa hiyo mama atapaswa kurudi klinic mara kwa mara Ili kuendelea kuangalia afya ya mama na mtoto, na kabla mama hajaondoka anapaswa kabisa kuangalia kama damu imeacha kutoka na watoa huduma wajihajikishie kwa sababu Kuna akina Mama ambao wamechoka kuishi hospital, na akina Mama wanapaswa kuwa wakweli na wawazi kuhusu afya zao na za watoto pia.

 

 

 

 

 

 

6. Pia tatizo likipona ni vizuri kutoa elimu ya kutosha kwa mama na ndugu Ili kuepuka Mila potofu ambazo zinaweza kuleta matatizo zaidi

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 11323

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto mchanga kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa, ni tatizo ambalo utokea kwa baadhi ya wajawazito kupata mtoto mwenye Uzito mkubwa, wengine uona kama ni sifa ila Kuna madhara yanaweza kujitokeza kwa Mama hasa wakati wa kujif

Soma Zaidi...
Habari, naomba kuulizia, nimadhara gani atayapata mwanamke akitolewa bikra bila kukusudia

Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali?

Soma Zaidi...
Yajue mazoezi ya kegel

Posti inahusu zaidi mazoezi ya kegel, ni mazoezi ambayo ufanywa na watu wengi na sehemu yoyote yanaweza kufanywa kama vile chumbani, sebuleni, uwanjani na sehemu yoyote ile na kwa watu tofauti.

Soma Zaidi...
Wanaopasawa kutumia PEP

PEP Ni dawa ambazo utumiwa na watu wanaojamiiana na watu wenye virus vya ukimwi ila wenyewe hawawezi kupata kwa sababu ya kutumia dawa hizo.

Soma Zaidi...