Post hii inahusu zaidi sababu za ugumba kwa wanawake, ni sababu ambazo upelekea wanawake wengi kuwa wagumba ukizingatia kuwa wanazaliwa wakiwa na uwezo kabisa wa kupata watoto lakini kwa sababu mbalimbali za kimazingira wanakoswa watoto, zifuatazo ni saba
Sababu za ugumba kwa wanawake.
1. Kwanza kabisa ugumba ni hali inayotokea ambapo mwanamke na mwanaume wanaishi kwa mwaka mmoja kwa kujamiiana pasipokutumia aina yoyote ya uzazi wa mpango lakini hawapati mtoto kwa kipindi cha mwaka huo mzima, kuna aina mbili za ugumba.Aina ya kwanza ni pale ambapo mwanaume na mwanamke wanapata moto mmoja na baadae hawapati kabisa na ya pili ni kwamba hawapati mtoto hata mmoja. Zifuatazo ni sababu za ugumba kwa mwanamke.
2. Kuaribika kwa mirija ambayo inasaidia katika mifumo mizima ya kusafirisha yai, kwa mwanamke kuna baadhi ya mirija ambayo usababisha kusafirisha yai wakati wa utungaji wa mimba, mirija hiyo ikiharibiwa ushindwa kupokea yai na kulifikisha sehemu usika, sababu za kuaribika kwa mirija inaweza kuwa ni maambukizi kwenye mirija hiyo au ni kwa sababu ya upasuaji kwa hiyo yai ushindwa kusafiri kutoka kwenye ovari mpaka kwenye follapian kwa ajili ya kurutubishwa.
3. Sababu nyingine ni kuwepo kwa matatizo kwenye mfuko wa uzazi, mfuko wa uzazi kawaida unapaswa kuwa na mazingira mazuri kwa ajili ya kumtunza mtoto, kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwenye mfumo wa uzazi pamoja na kuwepo kwa uvimbe mtoto hawezi kukua kwenye mfumo wa uzazi kwa hiyo kutibu maambukizi mapema ni vizuri ili kuepukana na tatizo hili la kukosa mtoto.
4.kuwepo kwa acid nyingi kwenye uke. Tunajua wazi kubwa kwenye uke kuna acidi ambayo inapaswa kutunza sehemu hiyo ila acidi ikiwa nyingi huwa inaua mbegu za kiume kwa hiyo acidi ya kwenye uke inapaswa kuwa nne na nusu kwa pH ikizidi hapo inaua mbegu kwa hiyo pakitokea tatizo la ugumba ni vizuri kupima kiwango cha acidi kwenye uke ili kupunguza tatizo la ugumba.
5. Kuwepo kwa ute mzito kwenye uke na cervix, tujue wazi kubwa kwenye uke kwa kawaida huwa kuna ute, ikitokea uke huo kubwa mzito usababisha mbegu kushindwa kupita na kulifikia yai kwa ajili ya kurutubishwa kwa hiyo tunapaswa kuangalia na tatizo la ute endapo kama kuna tatizo la ugumba na kuweza kutumia dawa za kurainisha ute na mbegu zinaweza kupita kwa urahisi.
6. Kuwepo kwa maambukizi kwenye via vya uzazi, tukumbuke kubwa via vya uzazi ni pamoja na uke, cervix na tumbo la uzazi hizi sehemu zikishambuliwa na Maambukizi ni vigumu kupata uja uzito. Hasa maambukizi yatokanayo na ngono zembe kwa hiyo tunapaswa kupima na kutibu mara moja Magonjwa haya ili kuweza kuondoa wimbi hili la ugumba kwa wanawake.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Faida za Uzazi wa mpango. Uzazi wa mpango ni huduma ambazo hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya mdalasini katika matibabu ya homoni kwa wanawake.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili za Mama mwenye kifafa cha mimba, ili kifafa cha mimba kiweze kutokea lazima kuna dalili ambazo uweza kutokea kwa Mama kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Maumivu ya matiti ni malalamiko ya kawaida miongoni mwa wanawake yanaweza kujumuisha uchungu wa matiti, maumivu makali ya kuungua au kubana kwenye tishu zako za matiti. Maumivu yanaweza kuwa ya mara kwa mara au yanaweza kutokea mara kwa mara tu. Maumiv
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza homoni za kiume kwa akina dada.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.
Soma Zaidi...Mimba inaweza kutoka kutokana na maradhi, majeraha ama misukosuko mimgine. Kutoka kwa mimva haimaanishi ndio mwisho wa kizazi.
Soma Zaidi...