Post hii inahusu zaidi sababu za ugumba kwa wanawake, ni sababu ambazo upelekea wanawake wengi kuwa wagumba ukizingatia kuwa wanazaliwa wakiwa na uwezo kabisa wa kupata watoto lakini kwa sababu mbalimbali za kimazingira wanakoswa watoto, zifuatazo ni saba
Sababu za ugumba kwa wanawake.
1. Kwanza kabisa ugumba ni hali inayotokea ambapo mwanamke na mwanaume wanaishi kwa mwaka mmoja kwa kujamiiana pasipokutumia aina yoyote ya uzazi wa mpango lakini hawapati mtoto kwa kipindi cha mwaka huo mzima, kuna aina mbili za ugumba.Aina ya kwanza ni pale ambapo mwanaume na mwanamke wanapata moto mmoja na baadae hawapati kabisa na ya pili ni kwamba hawapati mtoto hata mmoja. Zifuatazo ni sababu za ugumba kwa mwanamke.
2. Kuaribika kwa mirija ambayo inasaidia katika mifumo mizima ya kusafirisha yai, kwa mwanamke kuna baadhi ya mirija ambayo usababisha kusafirisha yai wakati wa utungaji wa mimba, mirija hiyo ikiharibiwa ushindwa kupokea yai na kulifikisha sehemu usika, sababu za kuaribika kwa mirija inaweza kuwa ni maambukizi kwenye mirija hiyo au ni kwa sababu ya upasuaji kwa hiyo yai ushindwa kusafiri kutoka kwenye ovari mpaka kwenye follapian kwa ajili ya kurutubishwa.
3. Sababu nyingine ni kuwepo kwa matatizo kwenye mfuko wa uzazi, mfuko wa uzazi kawaida unapaswa kuwa na mazingira mazuri kwa ajili ya kumtunza mtoto, kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi kwenye mfumo wa uzazi pamoja na kuwepo kwa uvimbe mtoto hawezi kukua kwenye mfumo wa uzazi kwa hiyo kutibu maambukizi mapema ni vizuri ili kuepukana na tatizo hili la kukosa mtoto.
4.kuwepo kwa acid nyingi kwenye uke. Tunajua wazi kubwa kwenye uke kuna acidi ambayo inapaswa kutunza sehemu hiyo ila acidi ikiwa nyingi huwa inaua mbegu za kiume kwa hiyo acidi ya kwenye uke inapaswa kuwa nne na nusu kwa pH ikizidi hapo inaua mbegu kwa hiyo pakitokea tatizo la ugumba ni vizuri kupima kiwango cha acidi kwenye uke ili kupunguza tatizo la ugumba.
5. Kuwepo kwa ute mzito kwenye uke na cervix, tujue wazi kubwa kwenye uke kwa kawaida huwa kuna ute, ikitokea uke huo kubwa mzito usababisha mbegu kushindwa kupita na kulifikia yai kwa ajili ya kurutubishwa kwa hiyo tunapaswa kuangalia na tatizo la ute endapo kama kuna tatizo la ugumba na kuweza kutumia dawa za kurainisha ute na mbegu zinaweza kupita kwa urahisi.
6. Kuwepo kwa maambukizi kwenye via vya uzazi, tukumbuke kubwa via vya uzazi ni pamoja na uke, cervix na tumbo la uzazi hizi sehemu zikishambuliwa na Maambukizi ni vigumu kupata uja uzito. Hasa maambukizi yatokanayo na ngono zembe kwa hiyo tunapaswa kupima na kutibu mara moja Magonjwa haya ili kuweza kuondoa wimbi hili la ugumba kwa wanawake.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Kutoka na majimaji ka uchache kwa mwanamke sio jambo lakishangaa sana. Damu hii inawezapiabkikbatana damu na maumivu makali.
Soma Zaidi...Je unasumbuliwa na maumivu ya tumbo. Unadhani ni dalili za mimba na ukapima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu za mimba kutoka, hili ni tatizo ambalo linawakumba wanawake wengi ambapo mimba utoka kabla ya kumfikisha mda wake, kwa kawaida Ili kawaida mimba nyingi utoka zikiwa na miezi chini ya Saba au wengine wanaweza kusema kwamba mim
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mimba iliyotunga nje na madhara yake kiafya
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea namna mwanamke anavyoweza kupata Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya HCG katika kupima mimba, HCG maana yake ni human chorionic gonadotropin ni homoni ambayo uonekanekana kwenye mkojo na damu kama mtu ana mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mbegu ambazo ni nzima na ambazo zina sifa ya kutungisha mimba kwa hiyo mbegu hizi utazigundua kwa kuwa na sifa zifuatazo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito
Soma Zaidi...