Faida na hasara za kutumia kondomu kama njia ya uzazi wa mpango
Kondomu ni mpira ambao uwekwa kwenye uke au uume kwa ajili ya kuzuia mimba wakati wa kujamiiana
Mtazamo juu ya matumizi ya kondonu umekuwa ukikabiliwa na imani za kidini. Zipo dini ambazo zinakataza kabisa, lakini zipo ambazo zinakubali endapo kutakuwa na haja ya kiulazima za kiafya. Kwa vyovyote itakavyokuwa haja ya kutumia kondomu ipo kulingana na sababu mbalimbali. Sababu nyingine zinakubaliwa na dini zote kwa mfano kuzuia kizazi endapo itaonekana ni hatari kwa mwanamke huwenda akapoteza maisha pindi akipata ujauzito, ama kulinda ndoa ambazo mmoja wao ameathirika. Zipo sababu nyingine ambazo zinaweza kukubalika katika dini zote.
Sasa kwa kuwa hali ya matumizi ya kondomu yapo kama hivyo basi ipo haja ya watu kuelezwa faida na hasara ambazo unaweza kuzipata kama utaamuwa kutumia kondomu. Faida hizi na hasara zitasaidia kukukumbusha kuendelea kuwa makini hata ukiwa unatumia kondomu.
Aina za kondomu
1. Kondomu ya kike ambayo huvaliwa na mwanamke wakati wa kujamiiana
2. Kondomu ya kiume, hii ni Aina ya kondomu inayovaliwa na mwanaume wakati wa kujamiiana
Faida za kutumia kondomu
1. Kuzuia kuongezeka kwa mimba zisizotarajiwa
2. Kuzuia magonjwa ya ngono
3. Kuzuia kuambukizwa kwa ugonjwa wa Ukimwi
Kati ya njia za uzazi wa mpango kondomu ndiyo njia pekee inayosaidia kupunguza kusambaa kwa magonjwa ya ngono na Ukimwi
Hasara za kutumia kondomu
1. Kondomu hukinga maambukizi ya magonjwa ya ngono, yanayoingia kwa njia ya ngono, lakini upo uwezekano wa kupata endapo kindomu itapasuka, ama itavuka wakati wa tendo. Pia kama kuna mikato iliyosababishwa na kunyoa na ikawa ipo wazi kuruhusu vijidudu kupendya kwa wawili hawa upo uwezekano wa kupata magonjwa. Ama kuvuka kwa kondomu au kupasuka upo uwezekano wa kupata ujauzito. Ijapokuwa hali hizi ni mara chache sana kutokea. hii inakuwa hasara endapo mtu atajiamini kwa asilimoa 100 kuwa yupo salama anapotumia kondomu bila ya kuchukuwa tahadhari nyingine.
2. kondomu kwa baadhi ya watu inawaletea allegi kama miwasho na mapele. Hii inatokana na mafuta yanayowekwa. Kwa baadhi ya watu miili yao haiendani na mafuta hayohivyo kuwasababishia aleji kila wanapotumia. Zungumza na daktari endapo una tatizo hili la aleji unapotumia kondomu.
3. kuna baadhi ya kondomu zinawekwa vilainishi vya Nonoxynol-9 kwa ajili ya kuuwa mbegu za kiume. Vilainishi hivi vinaweza kusababisha madhara kwenye uke kama kuwashwa hivyo kupelekea kuongezeka kwa hatari ya kupata maradhi ya ngono.
Kuwepo kwa hasara hizi inamaanisha kuwa watumiaji wa kondomu wawe makini wasijipe matumaini ya kuwa salama kwa asilimia 100, kwani chochote kinaweza kutokea.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Dalili ninazoziona kwangu chuchu zinauma na sjapata period mwezi huu na nlishiriki tarehe 19 mwezi wa tisa
Nini humaanisha kama chuchu zinauma na hupati period mwanaidi mrefu.
Soma Zaidi...Haya maji meupe hutokea wakat mimba ishatungwa au ukifanya tendo la ndoa lazima utokee?
Majimaji yanayitoka kwenye uke yanafungamana na taarifa nyingi kuhusu afya vya mwanamke. Ujauzito, maradhi, mabadiliko ya homoni na zaidi.
Soma Zaidi...Ongezeko la homoni ya estrogen
Posti hii inahusu zaidi ongezeko la homoni ya estrogen, kwa kawaida homoni hii ya estrogen inapaswa kulingana ikitokea ikaongezeka uleta madhara mbalimbali kwenye mwili na Kuna dalili ambazo zzz inaweza kujionesha wazi mpaka tukafahamu kuwa ni tatizo la o
Soma Zaidi...Imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba
Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...Vyakula hatari kwa mjamzito mwenye mimba na mimba changa
Vyakula hivi hapasi kuvila mwanamke mwenye ujauzito kwa kiasi kikubwa, hasa yule mwenye mimba chaga
Soma Zaidi...Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa
Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa
Soma Zaidi...