Faida na hasara za kutumia kondomu kama njia ya uzazi wa mpango

Kondomu ni mpira ambao uwekwa kwenye uke au uume kwa ajili ya kuzuia mimba wakati wa kujamiiana

Mtazamo juu ya matumizi ya kondonu umekuwa ukikabiliwa na imani za kidini. Zipo dini ambazo zinakataza kabisa, lakini zipo ambazo zinakubali endapo kutakuwa na haja ya kiulazima za kiafya. Kwa vyovyote itakavyokuwa haja ya kutumia kondomu ipo kulingana na sababu mbalimbali. Sababu nyingine zinakubaliwa na dini zote kwa mfano kuzuia kizazi endapo itaonekana ni hatari kwa mwanamke huwenda akapoteza maisha pindi akipata ujauzito, ama kulinda ndoa ambazo mmoja wao ameathirika. Zipo sababu nyingine ambazo zinaweza kukubalika katika dini zote.

 

Sasa kwa kuwa hali ya matumizi ya kondomu yapo kama hivyo basi ipo haja ya watu kuelezwa faida na hasara ambazo unaweza kuzipata kama utaamuwa kutumia kondomu. Faida hizi na hasara zitasaidia kukukumbusha kuendelea kuwa makini hata ukiwa unatumia kondomu.

 

Aina za kondomu

1. Kondomu ya kike ambayo huvaliwa na mwanamke wakati wa kujamiiana

2. Kondomu ya kiume, hii ni Aina ya kondomu inayovaliwa na mwanaume wakati wa kujamiiana

 

Faida za kutumia kondomu

1. Kuzuia kuongezeka kwa mimba zisizotarajiwa

2. Kuzuia magonjwa ya ngono

3. Kuzuia kuambukizwa kwa ugonjwa wa Ukimwi

Kati ya njia za uzazi wa mpango kondomu ndiyo njia pekee inayosaidia kupunguza kusambaa kwa magonjwa ya ngono na Ukimwi

 

Hasara za kutumia kondomu

1. Kondomu hukinga maambukizi ya magonjwa ya ngono, yanayoingia kwa njia ya ngono, lakini upo uwezekano wa kupata endapo kindomu itapasuka, ama itavuka wakati wa tendo. Pia kama kuna mikato iliyosababishwa na kunyoa na ikawa ipo wazi kuruhusu vijidudu kupendya kwa wawili hawa upo uwezekano wa kupata magonjwa. Ama kuvuka kwa kondomu au kupasuka upo uwezekano wa kupata ujauzito. Ijapokuwa hali hizi ni mara chache sana kutokea. hii inakuwa hasara endapo mtu atajiamini kwa asilimoa 100 kuwa yupo salama anapotumia kondomu bila ya kuchukuwa tahadhari nyingine.

 

2. kondomu kwa baadhi ya watu inawaletea allegi kama miwasho na mapele. Hii inatokana na mafuta yanayowekwa. Kwa baadhi ya watu miili yao haiendani na mafuta hayohivyo kuwasababishia aleji kila wanapotumia. Zungumza na daktari endapo una tatizo hili la aleji unapotumia kondomu.

 

3. kuna baadhi ya kondomu zinawekwa vilainishi vya Nonoxynol-9 kwa ajili ya kuuwa mbegu za kiume. Vilainishi hivi vinaweza kusababisha madhara kwenye uke kama kuwashwa hivyo kupelekea kuongezeka kwa hatari ya kupata maradhi ya ngono.

 

Kuwepo kwa hasara hizi inamaanisha kuwa watumiaji wa kondomu wawe makini wasijipe matumaini ya kuwa salama kwa asilimia 100, kwani chochote kinaweza kutokea.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 9976

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano

Posti hii inahusu malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano, huduma hii ilianzishwa na WHO na UNICEF mwaka 1990 ili kuweza kuzuia Magonjwa na kuwapatia watoto lishe pamoja na hayo walikuwa na malengo yafuatayo.

Soma Zaidi...
Uchafu unaotoka ukeni na rangi zake.

Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.

Soma Zaidi...
Sababu za mimba kutoka

Post hii inahusu zaidi sababu za mimba kutoka, hili ni tatizo ambalo linawakumba wanawake wengi ambapo mimba utoka kabla ya kumfikisha mda wake, kwa kawaida Ili kawaida mimba nyingi utoka zikiwa na miezi chini ya Saba au wengine wanaweza kusema kwamba mim

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujikinga na maradhi ya ini

Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kujiepusha na maradhi ya ini

Soma Zaidi...
Uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama.

Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n

Soma Zaidi...
Sababu za kupata hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja, mara nyingi kuna Watu ambao huwa wanalalamika kwa sababu ya kupata hedhi za mara kwa mara kwa mwezi mmoja.

Soma Zaidi...
Sababu za mwanamke kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa

Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazosababisha kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Mambo yanayopelekea ugumba.

Post huu inahusu zaidi mambo yanayopelekea ugumba kwa wanaume, ni mambo ambayo uchangia au upelekea mwanaume kukosa uzazi.

Soma Zaidi...
mambo HATARI KWA UJAUZITO (MIMBA) mambo yanayopelekea kujauzito kuwa hatarini kutoka

Tofauti na mambo matano yaliyotajwa hapo juu kuwa yanapelekea ujauzito kutoka, kuna mambo mengine ambayo yanaweza kuuweka ujauzito kuwa hatarini.

Soma Zaidi...
Maumivu wakati wa hedhi.

Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...