HTML - somo la 6: Jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la HTML
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la html na kuweka rangi ya background. Pia utajifunza kufanya ukurasa uwe responsive yaani uendani na ukubwa wa kifaa.
Karibu tena ndugu msomaji kwenye mafunzo ya HTML na hili ni somo la sita. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive. Kumbuka haya ni mafunzo ya HTML na jinsi ya kutengeneza website na blog.
Kama ndio mara ya kwanza kupata mfululizo wa masomo haya, somo hili linaendeshwa kwa kutumia App ya Treb Edit inatatikana playstore. Tunatumia App hii kwa kuwa masomo haya yanaendeshwa kwa kuzingatia zaidi wenye simu. Hata hivyo wenye kompyuta pia hawataachhwa mbali.
Fungua App yako, inga menu, kwenye folda laproject clic (maelekezo utayapata kwenye somo la kwanza link ipo hapo chini. Baada ya ku click hapo nenda new file, utatakiwa kuandika jina la faili lesson6.html kisha sevu. Funguwa hilo faili, kisha click HTML snippet, ukurasa wa code utafunguka, na kuanzia hapo ndipo tutaanzia na somo letu la sita.
Kupata masomo yaliotangulia bofya link za hapo chini:
1. Kuweka background color:
Background color ni rangi ya ukurasa wako. Yaani unaamuwa kama ukurasa wako unataka uwe na rangi nyingine tofauti na nyeupe. Kuweka background unaweza kufanya kwenye ukurasa wote. Kufanya hivi utaweka background kuanzia kwenye <body>. kama tulivyoona kuweka rangi basi hata background inakuwa hivyo huvyo tunatumia <style>. mfano:
<body style=”background-color:blue”> kwa kutumia code hii ukurasa wote utakuwa na rangi ya buluu. Angalia mfano kwenye picha.
Pia unaweza kuweka background kwenye tag ya heading kama <h1> ama kwenye paragraph <p>. kwa mfano kama background ni ya buluu, unaweza kuweka background ya rangi nyingine kwenye baadhi ya paragraph. Uwekaji wake ni kama unavyoweka rangi kwenye paragraph. Mfano:-
<p style=”backround-color:yellow”> kwa kutumia code hii rangi ya hiyo paragraph itakuwa ni ya njano. Angalia kwenye picha.
2. Kuweka menu (menyu)
Kuweka menu n kuweka machaguo ambayo yana mkusanyiko wa taarifa zinazolingana. Yaani unachaguwa chaguo kwa kubofya kicha unaletewa taarifa ama mkusanyiko wa taarifa ziinazo fanana.
Kutengenza menu utatumia tag ya menu ambayo ni <menu> pia utatumia tag ya link ambayo ni <a> tag ya link ni kuwezecha kubofya menyu na kupelekewa matokeo kwenye ukurasa mwingine. Baada ya hapo unaweza kutumia batani, ama ukaacha hivyo hivyo ama ukatumia kivuli.
Hapa tutaona menu yenye batani, link na tag ya menu.
<menu>
<a href=”link”><button>facebook</button></a>
<a href=”link”><button>youtube</button></a>
<a href=”link”><button>twitter</button></a>
<a href=”link”><button>whatsapp</button></a>
Utaj...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 web hosting 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
HTML - somo la 8: Mgawanyiko wa Tag za HTML na kazi zake
Katika somo hili tunakwenda kugawanya tag za HTML, pia nitakwenda kukuletea tag 70 za HTML
Soma Zaidi...HTML - somo la 7: Vitu vya kuzingatia unapoandika HTML
Katika somo hili utajifunza sehemu muhimu katika faili la HTML kama vile tag, attribute na element
Soma Zaidi...HTML - somo la 12: Sehemu kuu za faili la HTML
Katika somo hili utajifunza kuhusu sehemu kuu za faili la HTML
Soma Zaidi...HTML- somo la 2: Kazi za HTML, code na tag kwenye website.
Katika somo somo hili utajifunza maana ya code, tag na mpangilio wa faili la HTML
Soma Zaidi...HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Soma Zaidi...HTML - somo la 15: Jinsi ya kutengeneza website kwa kutumia HTML
Katika somo hili tutakwenda kutengeneza website yetu kutoka mwanzo hadi mwisho
Soma Zaidi...