HTML - somo la 6: Jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la HTML
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la html na kuweka rangi ya background. Pia utajifunza kufanya ukurasa uwe responsive yaani uendani na ukubwa wa kifaa.
Karibu tena ndugu msomaji kwenye mafunzo ya HTML na hili ni somo la sita. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive. Kumbuka haya ni mafunzo ya HTML na jinsi ya kutengeneza website na blog.
Kama ndio mara ya kwanza kupata mfululizo wa masomo haya, somo hili linaendeshwa kwa kutumia App ya Treb Edit inatatikana playstore. Tunatumia App hii kwa kuwa masomo haya yanaendeshwa kwa kuzingatia zaidi wenye simu. Hata hivyo wenye kompyuta pia hawataachhwa mbali.
Fungua App yako, inga menu, kwenye folda laproject clic (maelekezo utayapata kwenye somo la kwanza link ipo hapo chini. Baada ya ku click hapo nenda new file, utatakiwa kuandika jina la faili lesson6.html kisha sevu. Funguwa hilo faili, kisha click HTML snippet, ukurasa wa code utafunguka, na kuanzia hapo ndipo tutaanzia na somo letu la sita.
Kupata masomo yaliotangulia bofya link za hapo chini:
1. Kuweka background color:
Background color ni rangi ya ukurasa wako. Yaani unaamuwa kama ukurasa wako unataka uwe na rangi nyingine tofauti na nyeupe. Kuweka background unaweza kufanya kwenye ukurasa wote. Kufanya hivi utaweka background kuanzia kwenye <body>. kama tulivyoona kuweka rangi basi hata background inakuwa hivyo huvyo tunatumia <style>. mfano:
<body style=”background-color:blue”> kwa kutumia code hii ukurasa wote utakuwa na rangi ya buluu. Angalia mfano kwenye picha.
Pia unaweza kuweka background kwenye tag ya heading kama <h1> ama kwenye paragraph <p>. kwa mfano kama background ni ya buluu, unaweza kuweka background ya rangi nyingine kwenye baadhi ya paragraph. Uwekaji wake ni kama unavyoweka rangi kwenye paragraph. Mfano:-
<p style=”backround-color:yellow”> kwa kutumia code hii rangi ya hiyo paragraph itakuwa ni ya njano. Angalia kwenye picha.
2. Kuweka menu (menyu)
Kuweka menu n kuweka machaguo ambayo yana mkusanyiko wa taarifa zinazolingana. Yaani unachaguwa chaguo kwa kubofya kicha unaletewa taarifa ama mkusanyiko wa taarifa ziinazo fanana.
Kutengenza menu utatumia tag ya menu ambayo ni <menu> pia utatumia tag ya link ambayo ni <a> tag ya link ni kuwezecha kubofya menyu na kupelekewa matokeo kwenye ukurasa mwingine. Baada ya hapo unaweza kutumia batani, ama ukaacha hivyo hivyo ama ukatumia kivuli.
Hapa tutaona menu yenye batani, link na tag ya menu.
<menu>
<a href=”link”><button>facebook</button></a>
<a href=”link”><button>youtube</button></a>
<a href=”link”><button>twitter</button></a>
<a href=”link”><button>whatsapp</button></a>
Utaj...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Njia za kupambana na saratani
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na saratani
Soma Zaidi...HTML - somo la 1: Maana ya HTML na kazi zake
Somo hili linakufundisha maana ya HTML, kwa nini inatumika, na jinsi ya kuandaa simu au kompyuta yako kwa ajili ya kuanza kutengeneza tovuti. Pia tutatengeneza ukurasa wetu wa kwanza wa HTML hatua kwa hatua.
Soma Zaidi...HTML - somo la 3: Tags za HTML zinazotumiwa katika uandishi
Katika somo hili nitakuletea orodhabya tag 25 za html ambazo hugumiwa katikabuandishi.
Soma Zaidi...HTML somo la 17: Jinsi ya kuunganisha HTML na CSS au JavaScript
Katika somo hili utakwend akujifunz ahatuwa kwa hatuwa jinsi ya Kuunganisha HTML na CSS au JavaScript
Soma Zaidi...HTML - somo la 14: Hatua za kutengeneza website
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza website hatuwa kwa hatuwa
Soma Zaidi...HTML- somo la 2: Kazi za HTML, code na tag kwenye website.
Katika somo somo hili utajifunza maana ya code, tag na mpangilio wa faili la HTML
Soma Zaidi...