picha

HTML - somo la 7: Vitu vya kuzingatia unapoandika HTML

Katika somo hili utajifunza sehemu muhimu katika faili la HTML kama vile tag, attribute na element

HTML  NI NINI?

HTML ni katika lugha za kikompyuta iliyopo katika kundi la markup language. Tofauti na watu wengi wanavyodhani kuwa HTML ni programming language. Hii si sahihi, kwa kuwa HTML imekosa sifa ya kuwa logic hivyo haiwezi kuwa programming language. HTML ni kifupisho cha HyperText Markup language. Lugha nyingine zilizo katika kundi hili ni pamoja na css amyao tutakuja kuisoma kwenye muendelezo wa mafunzo haya?

 

Karibia tovuti zote zinakuwa na HTML. Hivyo HTML ni moja katika lugha zinazotumika kwa wingi katika kutengeneza kurasa za wavuti (web pages). tovuti ya kwanza kuanzishwa duniani ilitoshelezwa na HTML . cheki link hii kufunguwa website ya kwanza duniani World first website http://info.cern.ch/hypertext/WWW/TheProject.html

 

 

HISTORIA FUPI YA HTML:

HTML kwa mara ya kwanza ilianzishwa na Tim Berners-Lee, Robert Cailliau na wengineo mwaka 1989. maana halisi ya hypertext ni kuwa faili linaruhusu kuwa na link (kiungo) ambayo unaweza kuhama kutoka ukurasa mmoja kwenda mwengie. Na maana ya Markup Language ni ile hali ya ambayo maandishi kuchakatwa na kuonekana katika mpangilio mzuri. Kufanya hivi unatakiwa utumie tag na attributes. Kutoka miaka hiyo mpaka sasa html imetolewa katika matoleo mengi na sasa tupo katika toleo la 5 yaani html5.

 

MPANGILIO WA FAILI LA HTML.

Faili la HTML lina sehemu kuu tatu ambazo ni:-

1. Kutaja aina ya faili.

2. Head

3. Body

 

Ukiangalia code hizo hapo juu mwanzoni kabisa kumeanza na code hii <!DOCTYPE html> hii ndio sehemu kuu ya kwanza ya faili la HTML na kazi yake ni kutambulisha aina ya faili. Hapo mwanzo ilikuwa inatajwa na toleo la HTML lakini kwa sasa si lazima na huchukuliwa kuwa I html5.

 

Kisha sehemu ya pili ni head ambayo imeanza na <head> na kumaliziwa na </head>. ndani ya tag hizi mbili ndipo zinakaa taarifa muhimu zinazolihusu faili hilo. Nyingi katika taarifa hizi hazionekani na mtumiaji wa tovuti hiyo. Taarifa hizi ni kama link, icon, na title. Kwa kiasi kikubwa taarifa znazopatikana hapa ni zile zinazoitwa metadata ni taarifa ambazo hazipo kwa ajili ya msomaji ama mtumiaji wa website husika, hizi zipo kwa ajili ya ingini pekuzi na kufanyia SEO. HIVYO KWENYE <head> kuna metadata na taarifa nyingine.

 

Kisha baada ya head inafata <body na mweisho imemaliziwa na </body>. hapa ndipo ambapo utaweka taarifa zote unazozitakazikae kwenye faili lako. Yaani maudhui ya huo ukurasa yanakaa hapa. Na watumiaji wa website hiyo watasoma maudhui hayo.

 

 

VITU VINAVYOUNDA FAILI LA HTML

Faili la HTML linaundwa kwa vitu vikuu viwili ambavyo ni TAG na ATTIBUTE. Hata hivyo unatakiwa ujuwe kuwa tag na attribute kwa pamoja huunda Element. Hivyo kabla hatujaenda mbele zaidi tutaona maa na ya hivi vitu vitatu.

 

 

<!DOCTYPE html>

<html>

<head>

<title>My First Webpage</title>

<meta charset="UTF-8">

<meta name="description" content="This is my first website">

</head>

<body>

<h1>Welcome to my webpage</h1>

<p>Welcome to my brand new website.</p>

<a href="http://www.google.com">Google</a>

</body>

</html>

 

 

 

TAG

Katika HTML tag hufafanuliwa kama seti ya herufi zinazounda amri iliyoumbizwa kwa ukurasa wa Wavuti. Tag ni kama chombo cha kubebea code za HTML. Code zote huandikwa kwa tag. Hapo zamani code zote katika kutengeneza ukurasa wa wavuti zilitumia tag, ijaokuwa siku hizi baadhi ya sehemu akuna haja ya kutumia tag.

 

Tag hutumika katika html kwa ajili ya kuanzia kuandika elment, na kawaida tag zinakuwa na za kufungulia ambazo huanzwa na < kisha inakuwa na ya kufungia ambayo huazwa na </. mfano  wa tag ni kama huu <h1>hello</h1> hapo <h1> ni tag ya kufungulia na </h1> ni tag ya kufungia. 

 

Katika code zilizoonyeshwa hapo juu  mifano ya tag za kufungua ni <html>, <head>, <tittle>, <meta>, <body>, <h1>, <p> na <a>. mifano ya tag za kufunga ni </head>, </title>, </h1>, </p>, </a>, </body> na </jtml>

 

 

ATTRIBUTES

Hizi hutumika kwa ajili ya kuongeza taarifa za ziada katika...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: HTML Main: Masomo File: Download PDF Views 1075

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

HTML - somo la 13: Jinsi ya kugawa ukurasa wa HTML

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kugawanya ukurasa wa HTML katika column

Soma Zaidi...
HTML - somo la 6: Jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la HTML

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la html na kuweka rangi ya background. Pia utajifunza kufanya ukurasa uwe responsive yaani uendani na ukubwa wa kifaa.

Soma Zaidi...
HTML - somo la 12: Sehemu kuu za faili la HTML

Katika somo hili utajifunza kuhusu sehemu kuu za faili la HTML

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Speaker

Spika ni kifaa kinachobadilisha mawimbi ya umeme kuwa sauti tunayosikia. Ndani ya spika kuna sumaku na utando laini unaotikisika ili kutoa sauti. Spika inapogoma kufanya kazi, vyanzo vikuu huwa ni vitatu: matatizo ya kiufundi (waya/uchafu), matatizo ya mipangilio (settings), au hitilafu za mfumo wa kompyuta/simu.Uzuri ni kwamba, matatizo mengi yanayotokea kila siku unaweza kuyatatua mwenyewe kwa kufuata hatua rahisi tulizokuandalia hapa chini

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Mikrofoni

Je, unajaribu kupiga simu, kurekodi sauti, au kuingia kwenye mkutano wa mtandaoni lakini mikrofoni yako haifanyi kazi? Huu ni mwongozo rahisi na wa hatua kwa hatua unaoelezea jinsi ya kutatua matatizo yote ya mikrofoni kwenye simu au kompyuta yako. Tumeandika mwongozo huu kwa lugha rahisi ya Kiswahili ili kila mtu, hata asiye na ujuzi wa teknolojia, aweze kuelewa na kurekebisha kifaa chake mara moja bila kuhitaji fundi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kufanya Backup ya Simu

Simu ya mkononi imekuwa sehemu muhimu sana ya maisha yetu ya kila siku. Tunatumia simu kuhifadhi namba za watu tunaowajua, picha za familia, video muhimu, ujumbe, nyaraka, programu na taarifa nyingine nyingi. Lakini tatizo linaweza kutokea wakati wowote. Simu inaweza kupotea, kuharibika, kuibiwa au kufutika taarifa zake kwa bahati mbaya. Hapo ndipo umuhimu wa kufanya backup ya simu unapokuwa mkubwa. Backup ya simu ni njia ya kutengeneza nakala ya taarifa zako muhimu na kuzihifadhi sehemu salama ili uweze kuzirudisha pale unapohitaji. Kwa kufanya backup mara kwa mara, unapunguza hatari ya kupoteza vitu muhimu vilivyokuwa kwenye simu yako. Katika makala hii tutajifunza maana ya backup ya simu, umuhimu wake, njia mbalimbali za kufanya backup kwenye simu za Android na iPhone, vitu vinavyoweza kuhifadhiwa, makosa ya kuepuka na hatua rahisi ambazo kila mtu anaweza kufuata hata kama hana ujuzi mkubwa wa teknolojia.

Soma Zaidi...