picha

HTML - somo la 7: Vitu vya kuzingatia unapoandika HTML

Katika somo hili utajifunza sehemu muhimu katika faili la HTML kama vile tag, attribute na element

HTML  NI NINI?

HTML ni katika lugha za kikompyuta iliyopo katika kundi la markup language. Tofauti na watu wengi wanavyodhani kuwa HTML ni programming language. Hii si sahihi, kwa kuwa HTML imekosa sifa ya kuwa logic hivyo haiwezi kuwa programming language. HTML ni kifupisho cha HyperText Markup language. Lugha nyingine zilizo katika kundi hili ni pamoja na css amyao tutakuja kuisoma kwenye muendelezo wa mafunzo haya?

 

Karibia tovuti zote zinakuwa na HTML. Hivyo HTML ni moja katika lugha zinazotumika kwa wingi katika kutengeneza kurasa za wavuti (web pages). tovuti ya kwanza kuanzishwa duniani ilitoshelezwa na HTML . cheki link hii kufunguwa website ya kwanza duniani World first website http://info.cern.ch/hypertext/WWW/TheProject.html

 

 

HISTORIA FUPI YA HTML:

HTML kwa mara ya kwanza ilianzishwa na Tim Berners-Lee, Robert Cailliau na wengineo mwaka 1989. maana halisi ya hypertext ni kuwa faili linaruhusu kuwa na link (kiungo) ambayo unaweza kuhama kutoka ukurasa mmoja kwenda mwengie. Na maana ya Markup Language ni ile hali ya ambayo maandishi kuchakatwa na kuonekana katika mpangilio mzuri. Kufanya hivi unatakiwa utumie tag na attributes. Kutoka miaka hiyo mpaka sasa html imetolewa katika matoleo mengi na sasa tupo katika toleo la 5 yaani html5.

 

MPANGILIO WA FAILI LA HTML.

Faili la HTML lina sehemu kuu tatu ambazo ni:-

1. Kutaja aina ya faili.

2. Head

3. Body

 

Ukiangalia code hizo hapo juu mwanzoni kabisa kumeanza na code hii <!DOCTYPE html> hii ndio sehemu kuu ya kwanza ya faili la HTML na kazi yake ni kutambulisha aina ya faili. Hapo mwanzo ilikuwa inatajwa na toleo la HTML lakini kwa sasa si lazima na huchukuliwa kuwa I html5.

 

Kisha sehemu ya pili ni head ambayo imeanza na <head> na kumaliziwa na </head>. ndani ya tag hizi mbili ndipo zinakaa taarifa muhimu zinazolihusu faili hilo. Nyingi katika taarifa hizi hazionekani na mtumiaji wa tovuti hiyo. Taarifa hizi ni kama link, icon, na title. Kwa kiasi kikubwa taarifa znazopatikana hapa ni zile zinazoitwa metadata ni taarifa ambazo hazipo kwa ajili ya msomaji ama mtumiaji wa website husika, hizi zipo kwa ajili ya ingini pekuzi na kufanyia SEO. HIVYO KWENYE <head> kuna metadata na taarifa nyingine.

 

Kisha baada ya head inafata <body na mweisho imemaliziwa na </body>. hapa ndipo ambapo utaweka taarifa zote unazozitakazikae kwenye faili lako. Yaani maudhui ya huo ukurasa yanakaa hapa. Na watumiaji wa website hiyo watasoma maudhui hayo.

 

 

VITU VINAVYOUNDA FAILI LA HTML

Faili la HTML linaundwa kwa vitu vikuu viwili ambavyo ni TAG na ATTIBUTE. Hata hivyo unatakiwa ujuwe kuwa tag na attribute kwa pamoja huunda Element. Hivyo kabla hatujaenda mbele zaidi tutaona maa na ya hivi vitu vitatu.

 

 

<!DOCTYPE html>

<html>

<head>

<title>My First Webpage</title>

<meta charset="UTF-8">

<meta name="description" content="This is my first website">

</head>

<body>

<h1>Welcome to my webpage</h1>

<p>Welcome to my brand new website.</p>

<a href="http://www.google.com">Google</a>

</body>

</html>

 

 

 

TAG

Katika HTML tag hufafanuliwa kama seti ya herufi zinazounda amri iliyoumbizwa kwa ukurasa wa Wavuti. Tag ni kama chombo cha kubebea code za HTML. Code zote huandikwa kwa tag. Hapo zamani code zote katika kutengeneza ukurasa wa wavuti zilitumia tag, ijaokuwa siku hizi baadhi ya sehemu akuna haja ya kutumia tag.

 

Tag hutumika katika html kwa ajili ya kuanzia kuandika elment, na kawaida tag zinakuwa na za kufungulia ambazo huanzwa na < kisha inakuwa na ya kufungia ambayo huazwa na </. mfano  wa tag ni kama huu <h1>hello</h1> hapo <h1> ni tag ya kufungulia na </h1> ni tag ya kufungia. 

 

Katika code zilizoonyeshwa hapo juu  mifano ya tag za kufungua ni <html>, <head>, <tittle>, <meta>, <body>, <h1>, <p> na <a>. mifano ya tag za kufunga ni </head>, </title>, </h1>, </p>, </a>, </body> na </jtml>

 

 

ATTRIBUTES

Hizi hutumika kwa ajili ya kuongeza taarifa za ziada katika...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: HTML Main: Masomo File: Download PDF Views 1031

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 web hosting     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Jinsi ya Kuhifadhi Picha Kwenye Cloud

Picha ni kumbukumbu muhimu zinazohifadhi matukio ya maisha yetu kama vile harusi, sherehe, safari, watoto, familia na kazi mbalimbali. Tatizo kubwa ambalo watu wengi hukutana nalo ni kupoteza picha kutokana na simu kuharibika, kuibiwa, kupotea au kufutwa kimakosa. Njia salama ya kulinda picha zako ni kuzihifadhi kwenye Cloud. Katika makala hii utajifunza cloud ni nini, jinsi inavyofanya kazi, faida za kuhifadhi picha kwenye cloud, hatua za kuhifadhi picha zako kwa usalama pamoja na mambo muhimu ya kuzingatia ili kuhakikisha kumbukumbu zako zinabaki salama kwa muda mrefu.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Simu Kutopiga Simu

Kama simu yako haipigi au haipokei simu, usipaniki. Mara nyingi tatizo hili linasababishwa na mambo madogo unayoweza kuyarekebisha mwenyewe nyumbani. Angalia salio na bando lako, washa na uzime mfumo wa ndege (Airplane Mode), au zima simu na kuiwasha tena. Kama hayo hayajasaidia, hakikisha laini yako (SIM card) imekaa vizuri au wasiliana na kampuni yako ya simu. Kwenye makala hii, tutaenda hatua kwa hatua kwa lugha rahisi kabisa ili urudishe simu yako kwenye hali ya kawaida haraka

Soma Zaidi...
Sababu Zinazofanya Betri Iishe Haraka

Betri ni sehemu muhimu sana ya simu, kompyuta mpakato, saa janja na vifaa vingine vya kielektroniki. Hata hivyo, watu wengi hukutana na tatizo la betri kuisha haraka bila kujua chanzo chake. Wakati mwingine tatizo halitokani na ubora wa simu au betri, bali hutokana na namna kifaa kinavyotumika kila siku. Katika makala hii utajifunza sababu kuu zinazofanya betri iishe haraka, jinsi ya kutambua tatizo, pamoja na njia rahisi za kuongeza muda wa matumizi ya betri. Maelezo haya yameandikwa kwa lugha rahisi ili kila mtu ayaelewe, hata kama hana ujuzi wa teknolojia.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kuunganisha Simu na Wi-Fi

Wi-Fi ni njia rahisi inayowezesha simu kuunganishwa na intaneti bila kutumia bando la kawaida la simu. Kwa kutumia Wi-Fi, mtu anaweza kutumia intaneti kwa gharama ndogo au wakati mwingine bila gharama yoyote, hasa anapokuwa sehemu yenye mtandao wa Wi-Fi kama nyumbani, kazini, shuleni, hotelini au sehemu nyingine za umma. Kuunganisha simu na Wi-Fi ni jambo rahisi ambalo mtu yeyote anaweza kufanya hata kama hajawahi kutumia teknolojia sana. Unachohitaji ni simu yenye uwezo wa kutumia Wi-Fi, jina la mtandao wa Wi-Fi, na nenosiri kama mtandao huo umefungwa. Makala hii inaelezea hatua kwa hatua jinsi ya kuunganisha simu na Wi-Fi, mambo ya kuzingatia wakati wa kutumia Wi-Fi, sababu zinazoweza kufanya simu ishindwe kuunganishwa, pamoja na faida za kutumia mtandao wa Wi-Fi.

Soma Zaidi...
HTML - somo la 12: Sehemu kuu za faili la HTML

Katika somo hili utajifunza kuhusu sehemu kuu za faili la HTML

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Mtandao wa Simu

Posti hii inatoa mwongozo rahisi na wa hatua kwa hatua kuhusu jinsi ya kurekebisha matatizo ya mtandao kwenye simu yako ya mkononi. Umejifunza njia za haraka kama kuwasha ‘Upepo’ (Flight Mode), kuwasha upya simu, na kuangalia kadi ya SIM ili kurudisha mawasiliano haraka bila kuhitaji fundi.

Soma Zaidi...