HTML - somo la 7: Vitu vya kuzingatia unapoandika HTML
Katika somo hili utajifunza sehemu muhimu katika faili la HTML kama vile tag, attribute na element
HTML NI NINI?
HTML ni katika lugha za kikompyuta iliyopo katika kundi la markup language. Tofauti na watu wengi wanavyodhani kuwa HTML ni programming language. Hii si sahihi, kwa kuwa HTML imekosa sifa ya kuwa logic hivyo haiwezi kuwa programming language. HTML ni kifupisho cha HyperText Markup language. Lugha nyingine zilizo katika kundi hili ni pamoja na css amyao tutakuja kuisoma kwenye muendelezo wa mafunzo haya?
Karibia tovuti zote zinakuwa na HTML. Hivyo HTML ni moja katika lugha zinazotumika kwa wingi katika kutengeneza kurasa za wavuti (web pages). tovuti ya kwanza kuanzishwa duniani ilitoshelezwa na HTML . cheki link hii kufunguwa website ya kwanza duniani World first website http://info.cern.ch/hypertext/WWW/TheProject.html
HISTORIA FUPI YA HTML:
HTML kwa mara ya kwanza ilianzishwa na Tim Berners-Lee, Robert Cailliau na wengineo mwaka 1989. maana halisi ya hypertext ni kuwa faili linaruhusu kuwa na link (kiungo) ambayo unaweza kuhama kutoka ukurasa mmoja kwenda mwengie. Na maana ya Markup Language ni ile hali ya ambayo maandishi kuchakatwa na kuonekana katika mpangilio mzuri. Kufanya hivi unatakiwa utumie tag na attributes. Kutoka miaka hiyo mpaka sasa html imetolewa katika matoleo mengi na sasa tupo katika toleo la 5 yaani html5.
MPANGILIO WA FAILI LA HTML.
Faili la HTML lina sehemu kuu tatu ambazo ni:-
1. Kutaja aina ya faili.
2. Head
3. Body
Ukiangalia code hizo hapo juu mwanzoni kabisa kumeanza na code hii <!DOCTYPE html> hii ndio sehemu kuu ya kwanza ya faili la HTML na kazi yake ni kutambulisha aina ya faili. Hapo mwanzo ilikuwa inatajwa na toleo la HTML lakini kwa sasa si lazima na huchukuliwa kuwa I html5.
Kisha sehemu ya pili ni head ambayo imeanza na <head> na kumaliziwa na </head>. ndani ya tag hizi mbili ndipo zinakaa taarifa muhimu zinazolihusu faili hilo. Nyingi katika taarifa hizi hazionekani na mtumiaji wa tovuti hiyo. Taarifa hizi ni kama link, icon, na title. Kwa kiasi kikubwa taarifa znazopatikana hapa ni zile zinazoitwa metadata ni taarifa ambazo hazipo kwa ajili ya msomaji ama mtumiaji wa website husika, hizi zipo kwa ajili ya ingini pekuzi na kufanyia SEO. HIVYO KWENYE <head> kuna metadata na taarifa nyingine.
Kisha baada ya head inafata <body na mweisho imemaliziwa na </body>. hapa ndipo ambapo utaweka taarifa zote unazozitakazikae kwenye faili lako. Yaani maudhui ya huo ukurasa yanakaa hapa. Na watumiaji wa website hiyo watasoma maudhui hayo.
VITU VINAVYOUNDA FAILI LA HTML
Faili la HTML linaundwa kwa vitu vikuu viwili ambavyo ni TAG na ATTIBUTE. Hata hivyo unatakiwa ujuwe kuwa tag na attribute kwa pamoja huunda Element. Hivyo kabla hatujaenda mbele zaidi tutaona maa na ya hivi vitu vitatu.
<!DOCTYPE html>
<html>
<head>
<title>My First Webpage</title>
<meta charset="UTF-8">
<meta name="description" content="This is my first website">
</head>
<body>
<h1>Welcome to my webpage</h1>
<p>Welcome to my brand new website.</p>
<a href="http://www.google.com">Google</a>
</body>
</html>
TAG
Katika HTML tag hufafanuliwa kama seti ya herufi zinazounda amri iliyoumbizwa kwa ukurasa wa Wavuti. Tag ni kama chombo cha kubebea code za HTML. Code zote huandikwa kwa tag. Hapo zamani code zote katika kutengeneza ukurasa wa wavuti zilitumia tag, ijaokuwa siku hizi baadhi ya sehemu akuna haja ya kutumia tag.
Tag hutumika katika html kwa ajili ya kuanzia kuandika elment, na kawaida tag zinakuwa na za kufungulia ambazo huanzwa na < kisha inakuwa na ya kufungia ambayo huazwa na </. mfano wa tag ni kama huu <h1>hello</h1> hapo <h1> ni tag ya kufungulia na </h1> ni tag ya kufungia.
Katika code zilizoonyeshwa hapo juu mifano ya tag za kufungua ni <html>, <head>, <tittle>, <meta>, <body>, <h1>, <p> na <a>. mifano ya tag za kufunga ni </head>, </title>, </h1>, </p>, </a>, </body> na </jtml>
ATTRIBUTES
Hizi hutumika kwa ajili ya kuongeza taarifa za ziada katika...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
HTML - somo la 9: Jinsi ya kutumia tag za HTML katika uandishi wa maudhui
Katika somo hili utakwenda kuona jinsi ya kuzitumia tag balimbali za html
Soma Zaidi...Je, Kuchaji Simu Usiku Kucha Ni Salama?
Je, ni salama kuacha simu kwenye chaji usiku kucha unapolala? Watu wengi wanaamini kuwa tabia hii inalipua simu au kuharibu betri kabisa. Katika makala hii, utajifunza ukweli wa kisayansi kuhusu simu za kisasa, jinsi mifumo ya usalama inavyofanya kazi, na mbinu rahisi za kurefusha maisha ya betri yako bila hofu. Soma ujue jinsi ya kulinda simu yako leo!
Soma Zaidi...Jinsi ya Kusafisha Simu Isifanye Kazi Polepole
Je, simu yako imekuwa ikifungua programu kwa kuchelewa, kuganda mara kwa mara au kufanya kazi polepole kuliko ilivyokuwa mwanzo? Tatizo hili ni la kawaida kwa watumiaji wengi wa simu za Android na hata iPhone. Mara nyingi watu hudhani kuwa simu imeharibika au imezeeka, wakati ukweli ni kwamba kuna uchafu wa kidijitali unaokusanyika ndani ya simu na kuifanya ishindwe kufanya kazi kwa kasi. Katika makala hii utajifunza jinsi ya kusafisha simu ili irudi kufanya kazi vizuri. Utaelewa sababu zinazofanya simu iwe polepole, namna ya kufuta faili zisizo muhimu, kusafisha kumbukumbu ya programu, kuondoa programu zisizotumika, kusasisha mfumo wa simu pamoja na mbinu nyingine zinazoweza kuongeza kasi ya simu bila kutumia fedha.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kujua Kama Simu Yako Ina Virusi
Simu za kisasa zimekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Tunazitumia kuwasiliana, kufanya malipo, kuhifadhi picha, kuendesha biashara, kusoma taarifa mbalimbali na hata kufanya kazi. Kwa sababu simu zetu zina taarifa nyingi muhimu, wahalifu wa mtandao hutafuta njia za kuziathiri kwa kutumia programu hatari zinazojulikana kama virusi vya simu. Virusi kwenye simu vinaweza kusababisha matatizo mbalimbali kama simu kuwa polepole, betri kuisha haraka, matangazo yasiyoeleweka kujitokeza, matumizi makubwa ya intaneti, au hata kupotea kwa taarifa zako binafsi. Kujua dalili za simu yenye virusi mapema kunaweza kukusaidia kulinda taarifa zako na kuendelea kutumia simu yako kwa usalama. Katika makala hii utaelewa maana ya virusi vya simu, dalili zinazoonyesha kuwa simu yako inaweza kuwa imeambukizwa, sababu zinazoweza kusababisha virusi kuingia kwenye simu, na hatua unazoweza kuchukua kuiondoa na kuilinda.
Soma Zaidi...HTML-somo la 5: Jinsi ya kupangilia munekano wa maudhui kwenye website
Katika somo hili utajifunza Kuweka picha Kuweka rangi Kuweka linki Kupangilia position na alignment ya maandishi Kuongeza ukubwa wa herufi Kukoment
Soma Zaidi...