picha

HTML - somo la 13: Jinsi ya kugawa ukurasa wa HTML

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kugawanya ukurasa wa HTML katika column

KUGAWA UKURASA WA HTML
Kwa kutumia HTML unaweza kugawa ukurasa katia row. Kwa wale ambao wanatumia microsoft word hapa utaweza kunielewaa. Mfano unatye taarifa yako. Kisha ukataka kugawa doc katika sehemu tatu yaani kuli, katu na kushoto. Hiki ndio kitu ninachokizungumzia hapa. Katika kugawa huku tutatumia tag section ambayo ni <div>

Ili kufanikisha lengo letu kwa urahisi tutatumia baadhi ya element za CSS. Tutatumia class. Class itakuwa ndio attribute, div itakuwa tag na value itakuwa ni section tunazokwenda kuweka. Hapa unatakiwa pia ufanye hesabu. Kama ukurasa mzima una upana wa 100%, je nikiugawa sehemu tatu kwa upana kila kisehemu kitakuwa na upana gani? (100/3 = 33.3).

 

Unaweza kutumia style za nje ama ya ndani.ni vyema kutumia style ya nje ili kupunguza msongamano wa tag. Tunatumia style ili kuweza kupangilia muonekano wa sehemu zetu tutakazogawa.tunatumia class ili kuweza kubeba maudhui ya kila kisehemu, na dutatumia div iwe kama chombo cha kubebea maudhui (tag na content).

 

Kuweza kufgawa ukurasa fanya hivi:-
1.Tumia stayle ya nje
<style>

</style>

2.Weka alama za kutambulisha visehemu utakavyogawa ndani ya style. Anza na kuweka kidoto kabla ya kuweka hiyo alama. Kidoto ndio kitajulisha kuwa hiyo ni value kwenye attribute ya class. Mfano .left .right .middle

 

3.Iki kupangilia vigawany hivyo inatakiwa kimoja kiwe kulia, kingine kushoto na kingine kati. Kufanya hivi ndani ya kila kigawanyo unatakiwa ueleze kikae upande gani. Hivyo utatumia float. Hii ni kama vile tulivyoifanyia picha kwenye masomo yaliopita. Tuliona namna ya kuifanya picha ikae upande unaotaka. Mfano utafanya 

<style>
 .left {float: left; }
 .middle {float: left; }
 .right {float: right;}
</style>

Hapo utakuwa tayari umegawa ukurasa wako, kushoto, kati na kulia. Sasa ili kufanya kila sehemu ikae sawa mahala pale tunatakiwa tugawanye kihisabu, ili kila kimoja kikae mahala pake bila ya kuathiri vingine. 

 

4.Kwa kuwa contente zote zitakaa ndani ya div section hivyo tutakwenda kuigawa div. Fanya hivi weka style ya div ndani ya tag ya style, kisha width iwe ni 33.3%. kwa maana kuwa 100% ukiigwa sehemu tatu tunapata 33.3%.

<style>
 .left {float: left; }
 .middle {float: left; }
 .right {float: right;}
 div { width: 33.3%;}
</style>

5.Baada ya hapo sasa tunakwenda kutumia style zetu kwenye section ya div.badala ya kutumia style attribute sasa tunatumia class. Na kanuni ni ileile ya kuweka alama ya = ikifuatiwa na funga semi na kuweka value kisha funga semi. Kwa sharti kuwa haya yote yafanyike kwenye tag ya kufungulia.


Mfano: <div class="left"> utaweza maudhui yako unayotaka kuweka upande wa kushoto ,kisha kati, kwa ajili ya kuweka maudhui ya kati <div class="middle"> kisha ya kulia ili kuweka maudhui ya upande wa kulia  <div class="right">

<div class="left">
 <h1>HEADING ONE</h1>
 <p>hellow this is paragraph</p>
</div>
<div class="middle">
 <h1>HEADING TWO</h1>
 <p>hellow this is paragraph</p>
</div>
<div class="right">
 <h1>HEADING THREE</h1>
 <p>hellow this is paragraph</p>
</div>

Kwa kufanya hivi utakuwa umeweza kuugawa ukurasa wako katika pande tatu zilizo sawa. Kwa kufanya hivi kama unataka pande nyin...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: HTML Main: Masomo File: Download PDF Views 1023

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 web hosting     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Jinsi ya Kutatua Tatizo la Mtandao wa Simu

Posti hii inatoa mwongozo rahisi na wa hatua kwa hatua kuhusu jinsi ya kurekebisha matatizo ya mtandao kwenye simu yako ya mkononi. Umejifunza njia za haraka kama kuwasha ‘Upepo’ (Flight Mode), kuwasha upya simu, na kuangalia kadi ya SIM ili kurudisha mawasiliano haraka bila kuhitaji fundi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutumia Fingerprint Kwenye Simu

Fingerprint ni teknolojia inayokuwezesha kufungua simu yako kwa kutumia alama ya kidole badala ya kuandika namba ya siri au mchoro (Pattern). Mfumo huu umeifanya matumizi ya simu kuwa rahisi, ya haraka na salama zaidi. Mbali na kufungua simu, fingerprint pia inaweza kutumika kuthibitisha malipo, kufungua programu mbalimbali na kulinda taarifa binafsi zilizopo kwenye simu. Katika makala hii utajifunza fingerprint ni nini, jinsi inavyofanya kazi, namna ya kuiweka kwenye simu, jinsi ya kuitumia kwa usahihi, faida zake, changamoto zinazoweza kujitokeza pamoja na njia za kuzitatua. Pia utapata ukweli muhimu katika sehemu ya "Je! Wajua?" ambao unaweza kukusaidia kutumia fingerprint kwa ufanisi zaidi.

Soma Zaidi...
HTML - somo la 6: Jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la HTML

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuweka menyu kwenye faili la html na kuweka rangi ya background. Pia utajifunza kufanya ukurasa uwe responsive yaani uendani na ukubwa wa kifaa.

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kutatua Tatizo la Speaker

Spika ni kifaa kinachobadilisha mawimbi ya umeme kuwa sauti tunayosikia. Ndani ya spika kuna sumaku na utando laini unaotikisika ili kutoa sauti. Spika inapogoma kufanya kazi, vyanzo vikuu huwa ni vitatu: matatizo ya kiufundi (waya/uchafu), matatizo ya mipangilio (settings), au hitilafu za mfumo wa kompyuta/simu.Uzuri ni kwamba, matatizo mengi yanayotokea kila siku unaweza kuyatatua mwenyewe kwa kufuata hatua rahisi tulizokuandalia hapa chini

Soma Zaidi...
Jinsi ya Kuhifadhi Picha Kwenye Cloud

Picha ni kumbukumbu muhimu zinazohifadhi matukio ya maisha yetu kama vile harusi, sherehe, safari, watoto, familia na kazi mbalimbali. Tatizo kubwa ambalo watu wengi hukutana nalo ni kupoteza picha kutokana na simu kuharibika, kuibiwa, kupotea au kufutwa kimakosa. Njia salama ya kulinda picha zako ni kuzihifadhi kwenye Cloud. Katika makala hii utajifunza cloud ni nini, jinsi inavyofanya kazi, faida za kuhifadhi picha kwenye cloud, hatua za kuhifadhi picha zako kwa usalama pamoja na mambo muhimu ya kuzingatia ili kuhakikisha kumbukumbu zako zinabaki salama kwa muda mrefu.

Soma Zaidi...