picha

HTML - somo la 13: Jinsi ya kugawa ukurasa wa HTML

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kugawanya ukurasa wa HTML katika column

KUGAWA UKURASA WA HTML
Kwa kutumia HTML unaweza kugawa ukurasa katia row. Kwa wale ambao wanatumia microsoft word hapa utaweza kunielewaa. Mfano unatye taarifa yako. Kisha ukataka kugawa doc katika sehemu tatu yaani kuli, katu na kushoto. Hiki ndio kitu ninachokizungumzia hapa. Katika kugawa huku tutatumia tag section ambayo ni <div>

Ili kufanikisha lengo letu kwa urahisi tutatumia baadhi ya element za CSS. Tutatumia class. Class itakuwa ndio attribute, div itakuwa tag na value itakuwa ni section tunazokwenda kuweka. Hapa unatakiwa pia ufanye hesabu. Kama ukurasa mzima una upana wa 100%, je nikiugawa sehemu tatu kwa upana kila kisehemu kitakuwa na upana gani? (100/3 = 33.3).

 

Unaweza kutumia style za nje ama ya ndani.ni vyema kutumia style ya nje ili kupunguza msongamano wa tag. Tunatumia style ili kuweza kupangilia muonekano wa sehemu zetu tutakazogawa.tunatumia class ili kuweza kubeba maudhui ya kila kisehemu, na dutatumia div iwe kama chombo cha kubebea maudhui (tag na content).

 

Kuweza kufgawa ukurasa fanya hivi:-
1.Tumia stayle ya nje
<style>

</style>

2.Weka alama za kutambulisha visehemu utakavyogawa ndani ya style. Anza na kuweka kidoto kabla ya kuweka hiyo alama. Kidoto ndio kitajulisha kuwa hiyo ni value kwenye attribute ya class. Mfano .left .right .middle

 

3.Iki kupangilia vigawany hivyo inatakiwa kimoja kiwe kulia, kingine kushoto na kingine kati. Kufanya hivi ndani ya kila kigawanyo unatakiwa ueleze kikae upande gani. Hivyo utatumia float. Hii ni kama vile tulivyoifanyia picha kwenye masomo yaliopita. Tuliona namna ya kuifanya picha ikae upande unaotaka. Mfano utafanya 

<style>
 .left {float: left; }
 .middle {float: left; }
 .right {float: right;}
</style>

Hapo utakuwa tayari umegawa ukurasa wako, kushoto, kati na kulia. Sasa ili kufanya kila sehemu ikae sawa mahala pale tunatakiwa tugawanye kihisabu, ili kila kimoja kikae mahala pake bila ya kuathiri vingine. 

 

4.Kwa kuwa contente zote zitakaa ndani ya div section hivyo tutakwenda kuigawa div. Fanya hivi weka style ya div ndani ya tag ya style, kisha width iwe ni 33.3%. kwa maana kuwa 100% ukiigwa sehemu tatu tunapata 33.3%.

<style>
 .left {float: left; }
 .middle {float: left; }
 .right {float: right;}
 div { width: 33.3%;}
</style>

5.Baada ya hapo sasa tunakwenda kutumia style zetu kwenye section ya div.badala ya kutumia style attribute sasa tunatumia class. Na kanuni ni ileile ya kuweka alama ya = ikifuatiwa na funga semi na kuweka value kisha funga semi. Kwa sharti kuwa haya yote yafanyike kwenye tag ya kufungulia.


Mfano: <div class="left"> utaweza maudhui yako unayotaka kuweka upande wa kushoto ,kisha kati, kwa ajili ya kuweka maudhui ya kati <div class="middle"> kisha ya kulia ili kuweka maudhui ya upande wa kulia  <div class="right">

<div class="left">
 <h1>HEADING ONE</h1>
 <p>hellow this is paragraph</p>
</div>
<div class="middle">
 <h1>HEADING TWO</h1>
 <p>hellow this is paragraph</p>
</div>
<div class="right">
 <h1>HEADING THREE</h1>
 <p>hellow this is paragraph</p>
</div>

Kwa kufanya hivi utakuwa umeweza kuugawa ukurasa wako katika pande tatu zilizo sawa. Kwa kufanya hivi kama unataka pande nyin...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: HTML Main: Masomo File: Download PDF Views 920

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 ai web app     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

HTML - somo la 12: Sehemu kuu za faili la HTML

Katika somo hili utajifunza kuhusu sehemu kuu za faili la HTML

Soma Zaidi...
HTML - somo la 16: Jinsi ya ku host website bure

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website yako bila malipo

Soma Zaidi...
HTML - somo la 7: Vitu vya kuzingatia unapoandika HTML

Katika somo hili utajifunza sehemu muhimu katika faili la HTML kama vile tag, attribute na element

Soma Zaidi...
HTML - somo la 14: Hatua za kutengeneza website

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza website hatuwa kwa hatuwa

Soma Zaidi...
HTML - somo la 8: Mgawanyiko wa Tag za HTML na kazi zake

Katika somo hili tunakwenda kugawanya tag za HTML, pia nitakwenda kukuletea tag 70 za HTML

Soma Zaidi...
HTML-somo la 5: Jinsi ya kupangilia munekano wa maudhui kwenye website

Katika somo hili utajifunza Kuweka picha Kuweka rangi Kuweka linki Kupangilia position na alignment ya maandishi Kuongeza ukubwa wa herufi Kukoment

Soma Zaidi...